< Hesabu 30 >
1 Mose akawaambia viongozi wa makabila ya Israeli: “Hili ndilo Bwana analoagiza:
And Moses said to the heads of the tribes of the children of Israel, This is the order of the Lord.
2 Mwanaume awekapo nadhiri kwa Bwana, au anapoapa kujifunga kwa ahadi, kamwe asitangue neno lake, bali ni lazima afanye kila kitu alichosema.
When a man takes an oath to the Lord, or gives an undertaking having the force of an oath, let him not go back from his word, but let him do whatever he has said he will do.
3 “Wakati mwanamwali anayeishi bado nyumbani kwa baba yake atakapoweka nadhiri kwa Bwana, ama amejifunga mwenyewe kwa ahadi,
If a woman, being young and under the authority of her father, takes an oath to the Lord or gives an undertaking;
4 na baba yake akasikia kuhusu nadhiri au ahadi yake lakini asimwambie lolote, ndipo nadhiri zake zote na kila ahadi aliyoiweka na kujifunga kwayo itathibitika.
If her father, hearing of her oath or the undertaking she has given, says nothing to her, then all her oaths and every undertaking she has given will have force.
5 Lakini kama baba yake akimkataza wakati anapoisikia, hakuna nadhiri wala ahadi yake yoyote aliyojifunga kwayo itakayosimama; Bwana atamweka huru huyo mwanamwali kwa sababu baba yake amemkataza.
But if her father, hearing of it, makes her take back her word, then the oaths or the undertakings she has given will have no force; and she will have forgiveness from the Lord, because her oath was broken by her father.
6 “Ikiwa ataolewa baada ya kuweka nadhiri au baada ya midomo yake kutamka ahadi fulani bila kufikiri akawa amejifunga hivyo,
And if she is married to a husband at the time when she is under an oath or an undertaking given without thought;
7 na mume wake akasikia habari hiyo asimwambie neno lolote, ndipo nadhiri zake ama ahadi zake ambazo alikuwa amejifunga nazo zitathibitika.
If her husband, hearing of it, says nothing to her at the time, then the oaths she made and the undertakings she gave will have force.
8 Lakini ikiwa mume wake atamkataza atakaposikia kuhusu hilo, atakuwa ametangua nadhiri ambazo zilikuwa zimemfunga mkewe, ama ahadi aliyotamka pasipo kufikiri ambayo amejifunga kwayo, naye Bwana atamweka huru yule mwanamke.
But if her husband, hearing of it, makes her take it back, then the oath she made and the undertaking she gave without thought will have no force or effect, and she will have the Lord's forgiveness.
9 “Nadhiri yoyote ama patano ambalo limefanywa na mjane ama mwanamke aliyeachwa vitakuwa vimemfunga.
But an oath made by a widow or one who is no longer married to her husband, and every undertaking she has given, will have force.
10 “Ikiwa mwanamke anayeishi na mumewe ataweka nadhiri ama kujifunga mwenyewe kwa ahadi chini ya kiapo,
If she made an oath while she was under the authority of her husband,
11 na mumewe akasikia kuhusu jambo hili lakini asimwambie lolote wala hakumkataza, ndipo viapo vyake vyote au ahadi zinazomfunga zitakapothibitika.
And her husband, hearing of it, said nothing to her and did not put a stop to it, then all her oaths and every undertaking she gave will have force.
12 Lakini ikiwa mumewe atabatilisha nadhiri hizo baada ya kuzisikia, basi hakuna nadhiri au ahadi zozote alizoziweka kwa midomo yake zitakazothibitika. Mumewe atakuwa amezibatilisha, na Bwana atamweka huru yule mwanamke.
But if her husband, on hearing of it, made them without force or effect, then whatever she has said about her oaths or her undertaking has no force: her husband has made them without effect, and she will have the Lord's forgiveness.
13 Mumewe anaweza kuthibitisha au kutangua nadhiri yoyote anayoweka, au ahadi yoyote aliyoweka kwa kuapa ili kujikana mwenyewe.
Every oath, and every undertaking which she gives, to keep herself from pleasure, may be supported or broken by her husband.
14 Lakini ikiwa mumewe hasemi lolote kwake kuhusu jambo hilo siku baada ya siku, basi mumewe atakuwa amethibitisha nadhiri zote, na ahadi zote zinazomfunga mkewe. Anavithibitisha kwa kutokusema lolote kwa mkewe anapoyasikia hayo.
But if the days go on, and her husband says nothing whatever to her, then he is giving the support of his authority to her oaths and undertakings, because at the time of hearing them he said nothing to her.
15 Hata hivyo, ikiwa mumewe atavibatilisha baada ya kusikia hayo, basi atawajibika kwa hatia ya mkewe.”
But if at some time after hearing of them, he makes them without force, then he is responsible for her wrongdoing.
16 Haya ndiyo masharti ambayo Bwana alimpa Mose kuhusu mahusiano kati ya mtu na mkewe, na kati ya baba na binti yake ambaye bado anaishi nyumbani kwa baba yake.
These are the laws which the Lord gave Moses in relation to a man and his wife, or a father and a young daughter who is under his authority.