< Hesabu 3 >
1 Hii ni hesabu ya jamaa ya Aroni na Mose kwa wakati ambao Bwana alizungumza na Mose katika Mlima Sinai.
And these are the generations of Aaron and Moses, on the day that the Lord spoke with Moses on mount Sinai.
2 Majina ya wana wa Aroni yalikuwa: Nadabu mzaliwa wa kwanza na Abihu, Eleazari na Ithamari.
And these are the names of the sons of Aaron: the firstborn Nadab, and Abihu, Elazar, and Ithamar.
3 Hayo yalikuwa majina ya wana wa Aroni, makuhani wapakwa mafuta, waliokuwa wamesimikwa kuhudumu kama makuhani.
These are the names of the sons of Aaron, the priests that were anointed, who were consecrated to minister as priests.
4 Hata hivyo Nadabu na Abihu walikufa mbele za Bwana walipotoa sadaka kwa moto usioruhusiwa mbele zake katika Jangwa la Sinai. Hawakuwa na wana; kwa hiyo Eleazari na Ithamari walihudumu peke yao kama makuhani wakati wote wa maisha ya Aroni baba yao.
And Nadab and Abihu died before the Lord, when they offered a strange fire before the Lord, in the wilderness of Sinai, and they had no children: and Elazar and Ithamar ministered as priests in the life-time of Aaron their father.
And the Lord spoke unto Moses, saying,
6 “Walete watu wa kabila la Lawi mbele ya Aroni kuhani ili wamsaidie.
Bring the tribe of Levi near, and present the same before Aaron the priest, that they may serve him.
7 Watafanya huduma kwa ajili yake na kwa jumuiya yote katika Hema la Kukutania kwa kufanya kazi za Maskani.
And they shall keep his charge, and the charge of the whole congregation before the tent of the congregation, to do the service of the tabernacle.
8 Watatunza samani zote za Hema la Kukutania, wakitimiza wajibu wa kuhudumia Waisraeli kwa kufanya kazi ya Maskani.
And they shall keep all the vessels of the tent of the congregation, and the charge of the children of Israel, to do the service of the tabernacle.
9 Wakabidhi Walawi kwa Aroni na wanawe; hao ndio Waisraeli ambao wanakabidhiwa kwake kabisa.
And thou shalt give the Levites unto Aaron and to his sons: as associates are they given unto him out of the children of Israel.
10 Waweke Aroni na wanawe kuhudumu kama makuhani; mtu mwingine yeyote atakayesogea mahali patakatifu ni lazima auawe.”
And Aaron and his sons shalt thou instruct, that they shall guard well their priest's office; and the stranger that cometh nigh shall be put to death.
11 Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spoke unto Moses, saying,
12 “Nimewatwaa Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli badala ya mzaliwa wa kwanza wa kiume wa kila mwanamke wa Mwisraeli. Walawi ni wangu,
And I, behold, I have taken the Levites from the midst of the children of Israel instead of every first-born that openeth the womb among the children of Israel; and the Levites shall be mine.
13 kwa kuwa wazaliwa wote wa kwanza ni wangu. Nilipowaua wazaliwa wa kwanza huko Misri, nilimtenga kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli awe wangu, akiwa mwanadamu au mnyama. Watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.”
Because mine is every first-born; on the day when I smote every first-born in the land of Egypt I hallowed unto me every first-born in Israel, both man and beast: mine shall they be; I am the Lord.
14 Bwana akamwambia Mose katika Jangwa la Sinai,
And the Lord spoke unto Moses in the wilderness of Sinai, saying,
15 “Wahesabu Walawi kwa jamaa zao na koo zao. Mhesabu kila mwanaume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi.”
Number the children of Levi after their divisions, by their families; every male of them from a month old and upward shalt thou number.
16 Kwa hiyo Mose akawahesabu, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
And Moses numbered them according to the order of the Lord, as he had been commanded.
17 Haya yalikuwa majina ya wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
And these were the sons of Levi by their names: Gershon, and Kehath, and Merari.
18 Haya ndiyo yaliyokuwa majina ya koo za Wagershoni: Libni na Shimei.
And these are the names of the sons of Gershon after their families: Libni, and Shimi.
19 Koo za Wakohathi zilikuwa ni: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
And the sons of Kehath after their families: 'Amram, and Yizhar, Chebron, and 'Uzziel.
20 Koo za Wamerari zilikuwa ni: Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi, kufuatana na jamaa zao.
And the sons of Merari after their families: Machli, and Mushi; these are the families of the Levites according to their family divisions.
21 Kulikuwa na koo za Walibni na Washimei kwa Gershoni; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wagershoni.
Of Gershon: the family of the Libnites, and the family of the Shimites; these are the families of the Gershunites.
22 Idadi ya waume wote waliokuwa na mwezi mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 7,500.
Those that were numbered of them, by the numbering of all the males from a month old and upward, even those that were numbered of them, were seven thousand and five hundred.
23 Ukoo wa Wagershoni walitakiwa kuweka kambi zao upande wa magharibi, nyuma ya Maskani.
The families of the Gershunites used to encamp behind the tabernacle, westward.
24 Kiongozi wa jamaa za Wagershoni alikuwa Eliasafu mwana wa Laeli.
And the prince of the family division of the Gershunites was Elyassaph the son of Lael.
25 Katika Hema la Kukutania, Wagershoni walikuwa na wajibu wa kutunza Maskani na hema, vifuniko vyake, pazia katika mlango wa kuingilia ndani ya Hema la Kukutania,
And the charge of the sons of Gershon in the tabernacle of the congregation was the tabernacle and the tent, its covering, and the hanging for the door of the tabernacle of the congregation,
26 mapazia ya ua, pazia katika ingilio la ua unaozunguka Maskani na madhabahu, pamoja na kamba, na kila kinachohusika kwa matumizi yake.
And the hangings of the court, and the curtain for the door of the court, which is by the tabernacle and by the altar, round about, and its cords for all the service thereof.
27 Kwa Kohathi kulikuwepo koo za Waamramu, Waishari, Wahebroni na Wauzieli; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wakohathi.
And of Kehath: the family of the 'Amramites, and the family of the Yizharites, and the family of the Chebronites, and the family of the 'Uzzielites; these are the families of the Kehathites.
28 Hesabu ya waume wote wenye mwezi mmoja au zaidi ilikuwa watu 8,600. Wakohathi waliwajibika kutunza mahali patakatifu.
By the numbering of all the males, from a month old and upward, they were eight thousand and six hundred, keeping the charge of the sanctuary.
29 Koo za Wakohathi zilitakiwa kuweka kambi zao upande wa kusini wa Maskani.
The families of the sons of Kehath used to encamp on the side of the tabernacle, southward.
30 Kiongozi wa jamaa za koo za Wakohathi alikuwa Elisafani mwana wa Uzieli.
And the prince of the division of the families of the Kehathites was Elizaphan the son of 'Uzziel.
31 Waliwajibika kutunza Sanduku la Agano, meza, kinara cha taa, madhabahu, na vile vyombo vya mahali patakatifu vinavyotumika kuhudumu, pazia, na kila kitu kinachohusika na matumizi yake.
And their charge was the ark, and the table, and the candlestick, and the altars, and the vessels of the sanctuary which are used for the service, and the vail, and all belonging thereto.
32 Kiongozi mkuu wa Walawi alikuwa Eleazari mwana wa kuhani, Aroni. Aliwekwa juu ya wale waliowajibika kutunza mahali patakatifu.
And the chief over the princes of the Levites was Elazar the son of Aaron the priest, having the oversight of those that kept the charge of the sanctuary.
33 Kwa Merari kulikuwa na koo za Wamahli na Wamushi; hizi zilikuwa koo za Merari.
Of Merari: the family of the Machlites, and the family of the Mushites; these are the families of Merari.
34 Hesabu ya waume wote wenye umri wa mwaka mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 6,200.
And those that were numbered of them, by the numbering of all the males, from a month old and upward, were six thousand and two hundred.
35 Kiongozi wa jamaa za koo za Wamerari alikuwa Surieli mwana wa Abihaili; hawa walitakiwa kuweka kambi zao upande wa kaskazini mwa Maskani.
And the chief of the division of the families of Merari was Zuriel the son of Abichayil: they used to encamp on the side of the tabernacle, northward.
36 Wamerari waliwekwa kutunza miimo ya Maskani, mataruma yake, nguzo, vitako na vifaa vyake vyote na kila kitu kilichohusika na matumizi yake,
And under the custody and charge of the sons of Merari were the boards of the tabernacle, and its bars, and its pillars, and its sockets, and all its vessels, and all that belongeth thereto,
37 na pia nguzo za ua unaozunguka pamoja na vitako vyake, vigingi vya hema na kamba zake.
And the pillars of the court round about, and their sockets, and their pins, and their cords.
38 Mose, na Aroni na wanawe walitakiwa kuweka kambi zao mashariki mwa Maskani, kuelekea mawio ya jua, mbele ya Hema la Kukutania. Wao walihusika na utunzaji wa mahali patakatifu kwa niaba ya Waisraeli. Mtu mwingine yeyote aliyepasogelea mahali patakatifu angeuawa.
But those that encamped before the tabernacle toward the east, even before the tabernacle of the congregation toward the rising of the sun, were Moses, and Aaron, and his sons, keeping the charge of the sanctuary for the charge of the children of Israel; and the stranger that came nigh was to be put to death.
39 Jumla ya hesabu ya Walawi waliohesabiwa na Mose na Aroni kwa amri ya Bwana, kufuatana na koo, pamoja na kila mume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walikuwa 22,000.
All that were numbered of the Levites, whom Moses numbered with Aaron, at the order of the Lord, according to their families, all the males from a month old and upward, were twenty and two thousand.
40 Bwana akamwambia Mose, “Wahesabu wazaliwa wa kwanza wa kiume wote wa Waisraeli wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi na uorodheshe majina yao.
And the Lord said unto Moses, Number all the first-born males of the children of Israel from a month old and upward, and take the number of their names.
41 Nitwalie Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya wazaliwa wa mifugo ya Waisraeli. Mimi ndimi Bwana.”
And thou shalt take the Levites for me, I am the Lord, instead of all the first-born among the children of Israel; and the cattle of the Levites instead of all the first-born among the cattle of the children of Israel.
42 Hivyo Mose akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru.
And Moses numbered, as the Lord had commanded him, all the first-born among the children of Israel.
43 Jumla ya hesabu ya wazaliwa wa kwanza waume wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walioorodheshwa kwa majina, walikuwa 22,273.
And all the first-born males, by the numbering of the names, from a month old and upward, of those that were numbered of them, were twenty and two thousand two hundred and seventy and three.
44 Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spoke unto Moses, saying,
45 “Watwae Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya mifugo yao. Walawi watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.
Take the Levites instead of all the first-born among the children of Israel, and the cattle of the Levites instead of their cattle; and the Levites shall be mine: I am the Lord.
46 Ili kukomboa wazao wa kwanza 273 wa Waisraeli ambao wamezidi hesabu ya Walawi,
And [for] those that are to be redeemed, the two hundred and seventy and three of the first-born of the children of Israel, who are more than the Levites,
47 kusanya shekeli tano kwa kila mmoja, kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu, ambayo ina uzito wa gera ishirini.
Thou shalt take five shekels apiece for the poll; after the shekel of the sanctuary shalt thou take, twenty gerahs to the shekel;
48 Mpe Aroni na wanawe hizo fedha kwa ajili ya ukombozi wa idadi ya Waisraeli waliozidi.”
And thou shalt give unto Aaron and to his sons the money, [for] those who are to be redeemed of those that are over the number of them.
49 Kwa hiyo Mose akakusanya fedha za ukombozi kutoka kwa wale ambao hesabu yao ilizidi wale waliokombolewa na Walawi.
And Moses took the redemption-money of those that were over in number above those who were redeemed by the Levites:
50 Kutokana na wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli alikusanya fedha yenye uzito wa shekeli 1,365 kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu.
Of the first-born of the children of Israel did he take the money; a thousand three hundred and sixty and five shekels, after the shekel of the sanctuary.
51 Mose akampa Aroni na wanawe ile fedha ya ukombozi, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
And Moses gave the money of those who were redeemed unto Aaron and unto his sons, by the order of the Lord; as the Lord had commanded Moses.