< Hesabu 33 >

1 Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
Dies sind der Israeliten Züge, auf denen sie aus Ägypterland nach ihren Scharen unter Mosis und Aarons Führung gezogen sind.
2 Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
Moses schrieb ihre Ausfahrten zu ihren Zügen nieder auf des Herrn Befehl. Dies sind ihre Züge zu ihren Ausfahrten:
3 Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
Sie zogen von Ramses weg am fünfzehnten Tage des ersten Monats. Am Tage nach dem Passah zogen die Israeliten aus, in dichter Schar vor ganz Ägyptens Augen,
4 waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
während die Ägypter verkündeten, daß der Herr bei ihnen jede Erstgeburt erschlagen und daß der Herr an ihren Göttern Strafgerichte vollzogen habe.
5 Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
Die Israeliten zogen nun von Ramses fort und lagerten in Sukkot.
6 Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
Von Sukkot zogen sie fort und lagerten in Etam am Rande der Steppe.
7 Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
Von Etam zogen sie fort und wandten sich nach Pihachirot vor Baalsephon und lagerten vor Migdol.
8 Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
Sie zogen von Pihachirot fort und schritten mitten durch das Meer in die Wüste. Sie wanderten drei Tagereisen und lagerten in Mara.
9 Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
Sie zogen von Mara fort und kamen nach Elim. In Elim waren zwölf Quellen und siebzig Palmbäume, und sie lagerten dort.
10 Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
Sie zogen von Elim fort und lagerten am Schilfmeer.
11 Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
Sie zogen vom Schilfmeer fort und lagerten in der Wüste Sin.
12 Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
Von der Wüste Sin zogen sie fort und lagerten in Dophka.
13 Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
Sie zogen von Dophka fort und lagerten in Alus.
14 Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
Von Alus zogen sie fort und lagerten in Raphidim. Da war kein Wasser für das Volk zum Trinken.
15 Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
Von Raphidim zogen sie fort und lagerten in der Wüste Sinai.
16 Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
Von der Wüste Sinai zogen sie fort und lagerten bei den Gelüstegräbern.
17 Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
Von den Gelüstegräbern zogen sie nach Chaserot,
18 Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
von Chaserot nach Ritma,
19 Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
von Ritma nach Rimmon Peres,
20 Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
von Rimmon Peres nach Libna,
21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
von Libna nach Rissa,
22 Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
von Rissa nach Kehela,
23 Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
von Kehela zum Berge Sepher,
24 Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
vom Berge Sepher nach Charada,
25 Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
von Charada nach Makhelot,
26 Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
von Makhelot nach Tachat,
27 Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
von Tachat nach Tarach,
28 Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
von Tarach nach Mitka,
29 Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
von Mitka nach Chasmon,
30 Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
von Chasmon nach Moserot,
31 Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
von Moserot nach Bene Jaakan,
32 Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
von Bene Jaakan nach Chor Hagidgad,
33 Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
von Chor Hagidgad nach Jotba,
34 Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
von Jotba nach Abron,
35 Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
von Abron nach Esiongeber,
36 Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
von Esiongeber in die Wüste Sin, das ist Kades,
37 Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
von Kades zum Berge Hor an der Grenze des Landes Edom.
38 Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
Und der Priester Aaron stieg auf den Berg Hor nach des Herrn Befehl und starb hier, im vierzigsten Jahre nach dem Auszug der Israeliten aus Ägypterland, am ersten des fünften Monats.
39 Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
Aaron aber war 123 Jahre alt, als er auf dem Berge Hor starb.
40 Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
Da hörte der Kanaaniter, Arads König, der im Süden des Landes Kanaan saß, vom Anmarsch der Israeliten.
41 Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
Sie zogen dann vom Berge Hor fort und lagerten in Salmon.
42 Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
Von Salmon ging es nach Punon,
43 Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
Von Punon nach Obot,
44 Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
Von Obot nach Ijje Haabarim im Gebiete Moabs,
45 Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
von Ijjim nach Dibon Gad,
46 Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
von Dibon Gad nach Almon Diblataim,
47 Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
von Almon Diblataim zum Ufergebirge von Nebo.
48 Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
Vom Ufergebirge zogen sie fort und lagerten in den Steppen Moabs am Jordan bei Jericho,
49 Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
und zwar lagerten sie am Jordan von Bet Hajesimot bis Abel Hasittim in Moabs Steppen.
50 Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
Und der Herr sprach zu Moses in Moabs Steppen am Jordan bei Jericho:
51 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
"Rede mit den Söhnen Israels und sprich zu ihnen: 'Zieht ihr über den Jordan ins Land Kanaan,
52 wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
dann müßt ihr alle Insassen des Landes vor euch vertilgen und alle ihre Bilder vernichten. Auch alle ihre Gußbilder sollt ihr vernichten und alle ihre Höhen verwüsten!
53 Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
Vom Lande ergreift Besitz und siedelt darin! Denn euch gebe ich das Land zum Besitz.
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
Verteilt das Land nach euren Stämmen durch das Los! Dem, der viel zählt, sollt ihr seinen Besitz vermehren und dem, der wenig zählt, einen kleineren geben! Was jemandem durchs Los zufällt, soll ihm gehören! Nach euren väterlichen Stämmen sollt ihr es verteilen!
55 “‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
Vertreibt ihr aber nicht vor euch des Landes Insassen, dann werde, was ihr davon übriglaßt, euch zu Dornen in den Augen und zu Stacheln in den Seiten! Sie sollen euch bedrängen in eurem Lande, in dem ihr siedelt!
56 Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”
Dann tue ich mit euch, was ich jenen zugedacht.'"

< Hesabu 33 >