< Hesabu 33 >

1 Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
These [are] [the] settings out of [the] people of Israel who they came out from [the] land of Egypt to military groups their by [the] hand of Moses and Aaron.
2 Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
And he wrote down Moses points of departure their to settings out their on [the] mouth of Yahweh and these [are] settings out their to points of departure their.
3 Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
And they set out from Rameses in the month first on [the] fif-teen day of the month first from [the] next day of the passover they went out [the] people of Israel with a hand raised to [the] eyes all Egypt.
4 waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
And Egypt [were] burying [those] whom he had struck down Yahweh among them every firstborn and on gods their he had done Yahweh acts of judgment.
5 Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
And they set out [the] people of Israel from Rameses and they encamped at Succoth.
6 Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
And they set out from Succoth and they encamped at Etham which [is] on [the] edge of the wilderness.
7 Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
And they set out from Etham and he turned back to Pi-hahiroth which [is] on [the] face of Baal-Zephon and they encamped before Migdol.
8 Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
And they set out from before Hahiroth and they passed in [the] middle of the sea the wilderness towards and they went a journey of three days in [the] wilderness of Etham and they encamped at Marah.
9 Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
And they set out from Marah and they came Elim towards and [were] at Elim two [plus] ten springs of water and seventy palm trees and they encamped there.
10 Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
And they set out from Elim and they encamped at [the] sea of reed[s].
11 Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
And they set out from [the] sea of reed[s] and they encamped in [the] wilderness of Sin.
12 Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
And they set out from [the] wilderness of Sin and they encamped at Dophka.
13 Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
And they set out from Dophka and they encamped at Alush.
14 Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
And they set out from Alush and they encamped at Rephidim and not it belonged there water to the people to drink.
15 Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
And they set out from Rephidim and they encamped in [the] wilderness of Sinai.
16 Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
And they set out from [the] wilderness of Sinai and they encamped at Kibroth Hattaavah.
17 Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
And they set out from Kibroth Hattaavah and they encamped at Hazeroth.
18 Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
And they set out from Hazeroth and they encamped at Rithmah.
19 Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
And they set out from Rithmah and they encamped at Rimmon-perez.
20 Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
And they set out from Rimmon-perez and they encamped at Libnah.
21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
And they set out from Libnah and they encamped at Rissah.
22 Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
And they set out from Rissah and they encamped at Kehelathah.
23 Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
And they set out from Kehelathah and they encamped at [the] mountain of Shapher.
24 Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
And they set out from [the] mountain of Shapher and they encamped at Haradah.
25 Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
And they set out from Haradah and they encamped at Makheloth.
26 Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
And they set out from Makheloth and they encamped at Tahath.
27 Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
And they set out from Tahath and they encamped at Tarah.
28 Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
And they set out from Tarah and they encamped at Mithcah.
29 Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
And they set out from Mithcah and they encamped at Hashmoneh.
30 Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
And they set out from Hashmoneh and they encamped at Moseroth.
31 Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
And they set out from Moseroth and they encamped at Bene-jaakan.
32 Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
And they set out from Bene-jaakan and they encamped at Hor-haggidgad.
33 Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
And they set out from Hor-haggidgad and they encamped at Jotbathah.
34 Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
And they set out from Jotbathah and they encamped at Abronah.
35 Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
And they set out from Abronah and they encamped at Ezion Geber.
36 Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
And they set out from Ezion Geber and they encamped in [the] wilderness of Zin that [is] Kadesh.
37 Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
And they set out from Kadesh and they encamped at Hor the mountain on [the] border of [the] land of Edom.
38 Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
And he went up Aaron the priest to Hor the mountain on [the] mouth of Yahweh and he died there in [the] year forty of [the] coming out of [the] people of Israel from [the] land of Egypt in the month fifth on [day] one of the month.
39 Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
And Aaron [was] a son of three and twenty and one hundred year[s] when dying he on Hor the mountain.
40 Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
And he heard the Canaanite [the] king of Arad and he [was] dwelling in the Negev in [the] land of Canaan when came [the] people of Israel.
41 Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
And they set out from Hor the mountain and they encamped at Zalmonah.
42 Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
And they set out from Zalmonah and they encamped at Punan.
43 Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
And they set out from Punan and they encamped at Oboth.
44 Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
And they set out from Oboth and they encamped at Iye Abarim on [the] border of Moab.
45 Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
And they set out from Iim and they encamped at Dibon-gad.
46 Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
And they set out from Dibon-gad and they encamped at Almon-diblathaim.
47 Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
And they set out from Almon-diblathaim and they encamped in [the] mountains of the Abarim before Nebo.
48 Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
And they set out from [the] mountains of the Abarim and they encamped in [the] plains of Moab at [the] Jordan of Jericho.
49 Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
And they encamped at the Jordan from Beth Jeshimoth to Abel-shittim in [the] plains of Moab.
50 Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
And he spoke Yahweh to Moses in [the] plains of Moab at [the] Jordan of Jericho saying.
51 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
Speak to [the] people of Israel and you will say to them if you [are] about to pass over the Jordan into [the] land of Canaan.
52 wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
And you will dispossess all [the] inhabitants of the land from before you and you will destroy all carved images their and all [the] images of molten metal their you will destroy and all high places their you will demolish.
53 Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
And you will take possession of the land and you will dwell in it for to you I have given the land to take possession of it.
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
And you will inherit the land by lot to clans your for the many you will make great inheritance its and for the few you will make small inheritance its where it will come out for him there the lot to him it will belong to [the] tribes of fathers your you will inherit.
55 “‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
And if not you will dispossess [the] inhabitants of the land from before you and he will become [those] whom you will leave any of them thorns in view your and pricks in sides your and they will oppose you on the land which you [will be] dwelling in it.
56 Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”
And it will be just as I intended to do to them I will do to you.

< Hesabu 33 >