< Hesabu 30 >

1 Mose akawaambia viongozi wa makabila ya Israeli: “Hili ndilo Bwana analoagiza:
Moses told the tribal leaders of Israel, “This is what the Lord commands:
2 Mwanaume awekapo nadhiri kwa Bwana, au anapoapa kujifunga kwa ahadi, kamwe asitangue neno lake, bali ni lazima afanye kila kitu alichosema.
If a man makes a solemn promise to the Lord, or pledges to do something by swearing an oath, he must not break his promise. He must do everything he said he would.
3 “Wakati mwanamwali anayeishi bado nyumbani kwa baba yake atakapoweka nadhiri kwa Bwana, ama amejifunga mwenyewe kwa ahadi,
If a woman who's young and still living in her father's house makes a solemn promise to the Lord or pledges to do something by swearing an oath
4 na baba yake akasikia kuhusu nadhiri au ahadi yake lakini asimwambie lolote, ndipo nadhiri zake zote na kila ahadi aliyoiweka na kujifunga kwayo itathibitika.
and her father finds out about her promise or pledge but doesn't say anything to her, all the promises or pledges she has sworn to do will stand.
5 Lakini kama baba yake akimkataza wakati anapoisikia, hakuna nadhiri wala ahadi yake yoyote aliyojifunga kwayo itakayosimama; Bwana atamweka huru huyo mwanamwali kwa sababu baba yake amemkataza.
But if her father disallows them as soon as he finds out, then none of her promises or pledges remain valid. The Lord will release her from keeping them because her father has disallowed them.
6 “Ikiwa ataolewa baada ya kuweka nadhiri au baada ya midomo yake kutamka ahadi fulani bila kufikiri akawa amejifunga hivyo,
If a woman marries after having made a solemn promise or sworn an oath without thinking
7 na mume wake akasikia habari hiyo asimwambie neno lolote, ndipo nadhiri zake ama ahadi zake ambazo alikuwa amejifunga nazo zitathibitika.
and her husband finds out about it but doesn't say anything to her right away, all the promises or pledges she has sworn to do will stand.
8 Lakini ikiwa mume wake atamkataza atakaposikia kuhusu hilo, atakuwa ametangua nadhiri ambazo zilikuwa zimemfunga mkewe, ama ahadi aliyotamka pasipo kufikiri ambayo amejifunga kwayo, naye Bwana atamweka huru yule mwanamke.
But if her husband disallows them when he finds out about it, then none of her promises or oaths remain valid and the Lord will release her from keeping them.
9 “Nadhiri yoyote ama patano ambalo limefanywa na mjane ama mwanamke aliyeachwa vitakuwa vimemfunga.
Every solemn promise made by a widow or a woman who is divorced must be kept.
10 “Ikiwa mwanamke anayeishi na mumewe ataweka nadhiri ama kujifunga mwenyewe kwa ahadi chini ya kiapo,
If a woman living with her husband makes a solemn promise to the Lord or pledges to do something by swearing an oath,
11 na mumewe akasikia kuhusu jambo hili lakini asimwambie lolote wala hakumkataza, ndipo viapo vyake vyote au ahadi zinazomfunga zitakapothibitika.
and her husband finds out about her promise or pledge but doesn't say anything to her and doesn't disallow them, then none of her promises or pledges remain valid.
12 Lakini ikiwa mumewe atabatilisha nadhiri hizo baada ya kuzisikia, basi hakuna nadhiri au ahadi zozote alizoziweka kwa midomo yake zitakazothibitika. Mumewe atakuwa amezibatilisha, na Bwana atamweka huru yule mwanamke.
But if her husband disallows them as soon as he finds out about it, then none of her promises or oaths remain valid. The Lord will release her from keeping them because her husband has disallowed them.
13 Mumewe anaweza kuthibitisha au kutangua nadhiri yoyote anayoweka, au ahadi yoyote aliyoweka kwa kuapa ili kujikana mwenyewe.
Her husband may also confirm or disallow any solemn promise or pledge the woman may make for self-denial.
14 Lakini ikiwa mumewe hasemi lolote kwake kuhusu jambo hilo siku baada ya siku, basi mumewe atakuwa amethibitisha nadhiri zote, na ahadi zote zinazomfunga mkewe. Anavithibitisha kwa kutokusema lolote kwa mkewe anapoyasikia hayo.
But if her husband doesn't ever say a word to her about it, then he is assumed to have confirmed all the solemn promises and pledges she has made.
15 Hata hivyo, ikiwa mumewe atavibatilisha baada ya kusikia hayo, basi atawajibika kwa hatia ya mkewe.”
However, if he disallows them some time later after finding out about them, then he will bear the responsibility for her breaking them.”
16 Haya ndiyo masharti ambayo Bwana alimpa Mose kuhusu mahusiano kati ya mtu na mkewe, na kati ya baba na binti yake ambaye bado anaishi nyumbani kwa baba yake.
These are the regulations that the Lord gave to Moses regarding the relationship between a man and his wife, and between a father and a daughter who is young and still living at home.

< Hesabu 30 >