< Hesabu 33 >

1 Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
These are the journeys of the children of Israel, when they went forth out of the land of Egypt by their hosts under the hand of Moses and Aaron.
2 Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
And Moses wrote their goings out according to their journeys by the commandment of the LORD: and these are their journeys according to their goings out.
3 Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
And they journeyed from Rameses in the first month, on the fifteenth day of the first month; on the morrow after the passover the children of Israel went out with an high hand in the sight of all the Egyptians,
4 waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
while the Egyptians were burying all their firstborn, which the LORD had smitten among them: upon their gods also the LORD executed judgments.
5 Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
And the children of Israel journeyed from Rameses, and pitched in Succoth.
6 Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
And they journeyed from Succoth, and pitched in Etham, which is in the edge of the wilderness.
7 Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
And they journeyed from Etham, and turned back unto Pi-hahiroth, which is before Baal-zephon: and they pitched before Migdol.
8 Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
And they journeyed from before Hahiroth, and passed through the midst of the sea into the wilderness: and they went three days’ journey in the wilderness of Etham, and pitched in Marah.
9 Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
And they journeyed from Marah, and came unto Elim: and in Elim were twelve springs of water, and threescore and ten palm trees; and they pitched there.
10 Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
And they journeyed from Elim, and pitched by the Red Sea.
11 Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
And they journeyed from the Red Sea, and pitched in the wilderness of Sin.
12 Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
And they journeyed from the wilderness of Sin, and pitched in Dophkah.
13 Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
And they journeyed from Dophkah, and pitched in Alush.
14 Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
And they journeyed from Alush, and pitched in Rephidim, where was no water for the people to drink.
15 Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
And they journeyed from Rephidim, and pitched in the wilderness of Sinai.
16 Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
And they journeyed from the wilderness of Sinai, and pitched in Kibroth-hattaavah.
17 Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
And they journeyed from Kibroth-hattaavah, and pitched in Hazeroth.
18 Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
And they journeyed from Hazeroth, and pitched in Rithmah.
19 Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
And they journeyed from Rithmah, and pitched in Rimmon-perez.
20 Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
And they journeyed from Rimmon-perez, and pitched in Libnah.
21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
And they journeyed from Libnah, and pitched in Rissah.
22 Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
And they journeyed from Rissah, and pitched in Kehelathah.
23 Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
And they journeyed from Kehelathah, and pitched in mount Shepher.
24 Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
And they journeyed from mount Shepher, and pitched in Haradah.
25 Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
And they journeyed from Haradah, and pitched in Makheloth.
26 Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
And they journeyed from Makheloth, and pitched in Tahath.
27 Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
And they journeyed from Tahath, and pitched in Terah.
28 Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
And they journeyed from Terah, and pitched in Mithkah.
29 Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
And they journeyed from Mithkah, and pitched in Hashmonah.
30 Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
And they journeyed from Hashmonah, and pitched in Moseroth.
31 Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
And they journeyed from Moseroth, and pitch in Bene-jaakan.
32 Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
And they journeyed from Bene-jaakan, and pitched in Hor-haggidgad.
33 Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
And they journeyed from Hor-haggidgad, and pitched in Jotbathah.
34 Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
And they journeyed from Jotbathah, and pitched in Abronah.
35 Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
And they journeyed from Abronah, and pitched in Ezion-geber.
36 Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
And they journeyed from Ezion-geber, and pitched in the wilderness of Zin (the same is Kadesh).
37 Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
And they journeyed from Kadesh, and pitched in mount Hor, in the edge of the land of Edom.
38 Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
And Aaron the priest went up into mount Hor at the commandment of the LORD, and died there, in the fortieth year after the children of Israel were come out of the land of Egypt, in the fifth month, on the first day of the month.
39 Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
And Aaron was an hundred and twenty and three years old when he died in mount Hor.
40 Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
And the Canaanite, the king of Arad, which dwelt in the South in the land of Canaan, heard of the coming of the children of Israel.
41 Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
And they journeyed from mount Hor, and pitched in Zalmonah.
42 Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
And they journeyed from Zalmonah, and pitched in Punon.
43 Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
And they journeyed from Punon, and pitched in Oboth.
44 Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
And they journeyed from Oboth, and pitched in Iye-abarim, in the border of Moab.
45 Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
And they journeyed from Iyim, and pitched in Dibon-gad.
46 Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
And they journeyed from Dibon-gad, and pitched in Almon-diblathaim.
47 Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
And they journeyed from Almon-diblathaim, and pitched in the mountains of Abarim, before Nebo.
48 Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
And they journeyed from the mountains of Abarim, and pitched in the plains of Moab by the Jordan at Jericho.
49 Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
And they pitched by Jordan, from Beth-jeshimoth even unto Abel-shittim in the plains of Moab.
50 Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
And the LORD spake unto Moses in the plains of Moab by the Jordan at Jericho, saying,
51 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
Speak unto the children of Israel, and say unto them, When ye pass over Jordan into the land of Canaan,
52 wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
then ye shall drive out all the inhabitants of the land from before you, and destroy all their figured [stones], and destroy all their molten images, and demolish all their high places:
53 Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
and ye shall take possession of the land, and dwell therein: for unto you have I given the land to possess it.
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
And ye shall inherit the land by lot according to your families; to the more ye shall give the more inheritance, and to the fewer thou shalt give the less inheritance: wheresoever the lot falleth to any man, that shall be his; according to the tribes of your fathers shall ye inherit.
55 “‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
But if ye will not drive out the inhabitants of the land from before you; then shall those which ye let remain of them be as pricks in your eyes, and as thorns in your sides, and they shall vex you in the land wherein ye dwell.
56 Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”
And it shall come to pass, that as I thought to do unto them, so will I do unto you.

< Hesabu 33 >