< Hesabu 33 >

1 Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
אלה מסעי בני ישראל אשר יצאו מארץ מצרים--לצבאתם ביד משה ואהרן
2 Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
ויכתב משה את מוצאיהם למסעיהם--על פי יהוה ואלה מסעיהם למוצאיהם
3 Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
ויסעו מרעמסס בחדש הראשון בחמשה עשר יום לחדש הראשון ממחרת הפסח יצאו בני ישראל ביד רמה--לעיני כל מצרים
4 waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
ומצרים מקברים את אשר הכה יהוה בהם--כל בכור ובאלהיהם עשה יהוה שפטים
5 Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
ויסעו בני ישראל מרעמסס ויחנו בסכת
6 Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
ויסעו מסכת ויחנו באתם אשר בקצה המדבר
7 Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
ויסעו מאתם וישב על פי החירת אשר על פני בעל צפון ויחנו לפני מגדל
8 Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
ויסעו מפני החירת ויעברו בתוך הים המדברה וילכו דרך שלשת ימים במדבר אתם ויחנו במרה
9 Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
ויסעו ממרה ויבאו אילמה ובאילם שתים עשרה עינת מים ושבעים תמרים--ויחנו שם
10 Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
ויסעו מאילם ויחנו על ים סוף
11 Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
ויסעו מים סוף ויחנו במדבר סין
12 Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
ויסעו ממדבר סין ויחנו בדפקה
13 Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
ויסעו מדפקה ויחנו באלוש
14 Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
ויסעו מאלוש ויחנו ברפידם ולא היה שם מים לעם לשתות
15 Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
ויסעו מרפידם ויחנו במדבר סיני
16 Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
ויסעו ממדבר סיני ויחנו בקברת התאוה
17 Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
ויסעו מקברת התאוה ויחנו בחצרת
18 Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
ויסעו מחצרת ויחנו ברתמה
19 Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
ויסעו מרתמה ויחנו ברמן פרץ
20 Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
ויסעו מרמן פרץ ויחנו בלבנה
21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
ויסעו מלבנה ויחנו ברסה
22 Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
ויסעו מרסה ויחנו בקהלתה
23 Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
ויסעו מקהלתה ויחנו בהר שפר
24 Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
ויסעו מהר שפר ויחנו בחרדה
25 Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
ויסעו מחרדה ויחנו במקהלת
26 Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
ויסעו ממקהלת ויחנו בתחת
27 Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
ויסעו מתחת ויחנו בתרח
28 Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
ויסעו מתרח ויחנו במתקה
29 Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
ויסעו ממתקה ויחנו בחשמנה
30 Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
ויסעו מחשמנה ויחנו במסרות
31 Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
ויסעו ממסרות ויחנו בבני יעקן
32 Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
ויסעו מבני יעקן ויחנו בחר הגדגד
33 Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
ויסעו מחר הגדגד ויחנו ביטבתה
34 Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
ויסעו מיטבתה ויחנו בעברנה
35 Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
ויסעו מעברנה ויחנו בעצין גבר
36 Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
ויסעו מעצין גבר ויחנו במדבר צן הוא קדש
37 Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
ויסעו מקדש ויחנו בהר ההר בקצה ארץ אדום
38 Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
ויעל אהרן הכהן אל הר ההר על פי יהוה--וימת שם בשנת הארבעים לצאת בני ישראל מארץ מצרים בחדש החמישי באחד לחדש
39 Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
ואהרן בן שלש ועשרים ומאת שנה במתו בהר ההר
40 Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
וישמע הכנעני מלך ערד והוא ישב בנגב בארץ כנען--בבא בני ישראל
41 Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
ויסעו מהר ההר ויחנו בצלמנה
42 Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
ויסעו מצלמנה ויחנו בפונן
43 Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
ויסעו מפונן ויחנו באבת
44 Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
ויסעו מאבת ויחנו בעיי העברים בגבול מואב
45 Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
ויסעו מעיים ויחנו בדיבן גד
46 Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
ויסעו מדיבן גד ויחנו בעלמן דבלתימה
47 Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
ויסעו מעלמן דבלתימה ויחנו בהרי העברים לפני נבו
48 Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
ויסעו מהרי העברים ויחנו בערבת מואב על ירדן ירחו
49 Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
ויחנו על הירדן מבית הישמת עד אבל השטים בערבת מואב
50 Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
וידבר יהוה אל משה בערבת מואב על ירדן ירחו לאמר
51 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
דבר אל בני ישראל ואמרת אלהם כי אתם עברים את הירדן אל ארץ כנען
52 wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
והורשתם את כל ישבי הארץ מפניכם ואבדתם את כל משכיתם ואת כל צלמי מסכתם תאבדו ואת כל במותם תשמידו
53 Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
והורשתם את הארץ וישבתם בה כי לכם נתתי את הארץ לרשת אתה
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
והתנחלתם את הארץ בגורל למשפחתיכם לרב תרבו את נחלתו ולמעט תמעיט את נחלתו--אל אשר יצא לו שמה הגורל לו יהיה למטות אבתיכם תתנחלו
55 “‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
ואם לא תורישו את ישבי הארץ מפניכם--והיה אשר תותירו מהם לשכים בעיניכם ולצנינם בצדיכם וצררו אתכם--על הארץ אשר אתם ישבים בה
56 Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”
והיה כאשר דמיתי לעשות להם--אעשה לכם

< Hesabu 33 >