< Hesabu 33 >

1 Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
این است سفرنامهٔ قوم اسرائیل از روزی که به رهبری موسی و هارون از مصر بیرون آمدند.
2 Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
موسی طبق دستور خداوند مراحل سفر آنها را نوشته بود.
3 Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
آنها در روز پانزدهم از ماه اول، یعنی یک روز بعد از پِسَح از شهر رَمِسیس مصر خارج شدند. در حالی که مصری‌ها همۀ نخست‌زادگان خود را که خداوند شب قبل آنها را کشته بود دفن می‌کردند، قوم اسرائیل با سربلندی از مصر بیرون آمدند. این امر نشان داد که خداوند از تمامی خدایان مصر قویتر است.
4 waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
5 Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
پس از حرکت از رَمِسیس، قوم اسرائیل در سوکوت اردو زدند و از آنجا به ایتام که در حاشیهٔ بیابان است رفتند.
6 Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
7 Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
بعد به فی‌هاحیروت نزدیک بعل صفون رفته، در دامنهٔ کوه مجدل اردو زدند.
8 Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
سپس از آنجا کوچ کرده، از میان دریای سرخ گذشتند و به بیابان ایتام رسیدند. سه روز هم در بیابان ایتام پیش رفتند تا به ماره رسیدند و در آنجا اردو زدند.
9 Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
از ماره کوچ کرده، به ایلیم آمدند که در آنجا دوازده چشمهٔ آب و هفتاد درخت خرما بود، و مدتی در آنجا ماندند.
10 Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
از ایلیم به کنار دریای سرخ کوچ نموده، اردو زدند؛
11 Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
پس از آن به صحرای سین رفتند.
12 Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
سپس به ترتیب به دُفقه،
13 Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
الوش،
14 Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
و رفیدیم که در آنجا آب نوشیدنی یافت نمی‌شد، رفتند.
15 Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
از رفیدیم به صحرای سینا و از آنجا به قبروت هتاوه و سپس از قبروت هتاوه به حصیروت کوچ کردند و بعد به ترتیب به نقاط زیر رفتند: از حصیروت به رتمه، از رتمه به رمون فارص، از رمون فارص به لبنه، از لبنه به رسه، از رسه به قهیلاته، از قهیلاته به کوه شافر، از کوه شافر به حراده، از حراده به مقهیلوت، از مقهیلوت به تاحت، از تاحت به تارح، از تارح به متقه، از متقه به حشمونه، از حشمونه به مسیروت، از مسیروت به بنی‌یعقان، از بنی‌یعقان به حورالجدجاد، از حورالجدجاد به یطبات، از یطبات به عبرونه، از عبرونه به عصیون جابر، از عصیون جابر به قادش (در بیابان صین)، از قادش به کوه هور (در مرز سرزمین ادوم).
16 Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
17 Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
18 Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
19 Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
20 Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
22 Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
23 Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
24 Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
25 Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
26 Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
27 Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
28 Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
29 Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
30 Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
31 Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
32 Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
33 Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
34 Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
35 Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
36 Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
37 Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
38 Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
وقتی در دامنهٔ کوه هور بودند، هارون کاهن به دستور خداوند به بالای کوه هور رفت. وی در سن ۱۲۳ سالگی، در روز اول از ماه پنجم سال چهلم؛ بعد از بیرون آمدن بنی‌اسرائیل از مصر، در آنجا وفات یافت.
39 Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
40 Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
در این هنگام بود که پادشاه کنعانی سرزمین عراد (واقع در نِگِب کنعان)، اطلاع یافت که قوم اسرائیل به کشورش نزدیک می‌شوند.
41 Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
پس اسرائیلی‌ها از کوه هور به صلمونه کوچ کردند و در آنجا اردو زدند.
42 Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
بعد به فونون رفتند.
43 Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
پس از آن به اوبوت کوچ کردند
44 Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
و از آنجا به عیی‌عباریم در مرز موآب رفته، در آنجا اردو زدند.
45 Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
سپس به دیبون جاد رفتند
46 Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
و از دیبون جاد به علمون دبلاتایم
47 Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
و از آنجا به کوهستان عباریم، نزدیک کوه نبو کوچ کردند.
48 Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
سرانجام به دشت موآب رفتند که در کنار رود اردن در مقابل شهر اریحا بود.
49 Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
در دشت موآب، از بیت‌یشیموت تا آبل شطیم در جاهای مختلف، کنار رود اردن اردو زدند.
50 Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
زمانی که آنها در کنار رود اردن، در مقابل اریحا اردو زده بودند، خداوند به موسی فرمود که به قوم اسرائیل بگوید: «وقتی که از رود اردن عبور کردید و به سرزمین کنعان رسیدید،
51 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
52 wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
باید تمامی ساکنان آنجا را بیرون کنید و همهٔ بتها و مجسمه‌هایشان را از بین ببرید و عبادتگاهای واقع در بالای کوهها را که در آنجا بتهایشان را پرستش می‌کنند خراب کنید.
53 Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
من سرزمین کنعان را به شما داده‌ام. آن را تصرف کنید و در آن ساکن شوید.
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
زمین به تناسب جمعیت قبیله‌هایتان به شما داده خواهد شد. قطعه‌های بزرگتر زمین به قید قرعه بین قبیله‌های بزرگتر و قطعه‌های کوچکتر بین قبیله‌های کوچکتر تقسیم شود.
55 “‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
ولی اگر تمامی ساکنان آنجا را بیرون نکنید، باقیماندگان مثل خار به چشمهایتان و چون تیغ در پهلویتان فرو خواهند رفت و شما را در آن سرزمین آزار خواهند رساند.
56 Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”
آری، اگر آنان را بیرون نکنید آنگاه من شما را هلاک خواهم کرد همان‌طور که قصد داشتم شما آنها را هلاک کنید.»

< Hesabu 33 >