< Hesabu 3 >

1 Hii ni hesabu ya jamaa ya Aroni na Mose kwa wakati ambao Bwana alizungumza na Mose katika Mlima Sinai.
These ben the generaciouns of Aaron and of Moises, in the dai in which the Lord spak to Moises, in the hil of Synay.
2 Majina ya wana wa Aroni yalikuwa: Nadabu mzaliwa wa kwanza na Abihu, Eleazari na Ithamari.
And these ben the names of `the sones of Aaron; his first gendrid, Nadab; aftirward, Abyu, and Eleazar, and Ythamar; these ben the names of `Aarons sones,
3 Hayo yalikuwa majina ya wana wa Aroni, makuhani wapakwa mafuta, waliokuwa wamesimikwa kuhudumu kama makuhani.
preestis, that weren anoyntid, and whos hondis weren fillid and halewid, that thei schulden `be set in preesthod.
4 Hata hivyo Nadabu na Abihu walikufa mbele za Bwana walipotoa sadaka kwa moto usioruhusiwa mbele zake katika Jangwa la Sinai. Hawakuwa na wana; kwa hiyo Eleazari na Ithamari walihudumu peke yao kama makuhani wakati wote wa maisha ya Aroni baba yao.
Nadab and Abyu, whanne thei offeriden alien fier in the `siyt of the Lord, in the deseert of Synay, weren deed without fre children; and Eleazar and Ythamar `weren set in preesthod bifor Aaron hir fadir.
5 Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spak to Moises,
6 “Walete watu wa kabila la Lawi mbele ya Aroni kuhani ili wamsaidie.
`and seide, `Presente thou the lynage of Leuy, and make to stonde in the siyt of Aaron, preest, that thei mynystre to hym;
7 Watafanya huduma kwa ajili yake na kwa jumuiya yote katika Hema la Kukutania kwa kufanya kazi za Maskani.
and wake, and that thei kepe what euer thing perteyneth to the religioun of multitude, bifor the tabernacle of witnessyng;
8 Watatunza samani zote za Hema la Kukutania, wakitimiza wajibu wa kuhudumia Waisraeli kwa kufanya kazi ya Maskani.
and that thei kepe the vessels of the tabernacle, and serue in the seruyce therof.
9 Wakabidhi Walawi kwa Aroni na wanawe; hao ndio Waisraeli ambao wanakabidhiwa kwake kabisa.
And thou schalt yyue bi fre yifte the Leuytis to Aaron and hise sones, to whiche thei ben youun of the sones of Israel.
10 Waweke Aroni na wanawe kuhudumu kama makuhani; mtu mwingine yeyote atakayesogea mahali patakatifu ni lazima auawe.”
Sotheli thou schalt ordeyne Aaron and hise sones on the religioun of preesthod; a straungere, that neiyeth for to mynystre, and schal die.
11 Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spak to Moyses, `and seide,
12 “Nimewatwaa Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli badala ya mzaliwa wa kwanza wa kiume wa kila mwanamke wa Mwisraeli. Walawi ni wangu,
Y haue take the Leuytis of the sones of Israel for ech firste gendrid thing that openeth the womb in the sones of Israel; and the Leuytis schulen be myne,
13 kwa kuwa wazaliwa wote wa kwanza ni wangu. Nilipowaua wazaliwa wa kwanza huko Misri, nilimtenga kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli awe wangu, akiwa mwanadamu au mnyama. Watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.”
for ech firste gendrid thing is myn; sithen Y smoot the firste gendrid in the lond of Egipt, Y halewide to me what euer thing is borun first in Israel; fro man `til to beest thei ben myne; Y am the Lord.
14 Bwana akamwambia Mose katika Jangwa la Sinai,
And the Lord spak to Moises in the deseert
15 “Wahesabu Walawi kwa jamaa zao na koo zao. Mhesabu kila mwanaume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi.”
of Synay, and seide, Noumbre thou the sones of Leuy bi `the housis of her fadris, and bi meynees, ech male fro o monethe and aboue.
16 Kwa hiyo Mose akawahesabu, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
Moises noumbride, as the Lord comaundide.
17 Haya yalikuwa majina ya wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
And the sones of Leuy weren foundun, bi her names, Gerson, and Caath, and Merary;
18 Haya ndiyo yaliyokuwa majina ya koo za Wagershoni: Libni na Shimei.
the sones of Gerson weren Lebny, and Semey;
19 Koo za Wakohathi zilikuwa ni: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
the sones of Caath weren Amram, and Jessaar, Hebron, and Oziel;
20 Koo za Wamerari zilikuwa ni: Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi, kufuatana na jamaa zao.
and the sones of Merari weren Mooly, and Musi.
21 Kulikuwa na koo za Walibni na Washimei kwa Gershoni; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wagershoni.
Of Gerson weren twei meynees, of Lebny, and of Semei;
22 Idadi ya waume wote waliokuwa na mwezi mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 7,500.
of whiche the puple of male kynde was noumbrid, fro o monethe and aboue, seuene thousynde and fyue hundrid.
23 Ukoo wa Wagershoni walitakiwa kuweka kambi zao upande wa magharibi, nyuma ya Maskani.
These schulen sette tentis aftir the tabernacle at the west,
24 Kiongozi wa jamaa za Wagershoni alikuwa Eliasafu mwana wa Laeli.
vndur the prince Eliasaph, the sone of Jahel.
25 Katika Hema la Kukutania, Wagershoni walikuwa na wajibu wa kutunza Maskani na hema, vifuniko vyake, pazia katika mlango wa kuingilia ndani ya Hema la Kukutania,
And thei schulen haue kepyngis in the tabernacle of boond of pees, the tabernacle it silf, and the hilyng therof, the tente which is drawun bifor the yatis of the hilyng of the witnessyng of boond of pees;
26 mapazia ya ua, pazia katika ingilio la ua unaozunguka Maskani na madhabahu, pamoja na kamba, na kila kinachohusika kwa matumizi yake.
and the curteyns of the greet street, also the tente which is hangid in the entryng of the greet street of the tabernacle, and what euer thing perteyneth to the custom of the auter, the cordis of the tabernacle, and al the purtenaunce therof.
27 Kwa Kohathi kulikuwepo koo za Waamramu, Waishari, Wahebroni na Wauzieli; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wakohathi.
The kynrede of Caath schal haue the puplis of Amram, and of Jessaar, and of Ebron, and of Oziel;
28 Hesabu ya waume wote wenye mwezi mmoja au zaidi ilikuwa watu 8,600. Wakohathi waliwajibika kutunza mahali patakatifu.
these ben the meynees of Caathitis, noumbrid bi her names, alle of male kynde, fro o monethe and aboue, eiyte thousynde and sixe hundrid.
29 Koo za Wakohathi zilitakiwa kuweka kambi zao upande wa kusini wa Maskani.
Thei schulen haue kepyngis of the seyntuarie, and schulen sette tentis at the south coost;
30 Kiongozi wa jamaa za koo za Wakohathi alikuwa Elisafani mwana wa Uzieli.
and `the prince of hem schal be Elisaphan, the sone of Oziel.
31 Waliwajibika kutunza Sanduku la Agano, meza, kinara cha taa, madhabahu, na vile vyombo vya mahali patakatifu vinavyotumika kuhudumu, pazia, na kila kitu kinachohusika na matumizi yake.
And thei schulen kepe the arke, and the boord, and the candilstike, the auters, and vesselis of the seyntuarie in whiche it is mynystrid, and the veil, and al sich purtenaunce.
32 Kiongozi mkuu wa Walawi alikuwa Eleazari mwana wa kuhani, Aroni. Aliwekwa juu ya wale waliowajibika kutunza mahali patakatifu.
Sotheli the prince of princis of Leuytis schal be Eleazar, the sone of Aaron, preest; and he schal be on the keperis of the kepyng of the seyntuarie.
33 Kwa Merari kulikuwa na koo za Wamahli na Wamushi; hizi zilikuwa koo za Merari.
And sotheli of Merary schulen be the puplis of Mooli, and of Musi,
34 Hesabu ya waume wote wenye umri wa mwaka mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 6,200.
noumbrid bi her names, alle of male kynde fro o monethe and aboue, sixe thousynde and two hundrid;
35 Kiongozi wa jamaa za koo za Wamerari alikuwa Surieli mwana wa Abihaili; hawa walitakiwa kuweka kambi zao upande wa kaskazini mwa Maskani.
`the prince of hem schal be Suriel, the sone of Abiahiel; thei schulen sette tentis in the north coost.
36 Wamerari waliwekwa kutunza miimo ya Maskani, mataruma yake, nguzo, vitako na vifaa vyake vyote na kila kitu kilichohusika na matumizi yake,
And vndur `the kepyng of hem schulen be the tablis of the tabernacle, and the barris, and the pileris, and `the foundementis of tho, and alle thingis that perteynen to sich ournyng,
37 na pia nguzo za ua unaozunguka pamoja na vitako vyake, vigingi vya hema na kamba zake.
and the pileris of the greet street bi cumpas, with her foundementis, and the stakis with coordis.
38 Mose, na Aroni na wanawe walitakiwa kuweka kambi zao mashariki mwa Maskani, kuelekea mawio ya jua, mbele ya Hema la Kukutania. Wao walihusika na utunzaji wa mahali patakatifu kwa niaba ya Waisraeli. Mtu mwingine yeyote aliyepasogelea mahali patakatifu angeuawa.
Forsothe Moises and Aaron with hise sones schulen sette tentis bifor the tabernacle of boond of pees, that is, at the eest coost, and schulen haue the keping of the seyntuarie, in the myddis of the sones of Israel; what euer alien neiyeth, he schal die.
39 Jumla ya hesabu ya Walawi waliohesabiwa na Mose na Aroni kwa amri ya Bwana, kufuatana na koo, pamoja na kila mume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walikuwa 22,000.
Alle the Leuytis, whiche Moises and Aaron noumbriden, bi comaundement of the Lord, bi her meynees, in male kynde, fro o monethe and aboue, were two and twenti thousynd.
40 Bwana akamwambia Mose, “Wahesabu wazaliwa wa kwanza wa kiume wote wa Waisraeli wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi na uorodheshe majina yao.
And the Lord seide to Moises, Noumbre thou the firste gendrid children of male kynde of the sones of Israel, fro o monethe and aboue; and thou schalt haue the summe of hem; and
41 Nitwalie Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya wazaliwa wa mifugo ya Waisraeli. Mimi ndimi Bwana.”
thou schalt take Leuytis to me for alle the firste gendrid of the sones of Israel; Y am the Lord; and thou schalt take `the beestis of hem for alle the firste gendrid of the sones of Israel.
42 Hivyo Mose akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru.
And as the Lord comaundide, Moises noumbride the firste gendrid children of the sones of Israel; and the males weren bi her names,
43 Jumla ya hesabu ya wazaliwa wa kwanza waume wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walioorodheshwa kwa majina, walikuwa 22,273.
fro o monethe and aboue, two and twenti thousynde two hundrid and seuenti and thre.
44 Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spak to Moises, and seide,
45 “Watwae Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya mifugo yao. Walawi watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.
Take thou Leuytis for the firste gendrid children of the sones of Israel, and the beestis of Leuytis for the beestis of hem, and the Leuytis schulen be myne; Y am the Lord.
46 Ili kukomboa wazao wa kwanza 273 wa Waisraeli ambao wamezidi hesabu ya Walawi,
Forsothe in the prijs of two hundrid seuenti and thre, that passen the noumbre of `Leuytis, of the firste gendrid children of the sones of Israel,
47 kusanya shekeli tano kwa kila mmoja, kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu, ambayo ina uzito wa gera ishirini.
thou schalt take fyue ciclis bi ech heed, at the mesure of seyntuarie; a sicle hath xx. halpens;
48 Mpe Aroni na wanawe hizo fedha kwa ajili ya ukombozi wa idadi ya Waisraeli waliozidi.”
and thou schalt yyue the money to Aaron and to hise sones, the prijs of hem that ben aboue.
49 Kwa hiyo Mose akakusanya fedha za ukombozi kutoka kwa wale ambao hesabu yao ilizidi wale waliokombolewa na Walawi.
Therfor Moises took the money of hem that weren aboue, and whiche thei hadden ayenbouyt of the Leuytis, for the firste gendrid of the sones of Israel,
50 Kutokana na wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli alikusanya fedha yenye uzito wa shekeli 1,365 kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu.
a thousand thre hundrid sixti and fyue of siclis, bi the weiyte of seyntuarie;
51 Mose akampa Aroni na wanawe ile fedha ya ukombozi, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
and he yaf that money to Aaron and to hise sones, bi the word which the Lord comaundide to hym.

< Hesabu 3 >