< Hesabu 31 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Et l’Éternel parla à Moïse, disant:
2 “Uwalipize kisasi Wamidiani kwa ajili ya Waisraeli. Halafu baada ya hayo, utakufa.”
Exécute la vengeance des fils d’Israël sur les Madianites; ensuite tu seras recueilli vers tes peuples.
3 Kwa hiyo Mose akawaambia watu, “Waandaeni baadhi ya wanaume wenu waende vitani kupigana na Wamidiani ili wawalipize kisasi cha Bwana.
Et Moïse parla au peuple, disant: Équipez d’entre vous des hommes pour l’armée, afin qu’ils marchent contre Madian, pour exécuter la vengeance de l’Éternel sur Madian.
4 Peleka wanaume 1,000 vitani kutoka kila kabila la Israeli.”
Vous enverrez à l’armée 1 000 [hommes] par tribu, de toutes les tribus d’Israël.
5 Kwa hiyo waliandaliwa wanaume 12,000 kwa vita, wanaume 1,000 kutoka kila kabila, walitolewa kutoka koo za Israeli.
Et on détacha d’entre les milliers d’Israël 1 000 [hommes] par tribu, 12 000 [hommes] équipés en guerre;
6 Mose aliwatuma vitani, watu 1,000 kutoka kila kabila, pamoja na Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, ambaye alichukua vyombo vya mahali patakatifu na tarumbeta za kuashiria.
et Moïse les envoya à l’armée, 1 000 par tribu, à la guerre, eux et Phinées, fils d’Éléazar, le sacrificateur; et il avait en sa main les ustensiles du lieu saint, savoir les trompettes au son éclatant.
7 Walipigana dhidi ya Wamidiani, kama Bwana alivyomwagiza Mose, nao waliua kila mwanaume.
Et ils firent la guerre contre Madian, comme l’Éternel l’avait commandé à Moïse, et ils tuèrent tous les mâles.
8 Miongoni mwa watu waliouawa walikuwepo wafalme watano wa Midiani, nao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba. Vilevile walimuua Balaamu mwana wa Beori kwa upanga.
Et ils tuèrent les rois de Madian, outre ceux qui leur furent tués, Évi, et Rékem, et Tsur, et Hur, et Réba, cinq rois de Madian; et ils tuèrent par l’épée Balaam, fils de Béor.
9 Waisraeli waliwateka wanawake wa Kimidiani pamoja na watoto wao na walichukua makundi ya ngʼombe, kondoo na mali zao kama nyara.
Et les fils d’Israël emmenèrent captives les femmes de Madian et leurs petits enfants, et pillèrent tout leur bétail et tous leurs troupeaux et tout leur bien;
10 Walichoma moto miji yote ambayo Wamidiani walikuwa wanaishi, pamoja na kambi zao zote.
et ils brûlèrent par le feu toutes les villes de leurs habitations, et tous leurs campements;
11 Walichukua nyara zote na mateka, pamoja na watu na wanyama,
et ils emportèrent tout le butin et tout ce qu’ils avaient pris, en hommes et en bêtes;
12 nao waliwaleta wafungwa mateka na nyara kwa Mose na kwa kuhani Eleazari, nao Waisraeli walikusanyika kwenye kambi zao katika tambarare za nchi ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
et ils amenèrent les captifs, et ce qu’ils avaient pris, et le butin, à Moïse et à Éléazar, le sacrificateur, et à l’assemblée des fils d’Israël, au camp, dans les plaines de Moab, qui sont auprès du Jourdain de Jéricho.
13 Mose, kuhani Eleazari na viongozi wote wa jumuiya wakatoka kuwalaki nje ya kambi.
Et Moïse et Éléazar, le sacrificateur, et tous les princes de l’assemblée, sortirent à leur rencontre, hors du camp.
14 Mose aliwakasirikia maafisa wa jeshi, yaani hao wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, ambao walirudi kutoka vitani.
Et Moïse se mit en colère contre les commandants de l’armée, les chefs de milliers et les chefs de centaines, qui revenaient du service de la guerre.
15 Mose akawauliza, “Je, mmewaacha wanawake wote hai?”
Et Moïse leur dit: Avez-vous laissé en vie toutes les femmes?
16 “Wanawake hao ndio waliofuata ushauri wa Balaamu, nao ndio waliowasababisha Waisraeli wamwasi Bwana kwa kile kilichotokea kule Peori, na kwa hiyo pigo liliwapata watu wa Bwana.
Voici, ce sont elles qui, à la parole de Balaam, ont donné occasion aux fils d’Israël de commettre une infidélité contre l’Éternel, dans l’affaire de Péor, et il y eut une plaie sur l’assemblée de l’Éternel.
17 Sasa waue wavulana wote. Pia muue kila mwanamke ambaye alikwisha fanya tendo la ndoa,
Et maintenant, tuez tous les mâles parmi les enfants, et tuez toute femme qui a connu un homme, en couchant avec lui;
18 lakini mwacheni hai kwa ajili yenu kila msichana ambaye kamwe hajawahi kuzini na mwanaume.
et vous laisserez en vie, pour vous, tous les enfants, les jeunes filles qui n’ont pas eu compagnie d’homme.
19 “Ninyi nyote ambao mmeua mtu yeyote au kumgusa mtu yeyote ambaye ameuawa, lazima mkae nje ya kambi kwa muda wa siku saba. Katika siku ya tatu na ya saba lazima mjitakase wenyewe pamoja na wafungwa wenu.
Et vous, demeurez hors du camp, sept jours, quiconque aura tué un homme, et quiconque aura touché quelqu’un de tué; vous vous purifierez le troisième jour et le septième jour, vous et vos captifs.
20 Takaseni kila vazi pamoja na kila kitu kilichotengenezwa kwa ngozi, kwa singa za mbuzi au kwa mti.”
Et vous purifierez tout vêtement, et tout objet [fait] de peau, et tout ouvrage en poil de chèvres, et tout ustensile de bois.
21 Kisha kuhani Eleazari aliwaambia askari waliokuwa wamekwenda vitani, “Haya ndiyo matakwa ya sheria ambayo Bwana alimpa Mose:
Et Éléazar, le sacrificateur, dit aux hommes de l’armée, qui étaient allés à la guerre: C’est ici le statut de la loi que l’Éternel a commandée à Moïse:
22 Dhahabu, fedha, shaba, chuma, bati, risasi,
L’or, et l’argent, l’airain, le fer, l’étain, et le plomb,
23 na kitu kingine chochote ambacho kinaweza kuhimili moto lazima mkipitishe kwenye moto, kisha kitakuwa safi. Lakini ni lazima pia kitakaswe kwa maji ya utakaso. Kitu chochote kisichoweza kuhimili moto lazima kipitishwe kwenye yale maji ya utakaso.
tout ce qui peut supporter le feu, vous le ferez passer par le feu, et ce sera pur; seulement, on le purifiera avec l’eau de séparation; et tout ce qui ne peut pas supporter le feu, vous le ferez passer par l’eau.
24 Katika siku ya saba fueni nguo zenu, nanyi mtakuwa safi. Kisha mtaweza kuingia kambini.”
Et vous laverez vos vêtements le septième jour, et vous serez purs; et, après cela, vous entrerez dans le camp.
25 Bwana akamwambia Mose,
Et l’Éternel parla à Moïse, disant:
26 “Wewe na kuhani Eleazari pamoja na viongozi wa jamaa ya jumuiya mtahesabu watu wote na wanyama ambao walitekwa.
Relève la somme de ce qui a été pris et mené captif, en hommes et en bêtes, toi et Éléazar, le sacrificateur, et les chefs des pères de l’assemblée;
27 Gawanyeni hizo nyara kati ya askari ambao walishiriki katika vita na kwa jumuiya.
et partage le butin par moitié entre ceux qui ont pris part à la guerre, qui sont allés à l’armée, et toute l’assemblée.
28 Kutoka fungu la wale waliokwenda kupigana vitani, tenga kama ushuru kwa ajili ya Bwana kitu kimoja kati ya kila mia tano, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo au mbuzi.
Et tu lèveras pour l’Éternel un tribut sur les hommes de guerre qui sont allés à l’armée, un sur 500, tant des hommes que du gros bétail, et des ânes, et du menu bétail;
29 Chukua ushuru huu kutoka fungu lao, umpe kuhani Eleazari kama sehemu ya Bwana.
vous le prendrez de leur moitié, et tu le donneras à Éléazar, le sacrificateur, comme offrande élevée à l’Éternel.
30 Kutoka fungu la Waisraeli, chukua kitu kimoja kati ya kila hamsini, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo, mbuzi au wanyama wengine. Hivyo uwape Walawi, ambao wanawajibika kutunza Maskani ya Bwana.”
Et de la moitié qui revient aux fils d’Israël, tu prendras une part sur 50, des hommes, du gros bétail, des ânes, et du menu bétail, de toutes les bêtes, et tu les donneras aux Lévites, qui vaquent au service du tabernacle de l’Éternel.
31 Kwa hiyo Mose na kuhani Eleazari wakafanya kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Et Moïse et Éléazar, le sacrificateur, firent comme l’Éternel l’avait commandé à Moïse.
32 Nyara zilizobaki kutoka mateka ambayo askari walichukua ni kondoo 675,000,
Et ce qui fut pris, le reste du pillage dont le peuple de l’armée s’était emparé, était de 675 000 [têtes de] menu bétail,
33 ngʼombe 72,000,
72 000 [têtes de] gros bétail,
34 punda 61,000,
61 000 ânes,
35 na wanawake 32,000 ambao hawakumjua mume kwa kufanya tendo la ndoa.
et les personnes, les femmes qui n’avaient pas eu compagnie d’homme, en tout, 32 000 âmes.
36 Nusu ya fungu la wale waliokwenda kupigana vitani lilikuwa: Kondoo 337,500
Et la moitié, la part de ceux qui étaient allés à l’armée, fut, en nombre, de 337 500 [têtes de] menu bétail,
37 ambayo ushuru kwa ajili ya Bwana ilikuwa kondoo 675;
– et le tribut pour l’Éternel, du menu bétail, fut de 675;
38 ngʼombe 36,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa ngʼombe 72;
– et 36 000 [têtes de] gros bétail, dont le tribut pour l’Éternel fut de 72;
39 punda 30,500 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa punda 61;
et 30 500 ânes, dont le tribut pour l’Éternel fut de 61;
40 Watu 16,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa watu 32.
et 16 000 personnes, dont le tribut pour l’Éternel fut de 32 âmes.
41 Mose alimpa kuhani Eleazari ushuru kama sehemu ya Bwana, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Et Moïse donna le tribut de l’offrande élevée de l’Éternel à Éléazar, le sacrificateur, comme l’Éternel l’avait commandé à Moïse.
42 Ile nusu iliyokuwa ya Waisraeli, ambayo Mose aliitenga kutoka kwa ile ya watu waliokwenda vitani,
Et de la moitié qui revenait aux fils d’Israël, que Moïse avait séparée [de celle] des hommes qui avaient été à la guerre
43 nusu iliyokuwa ya jumuiya, ilikuwa kondoo 337,500,
(or la moitié qui était à l’assemblée fut de 337 500 [têtes de] menu bétail,
44 ngʼombe 36,000,
36 000 [têtes de] gros bétail,
45 punda 30,500,
30 500 ânes,
46 na wanadamu 16,000.
et 16 000 personnes ), …
47 Kutoka hiyo nusu iliyokuwa ya Waisraeli, Mose alichagua moja kati ya kila hamsini ya wanadamu na wanyama, kama Bwana alivyomwagiza, naye aliwapa Walawi, ambao waliwajibika kutunza Maskani ya Bwana.
de cette moitié qui était aux fils d’Israël, Moïse prit une part sur 50, tant des hommes que du bétail, et les donna aux Lévites, qui vaquent au service du tabernacle de l’Éternel, comme l’Éternel l’avait commandé à Moïse.
48 Kisha maafisa waliokuwa juu ya vikosi vya jeshi, wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, walimwendea Mose
Et ceux qui étaient préposés sur les milliers de l’armée, les chefs de milliers et les chefs de centaines, s’approchèrent de Moïse;
49 na kumwambia, “Watumishi wako wamehesabu askari walio chini ya amri yetu na hakuna hata mmoja aliyekosekana.
et ils dirent à Moïse: Tes serviteurs ont relevé la somme des hommes de guerre qui sont sous notre main, et il ne manque pas un seul homme d’entre nous.
50 Kwa hiyo tumeleta kama sadaka kwa Bwana vyombo vya dhahabu kila mmoja wetu alivyopata, yaani vikuku, bangili, pete za muhuri, vipuli na mikufu, ili kufanya upatanisho kwa ajili yetu mbele za Bwana.”
Et nous présentons une offrande à l’Éternel, chacun ce qu’il a trouvé, des objets d’or, des bracelets pour les bras, et des bracelets pour les mains, des anneaux, des pendants d’oreilles, et des colliers, afin de faire propitiation pour nos âmes devant l’Éternel.
51 Mose na kuhani Eleazari wakapokea kutoka kwao dhahabu, yaani vyombo vyote vilivyonakshiwa.
Et Moïse et Éléazar, le sacrificateur, prirent d’eux cet or, tous les objets ouvragés.
52 Dhahabu yote kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia ambavyo Mose na kuhani Eleazari walimletea Bwana kama zawadi ilikuwa shekeli 16,750
Et tout l’or de l’offrande élevée, qu’ils avaient offert à l’Éternel, fut de 16 750 sicles, de la part des chefs de milliers et des chefs de centaines;
53 Kila askari alikuwa amejichukulia nyara zake binafsi.
(les hommes de l’armée avaient pillé chacun pour soi).
54 Mose na kuhani Eleazari walipokea dhahabu kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, wakazileta katika Hema la Kukutania kama ukumbusho kwa Waisraeli mbele za Bwana.
Et Moïse et Éléazar, le sacrificateur, prirent l’or des chefs de milliers et des chefs de centaines, et l’apportèrent à la tente d’assignation, comme mémorial pour les fils d’Israël, devant l’Éternel.

< Hesabu 31 >