< Hesabu 33 >
1 Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
These are the lodging places of the sons of Israel, who departed from Egypt by their companies under the hand of Moses and Aaron,
2 Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
which Moses wrote down according to the places of the encampments, which they changed upon the order of the Lord.
3 Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
Thus the sons of Israel set out from Rameses in the first month, on the fifteenth day of the first month, on the day after the Passover, with an exalted hand, being seen by all the Egyptians.
4 waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
And these were burying their firstborn, whom the Lord had struck down (for so, too, did he carry out retribution against their gods).
5 Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
And they made camp at Soccoth.
6 Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
And from Soccoth they went to Etham, which is at the furthest limits of the wilderness.
7 Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
Departing from there, they arrived opposite Pi-hahiroth, which looks out toward Baal-zephon, and they were encamped before Migdol.
8 Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
And setting out from Pi-hahiroth, they crossed through the middle of the Sea into the wilderness. And having walked for three days through the desert of Etham, they made camp at Marah.
9 Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
And setting out from Marah, they arrived at Elim, where there were twelve fountains of water and seventy palm trees. And they set up camp there.
10 Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
But departing from there also, they fixed their tents above the Red Sea. And setting out from the Red Sea,
11 Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
they were encamped in the desert of Sin.
12 Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
Departing from there, they went to Dophkah.
13 Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
And setting out from Dophkah, they made camp at Alush.
14 Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
And departing from Alush, they fixed their tents at Rephidim, where the people lacked water to drink.
15 Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
And setting out from Rephidim, they camped in the desert of Sinai.
16 Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
But departing also from the wilderness of the Sinai, they arrived at the Graves of Lust.
17 Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
And setting out from the Graves of Lust, they were encamped at Hazeroth.
18 Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
And from Hazeroth, they went to Rithmah.
19 Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
And setting out from Rithmah, they made camp at Rimmon-perez.
20 Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
And departing from there, they arrived at Libnah.
21 Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
From Libnah, they made camp at Rissah.
22 Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
And departing from Rissah, they went to Kehelathah.
23 Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
Setting out from there, they were encamped at mount Shepher.
24 Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
Departing from mount Shepher, they went to Haradah.
25 Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
Continuing on from there, they made camp at Makheloth.
26 Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
And setting out from Makheloth, they went to Tahath.
27 Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
From Tahath, they made camp at Terah.
28 Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
Departing from there, they pitched their tents at Mithkah.
29 Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
And from Mithkah, they were encamped at Hashmonah.
30 Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
And setting out from Hashmonah, they went to Moseroth.
31 Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
And from Moseroth, they made camp at Bene-jaakan.
32 Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
And setting out from Bene-jaakan, they went to mount Gidgad.
33 Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
Setting out from there, they were encamped at Jotbathah.
34 Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
And from Jotbathah, they went to Abronah.
35 Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
And departing from Abronah, they made camp at Eziongeber.
36 Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
Setting out from there, they went into the desert of Sin, which is Kadesh.
37 Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
And departing from Kadesh, they encamped at mount Hor, at the furthermost limits of the land of Edom.
38 Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
And Aaron the priest ascended onto mount Hor, by the order of the Lord. And there he died, in the fortieth year of the departure of the sons of Israel from Egypt, in the fifth month, on the first day of the month,
39 Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
when he was one hundred twenty-three years old.
40 Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
And king Arad the Canaanite, who lived toward the south, heard that the sons of Israel had arrived in the land of Canaan.
41 Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
And setting out from mount Hor, they made camp at Zalmonah.
42 Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
Departing from there, they went to Punon.
43 Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
And setting out from Punon, they were encamped at Oboth.
44 Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
And from Oboth, they went to Iye-abarim, which is at the borders of the Moabites.
45 Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
And setting out from Iye-abarim, they fixed their tents at Dibon-gad.
46 Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
Departing from there, they made camp at Almon-diblathaim.
47 Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
And departing from Almon-diblathaim, they went to the mountains of Abarim, opposite Nebo.
48 Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
And setting out from the mountains of Abarim, they crossed over to the plains of Moab, above the Jordan, opposite Jericho.
49 Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
And they made camp there, from Beth-jeshimoth all the way to Abel-shittim, in the level places of the Moabites,
50 Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
where the Lord said to Moses:
51 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
“Instruct the sons of Israel, and say to them: When you will have crossed over the Jordan, entering into the land of Canaan,
52 wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
destroy all the inhabitants of that land. Break their monuments, and shatter their statues, and lay waste to every exalted thing,
53 Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
cleansing the land and living in it. For I have given it you as a possession,
54 Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
which you shall divide among you by lot. To the greater number you shall give more, and to the lesser number, less. To each one, just as the lot shall fall, so shall the inheritance be distributed. The possession shall be divided by the tribes and families.
55 “‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
But if you are not willing to put to death the inhabitants of the land, those who remain shall be to you like spikes in your eyes and lances in your sides, and they shall be adversaries to you in the land of your habitation.
56 Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”
And whatever I had decided to do to them, I will do to you.”