< Hesabu 33 >
1 Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
Voici les demeures des enfants d’Israël, qui sont sortis de l’Egypte, selon leurs bandes, par l’entremise de Moïse et d’Aaron;
2 Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
Lesquels Moïse décrivit, selon les lieux de leurs campements qu’ils changeaient par le commandement du Seigneur.
3 Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
Partis donc de Ramessès, au premier mois, au quinzième jour du premier mois, le lendemain de la Pâque, les enfants d’Israël, par une main élevée, tous les Egyptiens le voyant,
4 waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
Et ensevelissant leurs premiers-nés qu’avait frappés le Seigneur (or, même sur leurs dieux il avait exercé sa vengeance),
5 Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
Campèrent à Soccoth,
6 Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
Et de Soccoth ils vinrent à Etham, qui est aux derniers confins du désert.
7 Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
Sortis donc de là, ils vinrent contre Phihahiroth, qui regarde Béelséphon, et ils campèrent devant Magdalum.
8 Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
Et partis de Phihahiroth, ils passèrent par le milieu de la mer dans le désert; et marchant durant trois jours par le désert d’Etham, ils campèrent à Mara.
9 Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
Or, partis de Mara, ils vinrent à Elim, où étaient douze sources d’eaux, et soixante-dix palmiers; et ils y campèrent.
10 Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
Mais étant encore sortis de là, ils plantèrent leurs tentes sur la mer Rouge. Et partis de la mer Rouge,
11 Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
Ils campèrent dans le désert de Sin;
12 Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
D’où étant sortis, ils vinrent à Daphca.
13 Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
Et partis de Daphca, ils campèrent à Alus.
14 Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
Or, sortis d’Alus, ils plantèrent leurs tentes à Raphidim, où l’eau pour boire manqua au peuple.
15 Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
Et partis de Raphidim, ils campèrent dans le désert de Sinaï.
16 Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
Mais, sortis aussi du désert de Sinaï, ils vinrent aux Sépulcres de la concupiscence.
17 Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
Et partis des Sépulcres de la concupiscence, ils campèrent à Haséroth.
18 Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
Or, de Haséroth, ils vinrent à Rethma.
19 Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
Et partis de Rethma, ils campèrent à Remmompharès;
20 Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
D’où étant sortis, ils vinrent à Lebna.
21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
De Lebna, ils campèrent à Ressa.
22 Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
Et sortis de Cessa, ils vinrent à Céélatha;
23 Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
D’où étant partis, ils campèrent à la montagne de Sépher.
24 Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
Sortis de la montagne de Sépher, ils vinrent à Arada.
25 Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
Partant delà, ils campèrent à Macéloth.
26 Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
Et étant partis de Macéloth, ils vinrent à Thahath.
27 Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
De Thahath, ils campèrent à Tharé;
28 Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
D’où étant sortis, ils plantèrent leurs tentes à Methca.
29 Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
Et de Methca, ils campèrent à Hesmona.
30 Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
Or, partis de Hesmona, ils vinrent à Moséroth.
31 Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
Et de Moséroth, ils campèrent à Bénéjaacan.
32 Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
Mais partis de Bénéjaacan, ils vinrent à la montagne de Gadgad;
33 Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
D’où étant partis ils campèrent à Jétébatha.
34 Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
Et de Jétébatha, ils vinrent à Hébrona.
35 Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
Et, sortis d’Hébrona, ils campèrent à Asiongaber
36 Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
Partis de là, ils vinrent au désert de Sin; c’est Cadès.
37 Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
Et, sortis de Cadès, ils campèrent à la montagne de Hor, aux derniers confins de la terre d’Edom.
38 Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
Or, Aaron, le prêtre, monta sur la montagne de Hor, le Seigneur l’ordonnant, et là il mourut, en l’année quarantième de la sortie des enfants d’Israël de l’Egypte, au cinquième mois, au premier jour du mois,
39 Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
Comme il avait cent vingt-trois ans.
40 Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
Cependant le roi d’Arad, Chananéen, qui habitait vers le midi, apprit que les enfants d’Israël étaient venus dans la terre de Chanaan.
41 Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
Or, partis de la montagne de Hor, ils campèrent à Salmona;
42 Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
D’où étant sortis, ils vinrent à Phunon.
43 Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
Et partis de Phunon, ils campèrent à Oboth.
44 Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
Et d’Oboth ils vinrent à Jiéabarim, qui est aux confins des Moabites.
45 Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
Puis, partis de Jiéabarim, ils plantèrent leurs tentes à Dibongad;
46 Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
D’où étant sortis, ils campèrent à Helmondéblathaïm.
47 Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
Et sortis de Helmondéblathaïm, ils vinrent aux montagnes d’Abarim, contre Nabo.
48 Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
Or, partis des montagnes d’Abarim, ils passèrent dans les plaines de Moab, sur le Jourdain, contre Jéricho.
49 Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
Et là ils campèrent, depuis Bethsimoth jusqu’à Abelsatim, dans les lieux les plus plats des Moabites,
50 Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
Où le Seigneur dit à Moïse:
51 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
Ordonne aux enfants d’Israël, et dis-leur: Quand vous aurez passé le Jourdain, entrant dans la terre de Chanaan,
52 wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
Détruisez tous les habitants de cette terre; brisez les monuments, mettez en pièces les statues, et ravagez tous les hauts lieux,
53 Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
Purifiant la terre, et y habitant; car c’est moi qui vous l’ai donnée en possession;
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
Vous vous la partagerez par le sort. Au plus grand nombre, vous donnerez la partie la plus étendue, et au plus petit nombre, la partie la plus resserrée. Comme le sort sera échu à chacun, ainsi sera donné l’héritage. C’est par tribus et par familles que la possession sera partagée.
55 “‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
Mais si vous ne voulez pas tuer les habitants de la terre, ceux qui resteront seront comme des clous dans vos yeux et des lances dans vos côtés, et ils vous seront contraires dans la terre de votre habitation;
56 Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”
Et ce que j’avais pensé à leur faire, c’est à vous que je le ferai.