< Hesabu 33 >

1 Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
Voici les stations des fils d'Israël, après que Moïse et Aaron les eurent fait sortir d'Egypte.
2 Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
Par les ordres du Seigneur, Moïse écrivit leurs départs et leurs campements. Or, voici ces stations:
3 Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
Ils partirent de Rhamessès le premier mois, le quinzième jour de la lune; le lendemain de la pâque, les fils d'Israël partirent sous une haute et puissante main, devant tous les fils de l'Egypte.
4 waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
Les Egyptiens ensevelirent chez eux tous les morts qu'avait frappés le Seigneur, tous les premiers-nés de la terre d'Egypte, et le Seigneur tira vengeance de leurs dieux.
5 Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
Partis de Rhamessès, les fils d'Israël campèrent en Soccoth.
6 Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
Partis de Soccoth, ils campèrent à Etham (Othom), qui est à l'extrémité du désert.
7 Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
Ils partirent d'Etham, et campèrent vers le golfe de Phihahiroth, qui est en face de Béelséphon, et ils étaient campés vis-à-vis Magdole.
8 Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
Partis de Phihahiroth, ils passèrent au milieu de la mer Rouge pour gagner le désert, et ils firent trois journées de marche dans le désert, et ils campèrent à Mara.
9 Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
Ils quittèrent Mara, et vinrent en Elim. Or, il y avait à Elim douze fontaines et soixante-dix tiges de palmiers; ils campèrent en ce lieu, à cause de l'eau.
10 Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
Puis, ils partirent d'Elim, et ils campèrent au bord de la mer Rouge.
11 Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
Et ils partirent de la mer Rouge, et ils campèrent dans le désert de Sin.
12 Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
Partis du désert de Sin, ils vinrent camper en Daphca.
13 Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
Et ils partirent de Daphca, et ils campèrent en Alus.
14 Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
Et ils partirent d'Alus, et ils campèrent à Rhaphidin; or, il n'y avait point là de l'eau pour que le peuple put boire.
15 Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
Ayant quitte Rhaphidin, ils dressèrent leurs tentes dans le désert de Sina.
16 Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
Du désert de Sina, ils vinrent camper aux Sépulcres de concupiscence.
17 Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
Ils s'éloignèrent des Sépulcres de concupiscence, et campèrent à Haseroth.
18 Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
Partis d'Haseroth, ils allèrent camper à Rethma.
19 Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
De Rethma, ils vinrent camper en Rhemmompharès.
20 Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
Ils partirent de Rhemmompharès, et ils campèrent en Lebna.
21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
Partis de Lebna, ils campèrent en Ressa.
22 Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
De Ressa, ils vinrent dresser leurs tentes en Céélatha.
23 Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
Et ils partirent de Céélatha, pour aller camper à Sépher.
24 Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
Ayant quitté Sépher, ils campèrent en Arada.
25 Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
Ils partirent d'Arada, et campèrent en Maceloth.
26 Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
De Maceloth, ils dressèrent leurs tentes en Thabath.
27 Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
Et ils partirent de Thabath, pour venir camper à Tharé.
28 Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
Partis de Tharé, ils campèrent à Methca.
29 Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
De Methca, ils vinrent camper à Hesmona.
30 Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
Et ils partirent de Hesmona, pour aller camper à Moserotb.
31 Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
Ayant quitté Moseroth, ils campèrent à Béné-Jaacan.
32 Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
Partis de Béné-Jaacan, ils vinrent camper en la montagne de Gadgad.
33 Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
De la montagne de Gadgad, ils vinrent camper à Jétébatba.
34 Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
Et ils partirent de Jétébatba, pour aller dresser leurs tentes en Hébrona.
35 Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
Puis, ayant quitté Hebrona, ils campèrent en Asion-Gaber.
36 Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
Partis d'Asion-Gaber, ils vinrent camper dans le désert de Sin, d'où, étant sortis, ils campèrent dans le désert de Pharan qui est Cadès.
37 Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
Partis de Cadès-Barné, ils vinrent camper sur la montagne de Hor, près de la terre d'Edom.
38 Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
Et Aaron monta sur la montagne par ordre du Seigneur, et il y mourut, en la quarantième année de la sortie d'Egypte, le cinquième mois, le premier de la lune.
39 Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
Aaron avait cent vingt-trois ans lorsqu'il mourut sur la montagne de Hor.
40 Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
Et, le Chananéen, roi d'Arad, qui demeurait en la terre de Chanaan, apprit que les fils d'Israël étaient en marche.
41 Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
Ils partirent ensuite de la montagne de Hor, et vinrent camper en Salmona.
42 Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
Ayant quitté Salmona, ils campèrent en Phunon.
43 Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
Partis de Phunon, ils dressèrent leurs tentes à Oboth.
44 Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
Puis, ils s'éloignèrent d'Obotb, pour venir camper à Gié-Abarim, au delà et près des frontières de Moab.
45 Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
Et ils partirent de Gié-Abarim, pour séjourner à Dibon-Gad.
46 Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
De Dibon-Gad, ils vinrent camper à Helmon-Déblathaïm.
47 Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
Partis de Helmon-Déblathaïm, ils campèrent sur les montagnes d'Abarim, en face de Nébo.
48 Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
Ayant quitté les montagnes d'Abarim, ils campèrent à l'Occident de Moab, sur le Jourdain, en face de Jéricho.
49 Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
Ensuite, ils campèrent aux bords du Jourdain de Beth-Simoth, à Abelsatim, à l'occident de Moab.
50 Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
Et le Seigneur parla à Moïse, à l'occident de Moab, sur le Jourdain, en face de Jéricho, et il lui dit:
51 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
Parle aux fils d'Israël, et dis-leur: Vous allez traverser le Jourdain pour entrer en la terre de Chanaan.
52 wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
Et, devant vous, vous exterminerez tous ceux qui habitent cette terre; vous détruirez leurs tours, leurs idoles jetées en fonte, et leurs colonnes.
53 Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
Vous détruirez tous les peuples de la terre promise, et vous l'habiterez; car je vous la donne pour héritage.
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
Vous la partagerez entre vos tribus; donnant plus aux plus nombreux, et moins aux moindres en nombre. Quelle que soit la part qu'à chacun désignera le sort, chacun la possèdera; le partage se fera par tribus paternelles.
55 “‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
Mais, si vous n'exterminez pas devant vous tous les habitants de la terre, ceux que vous aurez épargnés seront des traits en vos yeux, des flèches en vos flancs; ils seront vos ennemis sur la terre que vous habiterez.
56 Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”
Et alors, je vous traiterai vous-mêmes comme j'avais résolu de les traiter.

< Hesabu 33 >