< Hesabu 33 >

1 Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
ESTAS son las estancias de los hijos de Israel, los cuales salieron de la tierra de Egipto por sus escuadrones, bajo la conducta de Moisés y Aarón.
2 Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
Y Moisés escribió sus salidas conforme á sus jornadas por mandato de Jehová. Estas, pues, son sus estancias con arreglo á sus partidas.
3 Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
De Rameses partieron en el mes primero, á los quince días del mes primero: el segundo día de la pascua salieron los hijos de Israel con mano alta, á ojos de todos los Egipcios.
4 waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
[Estaban] enterrando los Egipcios los que Jehová había muerto de ellos, á todo primogénito; habiendo Jehová hecho también juicios en sus dioses.
5 Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
Partieron, pues, los hijos de Israel de Rameses, y asentaron campo en Succoth.
6 Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
Y partiendo de Succoth, asentaron en Etham, que está al cabo del desierto.
7 Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
Y partiendo de Etham, volvieron sobre Pi-hahiroth, que está delante de Baalsephon, y asentaron delante de Migdol.
8 Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
Y partiendo de Pi-hahiroth, pasaron por medio de la mar al desierto, y anduvieron camino de tres días por el desierto de Etham, y asentaron en Mara.
9 Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
Y partiendo de Mara, vinieron á Elim, donde había doce fuentes de aguas, y setenta palmeras; y asentaron allí.
10 Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
Y partidos de Elim, asentaron junto al mar Bermejo.
11 Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
Y partidos del mar Bermejo, asentaron en el desierto de Sin.
12 Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
Y partidos del desierto de Sin, asentaron en Dophca.
13 Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
Y partidos de Dophca, asentaron en Alús.
14 Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
Y partidos de Alús, asentaron en Rephidim, donde el pueblo no tuvo aguas para beber.
15 Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
Y partidos de Rephidim, asentaron en el desierto de Sinaí.
16 Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
Y partidos del desierto de Sinaí, asentaron en Kibroth-hataava.
17 Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
Y partidos de Kibroth-hataava, asentaron en Haseroth.
18 Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
Y partidos de Haseroth, asentaron en Ritma.
19 Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
Y partidos de Ritma, asentaron en Rimmón-peres.
20 Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
Y partidos de Rimmón-peres, asentaron en Libna.
21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
Y partidos de Libna, asentaron en Rissa.
22 Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
Y partidos de Rissa, asentaron en Ceelatha.
23 Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
Y partidos de Ceelatha, asentaron en el monte de Sepher.
24 Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
Y partidos del monte de Sepher, asentaron en Harada.
25 Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
Y partidos de Harada, asentaron en Maceloth.
26 Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
Y partidos de Maceloth, asentaron en Tahath.
27 Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
Y partidos de Tahath, asentaron en Tara.
28 Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
Y partidos de Tara, asentaron en Mithca.
29 Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
Y partidos de Mithca, asentaron en Hasmona.
30 Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
Y partidos de Hasmona, asentaron en Moseroth.
31 Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
Y partidos de Moseroth, asentaron en Bene-jaacán.
32 Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
Y partidos de Bene-jaacán, asentaron en el monte de Gidgad.
33 Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
Y partidos del monte de Gidgad, asentaron en Jotbatha.
34 Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
Y partidos de Jotbatha, asentaron en Abrona.
35 Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
Y partidos de Abrona, asentaron en Esion-geber.
36 Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
Y partidos de Esion-geber, asentaron en el desierto de Zin, que es Cades.
37 Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
Y partidos de Cades, asentaron en el monte de Hor, en la extremidad del país de Edom.
38 Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
Y subió Aarón el sacerdote al monte de Hor, conforme al dicho de Jehová, y allí murió á los cuarenta años de la salida de los hijos de Israel de la tierra de Egipto, en el mes quinto, en el primero del mes.
39 Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
Y era Aarón de edad de ciento y veinte y tres años, cuando murió en el monte de Hor.
40 Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
Y el Cananeo, rey de Arad, que habitaba al mediodía en la tierra de Canaán, oyó como habían venido los hijos de Israel.
41 Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
Y partidos del monte de Hor, asentaron en Salmona.
42 Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
Y partidos de Salmona, asentaron en Phunón.
43 Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
Y partidos de Phunón, asentaron en Oboth.
44 Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
Y partidos de Oboth, asentaron en Ije-abarim; en el término de Moab.
45 Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
Y partidos de Ije-abarim, asentaron en Dibon-gad.
46 Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
Y partidos de Dibon-gad, asentaron en Almon-diblathaim.
47 Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
Y partidos de Almon-diblathaim, asentaron en los montes de Abarim, delante de Nebo.
48 Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
Y partidos de los montes de Abarim, asentaron en los campos de Moab, junto al Jordán de Jericó.
49 Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
Finalmente asentaron junto al Jordán, desde Beth-jesimoth hasta Abel-sitim, en los campos de Moab.
50 Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
Y habló Jehová á Moisés en los campos de Moab junto al Jordán de Jericó, diciendo:
51 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
Habla á los hijos de Israel, y diles: Cuando hubiereis pasado el Jordán á la tierra de Canaán,
52 wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
Echaréis á todos los moradores del país de delante de vosotros, y destruiréis todas sus pinturas, y todas sus imágenes de fundición, y arruinaréis todos sus altos;
53 Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
Y echaréis [los moradores de] la tierra, y habitaréis en ella; porque yo os la he dado para que la poseáis.
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
Y heredaréis la tierra por suertes por vuestras familias: á los muchos daréis mucho por su heredad, y á los pocos daréis menos por heredad suya: donde le saliere la suerte, allí la tendrá cada uno: por las tribus de vuestros padres heredaréis.
55 “‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
Y si no echareis los moradores del país de delante de vosotros, sucederá que los que dejareis de ellos serán por aguijones en vuestros ojos, y por espinas en vuestros costados, y afligiros han sobre la tierra en que vosotros habitareis.
56 Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”
Será además, que haré á vosotros como yo pensé hacerles á ellos.

< Hesabu 33 >