< Hesabu 34 >

1 Bwana akamwambia Mose,
RAB Musa'ya şöyle dedi:
2 “Waamuru Waisraeli na uwaambie: ‘Mtakapoingia nchi ya Kanaani, nchi ambayo itagawanywa kwenu kama urithi itakuwa na mipaka ifuatayo:
“İsrailliler'e de ki, ‘Mülk olarak size düşecek Kenan ülkesine girince, sınırlarınız şöyle olacak:
3 “‘Upande wenu wa kusini utajumuisha sehemu ya Jangwa la Sini kufuata mpaka wa Edomu. Upande wa mashariki mpaka wenu wa kusini utaanzia mwisho wa Bahari ya Chumvi,
“‘Güney sınırınız Zin Çölü'nden Edom sınırı boyunca uzanacak. Doğuda, güney sınırınız Lut Gölü'nün ucundan başlayacak,
4 katiza kusini mwa Pito la Akrabimu, endelea mpaka Sini na kwenda kusini ya Kadesh-Barnea. Kisha mpaka huo utaenda hadi Hasar-Adari hadi Azmoni,
Akrep Geçidi'nin güneyinden Zin'e geçip Kadeş-Barnea'nın güneyine dek uzanacak. Oradan Hasar-Addar'a ve Asmon'a,
5 mahali ambapo utapinda, na kuunganika na Kijito cha Misri na kumalizikia kwenye Bahari ya Kati.
oradan da Mısır Vadisi'ne uzanarak Akdeniz'de son bulacak.
6 “‘Mpaka wenu wa magharibi utakuwa Bahari ya Kati. Huu utakuwa mpaka wenu upande wa magharibi.
“‘Batı sınırınız Akdeniz ve kıyısı olacak. Batıda sınırınız bu olacak.
7 “‘Kwa mpaka wenu wa kaskazini, wekeni alama kuanzia Bahari ya Kati hadi mlima Hori,
“‘Kuzey sınırınız Akdeniz'den Hor Dağı'na dek uzanacak.
8 na kutoka mlima Hori hadi Pito la Hamathi. Kisha mpaka utaenda hadi Sedadi,
Hor Dağı'ndan Levo-Hamat'a, oradan Sedat'a,
9 kuendelea hadi Zifroni, na kuishia Hasar-Enani. Huu utakuwa mpaka wenu upande wa kaskazini.
Zifron'a doğru uzanarak Hasar-Enan'da son bulacak. Kuzeyde sınırınız bu olacak.
10 “‘Kwa mpaka wenu wa mashariki, wekeni alama kuanzia Hasar-Enani hadi Shefamu.
“‘Doğu sınırınız Hasar-Enan'dan Şefam'a dek uzanacak.
11 Mpaka utaelekea kusini kuanzia Shefamu hadi Ribla upande wa mashariki wa Aini, na kuendelea kwenye miteremko mashariki mwa Bahari ya Kinerethi.
Sınırınız Şefam'dan Ayin'in doğusundaki Rivla'ya dek inecek. Oradan Kinneret Gölü'nün doğu kıyısındaki yamaçlara dek uzanacak.
12 Kisha mpaka utashuka kuelekea Mto Yordani na kuishia katika Bahari ya Chumvi. “‘Hii itakuwa nchi yenu, ikiwa na mipaka yake kila upande.’”
Oradan Şeria Irmağı boyunca uzanacak ve Lut Gölü'nde son bulacak. “‘Her yandan ülkenizin sınırları bu olacaktır.’”
13 Mose akawaamuru Waisraeli: “Gawanyeni nchi hii kwa kura kama urithi. Bwana ameagiza kwamba itolewe kwa yale makabila tisa na nusu,
Musa İsrailliler'e, “Miras olarak kurayla paylaştıracağınız ülke budur” dedi, “RAB'bin buyruğu uyarınca ülke dokuz oymakla bir yarım oymak arasında paylaştırılacak.
14 kwa sababu jamaa ya kabila la Reubeni, kabila la Gadi, na nusu ya kabila la Manase wamekwishapokea urithi wao.
Çünkü Ruben oymağına bağlı ailelerle Gad oymağına bağlı aileler ve Manaşşe oymağının öbür yarısı mülklerini aldılar.
15 Haya makabila mawili na nusu wamekwishapokea urithi wao upande wa mashariki wa Yordani ngʼambo ya Yeriko, kuelekea mawio ya jua.”
Bu iki oymakla yarım oymak mülklerini Eriha'nın karşısındaki Şeria Irmağı'nın doğusunda aldılar.”
16 Bwana akamwambia Mose,
RAB Musa'ya şöyle dedi:
17 “Haya ndiyo majina ya watu ambao watakusaidia kugawanya nchi kama urithi: Eleazari kuhani na Yoshua mwana wa Nuni.
“Ülkeyi mülk olarak aranızda paylaştıracak adamlar şunlardır: Kâhin Elazar ve Nun oğlu Yeşu.
18 Tena uteue kiongozi mmoja kutoka kila kabila kusaidia kuigawanya nchi.
Ülkeyi mülk olarak paylaştırmaları için her oymaktan birer önder görevlendirin.
19 Haya ndiyo majina yao: “Kalebu mwana wa Yefune, kutoka kabila la Yuda;
Şu adamları görevlendireceksiniz: “Yahuda oymağından Yefunne oğlu Kalev,
20 Shemueli mwana wa Amihudi, kutoka kabila la Simeoni;
Şimon oymağından Ammihut oğlu Şemuel,
21 Elidadi mwana wa Kisloni, kutoka kabila la Benyamini;
Benyamin oymağından Kislon oğlu Elidat,
22 Buki mwana wa Yogli, kiongozi kutoka kabila la Dani;
Dan oymağından Yogli oğlu önder Bukki,
23 Hanieli mwana wa Efodi, kiongozi kutoka kabila la Manase mwana wa Yosefu;
Yusufoğulları'ndan: Manaşşe oymağından Efot oğlu önder Hanniel,
24 Kemueli mwana wa Shiftani, kiongozi kutoka kabila la Efraimu mwana wa Yosefu;
Efrayim oymağından Şiftan oğlu önder Kemuel,
25 Elisafani mwana wa Parnaki, kiongozi kutoka kabila la Zabuloni;
Zevulun oymağından Parnak oğlu önder Elisafan,
26 Paltieli mwana wa Azani, kiongozi kutoka kabila la Isakari;
İssakar oymağından Azzan oğlu önder Paltiel,
27 Ahihudi mwana wa Shelomi, kiongozi kutoka kabila la Asheri;
Aşer oymağından Şelomi oğlu önder Ahihut,
28 Pedaheli mwana wa Amihudi, kiongozi kutoka kabila la Naftali.”
Naftali oymağından Ammihut oğlu önder Pedahel.”
29 Hawa ndio watu ambao Bwana aliamuru wagawanye urithi kwa Waisraeli katika nchi ya Kanaani.
Kenan ülkesinde İsrailliler'e mülkü paylaştırmaları için RAB'bin görevlendirdiği adamlar bunlardı.

< Hesabu 34 >