< Hesabu 3 >

1 Hii ni hesabu ya jamaa ya Aroni na Mose kwa wakati ambao Bwana alizungumza na Mose katika Mlima Sinai.
Voici la postérité d’Aaron et de Moïse, au temps où Yahweh parla à Moïse sur la montagne de Sinaï
2 Majina ya wana wa Aroni yalikuwa: Nadabu mzaliwa wa kwanza na Abihu, Eleazari na Ithamari.
Voici les noms des fils d’Aaron: Nadab, le premier-né, Abiu, Eléazar et Ithamar.
3 Hayo yalikuwa majina ya wana wa Aroni, makuhani wapakwa mafuta, waliokuwa wamesimikwa kuhudumu kama makuhani.
Tels sont les noms des fils d’Aaron, des prêtres ayant reçu l’onction, installés pour exercer le sacerdoce.
4 Hata hivyo Nadabu na Abihu walikufa mbele za Bwana walipotoa sadaka kwa moto usioruhusiwa mbele zake katika Jangwa la Sinai. Hawakuwa na wana; kwa hiyo Eleazari na Ithamari walihudumu peke yao kama makuhani wakati wote wa maisha ya Aroni baba yao.
Nadab et Abiu moururent devant Yahweh, lorsqu’ils apportèrent devant Yahweh du feu étranger, dans le désert de Sinaï; ils n’avaient point de fils. Eléazar et Ithamar exercèrent le sacerdoce en présence d’Aaron, leur père.
5 Bwana akamwambia Mose,
Yahweh parla à Moïse, en disant:
6 “Walete watu wa kabila la Lawi mbele ya Aroni kuhani ili wamsaidie.
« Fais approcher la tribu de Lévi, et tu la placeras devant Aaron le prêtre, pour qu’elle soit à son service.
7 Watafanya huduma kwa ajili yake na kwa jumuiya yote katika Hema la Kukutania kwa kufanya kazi za Maskani.
Ils auront la charge de tout ce qui est commis à sa charge et à la charge de toute l’assemblée, devant la tente de réunion, faisant ainsi le service de la Demeure.
8 Watatunza samani zote za Hema la Kukutania, wakitimiza wajibu wa kuhudumia Waisraeli kwa kufanya kazi ya Maskani.
Ils seront chargés de tous les ustensiles de la tente de réunion, et de ce qui est commis à la charge des enfants d’Israël: ils feront ainsi le service de la Demeure.
9 Wakabidhi Walawi kwa Aroni na wanawe; hao ndio Waisraeli ambao wanakabidhiwa kwake kabisa.
Tu donneras les Lévites à Aaron et à ses fils; ils lui seront entièrement donnés, d’entre les enfants d’Israël.
10 Waweke Aroni na wanawe kuhudumu kama makuhani; mtu mwingine yeyote atakayesogea mahali patakatifu ni lazima auawe.”
Tu établiras Aaron et ses fils pour accomplir les fonctions de leur sacerdoce; l’étranger qui approchera du sanctuaire sera puni de mort. »
11 Bwana akamwambia Mose,
Yahweh parla à Moïse, en disant:
12 “Nimewatwaa Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli badala ya mzaliwa wa kwanza wa kiume wa kila mwanamke wa Mwisraeli. Walawi ni wangu,
« Voici, j’ai pris les Lévites du milieu des enfants d’Israël, à la place de tout premier-né qui ouvre le sein de sa mère parmi les enfants d’Israël, et les Lévites sont à moi.
13 kwa kuwa wazaliwa wote wa kwanza ni wangu. Nilipowaua wazaliwa wa kwanza huko Misri, nilimtenga kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli awe wangu, akiwa mwanadamu au mnyama. Watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.”
Car tout premier-né est à moi; le jour où j’ai frappé tous les premiers nés dans le pays d’Egypte, je me suis consacré tout premier-né en Israël, tant des hommes que des animaux: ils sont à moi. Je suis Yahweh. »
14 Bwana akamwambia Mose katika Jangwa la Sinai,
Yahweh parla à Moïse dans le désert de Sinaï, en disant:
15 “Wahesabu Walawi kwa jamaa zao na koo zao. Mhesabu kila mwanaume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi.”
« Fais le recensement des enfants de Lévi selon leurs maisons patriarcales, selon leurs familles. Tu feras le recensement de tous les mâles, depuis l’âge d’un mois et au-dessus. »
16 Kwa hiyo Mose akawahesabu, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
Moïse fit leur recensement sur l’ordre de Yahweh, selon qu’il lui avait été commandé.
17 Haya yalikuwa majina ya wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
Voici les fils de Lévi, d’après leurs noms: Gerson, Caath et Mérari. —
18 Haya ndiyo yaliyokuwa majina ya koo za Wagershoni: Libni na Shimei.
Voici les noms des fils de Gerson, selon leurs familles: Lebni et Séméi.
19 Koo za Wakohathi zilikuwa ni: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
Fils de Caath, selon leurs familles: Amram, Jésaar, Hébron et Oziel.
20 Koo za Wamerari zilikuwa ni: Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi, kufuatana na jamaa zao.
Fils de Mérari, selon leurs familles: Moholi et Musi. — Ce sont là les familles de Lévi selon leurs maisons patriarcales.
21 Kulikuwa na koo za Walibni na Washimei kwa Gershoni; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wagershoni.
De Gerson viennent la famille de Lebni et la famille de Séméi; ce sont les familles de Gersonites.
22 Idadi ya waume wote waliokuwa na mwezi mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 7,500.
Leurs recensés, en comptant tous les mâles depuis l’âge d’un mois et au-dessus, leurs recensés furent sept mille cinq cents.
23 Ukoo wa Wagershoni walitakiwa kuweka kambi zao upande wa magharibi, nyuma ya Maskani.
Les familles des Gersonites campaient derrière la Demeure, à l’occident.
24 Kiongozi wa jamaa za Wagershoni alikuwa Eliasafu mwana wa Laeli.
Le prince de la maison patriarcale des Gersonites était Eliasaph, fils de Laël.
25 Katika Hema la Kukutania, Wagershoni walikuwa na wajibu wa kutunza Maskani na hema, vifuniko vyake, pazia katika mlango wa kuingilia ndani ya Hema la Kukutania,
En ce qui concerne la tente de réunion, les fils de Gerson avaient la charge de la Demeure et de la tente, de sa couverture, du rideau qui est à l’entrée de la tente de réunion,
26 mapazia ya ua, pazia katika ingilio la ua unaozunguka Maskani na madhabahu, pamoja na kamba, na kila kinachohusika kwa matumizi yake.
des tentures du parvis et du rideau de l’entrée du parvis, tout autour de la Demeure et de l’autel, et de ses cordages pour tout son service.
27 Kwa Kohathi kulikuwepo koo za Waamramu, Waishari, Wahebroni na Wauzieli; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wakohathi.
De Caath viennent la famille des Amramites, la famille des Jésaarites, la famille des Hébronites et la famille des Oziélites; ce sont là les familles des Caathites.
28 Hesabu ya waume wote wenye mwezi mmoja au zaidi ilikuwa watu 8,600. Wakohathi waliwajibika kutunza mahali patakatifu.
En comptant tous les mâles depuis l’âge d’un mois et au-dessus, on en trouva huit mille six cents, chargés de la garde du sanctuaire.
29 Koo za Wakohathi zilitakiwa kuweka kambi zao upande wa kusini wa Maskani.
Les familles des fils de Caath campaient au côté méridional de la Demeure.
30 Kiongozi wa jamaa za koo za Wakohathi alikuwa Elisafani mwana wa Uzieli.
Le prince de la maison patriarcale des familles des Caathites était Elisaphan, fils d’Oziel.
31 Waliwajibika kutunza Sanduku la Agano, meza, kinara cha taa, madhabahu, na vile vyombo vya mahali patakatifu vinavyotumika kuhudumu, pazia, na kila kitu kinachohusika na matumizi yake.
On confia à leur garde l’arche, la table de proposition, le chandelier, les autels, les ustensiles du sanctuaire avec lesquels on fait le service, le voile et tout ce qui se rapporte à son service.
32 Kiongozi mkuu wa Walawi alikuwa Eleazari mwana wa kuhani, Aroni. Aliwekwa juu ya wale waliowajibika kutunza mahali patakatifu.
Le prince des princes des Lévites était Eléazar, fils du prêtre Aaron; il avait la surveillance de ceux qui étaient chargés de la garde du sanctuaire.
33 Kwa Merari kulikuwa na koo za Wamahli na Wamushi; hizi zilikuwa koo za Merari.
De Mérari viennent la famille des Moholites et la famille des Musites: ce sont là les familles des Mérarites.
34 Hesabu ya waume wote wenye umri wa mwaka mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 6,200.
Leurs recensés, en comptant tous les mâles depuis l’âge d’un mois et au-dessus, furent six mille deux cents.
35 Kiongozi wa jamaa za koo za Wamerari alikuwa Surieli mwana wa Abihaili; hawa walitakiwa kuweka kambi zao upande wa kaskazini mwa Maskani.
Le prince de la maison patriarcale des familles de Mérari était Suriel, fils d’Abihaiel. Ils campaient au côté septentrional de la Demeure.
36 Wamerari waliwekwa kutunza miimo ya Maskani, mataruma yake, nguzo, vitako na vifaa vyake vyote na kila kitu kilichohusika na matumizi yake,
Les fils de Mérari eurent le soin et la garde des ais de la Demeure, de ses traverses, de ses colonnes et de leurs socles, de tous ses ustensiles et de tout son service,
37 na pia nguzo za ua unaozunguka pamoja na vitako vyake, vigingi vya hema na kamba zake.
des colonnes du parvis tout autour, de leurs socles, de leurs pieux et de leurs cordages.
38 Mose, na Aroni na wanawe walitakiwa kuweka kambi zao mashariki mwa Maskani, kuelekea mawio ya jua, mbele ya Hema la Kukutania. Wao walihusika na utunzaji wa mahali patakatifu kwa niaba ya Waisraeli. Mtu mwingine yeyote aliyepasogelea mahali patakatifu angeuawa.
En face de la Demeure, à l’orient, devant la tente de réunion, au levant, campaient Moïse, Aaron et ses fils; ils avaient la garde du sanctuaire, pour ce qui était remis à la garde des enfants d’Israël; l’étranger qui s’en approcherait devait être puni de mort.
39 Jumla ya hesabu ya Walawi waliohesabiwa na Mose na Aroni kwa amri ya Bwana, kufuatana na koo, pamoja na kila mume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walikuwa 22,000.
Total des Lévites recensés dont Moïse fit le recensement sur l’ordre de Yahweh selon leurs familles, de tous les mâles depuis l’âge d’un mois et au-dessus: vingt-deux mille.
40 Bwana akamwambia Mose, “Wahesabu wazaliwa wa kwanza wa kiume wote wa Waisraeli wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi na uorodheshe majina yao.
Yahweh dit à Moïse: « Fais le recensement de tous les premiers-nés mâles parmi les enfants d’Israël, depuis l’âge d’un mois et au-dessus, et fais le compte de leurs noms.
41 Nitwalie Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya wazaliwa wa mifugo ya Waisraeli. Mimi ndimi Bwana.”
Tu prendras les Lévites pour moi, — je suis Yahweh, — à la place de tous les premiers-nés des enfants d’Israël, et le bétail des Lévites à la place de tous les premiers-nés du bétail des enfants d’Israël. »
42 Hivyo Mose akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru.
Moïse fit le recensement de tous les premiers-nés parmi les enfants d’Israël, selon l’ordre que Yahweh lui avait donné.
43 Jumla ya hesabu ya wazaliwa wa kwanza waume wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walioorodheshwa kwa majina, walikuwa 22,273.
Tous les premiers-nés mâles, comptés par leurs noms, depuis l’âge d’un mois et au-dessus, dont on fit le recensement, furent vingt-deux mille deux cent soixante-treize.
44 Bwana akamwambia Mose,
Yahweh parla à Moïse, en disant:
45 “Watwae Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya mifugo yao. Walawi watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.
« Prends les Lévites à la place de tous les premiers-nés des enfants d’Israël, et le bétail des Lévites à la place de leur bétail; et les Lévites seront à moi. Je suis Yahweh.
46 Ili kukomboa wazao wa kwanza 273 wa Waisraeli ambao wamezidi hesabu ya Walawi,
Pour le rachat des deux cent soixante-treize d’entre les premiers-nés des enfants d’Israël qui dépassent le nombre des Lévites,
47 kusanya shekeli tano kwa kila mmoja, kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu, ambayo ina uzito wa gera ishirini.
tu prendras cinq sicles par tête; tu les prendras selon le sicle du sanctuaire, qui est de vingt guéras.
48 Mpe Aroni na wanawe hizo fedha kwa ajili ya ukombozi wa idadi ya Waisraeli waliozidi.”
Tu donneras l’argent à Aaron et à ses fils pour le rachat de ceux qui dépassent le nombre des Lévites. »
49 Kwa hiyo Mose akakusanya fedha za ukombozi kutoka kwa wale ambao hesabu yao ilizidi wale waliokombolewa na Walawi.
Moïse prit l’argent pour le rachat de ceux qui dépassaient le nombre des premiers-nés rachetés par les Lévites;
50 Kutokana na wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli alikusanya fedha yenye uzito wa shekeli 1,365 kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu.
il prit l’argent des premiers-nés des enfants d’Israël, mille trois cent soixante-cinq sicles, selon le sicle du sanctuaire.
51 Mose akampa Aroni na wanawe ile fedha ya ukombozi, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
Et Moïse donna l’argent du rachat à Aaron et à ses fils, sur l’ordre de Yahweh, selon que Yahweh l’avait ordonné à Moïse.

< Hesabu 3 >