< Hesabu 33 >

1 Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
Dies sind die Lagerorte der Söhne Israels, da sie aus Ägyptenland ausgingen, nach ihren Heerscharen unter der Hand des Mose und Aharon.
2 Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
Und Mose schrieb auf ihre Auszüge nach ihren Lagerorten auf Befehl Jehovahs; und dies sind ihre Lagerorte nach ihren Auszügen:
3 Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
Und sie brachen auf von Ramses im ersten Monat am fünfzehnten Tage des ersten Monats. Am morgenden Tag nach dem Passah zogen die Söhne Israels aus mit erhöhter Hand vor den Augen aller Ägypter.
4 waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
Und die Ägypter begruben all die Erstgeburt, die Jehovah unter ihnen geschlagen hatte; und an ihren Göttern hatte Jehovah Gerichte geübt.
5 Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
Und die Söhne Israels brachen von Ramses auf und lagerten in Sukkoth.
6 Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
Und von Sukkoth brachen sie auf und lagerten in Etham, das am Ende der Wüste ist.
7 Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
Und von Etham brachen sie auf und wandten sich zurück nach Pi Hachiroth, das vor Baal Zephon ist und lagerten vor Migdol.
8 Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
Und vor Hachiroth brachen sie auf und zogen mitten durch das Meer nach der Wüste hin und gingen einen Weg von drei Tagen in der Wüste Etham und lagerten in Marah.
9 Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
Und von Marah brachen sie auf und kamen nach Elim; und in Elim waren zwölf Wasserquellen und siebzig Palmbäume, und sie lagerten daselbst.
10 Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
Und sie brachen auf von Elim und lagerten am Schilfmeer.
11 Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
Und vom Schilfmeer brachen sie auf und lagerten in der Wüste Sin.
12 Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
Und von der Wüste Sin brachen sie auf und lagerten in Dophkah.
13 Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
Und von Dophkah brachen sie auf und lagerten in Alusch.
14 Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
Und von Alusch brachen sie auf und lagerten in Rephidim, und daselbst war kein Wasser für das Volk zum Trinken.
15 Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
Und sie brachen auf von Rephidim und lagerten sich in der Wüste Sinai.
16 Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
Und aus der Wüste Sinai brachen sie auf und lagerten in Kibroth Thaavah.
17 Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
Und von Kibroth Thaavah brachen sie auf und lagerten in Chazeroth.
18 Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
Und von Chazeroth brachen sie auf und lagerten in Rithmah.
19 Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
Und von Rithmah brachen sie auf und lagerten in Rimmon Parez.
20 Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
Und von Rimmon Parez brachen sie auf und lagerten in Libnah.
21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
Und von Libnah brachen sie auf und lagerten in Rissah.
22 Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
Und von Rissah brachen sie auf und lagerten in Kehelathah.
23 Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
Und von Kehelathah brachen sie auf und lagerten am Berge Schapher.
24 Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
Und vom Berge Schapher brachen sie auf und lagerten in Charadah.
25 Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
Und von Charadah brachen sie auf und lagerten sich in Makheloth.
26 Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
Und von Makheloth brachen sie auf und lagerten in Thachath.
27 Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
Und von Thachath brachen sie auf und lagerten in Tharach.
28 Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
Und von Tharach brachen sie auf und lagerten sich in Mithkah.
29 Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
Und von Mithkah brachen sie auf und lagerten in Chaschmonah.
30 Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
Und von Chaschmonah brachen sie auf und lagerten in Moseroth.
31 Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
Und von Moseroth brachen sie auf und lagerten in Bene Jaakan.
32 Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
Und von Bene Jaakan brachen sie auf und lagerten in Chor Gidgad.
33 Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
Und von Chor Gidgad brachen sie auf und lagerten in Jotbathah.
34 Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
Und von Jotbathah brachen sie auf und lagerten in Abronah.
35 Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
Und von Abronah aber brachen sie auf und lagerten in Ezjon Geber.
36 Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
Und von Ezjon Geber brachen sie auf und lagerten in der Wüste Zin, das ist Kadesch.
37 Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
Und sie brachen auf von Kadesch und lagerten am Hor, dem Berge an dem Ende vom Lande Edom.
38 Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
Und Aharon, der Priester, stieg auf den Berg Hor nach dem Befehl Jehovahs und starb allda im vierzigsten Jahre des Auszugs der Söhne Israels aus Ägyptenland, im fünften Monat im ersten des Monats.
39 Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
Und Aharon war hundertdreiundzwanzig Jahre alt, da er starb auf dem Berge Hor.
40 Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
Und der Kanaaniterkönig Arad, der da wohnte im Mittag im Lande Kanaan, hörte von dem Kommen der Söhne Israels.
41 Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
Und sie brachen auf vom Berge Hor und lagerten in Zalmonah.
42 Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
Und von Zalmonah brachen sie auf und lagerten in Phunon.
43 Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
Und von Phunon brachen sie auf und lagerten in Oboth.
44 Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
Und von Oboth brachen sie auf und lagerten in Ijim Haabarim, an der Grenze Moabs.
45 Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
Und von Ijim brachen sie auf und lagerten in Dibon Gad.
46 Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
Und von Dibon Gad brachen sie auf und lagerten in Almon Diblathaim.
47 Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
Und von Almon Diblathaim brachen sie auf und lagerten in den Bergen Abarim vor Nebo.
48 Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
Und von den Bergen Abarim brachen sie auf und lagerten in Arboth Moab am Jordan bei Jericho.
49 Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
Und sie lagerten am Jordan von Beth Jeschimoth bis Abel Schittim in Moabs Flachland.
50 Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
Und Jehovah redete zu Mose in dem Flachland Moabs am Jordan bei Jericho und sprach:
51 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
Rede zu den Söhnen Israels und sprich zu ihnen: Wenn ihr über den Jordan setzet in das Land Kanaan,
52 wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
So sollet ihr alle, die im Lande wohnen, vor eurem Angesichte austreiben, und all ihr Gebilde und all ihre gegossenen Bilder sollt ihr zerstören, und alle ihre Opferhöhen vernichten.
53 Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
Und sollt das Land erblich besitzen und darin wohnen: denn euch habe Ich das Land gegeben, es erblich zu besitzen.
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
Und nach dem Lose sollt ihr das Land unter euch zum Erbe verteilen nach euren Familien; dem, der viele hat, mehrt sein Erbe, und dem der wenige hat, mindert das Erbe. Wohin das Los ihm ausgeht, das soll das Seinige sein. Nach den Stämmen eurer Väter sollt ihr es zum Erbe unter euch verteilen.
55 “‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
Und so ihr, die im Lande wohnen, nicht austreibet vor eurem Angesicht, so sollen die, so ihr von ihnen übriglasset, euch zu Dornen in den Augen und zu Stacheln in den Seiten werden und euch bedrängen auf dem Lande, da ihr innen wohnet.
56 Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”
Und es wird geschehen, daß, wie Ich ihnen zu tun gesonnen war, Ich euch tun werde.

< Hesabu 33 >