< Hesabu 36 >

1 Viongozi wa jamaa ya ukoo wa Gileadi mwana wa Makiri, mwana wa Manase, waliokuwa wametoka katika koo za wazao wa Yosefu, walikuja na kuzungumza mbele ya Mose na viongozi, wakuu wa jamaa ya Waisraeli.
Og de Øverste for Fædrenehusene i Gileads Børns Slægt, hans, som var en Søn af Makir, Manasse Søn, af Josefs Børns Slægt, gik frem, og de talede for Mose Ansigt og for Fyrsternes Ansigt, dem, som vare de Øverste for Fædrenehusene blandt Israels Børn,
2 Wakasema, “Bwana alipomwamuru bwana wangu kuwapa Waisraeli nchi kama urithi kwa kura, alikuamuru kutoa urithi wa ndugu yetu Selofehadi kwa binti zake.
og de sagde: Herren har budet min Herre at give Israels Børn Landet til Arv ved Lod; og min Herre er befalet af Herren at give vor Broder Zelafehads Arv til hans Døtre;
3 Sasa ikiwa wataolewa na watu wa makabila mengine ya Kiisraeli, itakuwa kwamba urithi wao utaondolewa kutoka urithi wa mababu zetu na kuongezwa katika urithi wa kabila ambalo dada hao wameolewa. Kwa hiyo sehemu ya urithi tuliyogawiwa itachukuliwa kutoka kwetu.
men blive de en af de Sønner, som høre til de andre Israels Børns Stammer, til Hustruer, da vil deres Arv gaa bort fra vore Fædres Arv og lægges til den Stamme, som de gaa over til, og gaa bort fra vor Arvs Lod;
4 Wakati mwaka wa Yubile kwa Waisraeli utafika, urithi wao utaongezwa kwa lile kabila ambalo wameolewa, na mali yao itaondolewa kutoka urithi wa kabila la mababu zetu.”
og naar det bliver Jubelaar for Israels Børn, da lægges deres Arv til den Stammes Arv, som de gik over til; og dermed vil deres Arv gaa bort fra vore Fædres Stammes Arv.
5 Ndipo kwa agizo la Bwana Mose akatoa amri ifuatayo kwa Waisraeli: “Kile wazao wa kabila la Yosefu wanachosema ni kweli.
Og Mose bød Israels Børn efter Herrens Mund og sagde: Josefs Børns Stamme taler ret.
6 Hivi ndivyo Bwana anavyoamuru kwa binti za Selofehadi: Wanaweza kuolewa na mtu yeyote wampendaye, mradi tu waolewe miongoni mwa koo za kabila za baba yao.
Dette er det Ord, som Herren byder om Zelafehads Døtre og siger: De maa vorde dem til Hustruer, som synes gode for deres Øjne, kun at de vorde dem til Hustruer, som ere af deres Fædres Stammes Slægtskab,
7 Hakuna urithi katika Israeli utakaohamishwa kutoka kabila moja kwenda kabila jingine, kwa kuwa kila Mwisraeli atatunza ardhi ya kabila lake aliyoirithi kutoka kwa baba zake.
at Israels Børns Arv ej skal komme omkring fra en Stamme til en anden; men hver iblandt Israels Børn skal hænge ved sine Fædres Stammes Arv.
8 Kila binti atakayerithi ardhi katika kabila lolote la Israeli ni lazima aolewe na mtu kutoka kabila na ukoo wa baba yake, ili kila Mwisraeli amiliki urithi wa baba zake.
Og hver Datter af Israels Børns Stammer, som arver nogen Arv, skal vorde en af sin Faders Stammes Slægtskab til Hustru, paa det Israels Børn kunne arve hver sine Fædres Arv,
9 Hakuna urithi uwezao kuhamishwa kutoka kabila moja kwenda kabila jingine, kwa kuwa kila kabila la Israeli litatunza nchi linayorithi.”
og at en Arv ikke skal komme omkring fra en Stamme til en anden Stamme; men Israels Børns Stammer skulle hænge hver ved sin Arv.
10 Kwa hiyo binti za Selofehadi wakafanya kama Bwana alivyomwamuru Mose.
Som Herren havde befalet Mose, saa gjorde Zelafehads Døtre.
11 Binti za Selofehadi, ambao ni Mahla, Tirsa, Hogla, Milka na Noa, wakaolewa na waume, wana wa ndugu za baba yao.
Og Mahela, Tirza og Hogla og Milka og Noa, Zelafehads Døtre, bleve deres Farbroders Sønners Hustruer.
12 Waliolewa ndani ya koo za wazao wa Manase mwana wa Yosefu, na urithi wao ukabaki katika ukoo na kabila la baba yao.
Dem, som vare af Manasse Børns, Josefs Søns, Slægter, bleve de til Hustruer, og deres Arv blev hos deres Faders Slægtskabs Stamme.
13 Haya ndiyo maagizo na masharti ambayo Bwana aliwapa Waisraeli kupitia Mose katika tambarare za Moabu, karibu na Yordani ngʼambo ya Yeriko.
Disse ere de Bud og de Love, som Herren bød ved Mose for Israels Børn paa Moabiternes slette Marker, ved Jordanen over for Jeriko.

< Hesabu 36 >