< Hesabu 30 >
1 Mose akawaambia viongozi wa makabila ya Israeli: “Hili ndilo Bwana analoagiza:
Moses spoke to the leaders of the tribes of the people of Israel. He said, “This is what Yahweh has commanded.
2 Mwanaume awekapo nadhiri kwa Bwana, au anapoapa kujifunga kwa ahadi, kamwe asitangue neno lake, bali ni lazima afanye kila kitu alichosema.
When anyone makes a vow to Yahweh, or swears an oath to bind himself with a promise, he must not break his word. He must keep his promise to do everything that comes out of his mouth.
3 “Wakati mwanamwali anayeishi bado nyumbani kwa baba yake atakapoweka nadhiri kwa Bwana, ama amejifunga mwenyewe kwa ahadi,
When a young woman living in her father's house makes a vow to Yahweh and binds herself with a promise,
4 na baba yake akasikia kuhusu nadhiri au ahadi yake lakini asimwambie lolote, ndipo nadhiri zake zote na kila ahadi aliyoiweka na kujifunga kwayo itathibitika.
if her father hears the vow and the promise by which she has bound herself, and if he says nothing to reverse her, then all her vows will remain in force. Every promise by which she has bound herself will remain in force.
5 Lakini kama baba yake akimkataza wakati anapoisikia, hakuna nadhiri wala ahadi yake yoyote aliyojifunga kwayo itakayosimama; Bwana atamweka huru huyo mwanamwali kwa sababu baba yake amemkataza.
But if her father hears about her vow and her promise, and if he says nothing to her, then all the vows and promises that she took on herself will remain in force.
6 “Ikiwa ataolewa baada ya kuweka nadhiri au baada ya midomo yake kutamka ahadi fulani bila kufikiri akawa amejifunga hivyo,
However, if her father hears all the vows she made and her solemn promises with which she has bound herself, and if he overrules her on that same day, then they will not remain in force. Yahweh will forgive her because her father had overruled her.
7 na mume wake akasikia habari hiyo asimwambie neno lolote, ndipo nadhiri zake ama ahadi zake ambazo alikuwa amejifunga nazo zitathibitika.
If she marries a man while she is under those vows, or if she makes rash promises with which she obligates herself, those obligations will remain in force.
8 Lakini ikiwa mume wake atamkataza atakaposikia kuhusu hilo, atakuwa ametangua nadhiri ambazo zilikuwa zimemfunga mkewe, ama ahadi aliyotamka pasipo kufikiri ambayo amejifunga kwayo, naye Bwana atamweka huru yule mwanamke.
But if her husband stops her on the day that he hears about it, then he cancels the vow that she has made, the rash talk of her lips with which she has bound herself. Yahweh will release her.
9 “Nadhiri yoyote ama patano ambalo limefanywa na mjane ama mwanamke aliyeachwa vitakuwa vimemfunga.
But as for a widow or a divorced woman, everything by which she has bound herself will remain in force against her.
10 “Ikiwa mwanamke anayeishi na mumewe ataweka nadhiri ama kujifunga mwenyewe kwa ahadi chini ya kiapo,
If a woman made a vow in her husband's house or obligates herself by taking an oath,
11 na mumewe akasikia kuhusu jambo hili lakini asimwambie lolote wala hakumkataza, ndipo viapo vyake vyote au ahadi zinazomfunga zitakapothibitika.
and her husband hears of it, but he says nothing to her and he does oppose her, then all her vows must stand and the obligations she made must remain in force.
12 Lakini ikiwa mumewe atabatilisha nadhiri hizo baada ya kuzisikia, basi hakuna nadhiri au ahadi zozote alizoziweka kwa midomo yake zitakazothibitika. Mumewe atakuwa amezibatilisha, na Bwana atamweka huru yule mwanamke.
But if her husband cancels them on the day that he heard about them, then whatever came out of her lips about her vows or promises will not remain in force. Her husband has canceled them. Yahweh will release her.
13 Mumewe anaweza kuthibitisha au kutangua nadhiri yoyote anayoweka, au ahadi yoyote aliyoweka kwa kuapa ili kujikana mwenyewe.
Every vow or oath a woman takes that binds her to deny herself something may be confirmed or canceled by her husband.
14 Lakini ikiwa mumewe hasemi lolote kwake kuhusu jambo hilo siku baada ya siku, basi mumewe atakuwa amethibitisha nadhiri zote, na ahadi zote zinazomfunga mkewe. Anavithibitisha kwa kutokusema lolote kwa mkewe anapoyasikia hayo.
But if he says nothing at all to her day after day, then he confirms all her vows and binding promises that she has made. He has confirmed them because he has said nothing to her at the time that he heard about them.
15 Hata hivyo, ikiwa mumewe atavibatilisha baada ya kusikia hayo, basi atawajibika kwa hatia ya mkewe.”
If her husband tries to cancel his wife's vow a long time after he has heard about it, then he will be responsible for her sin.”
16 Haya ndiyo masharti ambayo Bwana alimpa Mose kuhusu mahusiano kati ya mtu na mkewe, na kati ya baba na binti yake ambaye bado anaishi nyumbani kwa baba yake.
These are the statutes that Yahweh commanded Moses to announce—statutes for what is between a man and his wife and between a father and his daughter when she is in her youth in her father's family.