< Hesabu 35 >

1 Bwana akamwambia Mose katika nchi tambarare ya Moabu, kando ya Mto Yordani kuvukia Yeriko,
And Jehovah spoke to Moses in the plains of Moab by the Jordan at Jericho, saying,
2 “Waagize Waisraeli kuwapa Walawi miji ya kuishi kutoka urithi ambao Waisraeli wataumiliki. Wape maeneo ya malisho kuzunguka hiyo miji.
Command the sons of Israel, that they give to the Levites from the inheritance of their possession cities to dwell in. And ye shall give suburbs for the cities round about them to the Levites.
3 Kisha watakuwa na miji ya kuishi na maeneo ya malisho kwa ajili ya ngʼombe zao, mbuzi, kondoo na mifugo yao mingine yote.
And they shall have the cities to dwell in, and their suburbs shall be for their cattle, and for their substance, and for all their beasts.
4 “Maeneo ya malisho kuzunguka miji hiyo ambayo mtawapa Walawi yataenea mita 450 kutoka kwenye ukuta wa miji.
And the suburbs of the cities, which ye shall give to the Levites, shall be from the wall of the city and outward a thousand cubits round about.
5 Nje ya mji, pima mita 900 upande wa mashariki, upande wa kusini mita 900, upande wa magharibi mita 900, na upande wa kaskazini mita 900, na mji utakuwa katikati. Eneo hili litakuwa lao kwa ajili ya malisho.
And ye shall measure outside the city for the east side two thousand cubits, and for the south side two thousand cubits, and for the west side two thousand cubits, and for the north side two thousand cubits, the city being in the midst. This shall be to them the suburbs of the cities.
6 “Miji sita mtakayowapa Walawi itakuwa ya makimbilio, ambayo mtu anayemuua mwenzake aweza kukimbilia humo. Zaidi ya hiyo, wapeni miji mingine arobaini na miwili.
And of the cities which ye shall give to the Levites, there shall be the six cities of refuge, which ye shall give for the manslayer to flee to. And besides them ye shall give forty-two cities.
7 Kwa jumla inawapasa kuwapa Walawi miji arobaini na minane, pamoja na maeneo ya malisho yao.
All the cities which ye shall give to the Levites shall be forty-eight cities, them with their suburbs.
8 Miji ambayo mtawapa Walawi kutoka nchi ambayo Waisraeli wanamiliki itatolewa kwa uwiano wa urithi wa kila kabila. Chukua miji mingi kutoka lile kabila lenye miji mingi, lakini uchukue miji michache kutoka kwa kabila lile lenye miji michache.”
And concerning the cities which ye shall give of the possession of the sons of Israel, from the many ye shall take many, and from the few ye shall take few. Everyone according to his inheritance which he inherits shall give of his cities to the Levites.
9 Kisha Bwana akamwambia Mose:
And Jehovah spoke to Moses, saying,
10 “Sema na Waisraeli, uwaambie: ‘Mtakapovuka Yordani kuingia Kanaani,
Speak to the sons of Israel, and say to them, When ye pass over the Jordan into the land of Canaan,
11 chagueni baadhi ya miji iwe miji yenu ya makimbilio, ambayo mtu ambaye ameua mwenzake bila kukusudia aweza kukimbilia humo.
then ye shall appoint cities to be cities of refuge for you, that the manslayer who kills any person unwittingly may flee there.
12 Itakuwa mahali pa kukimbilia kutoka mlipiza kisasi, ili kwamba mtu aliyeshtakiwa kwa mauaji asife kabla ya kujitetea mbele ya mkutano.
And the cities shall be to you for refuge from the avenger, that the manslayer not die until he stands before the congregation for judgment.
13 Miji hii sita mtakayoitoa itakuwa miji yenu ya makimbilio.
And the cities which ye shall give shall be for you six cities of refuge.
14 Mtatoa miji mitatu ngʼambo hii ya Yordani na miji mingine mitatu upande wa Kanaani kama miji ya makimbilio.
Ye shall give three cities beyond the Jordan, and three cities ye shall give in the land of Canaan. They shall be cities of refuge.
15 Miji hii sita itakuwa mahali pa makimbilio kwa ajili ya Waisraeli, wageni na watu wengine wanaoishi katikati yenu, ili kwamba mtu yeyote ambaye ameua mtu mwingine pasipo kukusudia aweze kukimbilia humo.
For the sons of Israel, and for the stranger and for the sojourner among them, these six cities shall be for refuge, that everyone who kills any person unwittingly may flee there.
16 “‘Kama mtu akimpiga mwenzake kwa chuma naye mtu huyo akafa, mtu huyo ni muuaji; muuaji sharti atauawa.
But if he smote him with an instrument of iron, so that he died, he is a murderer. The murderer shall surely be put to death.
17 Au kama mtu analo jiwe mkononi mwake ambalo laweza kuua, naye akampiga mwenzake akafa, yeye ni muuaji; muuaji huyo sharti atauawa.
And if he smote him with a stone in the hand, by which a man may die, and he died, he is a murderer. The murderer shall surely be put to death.
18 Au kama mtu ana chombo cha mti mkononi mwake ambacho chaweza kuua, naye akampiga mwenzake akafa, yeye ni muuaji; muuaji huyo sharti atauawa.
Or if he smote him with a weapon of wood in the hand, by which a man may die, and he died, he is a murderer. The murderer shall surely be put to death.
19 Mlipiza kisasi cha damu atamuua muuaji; wakati akikutana naye, atamuua.
The avenger of blood shall himself put the murderer to death. When he meets him, he shall put him to death.
20 Ikiwa mtu ana chuki ya siku nyingi na mwenzake akamsukuma au akamtupia kitu kwa kukusudia naye akafa,
And if he thrust him from hatred, or hurled at him, lying in wait, so that he died,
21 au ikiwa katika uadui akampiga ngumi naye akafa, mtu yule sharti atauawa; yeye ni muuaji. Mlipiza kisasi cha damu atamuua muuaji atakapokutana naye.
or in enmity smote him with his hand, so that he died, he who smote him shall surely be put to death. He is a murderer. The avenger of blood shall put the murderer to death, when he meets him.
22 “‘Lakini kama mtu akimsukuma mwenziwe ghafula pasipo chuki, au kumtupia kitu pasipo kukusudia,
But if he thrust him suddenly without enmity, or hurled upon him anything without lying in wait,
23 au, pasipo kumwona, akimwangushia jiwe ambalo laweza kumuua naye akafa, basi kwa kuwa hakuwa adui yake naye hakukusudia kumuumiza,
or with any stone, by which a man may die, not seeing him, and cast it upon him, so that he died, and he was not his enemy, nor sought his harm,
24 kusanyiko lazima liamue kati yake na mlipiza kisasi wa damu kufuatana na sheria hizi.
then the congregation shall judge between the smiter and the avenger of blood according to these ordinances.
25 Kusanyiko ni lazima limlinde yule anayeshtakiwa kuua kutoka kwa mlipiza kisasi wa damu, na kumrudisha katika mji wa makimbilio alikokuwa amekimbilia. Lazima akae humo mpaka atakapokufa kuhani mkuu ambaye alikuwa amepakwa mafuta matakatifu.
And the congregation shall deliver the manslayer out of the hand of the avenger of blood, and the congregation shall restore him to his city of refuge where he fled. And he shall dwell in it until the death of the high priest, who was anointed with the holy oil.
26 “‘Lakini kama mshtakiwa atatoka nje ya mipaka ya mji wa makimbilio ambao amekimbilia,
But if the manslayer shall at any time go beyond the border of his city of refuge where he flees,
27 na mlipiza kisasi wa damu akamkuta nje ya mji, mlipiza kisasi wa damu anaweza kumuua mshtakiwa huyo bila kuwa na hatia ya kuua.
and the avenger of blood find him outside the border of his city of refuge, and the avenger of blood kills the manslayer, he shall not be guilty of blood,
28 Mshtakiwa lazima akae katika mji wake wa makimbilio mpaka atakapokufa kuhani mkuu; atarudi tu kwenye mali yake baada ya kifo cha kuhani mkuu.
because he should have remained in his city of refuge until the death of the high priest. But after the death of the high priest the manslayer shall return into the land of his possession.
29 “‘Hizi ndizo kanuni za sheria zitakazohitajiwa kwenu na katika vizazi vyenu vijavyo, popote mtakapoishi.
And these things shall be for a statute and ordinance to you throughout your generations in all your dwellings.
30 “‘Yeyote anayeua mtu atauawa kama muuaji ikiwa tu kuna ushuhuda wa mashahidi. Lakini hakuna mtu atakayeuawa kwa ushuhuda wa shahidi mmoja tu.
Whoever kills any person, the murderer shall be slain at the mouth of witnesses, but one witness shall not testify against any person so that he dies.
31 “‘Usikubali fidia yoyote ya kuokoa uhai wa muuaji ambaye anastahili kufa. Mtu huyo hakika lazima auawe.
Moreover ye shall take no ransom for the life of a murderer who is guilty of death, but he shall surely be put to death.
32 “‘Usikubali fidia ya mtu yeyote ambaye amekimbilia katika mji wa makimbilio na kumruhusu kurudi kuishi katika nchi yake kabla ya kifo cha kuhani mkuu.
And ye shall take no ransom for him who has fled to his city of refuge, that he may come again to dwell in the land, until the death of the priest.
33 “‘Msiinajisi nchi mnayoishi. Umwagaji damu hunajisi nchi, na upatanisho hauwezekani kufanyika katika nchi ambayo damu imemwagwa, isipokuwa tu kwa damu ya yule aliyeimwaga damu.
So ye shall not pollute the land in which ye are, for blood, it pollutes the land. And no expiation can be made for the land for the blood that is shed in it, but by the blood of him who shed it.
34 Msiinajisi nchi mnayoishi, ambayo nami ninakaa, kwa kuwa Mimi, Bwana, ninakaa katikati ya Waisraeli.’”
And thou shall not defile the land which ye inhabit, in the midst of which I dwell, for I, Jehovah, dwell in the midst of the sons of Israel.

< Hesabu 35 >