< Hesabu 33 >

1 Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
These are the journeys of the children of Israel, which went forth out of the land of Egypt with their armies under the hand of Moses and Aaron.
2 Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
And Moses wrote their goings out according to their journeys by the commandment of the LORD: and these are their journeys according to their goings out.
3 Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
And they departed from Rameses in the first month, on the fifteenth day of the first month; on the morrow after the passover the children of Israel went out with an high hand in the sight of all the Egyptians.
4 waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
For the Egyptians buried all their firstborn, which the LORD had smitten among them: on their gods also the LORD executed judgments.
5 Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
And the children of Israel removed from Rameses, and pitched in Succoth.
6 Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
And they departed from Succoth, and pitched in Etham, which is in the edge of the wilderness.
7 Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
And they removed from Etham, and turned again to Pihahiroth, which is before Baalzephon: and they pitched before Migdol.
8 Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
And they departed from before Pihahiroth, and passed through the middle of the sea into the wilderness, and went three days’ journey in the wilderness of Etham, and pitched in Marah.
9 Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
And they removed from Marah, and came to Elim: and in Elim were twelve fountains of water, and three score and ten palm trees; and they pitched there.
10 Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
And they removed from Elim, and encamped by the Red sea.
11 Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
And they removed from the Red sea, and encamped in the wilderness of Sin.
12 Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
And they took their journey out of the wilderness of Sin, and encamped in Dophkah.
13 Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
And they departed from Dophkah, and encamped in Alush.
14 Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
And they removed from Alush, and encamped at Rephidim, where was no water for the people to drink.
15 Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
And they departed from Rephidim, and pitched in the wilderness of Sinai.
16 Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
And they removed from the desert of Sinai, and pitched at Kibrothhattaavah.
17 Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
And they departed from Kibrothhattaavah, and encamped at Hazeroth.
18 Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
And they departed from Hazeroth, and pitched in Rithmah.
19 Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
And they departed from Rithmah, and pitched at Rimmonparez.
20 Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
And they departed from Rimmonparez, and pitched in Libnah.
21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
And they removed from Libnah, and pitched at Rissah.
22 Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
And they journeyed from Rissah, and pitched in Kehelathah.
23 Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
And they went from Kehelathah, and pitched in mount Shapher.
24 Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
And they removed from mount Shapher, and encamped in Haradah.
25 Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
And they removed from Haradah, and pitched in Makheloth.
26 Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
And they removed from Makheloth, and encamped at Tahath.
27 Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
And they departed from Tahath, and pitched at Tarah.
28 Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
And they removed from Tarah, and pitched in Mithcah.
29 Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
And they went from Mithcah, and pitched in Hashmonah.
30 Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
And they departed from Hashmonah, and encamped at Moseroth.
31 Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
And they departed from Moseroth, and pitched in Benejaakan.
32 Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
And they removed from Benejaakan, and encamped at Horhagidgad.
33 Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
And they went from Horhagidgad, and pitched in Jotbathah.
34 Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
And they removed from Jotbathah, and encamped at Ebronah.
35 Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
And they departed from Ebronah, and encamped at Eziongaber.
36 Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
And they removed from Eziongaber, and pitched in the wilderness of Zin, which is Kadesh.
37 Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
And they removed from Kadesh, and pitched in mount Hor, in the edge of the land of Edom.
38 Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
And Aaron the priest went up into mount Hor at the commandment of the LORD, and died there, in the fortieth year after the children of Israel were come out of the land of Egypt, in the first day of the fifth month.
39 Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
And Aaron was an hundred and twenty and three years old when he died in mount Hor.
40 Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
And king Arad the Canaanite, which dwelled in the south in the land of Canaan, heard of the coming of the children of Israel.
41 Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
And they departed from mount Hor, and pitched in Zalmonah.
42 Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
And they departed from Zalmonah, and pitched in Punon.
43 Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
And they departed from Punon, and pitched in Oboth.
44 Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
And they departed from Oboth, and pitched in Ijeabarim, in the border of Moab.
45 Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
And they departed from Iim, and pitched in Dibongad.
46 Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
And they removed from Dibongad, and encamped in Almondiblathaim.
47 Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
And they removed from Almondiblathaim, and pitched in the mountains of Abarim, before Nebo.
48 Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
And they departed from the mountains of Abarim, and pitched in the plains of Moab by Jordan near Jericho.
49 Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
And they pitched by Jordan, from Bethjesimoth even to Abelshittim in the plains of Moab.
50 Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
And the LORD spoke to Moses in the plains of Moab by Jordan near Jericho, saying,
51 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
Speak to the children of Israel, and say to them, When you are passed over Jordan into the land of Canaan;
52 wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
Then you shall drive out all the inhabitants of the land from before you, and destroy all their pictures, and destroy all their molten images, and quite pluck down all their high places:
53 Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
And you shall dispossess the inhabitants of the land, and dwell therein: for I have given you the land to possess it.
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
And you shall divide the land by lot for an inheritance among your families: and to the more you shall give the more inheritance, and to the fewer you shall give the less inheritance: every man’s inheritance shall be in the place where his lot falls; according to the tribes of your fathers you shall inherit.
55 “‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
But if you will not drive out the inhabitants of the land from before you; then it shall come to pass, that those which you let remain of them shall be pricks in your eyes, and thorns in your sides, and shall vex you in the land wherein you dwell.
56 Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”
Moreover it shall come to pass, that I shall do to you, as I thought to do to them.

< Hesabu 33 >