< Hesabu 30 >

1 Mose akawaambia viongozi wa makabila ya Israeli: “Hili ndilo Bwana analoagiza:
And Moses spoke to the heads of the tribes concerning the children of Israel, saying, This [is] the thing which the LORD hath commanded.
2 Mwanaume awekapo nadhiri kwa Bwana, au anapoapa kujifunga kwa ahadi, kamwe asitangue neno lake, bali ni lazima afanye kila kitu alichosema.
If a man shall vow a vow to the LORD, or swear an oath to bind his soul with a bond; he shall not break his word; he shall do according to all that proceedeth out of his mouth.
3 “Wakati mwanamwali anayeishi bado nyumbani kwa baba yake atakapoweka nadhiri kwa Bwana, ama amejifunga mwenyewe kwa ahadi,
If a woman also shall vow a vow to the LORD, and bind [herself] by a bond, [being] in her father's house in her youth;
4 na baba yake akasikia kuhusu nadhiri au ahadi yake lakini asimwambie lolote, ndipo nadhiri zake zote na kila ahadi aliyoiweka na kujifunga kwayo itathibitika.
And her father shall hear her vow, and her bond with which she hath bound her soul, and her father shall hold his peace at her: then all her vows shall stand, and every bond with which she hath bound her soul shall stand.
5 Lakini kama baba yake akimkataza wakati anapoisikia, hakuna nadhiri wala ahadi yake yoyote aliyojifunga kwayo itakayosimama; Bwana atamweka huru huyo mwanamwali kwa sababu baba yake amemkataza.
But if her father shall disallow her in the day that he heareth; not any of her vows or of her bonds with which she hath bound her soul shall stand: and the LORD shall forgive her, because her father disallowed her.
6 “Ikiwa ataolewa baada ya kuweka nadhiri au baada ya midomo yake kutamka ahadi fulani bila kufikiri akawa amejifunga hivyo,
And if she had a husband when she vowed, or uttered aught from her lips, with which she bound her soul;
7 na mume wake akasikia habari hiyo asimwambie neno lolote, ndipo nadhiri zake ama ahadi zake ambazo alikuwa amejifunga nazo zitathibitika.
And her husband heard [it], and held his peace at her in the day that he heard [it]: then her vows shall stand, and her bonds with which she bound her soul shall stand.
8 Lakini ikiwa mume wake atamkataza atakaposikia kuhusu hilo, atakuwa ametangua nadhiri ambazo zilikuwa zimemfunga mkewe, ama ahadi aliyotamka pasipo kufikiri ambayo amejifunga kwayo, naye Bwana atamweka huru yule mwanamke.
But if her husband disallowed her on the day that he heard [it]; then he shall make of no effect her vow which she vowed, and that which she uttered with her lips, with which she bound her soul: and the LORD shall forgive her.
9 “Nadhiri yoyote ama patano ambalo limefanywa na mjane ama mwanamke aliyeachwa vitakuwa vimemfunga.
But every vow of a widow, and of her that is divorced, with which they have bound their souls, shall stand against her.
10 “Ikiwa mwanamke anayeishi na mumewe ataweka nadhiri ama kujifunga mwenyewe kwa ahadi chini ya kiapo,
And if she vowed in her husband's house, or bound her soul by a bond with an oath;
11 na mumewe akasikia kuhusu jambo hili lakini asimwambie lolote wala hakumkataza, ndipo viapo vyake vyote au ahadi zinazomfunga zitakapothibitika.
And her husband heard [it], and held his peace at her, [and] disallowed her not: then all her vows shall stand, and every bond with which she bound her soul shall stand.
12 Lakini ikiwa mumewe atabatilisha nadhiri hizo baada ya kuzisikia, basi hakuna nadhiri au ahadi zozote alizoziweka kwa midomo yake zitakazothibitika. Mumewe atakuwa amezibatilisha, na Bwana atamweka huru yule mwanamke.
But if her husband hath utterly made them void on the day he heard [them]; [then] whatever proceeded out of her lips concerning her vows, or concerning the bond of her soul, shall not stand: her husband hath made them void; and the LORD shall forgive her.
13 Mumewe anaweza kuthibitisha au kutangua nadhiri yoyote anayoweka, au ahadi yoyote aliyoweka kwa kuapa ili kujikana mwenyewe.
Every vow, and every binding oath to afflict the soul, her husband may establish it, or her husband may make it void.
14 Lakini ikiwa mumewe hasemi lolote kwake kuhusu jambo hilo siku baada ya siku, basi mumewe atakuwa amethibitisha nadhiri zote, na ahadi zote zinazomfunga mkewe. Anavithibitisha kwa kutokusema lolote kwa mkewe anapoyasikia hayo.
But if her husband altogether holds his peace at her from day to day; then he establisheth all her vows, or all her bonds, which [are] upon her: he confirmeth them, because he held his peace at her in the day that he heard [them].
15 Hata hivyo, ikiwa mumewe atavibatilisha baada ya kusikia hayo, basi atawajibika kwa hatia ya mkewe.”
But if he shall any way make them void after that he hath heard [them]; then he shall bear her iniquity.
16 Haya ndiyo masharti ambayo Bwana alimpa Mose kuhusu mahusiano kati ya mtu na mkewe, na kati ya baba na binti yake ambaye bado anaishi nyumbani kwa baba yake.
These [are] the statutes which the LORD commanded Moses, between a man and his wife, between the father and his daughter, [being yet] in her youth in her father's house.

< Hesabu 30 >