< Hesabu 35 >

1 Bwana akamwambia Mose katika nchi tambarare ya Moabu, kando ya Mto Yordani kuvukia Yeriko,
Reče Jahve Mojsiju na Moapskim poljanama kod Jordana, nasuprot Jerihonu:
2 “Waagize Waisraeli kuwapa Walawi miji ya kuishi kutoka urithi ambao Waisraeli wataumiliki. Wape maeneo ya malisho kuzunguka hiyo miji.
“Naredi Izraelcima da ustupe levitima od baštine koju posjeduju gradove gdje će stanovati i pašnjake oko gradova. To dajte levitima.
3 Kisha watakuwa na miji ya kuishi na maeneo ya malisho kwa ajili ya ngʼombe zao, mbuzi, kondoo na mifugo yao mingine yote.
Neka gradovi budu njima za stanovanje, a okolni pašnjaci neka budu za njihova goveda, njihovo blago i sve njihove životinje.
4 “Maeneo ya malisho kuzunguka miji hiyo ambayo mtawapa Walawi yataenea mita 450 kutoka kwenye ukuta wa miji.
Pašnjaci uz gradove koje ustupite levitima neka zahvate od gradskih zidina van do tisuću lakata naokolo.
5 Nje ya mji, pima mita 900 upande wa mashariki, upande wa kusini mita 900, upande wa magharibi mita 900, na upande wa kaskazini mita 900, na mji utakuwa katikati. Eneo hili litakuwa lao kwa ajili ya malisho.
Izmjerite od grada van dvije tisuće lakata s istočne strane, dvije tisuće lakata s južne strane, dvije tisuće lakata sa zapadne strane i sa sjeverne strane dvije tisuće lakata, tako da grad bude u sredini. To neka im budu gradski pašnjaci.
6 “Miji sita mtakayowapa Walawi itakuwa ya makimbilio, ambayo mtu anayemuua mwenzake aweza kukimbilia humo. Zaidi ya hiyo, wapeni miji mingine arobaini na miwili.
Od gradova koje budete dali levitima šest će ih biti gradovi-utočišta, koje ćete ustupiti da ubojica može tamo pobjeći. Ovima dodajte još četrdeset i dva grada.
7 Kwa jumla inawapasa kuwapa Walawi miji arobaini na minane, pamoja na maeneo ya malisho yao.
Tako će svih gradova koje ustupite levitima biti četrdeset i osam gradova s njihovim pašnjacima.
8 Miji ambayo mtawapa Walawi kutoka nchi ambayo Waisraeli wanamiliki itatolewa kwa uwiano wa urithi wa kila kabila. Chukua miji mingi kutoka lile kabila lenye miji mingi, lakini uchukue miji michache kutoka kwa kabila lile lenye miji michache.”
A gradove koje budete izdvajali od vlasništva Izraelaca, od onih koji ih imaju mnogo uzmite više, a manje od onih koji imaju malo. Neka svatko ustupi gradove levitima prema omjeru baštine koju bude primio.”
9 Kisha Bwana akamwambia Mose:
Nadalje reče Jahve Mojsiju:
10 “Sema na Waisraeli, uwaambie: ‘Mtakapovuka Yordani kuingia Kanaani,
“Govori Izraelcima i reci im: 'Kad prijeđete preko Jordana u zemlju kanaansku,
11 chagueni baadhi ya miji iwe miji yenu ya makimbilio, ambayo mtu ambaye ameua mwenzake bila kukusudia aweza kukimbilia humo.
označite sebi gradove koji će vam služiti kao gradovi-utočišta, kamo može pobjeći ubojica koji nehotice koga ubije.
12 Itakuwa mahali pa kukimbilia kutoka mlipiza kisasi, ili kwamba mtu aliyeshtakiwa kwa mauaji asife kabla ya kujitetea mbele ya mkutano.
Ti gradovi neka vam budu utočište od osvetnika, tako da ubojica ne moradne poginuti dok ne stane na sud pred zajednicu.
13 Miji hii sita mtakayoitoa itakuwa miji yenu ya makimbilio.
Od gradova koje ustupite bit će vam šest gradova za utočište.
14 Mtatoa miji mitatu ngʼambo hii ya Yordani na miji mingine mitatu upande wa Kanaani kama miji ya makimbilio.
Dodijelite tri grada s onu stranu Jordana, a tri grada u zemlji kanaanskoj. Neka to budu gradovi-utočišta.
15 Miji hii sita itakuwa mahali pa makimbilio kwa ajili ya Waisraeli, wageni na watu wengine wanaoishi katikati yenu, ili kwamba mtu yeyote ambaye ameua mtu mwingine pasipo kukusudia aweze kukimbilia humo.
Tih šest gradova neka budu za utočište kako Izraelcima tako i strancu i došljaku koji među njima borave, kamo može pobjeći tko god ubije koga nehotice.
16 “‘Kama mtu akimpiga mwenzake kwa chuma naye mtu huyo akafa, mtu huyo ni muuaji; muuaji sharti atauawa.
Ali ako tko udari koga gvozdenim predmetom te ga usmrti, to je onda ubojica. Ubojica mora glavom platiti.
17 Au kama mtu analo jiwe mkononi mwake ambalo laweza kuua, naye akampiga mwenzake akafa, yeye ni muuaji; muuaji huyo sharti atauawa.
Udari li ga iz ruke kamenom od kojega čovjek može poginuti i zbilja pogine, to je opet ubojica. Ubojica mora glavom platiti.
18 Au kama mtu ana chombo cha mti mkononi mwake ambacho chaweza kuua, naye akampiga mwenzake akafa, yeye ni muuaji; muuaji huyo sharti atauawa.
Ili ako ga udari iz ruke kakvim drvenim predmetom od kojega može umrijeti i zbilja umre, i to je ubojica. Ubojica mora glavom platiti.
19 Mlipiza kisasi cha damu atamuua muuaji; wakati akikutana naye, atamuua.
Krvni osvetnik mora sam ubojicu usmrtiti. Kad ga sretne, neka ga ubije.
20 Ikiwa mtu ana chuki ya siku nyingi na mwenzake akamsukuma au akamtupia kitu kwa kukusudia naye akafa,
Nadalje, ako tko koga gurne iz mržnje ili na nj nešto baci namjerno te ga usmrti,
21 au ikiwa katika uadui akampiga ngumi naye akafa, mtu yule sharti atauawa; yeye ni muuaji. Mlipiza kisasi cha damu atamuua muuaji atakapokutana naye.
ili ga udari rukom iz zlobe te udareni umre, napadač mora zaglaviti - on je ubojica. Krvni osvetnik neka ubojicu ubije čim ga sretne.
22 “‘Lakini kama mtu akimsukuma mwenziwe ghafula pasipo chuki, au kumtupia kitu pasipo kukusudia,
No gurne li ga slučajno, ne iz neprijateljstva, ili nešto na nj baci, ali ne iz zasjede,
23 au, pasipo kumwona, akimwangushia jiwe ambalo laweza kumuua naye akafa, basi kwa kuwa hakuwa adui yake naye hakukusudia kumuumiza,
ili iz nepažnje na njega obori kakav kamen od kojega čovjek može poginuti te ga usmrti, a nije mu bio neprijatelj niti mu je zlo želio -
24 kusanyiko lazima liamue kati yake na mlipiza kisasi wa damu kufuatana na sheria hizi.
tada neka zajednica prosudi između ubojice i krvnog osvetnika prema ovim pravilima:
25 Kusanyiko ni lazima limlinde yule anayeshtakiwa kuua kutoka kwa mlipiza kisasi wa damu, na kumrudisha katika mji wa makimbilio alikokuwa amekimbilia. Lazima akae humo mpaka atakapokufa kuhani mkuu ambaye alikuwa amepakwa mafuta matakatifu.
Zajednica mora izbaviti ubojicu iz ruku krvnog osvetnika; onda neka ga zajednica vrati u grad-utočište kamo je pobjegao; tu neka on ostane do smrti velikoga svećenika koji je bio pomazan svetim uljem.
26 “‘Lakini kama mshtakiwa atatoka nje ya mipaka ya mji wa makimbilio ambao amekimbilia,
Ali ako ubojica ikad izađe izvan granice utočišta kamo je pobjegao,
27 na mlipiza kisasi wa damu akamkuta nje ya mji, mlipiza kisasi wa damu anaweza kumuua mshtakiwa huyo bila kuwa na hatia ya kuua.
pa na nj nabasa krvni osvetnik izvan granica njegova grada-utočišta te krvni osvetnik ubije ubojicu, to mu se ne računa u krvoproliće,
28 Mshtakiwa lazima akae katika mji wake wa makimbilio mpaka atakapokufa kuhani mkuu; atarudi tu kwenye mali yake baada ya kifo cha kuhani mkuu.
jer ubojica mora ostati u gradu-utočištu do smrti velikoga svećenika. A poslije smrti velikoga svećenika može se vratiti na svoj posjed.
29 “‘Hizi ndizo kanuni za sheria zitakazohitajiwa kwenu na katika vizazi vyenu vijavyo, popote mtakapoishi.
Neka vam takvi budu sudbeni postupci od naraštaja do naraštaja svuda gdje budete boravili.
30 “‘Yeyote anayeua mtu atauawa kama muuaji ikiwa tu kuna ushuhuda wa mashahidi. Lakini hakuna mtu atakayeuawa kwa ushuhuda wa shahidi mmoja tu.
Za svako ubojstvo čovjeka kazna smrti nad ubojicom može se izvršiti na dokaz svjedoka. Nitko se ne može smrću kazniti na dokaz samo jednog svjedoka.
31 “‘Usikubali fidia yoyote ya kuokoa uhai wa muuaji ambaye anastahili kufa. Mtu huyo hakika lazima auawe.
Ne smijete primati otkupnine za život ubojice koji je zaslužio smrt: on mora umrijeti.
32 “‘Usikubali fidia ya mtu yeyote ambaye amekimbilia katika mji wa makimbilio na kumruhusu kurudi kuishi katika nchi yake kabla ya kifo cha kuhani mkuu.
Niti smijete primati otkupnine od bilo koga koji, pošto je pobjegao u svoj grad-utočište, hoće da se vrati i da živi na svome tlu prije smrti velikoga svećenika.
33 “‘Msiinajisi nchi mnayoishi. Umwagaji damu hunajisi nchi, na upatanisho hauwezekani kufanyika katika nchi ambayo damu imemwagwa, isipokuwa tu kwa damu ya yule aliyeimwaga damu.
Nemojte oskvrnjivati zemlje u kojoj živite. A krvoprolićem zemlja se oskvrnjuje. Za zemlju na kojoj je krv prolivena pomirenje se ne može pribaviti, osim krvlju onoga koji ju je prolio.
34 Msiinajisi nchi mnayoishi, ambayo nami ninakaa, kwa kuwa Mimi, Bwana, ninakaa katikati ya Waisraeli.’”
Ne smije se obeščašćivati zemlja u kojoj živite i usred koje ja boravim, jer ja, Jahve, prebivam među sinovima Izraelovim.'”

< Hesabu 35 >