< Hesabu 33 >

1 Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
Stations des enfants d'Israël sortis du pays d'Egypte, formant leurs divisions sous la conduite de Moïse et d'Aaron.
2 Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
Moïse mit par écrit leurs marches selon leurs stations sur l'ordre de l'Éternel, et voici les stations qu'ils firent dans leurs marches.
3 Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
Ils partirent de Raemsès dans le premier mois, le quinzième jour du premier mois; le lendemain de la Pâque, les enfants d'Israël sortirent la main haute, aux yeux de toute l'Egypte,
4 waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
tandis que les Égyptiens donnaient la sépulture à ceux que l'Éternel avait frappés parmi eux, à tous les premiers-nés; et l'Éternel exerçait ses jugements sur leurs dieux.
5 Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
Étant donc partis de Raemsès, ils vinrent camper à Succoth.
6 Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
Et partis de Succoth ils vinrent camper à Etham situé à l'extrémité du désert.
7 Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
Et partis d'Etham ils revinrent sur Pi-Hahiroth située vis-à-vis de Baal-Tsephon et campèrent devant Migdol.
8 Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
Et partis de Hahiroth ils arrivèrent au travers de la mer dans le désert, et firent trois journées de marche dans le désert d'Etham et campèrent à Mara.
9 Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
Et partis de Mara ils parvinrent à Elim, or à Elim il y avait douze sources d'eau et soixante-dix palmiers; et ils y campèrent.
10 Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
Et partis d'Elim ils vinrent camper vers la Mer aux algues.
11 Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
Et partis de la Mer aux algues ils vinrent camper dans le désert de Sin.
12 Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
Et partis du désert de Sin ils vinrent camper à Dophka.
13 Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
Et partis de Dophka ils vinrent camper à Alus.
14 Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
Et partis d'Alus ils vinrent camper à Raphidim; or le peuple n'y trouva point d'eau à boire.
15 Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
Et partis de Raphidim ils vinrent camper dans le désert de Sinaï.
16 Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
Et partis du désert de Sinaï ils vinrent camper aux Tombeaux de la convoitise.
17 Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
Et partis des Tombeaux de la convoitise ils vinrent camper à Hatseroth.
18 Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
Et partis de Hatseroth ils vinrent camper à Rithma.
19 Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
Et partis de Rithma ils vinrent camper à Rimmon-Parets.
20 Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
Et partis de Rimmon-Parets ils vinrent camper à Libna.
21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
Et partis de Libna ils vinrent camper à Rissa.
22 Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
Et partis de Rissa ils vinrent camper à Kehelatha.
23 Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
Et partis de Kehelatha ils vinrent camper au mont Sapher.
24 Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
Et partis du mont Sapher ils vinrent camper à Harada.
25 Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
Et partis de Harada ils vinrent camper à Makheloth.
26 Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
Et partis de Makheloth ils vinrent camper à Thahath.
27 Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
Et partis de Thahath ils vinrent camper à Tharach.
28 Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
Et partis de Tharach ils vinrent camper à Mithka.
29 Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
Et partis de Mithka ils vinrent camper à Hasmona.
30 Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
Et partis de Hasmona ils vinrent camper à Moseroth.
31 Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
Et partis de Moseroth ils vinrent camper à Bnei-Jaakan.
32 Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
Et partis de Bnei-Jaakan ils vinrent camper à Hor-Gidgad.
33 Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
Et partis de Hor-Gidgad ils vinrent camper à Jotbatha.
34 Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
Et partis de Jotbatha ils vinrent camper à Abrona.
35 Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
Et partis de Abrona ils vinrent camper à Etsion-Géber.
36 Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
Et partis de Etsion-Géber ils vinrent camper dans le désert de Tsin: c'est Cadès.
37 Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
Et partis de Cadès ils vinrent camper au mont Hor, sur la frontière du pays d'Edom.
38 Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
C'est alors que le Prêtre Aaron monta sur le mont Hor, d'après l'ordre de l'Éternel, et qu'il y mourut la quarantième année après la sortie des enfants d'Israël hors du pays d'Egypte, le cinquième mois, le premier jour du mois;
39 Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
(or Aaron était âgé de cent vingt-trois ans, lorsqu'il mourut sur le mont Hor).
40 Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
Et le Cananéen, Roi de Arad, établi dans le Midi du pays de Canaan entendit parler de l'arrivée des enfants d'Israël.
41 Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
Et étant partis du mont Hor ils vinrent camper à Tsalmona.
42 Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
Et partis de Tsalmona ils vinrent camper à Punon.
43 Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
Et partis de Punon ils vinrent camper à Oboth.
44 Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
Et partis d'Oboth ils vinrent camper à Jiim, à la frontière de Moab.
45 Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
Et partis de Jiim ils vinrent camper à Dibon-Gad.
46 Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
Et partis de Dibon-Gad ils vinrent camper à Almon-Diblathaïm.
47 Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
Et partis de Almon-Diblathaïm ils vinrent camper aux monts Abarim devant le Nébo.
48 Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
Et partis des monts Abarim ils vinrent camper dans les plaines de Moab sur le Jourdain près de Jéricho.
49 Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
Et ils campèrent sur le Jourdain, de Beth-Jesimoth à Abel-Sittim dans les plaines de Moab.
50 Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
Et l'Éternel parla à Moïse dans les plaines de Moab sur le Jourdain près de Jéricho, en ces termes:
51 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
Parle aux enfants d'Israël et dis-leur: Quand après le passage du Jourdain vous serez entrés dans le pays de Canaan,
52 wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
vous chasserez tous les habitants du pays devant vous, détruirez toutes leurs [pierres] figurées et détruirez toutes leurs images de fonte et raserez tous leurs tertres,
53 Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
et vous occuperez le pays et vous y établirez, car je vous ai donné ce pays pour en prendre possession.
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
Et vous vous partagerez le pays au sort selon vos familles; aux plus nombreux vous adjugerez un lot plus étendu; aux moins nombreux, un lot plus restreint; l'emplacement échu par le sort à quelqu'un, c'est ce qu'il aura; vous vous le partagerez d'après vos Tribus patriarcales.
55 “‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
Mais si vous ne chassez pas devant vous les habitants du pays, ceux d'entre eux que vous laisserez, deviendront des épines pour vos yeux, et des aiguillons dans vos flancs et ils vous mettront à la gêne dans le pays où vous serez établis.
56 Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”
Et il arrivera que ce que j'avais résolu de leur faire, c'est à vous que je le ferai.

< Hesabu 33 >