< Hesabu 33 >

1 Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
These were the movements of the people of Israel after they left the land of Egypt by their armed groups under the leadership of Moses and Aaron.
2 Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
Moses wrote down the places from where they left to where they went, as commanded by Yahweh. These were their movements, departure after departure.
3 Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
They traveled from Rameses during the first month, leaving on the fifteenth day of the first month. On the morning after the Passover, the people of Israel left openly, in the sight of all the Egyptians.
4 waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
This happened while the Egyptians were burying all their firstborn, those whom Yahweh had killed among them, for he also inflicted punishment on their gods.
5 Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
The people of Israel set out from Rameses and camped at Succoth.
6 Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
They set out from Succoth and camped at Etham, on the edge of the wilderness.
7 Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
They set out from Etham and turned back to Pi Hahiroth, which is opposite Baal Zephon, where they camped opposite Migdol.
8 Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
Then they set out from opposite Pi Hahiroth and passed through the middle of the sea into the wilderness. They traveled three days' journey into the wilderness of Etham and camped at Marah.
9 Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
They set out from Marah and arrived at Elim. At Elim were twelve springs of water and seventy palm trees. That is where they camped.
10 Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
They set out from Elim and camped by the Sea of Reeds.
11 Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
They set out from the Sea of Reeds and camped in the wilderness of Sin.
12 Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
They set out from the wilderness of Sin and camped at Dophkah.
13 Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
They set out from Dophkah and camped at Alush.
14 Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
They set out from Alush and camped at Rephidim, where no water was found for the people to drink.
15 Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
They set out from Rephidim and camped in the wilderness of Sinai.
16 Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
They set out from the wilderness of Sinai and camped at Kibroth Hattaavah.
17 Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
They set out from Kibroth Hattaavah and camped at Hazeroth.
18 Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
They set out from Hazeroth and camped at Rithmah.
19 Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
They set out from Rithmah and camped at Rimmon Perez.
20 Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
They set out from Rimmon Perez and camped at Libnah.
21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
They set out from Libnah and camped at Rissah.
22 Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
They set out from Rissah and camped at Kehelathah.
23 Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
They set out from Kehelathah and camped at Mount Shepher.
24 Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
They set out from Mount Shepher and camped at Haradah.
25 Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
They set out from Haradah and camped at Makheloth.
26 Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
They set out from Makheloth and camped at Tahath.
27 Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
They set out from Tahath and camped at Terah.
28 Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
They set out from Terah and camped at Mithkah.
29 Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
They set out from Mithkah and camped at Hashmonah.
30 Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
They set out from Hashmonah and camped at Moseroth.
31 Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
They set out from Moseroth and camped at Bene Jaakan.
32 Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
They set out from Bene Jaakan and camped at Hor Haggidgad.
33 Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
They set out from Hor Haggidgad and camped at Jotbathah.
34 Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
They set out from Jotbathah and camped at Abronah.
35 Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
They set out from Abronah and camped at Ezion Geber.
36 Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
They set out from Ezion Geber and camped in the wilderness of Zin at Kadesh.
37 Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
They set out from Kadesh and camped at Mount Hor, at the edge of the land of Edom.
38 Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
Aaron the priest went up Mount Hor at Yahweh's command and died there in the fortieth year after the people of Israel had come out of the land of Egypt, in the fifth month, on the first day of the month.
39 Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
Aaron was a 123 years old when he died on Mount Hor.
40 Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
The Canaanite, the king of Arad, who lived in the southern wilderness in the land of Canaan, heard of the coming of the people of Israel.
41 Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
They set out from Mount Hor and camped at Zalmonah.
42 Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
They set out from Zalmonah and camped at Punon.
43 Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
They set out from Punon and camped at Oboth.
44 Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
They set out from Oboth and camped at Iye Abarim, on the border of Moab.
45 Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
They set out from Iye Abarim and camped at Dibon Gad.
46 Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
They set out from Dibon Gad and camped at Almon Diblathaim.
47 Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
They set out from Almon Diblathaim and camped in the mountains of Abarim, opposite Nebo.
48 Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
They set out from the mountains of Abarim and camped in the plains of Moab by the Jordan at Jericho.
49 Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
They camped by the Jordan, from Beth Jeshimoth to Abel Shittim in the plains of Moab.
50 Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
Yahweh spoke to Moses in the plains of Moab by the Jordan at Jericho and said,
51 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
“Speak to the people of Israel and say to them, 'When you cross over the Jordan into the land of Canaan,
52 wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
then you must drive out all the land's inhabitants before you. You must destroy all their carved figures. You must destroy all their cast figures and demolish all their high places.
53 Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
You must take possession of the land and settle in it, because I have given you the land to possess.
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
You must inherit the land by lot, according to each clan. To the larger clans you must give a larger share of land, and to the smaller clans you must give a smaller share of land. Wherever the lot falls to each clan, that land will belong to it. You will inherit the land according to your ancestors' tribes.
55 “‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
But if you do not drive out the land's inhabitants before you, then the people you allow to stay will become like objects in your eyes and thorns in your sides. They will make your lives difficult in the land where you settle.
56 Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”
Then it will happen that what I now intend to do to those people, I will do also to you.'”

< Hesabu 33 >