< Hesabu 3 >

1 Hii ni hesabu ya jamaa ya Aroni na Mose kwa wakati ambao Bwana alizungumza na Mose katika Mlima Sinai.
Or ce sont ici les générations d'Aaron et de Moïse, au temps que l'Eternel parla à Moïse sur la montagne de Sinaï.
2 Majina ya wana wa Aroni yalikuwa: Nadabu mzaliwa wa kwanza na Abihu, Eleazari na Ithamari.
Et ce sont ici les noms des enfants d'Aaron; Nadab, qui était l'aîné, Abihu, Eléazar, et Ithamar.
3 Hayo yalikuwa majina ya wana wa Aroni, makuhani wapakwa mafuta, waliokuwa wamesimikwa kuhudumu kama makuhani.
Ce sont là les noms des enfants d'Aaron Sacrificateurs, qui furent oints et consacrés pour exercer la Sacrificature.
4 Hata hivyo Nadabu na Abihu walikufa mbele za Bwana walipotoa sadaka kwa moto usioruhusiwa mbele zake katika Jangwa la Sinai. Hawakuwa na wana; kwa hiyo Eleazari na Ithamari walihudumu peke yao kama makuhani wakati wote wa maisha ya Aroni baba yao.
Mais Nadab et Abihu moururent en la présence de l'Eternel, quand ils offrirent un feu étranger devant l'Eternel au désert de Sinaï, et ils n'eurent point d'enfants; mais Eléazar et Ithamar exercèrent la Sacrificature en la présence d'Aaron leur père.
5 Bwana akamwambia Mose,
Et l'Eternel parla à Moïse, en disant:
6 “Walete watu wa kabila la Lawi mbele ya Aroni kuhani ili wamsaidie.
Fais approcher la Tribu de Lévi, et fais qu'elle se tienne devant Aaron Sacrificateur, afin qu'ils le servent.
7 Watafanya huduma kwa ajili yake na kwa jumuiya yote katika Hema la Kukutania kwa kufanya kazi za Maskani.
Et qu'ils aient la charge de ce qu'il leur ordonnera de garder, et de ce que toute l'assemblée leur ordonnera de garder, devant le Tabernacle d'assignation, en faisant le service du Tabernacle.
8 Watatunza samani zote za Hema la Kukutania, wakitimiza wajibu wa kuhudumia Waisraeli kwa kufanya kazi ya Maskani.
Et qu'ils gardent tous les ustensiles du Tabernacle d'assignation, et ce qui leur sera donné en charge par les enfants d'Israël, pour faire le service du Tabernacle.
9 Wakabidhi Walawi kwa Aroni na wanawe; hao ndio Waisraeli ambao wanakabidhiwa kwake kabisa.
Ainsi tu donneras les Lévites à Aaron et à ses fils; ils lui sont absolument donnés d'entre les enfants d'Israël.
10 Waweke Aroni na wanawe kuhudumu kama makuhani; mtu mwingine yeyote atakayesogea mahali patakatifu ni lazima auawe.”
Tu donneras donc la surintendance à Aaron et à ses fils, et ils exerceront leur Sacrificature. Que si quelque étranger en approche, on le fera mourir.
11 Bwana akamwambia Mose,
Et l'Eternel parla à Moïse, en disant:
12 “Nimewatwaa Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli badala ya mzaliwa wa kwanza wa kiume wa kila mwanamke wa Mwisraeli. Walawi ni wangu,
Voici, j'ai pris les Lévites d'entre les enfants d'Israël, au lieu de tout premier-né qui ouvre la matrice entre les enfants d'Israël; c'est pourquoi les Lévites seront à moi.
13 kwa kuwa wazaliwa wote wa kwanza ni wangu. Nilipowaua wazaliwa wa kwanza huko Misri, nilimtenga kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli awe wangu, akiwa mwanadamu au mnyama. Watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.”
Car tout premier-né m'appartient, depuis que je frappai tout premier-né au pays d'Egypte; je me suis sanctifié tout premier-né en Israël, depuis les hommes jusqu'aux bêtes; ils seront à moi, je suis l'Eternel.
14 Bwana akamwambia Mose katika Jangwa la Sinai,
L'Eternel parla aussi à Moïse au désert de Sinaï, en disant:
15 “Wahesabu Walawi kwa jamaa zao na koo zao. Mhesabu kila mwanaume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi.”
Dénombre les enfants de Lévi, par les maisons de leurs pères, [et] par leurs familles, en comptant tout mâle depuis l'âge d'un mois, et au dessus.
16 Kwa hiyo Mose akawahesabu, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
Moïse donc les dénombra selon le commandement de l'Eternel, ainsi qu'il lui avait été commandé.
17 Haya yalikuwa majina ya wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
r ce sont ici les fils de Lévi selon leurs noms: Guerson, Kéhath, et Mérari.
18 Haya ndiyo yaliyokuwa majina ya koo za Wagershoni: Libni na Shimei.
Et ce sont ici les noms des fils de Guerson, selon leurs familles, Libni, et Simhi.
19 Koo za Wakohathi zilikuwa ni: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
Et les fils de Kéhath selon leurs familles, Hamram, Jitshar, Hébron et Huziel.
20 Koo za Wamerari zilikuwa ni: Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi, kufuatana na jamaa zao.
Et les fils de Mérari, selon leurs familles, Mahli et Musi; ce sont là les familles de Lévi, selon les maisons de leurs pères.
21 Kulikuwa na koo za Walibni na Washimei kwa Gershoni; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wagershoni.
De Guerson [est sortie] la famille des Libnites, et la famille des Simhites; ce sont les familles des Guersonites;
22 Idadi ya waume wote waliokuwa na mwezi mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 7,500.
Desquelles ceux dont on fit le dénombrement, après le compte [qui fut fait] de tous les mâles depuis l'âge d'un mois et au dessus, furent au nombre de sept mille cinq cents.
23 Ukoo wa Wagershoni walitakiwa kuweka kambi zao upande wa magharibi, nyuma ya Maskani.
Les familles des Guersonites camperont derrière le Tabernacle à l'Occident.
24 Kiongozi wa jamaa za Wagershoni alikuwa Eliasafu mwana wa Laeli.
Et Eliasaph, fils de Laël, sera le chef de la maison des pères des Guersonites.
25 Katika Hema la Kukutania, Wagershoni walikuwa na wajibu wa kutunza Maskani na hema, vifuniko vyake, pazia katika mlango wa kuingilia ndani ya Hema la Kukutania,
Et les enfants de Guerson auront en charge au Tabernacle d'assignation, la tente, le Tabernacle, sa couverture, la tapisserie de l'entrée du Tabernacle d'assignation;
26 mapazia ya ua, pazia katika ingilio la ua unaozunguka Maskani na madhabahu, pamoja na kamba, na kila kinachohusika kwa matumizi yake.
Et les courtines du parvis avec la tapisserie de l'entrée du parvis, qui servent pour le pavillon et pour l'autel, tout autour, et son cordage, pour tout son service.
27 Kwa Kohathi kulikuwepo koo za Waamramu, Waishari, Wahebroni na Wauzieli; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wakohathi.
Et de Kéhath [est sortie] la famille des Hamramites, la famille des Jitsharites, la famille des Hébronites, et la famille des Huziélites; ce furent là les familles des Kéhathites;
28 Hesabu ya waume wote wenye mwezi mmoja au zaidi ilikuwa watu 8,600. Wakohathi waliwajibika kutunza mahali patakatifu.
Dont tous les mâles depuis l'âge d'un mois, et au dessus, furent au nombre de huit mille six cents, ayant la charge du Sanctuaire.
29 Koo za Wakohathi zilitakiwa kuweka kambi zao upande wa kusini wa Maskani.
Les familles des enfants de Kéhath camperont du côté du Tabernacle vers le Midi.
30 Kiongozi wa jamaa za koo za Wakohathi alikuwa Elisafani mwana wa Uzieli.
Et Elitsaphan, fils de Huziel, [sera] le chef de la maison des pères des familles des Kéhathites.
31 Waliwajibika kutunza Sanduku la Agano, meza, kinara cha taa, madhabahu, na vile vyombo vya mahali patakatifu vinavyotumika kuhudumu, pazia, na kila kitu kinachohusika na matumizi yake.
Et ils auront en charge l'Arche, la Table, le chandelier, les autels, et les ustensiles du Sanctuaire avec lesquels on fait le service, et la tapisserie, avec tout ce qui y sert.
32 Kiongozi mkuu wa Walawi alikuwa Eleazari mwana wa kuhani, Aroni. Aliwekwa juu ya wale waliowajibika kutunza mahali patakatifu.
Et le chef des chefs des Lévites [sera] Eléazar, fils d'Aaron Sacrificateur; qui aura la surintendance sur ceux qui auront la charge du Sanctuaire.
33 Kwa Merari kulikuwa na koo za Wamahli na Wamushi; hizi zilikuwa koo za Merari.
Et de Mérari [est sortie] la famille des Mahlites, et la famille des Musites; ce furent là les familles de Mérari;
34 Hesabu ya waume wote wenye umri wa mwaka mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 6,200.
Desquelles ceux dont on fit le dénombrement [après] le compte [qui fut fait] de tous les mâles, depuis l'âge d'un mois et au dessus, furent six mille deux cents.
35 Kiongozi wa jamaa za koo za Wamerari alikuwa Surieli mwana wa Abihaili; hawa walitakiwa kuweka kambi zao upande wa kaskazini mwa Maskani.
Et Esuriel, fils d'Abihaïl, sera le chef de la maison des pères des familles des Mérarites; ils camperont du côté du Tabernacle vers l'Aquilon.
36 Wamerari waliwekwa kutunza miimo ya Maskani, mataruma yake, nguzo, vitako na vifaa vyake vyote na kila kitu kilichohusika na matumizi yake,
Et on donnera aux enfants de Mérari la charge des ais du Tabernacle, de ses barres, de ses piliers, de ses soubassements, et de tous ses ustensiles, avec tout ce qui y sera;
37 na pia nguzo za ua unaozunguka pamoja na vitako vyake, vigingi vya hema na kamba zake.
Et des piliers du parvis tout autour, avec leurs soubassements, leurs pieux, et leurs cordes.
38 Mose, na Aroni na wanawe walitakiwa kuweka kambi zao mashariki mwa Maskani, kuelekea mawio ya jua, mbele ya Hema la Kukutania. Wao walihusika na utunzaji wa mahali patakatifu kwa niaba ya Waisraeli. Mtu mwingine yeyote aliyepasogelea mahali patakatifu angeuawa.
Et Moïse, et Aaron, et ses fils ayant la charge du Sanctuaire, pour la garde des enfants d'Israël, camperont devant le Tabernacle d'assignation vers l'Orient. Que si quelque étranger en approche, on le fera mourir.
39 Jumla ya hesabu ya Walawi waliohesabiwa na Mose na Aroni kwa amri ya Bwana, kufuatana na koo, pamoja na kila mume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walikuwa 22,000.
Tous ceux des Lévites dont on fit le dénombrement, lesquels Moïse et Aaron comptèrent par leurs familles, suivant le commandement de l'Eternel, tous les mâles de l'âge d'un mois et au dessus, furent de vingt-deux mille.
40 Bwana akamwambia Mose, “Wahesabu wazaliwa wa kwanza wa kiume wote wa Waisraeli wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi na uorodheshe majina yao.
Et l'Eternel dit à Moïse: Fais le dénombrement de tous les premiers-nés mâles des enfants d'Israël, depuis l'âge d'un mois, et au dessus, et lève le compte de leurs noms.
41 Nitwalie Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya wazaliwa wa mifugo ya Waisraeli. Mimi ndimi Bwana.”
Et tu prendras pour moi, je suis l'Eternel, les Lévites, au lieu de tous les premiers-nés qui sont entre les enfants d'Israël; [tu prendras] aussi les bêtes des Lévites, au lieu de tous les premiers-nés des bêtes des enfants d'Israël.
42 Hivyo Mose akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru.
Moïse donc dénombra, comme l'Eternel lui avait commandé, tous les premiers-nés qui étaient entre les enfants d'Israël.
43 Jumla ya hesabu ya wazaliwa wa kwanza waume wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walioorodheshwa kwa majina, walikuwa 22,273.
Et tous les premiers-nés des mâles, le compte des noms étant fait, depuis l'âge d'un mois et au dessus, selon qu ils furent dénombrés, furent vingt-deux mille deux cent soixante et treize.
44 Bwana akamwambia Mose,
Et l'Eternel parla à Moïse, en disant:
45 “Watwae Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya mifugo yao. Walawi watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.
Prends les Lévites au lieu de tous les premiers-nés qui sont entre les enfants d'Israël, et les bêtes des Lévites, au lieu de leurs bêtes; et les Lévites seront à moi; je suis l'Eternel.
46 Ili kukomboa wazao wa kwanza 273 wa Waisraeli ambao wamezidi hesabu ya Walawi,
Et quant à ceux qu'il faudra racheter des premiers-nés des enfants d'Israël, qui sont deux cent soixante et treize, plus que les Lévites;
47 kusanya shekeli tano kwa kila mmoja, kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu, ambayo ina uzito wa gera ishirini.
Tu prendras cinq sicles par tête, tu les prendras selon le sicle du Sanctuaire; le sicle est de vingt oboles.
48 Mpe Aroni na wanawe hizo fedha kwa ajili ya ukombozi wa idadi ya Waisraeli waliozidi.”
Et tu donneras à Aaron et à ses fils l'argent de ceux qui auront été rachetés, passant le nombre des Lévites.
49 Kwa hiyo Mose akakusanya fedha za ukombozi kutoka kwa wale ambao hesabu yao ilizidi wale waliokombolewa na Walawi.
Moïse donc prit l'argent du rachat de ceux qui étaient de plus, outre ceux qui avaient été rachetés par l'échange des Lévites.
50 Kutokana na wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli alikusanya fedha yenye uzito wa shekeli 1,365 kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu.
Et il reçut l'argent des premiers-nés des enfants d'Israël, qui fut mille trois cent soixante-cinq sicles, selon le sicle du Sanctuaire.
51 Mose akampa Aroni na wanawe ile fedha ya ukombozi, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
Et Moïse donna l'argent des rachetés à Aaron, et à ses fils, selon le commandement de l'Eternel, ainsi que l'Eternel le lui avait commandé.

< Hesabu 3 >