< Hesabu 33 >
1 Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
Folgendes sind die einzelnen Züge der Israeliten, in denen sie aus Ägypten nach ihren Heerscharen unter der Führung Moses und Aarons ausgezogen sind.
2 Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
Mose hatte nämlich auf Befehl des HERRN die Orte aufgeschrieben, von denen ihre Auszüge erfolgt waren; und folgendes sind ihre Züge von einem Aufbruchsort zum andern:
3 Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
Sie brachen von Ramses am fünfzehnten Tage des ersten Monats auf; am Tage nach dem Passah zogen die Israeliten mit hoch erhobener Hand vor den Augen aller Ägypter aus,
4 waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
während die Ägypter alle Erstgeborenen begruben, die der HERR unter ihnen hatte sterben lassen; denn der HERR hatte auch an ihren Göttern ein Strafgericht vollzogen.
5 Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
Die Israeliten brachen also von Ramses auf und lagerten in Sukkoth.
6 Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
Von Sukkoth zogen sie dann weiter und lagerten in Etham, das am Rande der Wüste liegt.
7 Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
Von Etham zogen sie weiter und wandten sich nach Pi-Hahiroth, das Baal-Zephon gegenüber liegt, und lagerten östlich von Migdol.
8 Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
Von Pi-Hahiroth brachen sie auf und zogen mitten durch das Meer nach der Wüste hin; sie wanderten dann drei Tagereisen weit in der Wüste Etham und lagerten in Mara.
9 Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
Von Mara zogen sie weiter und kamen nach Elim; dort waren zwölf Wasserquellen und siebzig Palmbäume, und sie lagerten daselbst.
10 Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
Von Elim zogen sie weiter und lagerten am Schilfmeer.
11 Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
Vom Schilfmeer zogen sie weiter und lagerten in der Wüste Sin.
12 Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
Aus der Wüste Sin zogen sie weiter und lagerten in Dophka.
13 Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
Von Dophka zogen sie weiter und lagerten in Alus.
14 Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
Von Alus zogen sie weiter und lagerten in Rephidim; dort hatte das Volk kein Wasser zu trinken.
15 Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
Von Rephidim zogen sie weiter und lagerten in der Wüste Sinai.
16 Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
Aus der Wüste Sinai zogen sie weiter und lagerten bei den Lustgräbern.
17 Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
Von den Lustgräbern zogen sie weiter und lagerten in Hazeroth.
18 Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
Von Hazeroth zogen sie weiter und lagerten in Rithma.
19 Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
Von Rithma zogen sie weiter und lagerten in Rimmon-Perez.
20 Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
Von Rimmon-Perez zogen sie weiter und lagerten in Libna.
21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
Von Libna zogen sie weiter und lagerten in Rissa.
22 Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
Von Rissa zogen sie weiter und lagerten in Kehelatha.
23 Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
Von Kehelatha zogen sie weiter und lagerten am Berge Sepher.
24 Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
Vom Berge Sepher zogen sie weiter und lagerten in Harada.
25 Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
Von Harada zogen sie weiter und lagerten in Makheloth.
26 Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
Von Makheloth zogen sie weiter und lagerten in Thahath.
27 Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
Von Thahath zogen sie weiter und lagerten in Therah.
28 Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
Von Therah zogen sie weiter und lagerten in Mithka.
29 Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
Von Mithka zogen sie weiter und lagerten in Hasmona.
30 Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
Von Hasmona zogen sie weiter und lagerten in Moseroth.
31 Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
Von Moseroth zogen sie weiter und lagerten in Bene-Jaakan.
32 Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
Von Bene-Jaakan zogen sie weiter und lagerten in Hor-Hagidgad.
33 Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
Von Hor-Hagidgad zogen sie weiter und lagerten in Jotbatha.
34 Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
Von Jotbatha zogen sie weiter und lagerten in Abrona.
35 Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
Von Abrona zogen sie weiter und lagerten in Ezjon-Geber.
36 Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
Von Ezjon-Geber zogen sie weiter und lagerten in der Wüste Zin, das ist Kades.
37 Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
Von Kades zogen sie weiter und lagerten am Berge Hor, an der Grenze des Landes der Edomiter.
38 Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
Da stieg der Priester Aaron nach dem Befehl des HERRN auf den Berg Hor hinauf und starb daselbst im vierzigsten Jahr nach dem Auszug der Israeliten aus dem Lande Ägypten am ersten Tage des fünften Monats;
39 Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
Aaron war aber 123 Jahre alt, als er auf dem Berge Hor starb.
40 Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
[Und der Kanaanäer, der König von Arad, der im südlichen Teile des Landes Kanaan wohnte, hörte vom Heranrücken der Israeliten.]
41 Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
Vom Berge Hor zogen sie dann weiter und lagerten in Zalmona.
42 Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
Von Zalmona zogen sie weiter und lagerten in Phunon.
43 Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
Von Phunon zogen sie weiter und lagerten in Oboth.
44 Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
Von Oboth zogen sie weiter und lagerten in Ijje-Abarim an der Grenze des Moabiterlandes.
45 Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
Von Ijjim zogen sie weiter und lagerten in Dibon-Gad.
46 Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
Von Dibon-Gad zogen sie weiter und lagerten in Almon-Diblathaim.
47 Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
Von Almon-Diblathaim zogen sie weiter und lagerten am Gebirge Abarim östlich vom Nebo.
48 Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
Vom Gebirge Abarim zogen sie weiter und lagerten sich in den Steppen der Moabiter am Jordan, Jericho gegenüber;
49 Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
und zwar lagerten sie am Jordan von Beth-Jesimoth bis Abel-Sittim in den Steppen der Moabiter.
50 Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
Der HERR gebot dann dem Mose in den Steppen der Moabiter am Jordan, Jericho gegenüber: »Teile den Israeliten folgende Verordnungen mit:
51 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
Wenn ihr über den Jordan in das Land Kanaan hinübergezogen seid,
52 wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
sollt ihr alle Bewohner des Landes vor euch her austreiben und alle ihre Götzenbilder vernichten; auch alle ihre Gußbilder sollt ihr vernichten und alle ihre Höhen zerstören.
53 Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
Ihr sollt dann das Land in Besitz nehmen und darin wohnen; denn euch habe ich das Land als Eigentum verliehen.
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
Und zwar sollt ihr euch das Land durch das Los als Erbbesitz zuteilen entsprechend euren Stämmen: den größeren Stämmen sollt ihr einen größeren Erbbesitz geben und den kleineren einen weniger großen Erbbesitz zuteilen; doch wohin immer einem jeden das Los fällt, da soll es ihm als Eigentum zuteil werden: nach euren väterlichen Stämmen sollt ihr euch das Land als Erbbesitz zuteilen.
55 “‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
Wenn ihr aber die Bewohner des Landes nicht vor euch her austreibt, so werden die, welche ihr von ihnen übriglaßt, zu Dornen in euren Augen und zu Stacheln in euren Seiten werden und euch in dem Lande, in dem ihr wohnen werdet, bedrängen.
56 Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”
Die Folge wird dann sein, daß ich euch das Geschick widerfahren lasse, das ich ihnen zugedacht hatte.«