< Hesabu 34 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Jahve reče Mojsiju:
2 “Waamuru Waisraeli na uwaambie: ‘Mtakapoingia nchi ya Kanaani, nchi ambayo itagawanywa kwenu kama urithi itakuwa na mipaka ifuatayo:
“Izdaj Izraelcima naredbu i reci im: 'Kad uđete u kanaansku zemlju, ta će vam zemlja pripasti u baštinu, zemlja kanaanska sa svojim granicama.
3 “‘Upande wenu wa kusini utajumuisha sehemu ya Jangwa la Sini kufuata mpaka wa Edomu. Upande wa mashariki mpaka wenu wa kusini utaanzia mwisho wa Bahari ya Chumvi,
Južna strana protezat će vam se od pustinje Sina uz Edom. Južna će vam granica početi s kraja Slanog mora na istočnoj strani.
4 katiza kusini mwa Pito la Akrabimu, endelea mpaka Sini na kwenda kusini ya Kadesh-Barnea. Kisha mpaka huo utaenda hadi Hasar-Adari hadi Azmoni,
Onda će vam granica skrenuti na jug, prema Akrabimskoj strmini, i nastaviti se preko Sina. Doprijet će na jugu do Kadeš Barnee; zatim će izaći prema Hasar Adaru i nastaviti se do Asmone.
5 mahali ambapo utapinda, na kuunganika na Kijito cha Misri na kumalizikia kwenye Bahari ya Kati.
Od Asmone granica će skrenuti prema Egipatskom potoku i izaći će na more.
6 “‘Mpaka wenu wa magharibi utakuwa Bahari ya Kati. Huu utakuwa mpaka wenu upande wa magharibi.
Zapadna granica bit će vam Veliko more; neka vam je to granica prema zapadu.
7 “‘Kwa mpaka wenu wa kaskazini, wekeni alama kuanzia Bahari ya Kati hadi mlima Hori,
A ovo će vam biti sjeverna granica: od Velikog mora povucite crtu na brdo Hor;
8 na kutoka mlima Hori hadi Pito la Hamathi. Kisha mpaka utaenda hadi Sedadi,
s brda Hora onda potegnite crtu do ulaza u Hamat; završetak granice bit će Sedada.
9 kuendelea hadi Zifroni, na kuishia Hasar-Enani. Huu utakuwa mpaka wenu upande wa kaskazini.
Onda će se granica protegnuti do Zifrona i završiti u Hasar Enanu. To će vam biti sjeverna granica.
10 “‘Kwa mpaka wenu wa mashariki, wekeni alama kuanzia Hasar-Enani hadi Shefamu.
Za svoju istočnu granicu povucite crtu od Hasar Enana do Šefama.
11 Mpaka utaelekea kusini kuanzia Shefamu hadi Ribla upande wa mashariki wa Aini, na kuendelea kwenye miteremko mashariki mwa Bahari ya Kinerethi.
Granica će se spuštati od Šefama do Rible, istočno od Ajina. Odande će se granica spustiti i doprijeti do istočne obale Kineretskog jezera.
12 Kisha mpaka utashuka kuelekea Mto Yordani na kuishia katika Bahari ya Chumvi. “‘Hii itakuwa nchi yenu, ikiwa na mipaka yake kila upande.’”
Iza toga spustit će se granica niz Jordan da završi u Slanome moru. To će biti vaša zemlja sa svojim granicama naokolo.'”
13 Mose akawaamuru Waisraeli: “Gawanyeni nchi hii kwa kura kama urithi. Bwana ameagiza kwamba itolewe kwa yale makabila tisa na nusu,
Tada Mojsije naredi Izraelcima: “To je zemlja koju ćete kockom dobiti u baštinu, a za koju je zapovjedio Jahve da je dobije devet plemena i polovica jednog plemena.
14 kwa sababu jamaa ya kabila la Reubeni, kabila la Gadi, na nusu ya kabila la Manase wamekwishapokea urithi wao.
Jer pleme Rubenovaca prema svojim porodicama, zatim pleme Gadovaca prema svojim porodicama već primiše svoju baštinu, kao što je svoju baštinu primila i polovica plemena Manašeova.
15 Haya makabila mawili na nusu wamekwishapokea urithi wao upande wa mashariki wa Yordani ngʼambo ya Yeriko, kuelekea mawio ya jua.”
Ta dva plemena i pol primila su svoje baštine s one strane Jordana, nasuprot Jerihonu, s istočne strane.”
16 Bwana akamwambia Mose,
Jahve reče Mojsiju:
17 “Haya ndiyo majina ya watu ambao watakusaidia kugawanya nchi kama urithi: Eleazari kuhani na Yoshua mwana wa Nuni.
“Ovo su imena ljudi koji će vam zemlju podijeliti: svećenik Eleazar i Nunov sin Jošua;
18 Tena uteue kiongozi mmoja kutoka kila kabila kusaidia kuigawanya nchi.
i od svakoga plemena uzmi po jednoga glavara za razdiobu zemlje.
19 Haya ndiyo majina yao: “Kalebu mwana wa Yefune, kutoka kabila la Yuda;
Ovo su imena tih ljudi: Kaleb, sin Jefuneov; od plemena Judina;
20 Shemueli mwana wa Amihudi, kutoka kabila la Simeoni;
Šemuel, sin Amihudov, od plemena Šimunova;
21 Elidadi mwana wa Kisloni, kutoka kabila la Benyamini;
Elidad, sin Kislonov, od plemena Benjaminova;
22 Buki mwana wa Yogli, kiongozi kutoka kabila la Dani;
knez Buki, sin Joglijev, od plemena Danovaca.
23 Hanieli mwana wa Efodi, kiongozi kutoka kabila la Manase mwana wa Yosefu;
Od sinova Josipovih: knez Haniel, sin Efodov, od plemena Manašeovaca;
24 Kemueli mwana wa Shiftani, kiongozi kutoka kabila la Efraimu mwana wa Yosefu;
knez Kemuel, sin Šiftanov, od plemena Efrajimovaca;
25 Elisafani mwana wa Parnaki, kiongozi kutoka kabila la Zabuloni;
knez Elisafan, sin Parnakov, od plemena Zebulunovaca;
26 Paltieli mwana wa Azani, kiongozi kutoka kabila la Isakari;
knez Paltiel, sin Azanov, od plemena Jisakarovaca;
27 Ahihudi mwana wa Shelomi, kiongozi kutoka kabila la Asheri;
knez Ahihud, sin Šelomijev, od plemena Ašerovaca;
28 Pedaheli mwana wa Amihudi, kiongozi kutoka kabila la Naftali.”
knez Pedahel, sin Amihudov, od plemena Naftalijevaca.”
29 Hawa ndio watu ambao Bwana aliamuru wagawanye urithi kwa Waisraeli katika nchi ya Kanaani.
To su oni kojima je Jahve naložio da Izraelcima izdijele baštinu u zemlji kanaanskoj.

< Hesabu 34 >