< Hesabu 3 >

1 Hii ni hesabu ya jamaa ya Aroni na Mose kwa wakati ambao Bwana alizungumza na Mose katika Mlima Sinai.
and these generation Aaron and Moses in/on/with day to speak: speak LORD with Moses in/on/with mountain: mount Sinai
2 Majina ya wana wa Aroni yalikuwa: Nadabu mzaliwa wa kwanza na Abihu, Eleazari na Ithamari.
and these name son: child Aaron [the] firstborn Nadab and Abihu Eleazar and Ithamar
3 Hayo yalikuwa majina ya wana wa Aroni, makuhani wapakwa mafuta, waliokuwa wamesimikwa kuhudumu kama makuhani.
these name son: child Aaron [the] priest [the] to anoint which to fill hand: donate their to/for to minister
4 Hata hivyo Nadabu na Abihu walikufa mbele za Bwana walipotoa sadaka kwa moto usioruhusiwa mbele zake katika Jangwa la Sinai. Hawakuwa na wana; kwa hiyo Eleazari na Ithamari walihudumu peke yao kama makuhani wakati wote wa maisha ya Aroni baba yao.
and to die Nadab and Abihu to/for face: before LORD in/on/with to present: bring they fire be a stranger to/for face: before LORD in/on/with wilderness (Wilderness of) Sinai and son: child not to be to/for them and to minister Eleazar and Ithamar upon face: before Aaron father their
5 Bwana akamwambia Mose,
and to speak: speak LORD to(wards) Moses to/for to say
6 “Walete watu wa kabila la Lawi mbele ya Aroni kuhani ili wamsaidie.
to present: bring [obj] tribe Levi and to stand: stand [obj] him to/for face: before Aaron [the] priest and to minister [obj] him
7 Watafanya huduma kwa ajili yake na kwa jumuiya yote katika Hema la Kukutania kwa kufanya kazi za Maskani.
and to keep: guard [obj] charge his and [obj] charge all [the] congregation to/for face: before tent meeting to/for to serve: minister [obj] service: ministry [the] tabernacle
8 Watatunza samani zote za Hema la Kukutania, wakitimiza wajibu wa kuhudumia Waisraeli kwa kufanya kazi ya Maskani.
and to keep: guard [obj] all article/utensil tent meeting and [obj] charge son: descendant/people Israel to/for to serve: minister [obj] service: ministry [the] tabernacle
9 Wakabidhi Walawi kwa Aroni na wanawe; hao ndio Waisraeli ambao wanakabidhiwa kwake kabisa.
and to give: give [obj] [the] Levi to/for Aaron and to/for son: child his to give: give to give: give they(masc.) to/for him from with son: descendant/people Israel
10 Waweke Aroni na wanawe kuhudumu kama makuhani; mtu mwingine yeyote atakayesogea mahali patakatifu ni lazima auawe.”
and [obj] Aaron and [obj] son: child his to reckon: overseer and to keep: guard [obj] priesthood their and [the] be a stranger [the] approaching to die
11 Bwana akamwambia Mose,
and to speak: speak LORD to(wards) Moses to/for to say
12 “Nimewatwaa Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli badala ya mzaliwa wa kwanza wa kiume wa kila mwanamke wa Mwisraeli. Walawi ni wangu,
and I behold to take: take [obj] [the] Levi from midst son: descendant/people Israel underneath: instead all firstborn firstborn womb from son: descendant/people Israel and to be to/for me [the] Levi
13 kwa kuwa wazaliwa wote wa kwanza ni wangu. Nilipowaua wazaliwa wa kwanza huko Misri, nilimtenga kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli awe wangu, akiwa mwanadamu au mnyama. Watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.”
for to/for me all firstborn in/on/with day to smite I all firstborn in/on/with land: country/planet Egypt to consecrate: consecate to/for me all firstborn in/on/with Israel from man till animal to/for me to be I LORD
14 Bwana akamwambia Mose katika Jangwa la Sinai,
and to speak: speak LORD to(wards) Moses in/on/with wilderness (Wilderness of) Sinai to/for to say
15 “Wahesabu Walawi kwa jamaa zao na koo zao. Mhesabu kila mwanaume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi.”
to reckon: list [obj] son: child Levi to/for house: household father their to/for family their all male from son: aged month and above [to] to reckon: list them
16 Kwa hiyo Mose akawahesabu, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
and to reckon: list [obj] them Moses upon lip: word LORD like/as as which to command
17 Haya yalikuwa majina ya wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
and to be these son: child Levi in/on/with name their Gershon and Kohath and Merari
18 Haya ndiyo yaliyokuwa majina ya koo za Wagershoni: Libni na Shimei.
and these name son: child Gershon to/for family their Libni and Shimei
19 Koo za Wakohathi zilikuwa ni: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
and son: child Kohath to/for family their Amram and Izhar Hebron and Uzziel
20 Koo za Wamerari zilikuwa ni: Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi, kufuatana na jamaa zao.
and son: child Merari to/for family their Mahli and Mushi these they(masc.) family [the] Levi to/for house: household father their
21 Kulikuwa na koo za Walibni na Washimei kwa Gershoni; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wagershoni.
to/for Gershon family [the] Libnite and family [the] Shimeite these they(masc.) family [the] Gershonite
22 Idadi ya waume wote waliokuwa na mwezi mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 7,500.
to reckon: list their in/on/with number all male from son: aged month and above [to] to reckon: list their seven thousand and five hundred
23 Ukoo wa Wagershoni walitakiwa kuweka kambi zao upande wa magharibi, nyuma ya Maskani.
family [the] Gershonite after [the] tabernacle to camp sea: west [to]
24 Kiongozi wa jamaa za Wagershoni alikuwa Eliasafu mwana wa Laeli.
and leader house: household father to/for Gershonite Eliasaph son: child Lael
25 Katika Hema la Kukutania, Wagershoni walikuwa na wajibu wa kutunza Maskani na hema, vifuniko vyake, pazia katika mlango wa kuingilia ndani ya Hema la Kukutania,
and charge son: child Gershon in/on/with tent meeting [the] tabernacle and [the] tent covering his and covering entrance tent meeting
26 mapazia ya ua, pazia katika ingilio la ua unaozunguka Maskani na madhabahu, pamoja na kamba, na kila kinachohusika kwa matumizi yake.
and curtain [the] court and [obj] covering entrance [the] court which upon [the] tabernacle and upon [the] altar around and [obj] cord his to/for all service: ministry his
27 Kwa Kohathi kulikuwepo koo za Waamramu, Waishari, Wahebroni na Wauzieli; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wakohathi.
and to/for Kohath family [the] Amramite and family [the] Izharite and family [the] Hebronite and family [the] Uzzielite these they(masc.) family [the] Kohathite
28 Hesabu ya waume wote wenye mwezi mmoja au zaidi ilikuwa watu 8,600. Wakohathi waliwajibika kutunza mahali patakatifu.
in/on/with number all male from son: aged month and above [to] eight thousand and six hundred to keep: guard charge [the] holiness
29 Koo za Wakohathi zilitakiwa kuweka kambi zao upande wa kusini wa Maskani.
family son: child Kohath to camp upon thigh [the] tabernacle south [to]
30 Kiongozi wa jamaa za koo za Wakohathi alikuwa Elisafani mwana wa Uzieli.
and leader house: household father to/for family [the] Kohathite Elizaphan son: child Uzziel
31 Waliwajibika kutunza Sanduku la Agano, meza, kinara cha taa, madhabahu, na vile vyombo vya mahali patakatifu vinavyotumika kuhudumu, pazia, na kila kitu kinachohusika na matumizi yake.
and charge their [the] ark and [the] table and [the] lampstand and [the] altar and article/utensil [the] holiness which to minister in/on/with them and [the] covering and all service: ministry his
32 Kiongozi mkuu wa Walawi alikuwa Eleazari mwana wa kuhani, Aroni. Aliwekwa juu ya wale waliowajibika kutunza mahali patakatifu.
and leader leader [the] Levi Eleazar son: child Aaron [the] priest punishment to keep: guard charge [the] holiness
33 Kwa Merari kulikuwa na koo za Wamahli na Wamushi; hizi zilikuwa koo za Merari.
to/for Merari family [the] Mahlite and family [the] Mushite these they(masc.) family Merari
34 Hesabu ya waume wote wenye umri wa mwaka mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 6,200.
and to reckon: list their in/on/with number all male from son: aged month and above [to] six thousand and hundred
35 Kiongozi wa jamaa za koo za Wamerari alikuwa Surieli mwana wa Abihaili; hawa walitakiwa kuweka kambi zao upande wa kaskazini mwa Maskani.
and leader house: household father to/for family Merari Zuriel son: child Abihail upon thigh [the] tabernacle to camp north [to]
36 Wamerari waliwekwa kutunza miimo ya Maskani, mataruma yake, nguzo, vitako na vifaa vyake vyote na kila kitu kilichohusika na matumizi yake,
and punishment charge son: child Merari board [the] tabernacle and bar his and pillar his and socket his and all article/utensil his and all service: ministry his
37 na pia nguzo za ua unaozunguka pamoja na vitako vyake, vigingi vya hema na kamba zake.
and pillar [the] court around and socket their and peg their and cord their
38 Mose, na Aroni na wanawe walitakiwa kuweka kambi zao mashariki mwa Maskani, kuelekea mawio ya jua, mbele ya Hema la Kukutania. Wao walihusika na utunzaji wa mahali patakatifu kwa niaba ya Waisraeli. Mtu mwingine yeyote aliyepasogelea mahali patakatifu angeuawa.
and [the] to camp to/for face: before [the] tabernacle east [to] to/for face: before tent meeting east [to] Moses and Aaron and son: child his to keep: guard charge [the] sanctuary to/for charge son: descendant/people Israel and [the] be a stranger [the] approaching to die
39 Jumla ya hesabu ya Walawi waliohesabiwa na Mose na Aroni kwa amri ya Bwana, kufuatana na koo, pamoja na kila mume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walikuwa 22,000.
all to reckon: list [the] Levi which to reckon: list Moses and Aaron upon lip: word LORD to/for family their all male from son: aged month and above [to] two and twenty thousand
40 Bwana akamwambia Mose, “Wahesabu wazaliwa wa kwanza wa kiume wote wa Waisraeli wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi na uorodheshe majina yao.
and to say LORD to(wards) Moses to reckon: list all firstborn male to/for son: descendant/people Israel from son: aged month and above [to] and to lift: count [obj] number name their
41 Nitwalie Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya wazaliwa wa mifugo ya Waisraeli. Mimi ndimi Bwana.”
and to take: take [obj] [the] Levi to/for me I LORD underneath: instead all firstborn in/on/with son: descendant/people Israel and [obj] animal [the] Levi underneath: instead all firstborn in/on/with animal son: descendant/people Israel
42 Hivyo Mose akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru.
and to reckon: list Moses like/as as which to command LORD [obj] him [obj] all firstborn in/on/with son: descendant/people Israel
43 Jumla ya hesabu ya wazaliwa wa kwanza waume wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walioorodheshwa kwa majina, walikuwa 22,273.
and to be all firstborn male in/on/with number name from son: aged month and above [to] to/for to reckon: list their two and twenty thousand three and seventy and hundred
44 Bwana akamwambia Mose,
and to speak: speak LORD to(wards) Moses to/for to say
45 “Watwae Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya mifugo yao. Walawi watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.
to take: take [obj] [the] Levi underneath: instead all firstborn in/on/with son: descendant/people Israel and [obj] animal [the] Levi underneath: instead animal their and to be to/for me [the] Levi I LORD
46 Ili kukomboa wazao wa kwanza 273 wa Waisraeli ambao wamezidi hesabu ya Walawi,
and [obj] ransomed [the] three and [the] seventy and [the] hundred [the] to remain upon [the] Levi from firstborn son: descendant/people Israel
47 kusanya shekeli tano kwa kila mmoja, kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu, ambayo ina uzito wa gera ishirini.
and to take: take five five shekel to/for head in/on/with shekel [the] holiness to take: take twenty gerah [the] shekel
48 Mpe Aroni na wanawe hizo fedha kwa ajili ya ukombozi wa idadi ya Waisraeli waliozidi.”
and to give: give [the] silver: money to/for Aaron and to/for son: child his ransomed [the] to remain in/on/with them
49 Kwa hiyo Mose akakusanya fedha za ukombozi kutoka kwa wale ambao hesabu yao ilizidi wale waliokombolewa na Walawi.
and to take: take Moses [obj] silver: money [the] redemption from with [the] to remain upon ransomed [the] Levi
50 Kutokana na wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli alikusanya fedha yenye uzito wa shekeli 1,365 kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu.
from with firstborn son: descendant/people Israel to take: take [obj] [the] silver: money five and sixty and three hundred and thousand in/on/with shekel [the] holiness
51 Mose akampa Aroni na wanawe ile fedha ya ukombozi, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
and to give: give Moses [obj] silver: money ([the] ransomed *Q(k)*) to/for Aaron and to/for son: child his upon lip: word LORD like/as as which to command LORD [obj] Moses

< Hesabu 3 >