< Hesabu 3 >
1 Hii ni hesabu ya jamaa ya Aroni na Mose kwa wakati ambao Bwana alizungumza na Mose katika Mlima Sinai.
Now these are the generations of Aaron and Moses in the day that Jehovah spoke with Moses in mount Sinai:
2 Majina ya wana wa Aroni yalikuwa: Nadabu mzaliwa wa kwanza na Abihu, Eleazari na Ithamari.
And these are the names of the sons of Aaron: Nadab the firstborn, and Abihu, Eleazar, and Ithamar.
3 Hayo yalikuwa majina ya wana wa Aroni, makuhani wapakwa mafuta, waliokuwa wamesimikwa kuhudumu kama makuhani.
These are the names of the sons of Aaron, the priests who were anointed, whom he consecrated to minister in the priest's office.
4 Hata hivyo Nadabu na Abihu walikufa mbele za Bwana walipotoa sadaka kwa moto usioruhusiwa mbele zake katika Jangwa la Sinai. Hawakuwa na wana; kwa hiyo Eleazari na Ithamari walihudumu peke yao kama makuhani wakati wote wa maisha ya Aroni baba yao.
And Nadab and Abihu died before Jehovah when they offered strange fire before Jehovah in the wilderness of Sinai, and they had no sons. And Eleazar and Ithamar ministered in the priest's office in the presence of Aaron their father.
And Jehovah spoke to Moses, saying,
6 “Walete watu wa kabila la Lawi mbele ya Aroni kuhani ili wamsaidie.
Bring the tribe of Levi near, and set them before Aaron the priest, that they may minister to him.
7 Watafanya huduma kwa ajili yake na kwa jumuiya yote katika Hema la Kukutania kwa kufanya kazi za Maskani.
And they shall keep his charge, and the charge of the whole congregation before the tent of meeting, to do the service of the tabernacle.
8 Watatunza samani zote za Hema la Kukutania, wakitimiza wajibu wa kuhudumia Waisraeli kwa kufanya kazi ya Maskani.
And they shall keep all the furniture of the tent of meeting, and the charge of the sons of Israel, to do the service of the tabernacle.
9 Wakabidhi Walawi kwa Aroni na wanawe; hao ndio Waisraeli ambao wanakabidhiwa kwake kabisa.
And thou shall give the Levites to Aaron and to his sons. They are wholly given to him on the behalf of the sons of Israel.
10 Waweke Aroni na wanawe kuhudumu kama makuhani; mtu mwingine yeyote atakayesogea mahali patakatifu ni lazima auawe.”
And thou shall appoint Aaron and his sons, and they shall keep their priesthood. And the stranger who comes near shall be put to death.
11 Bwana akamwambia Mose,
And Jehovah spoke to Moses, saying,
12 “Nimewatwaa Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli badala ya mzaliwa wa kwanza wa kiume wa kila mwanamke wa Mwisraeli. Walawi ni wangu,
And I, behold, I have taken the Levites from among the sons of Israel instead of all the firstborn who opens the womb among the sons of Israel. And the Levites shall be mine,
13 kwa kuwa wazaliwa wote wa kwanza ni wangu. Nilipowaua wazaliwa wa kwanza huko Misri, nilimtenga kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli awe wangu, akiwa mwanadamu au mnyama. Watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.”
for all the firstborn are mine. On the day that I smote all the firstborn in the land of Egypt I hallowed to me all the firstborn in Israel, both man and beast. They shall be mine. I am Jehovah.
14 Bwana akamwambia Mose katika Jangwa la Sinai,
And Jehovah spoke to Moses in the wilderness of Sinai, saying,
15 “Wahesabu Walawi kwa jamaa zao na koo zao. Mhesabu kila mwanaume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi.”
Number the sons of Levi by their fathers' houses, by their families. Thou shall number them, every male from a month old and upward.
16 Kwa hiyo Mose akawahesabu, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
And Moses numbered them according to the word of Jehovah, as he was commanded.
17 Haya yalikuwa majina ya wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
And these were the sons of Levi by their names: Gershon, and Kohath, and Merari.
18 Haya ndiyo yaliyokuwa majina ya koo za Wagershoni: Libni na Shimei.
And these are the names of the sons of Gershon by their families: Libni and Shimei.
19 Koo za Wakohathi zilikuwa ni: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
And the sons of Kohath by their families: Amram, and Izhar, Hebron, and Uzziel.
20 Koo za Wamerari zilikuwa ni: Mahli na Mushi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi, kufuatana na jamaa zao.
And the sons of Merari by their families: Mahli and Mushi. These are the families of the Levites according to their fathers' houses.
21 Kulikuwa na koo za Walibni na Washimei kwa Gershoni; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wagershoni.
Of Gershon was the family of the Libnites, and the family of the Shimeites. These are the families of the Gershonites.
22 Idadi ya waume wote waliokuwa na mwezi mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 7,500.
Those who were numbered of them, according to the number of all the males, from a month old and upward, even those who were numbered of them were seven thousand and five hundred.
23 Ukoo wa Wagershoni walitakiwa kuweka kambi zao upande wa magharibi, nyuma ya Maskani.
The families of the Gershonites shall encamp behind the tabernacle westward.
24 Kiongozi wa jamaa za Wagershoni alikuwa Eliasafu mwana wa Laeli.
And the ruler of the fathers' house of the Gershonites shall be Eliasaph the son of Lael.
25 Katika Hema la Kukutania, Wagershoni walikuwa na wajibu wa kutunza Maskani na hema, vifuniko vyake, pazia katika mlango wa kuingilia ndani ya Hema la Kukutania,
And the charge of the sons of Gershon in the tent of meeting shall be the tabernacle, and the tent, the covering of it, and the screen for the door of the tent of meeting,
26 mapazia ya ua, pazia katika ingilio la ua unaozunguka Maskani na madhabahu, pamoja na kamba, na kila kinachohusika kwa matumizi yake.
and the hangings of the court, and the screen for the door of the court, which is by the tabernacle, and by the altar round about, and the cords of it for all the service thereof.
27 Kwa Kohathi kulikuwepo koo za Waamramu, Waishari, Wahebroni na Wauzieli; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wakohathi.
And of Kohath was the family of the Amramites, and the family of the Izharites, and the family of the Hebronites, and the family of the Uzzielites. These are the families of the Kohathites.
28 Hesabu ya waume wote wenye mwezi mmoja au zaidi ilikuwa watu 8,600. Wakohathi waliwajibika kutunza mahali patakatifu.
According to the number of all the males, from a month old and upward, there were eight thousand and six hundred, keeping the charge of the sanctuary.
29 Koo za Wakohathi zilitakiwa kuweka kambi zao upande wa kusini wa Maskani.
The families of the sons of Kohath shall encamp on the side of the tabernacle southward.
30 Kiongozi wa jamaa za koo za Wakohathi alikuwa Elisafani mwana wa Uzieli.
And the ruler of the fathers' house of the families of the Kohathites shall be Elizaphan the son of Uzziel.
31 Waliwajibika kutunza Sanduku la Agano, meza, kinara cha taa, madhabahu, na vile vyombo vya mahali patakatifu vinavyotumika kuhudumu, pazia, na kila kitu kinachohusika na matumizi yake.
And their charge shall be the ark, and the table, and the lampstand, and the altars, and the vessels of the sanctuary with which they minister, and the screen, and all the service thereof.
32 Kiongozi mkuu wa Walawi alikuwa Eleazari mwana wa kuhani, Aroni. Aliwekwa juu ya wale waliowajibika kutunza mahali patakatifu.
And Eleazar the son of Aaron the priest shall be ruler of the rulers of the Levites, with the oversight of those who keep the charge of the sanctuary.
33 Kwa Merari kulikuwa na koo za Wamahli na Wamushi; hizi zilikuwa koo za Merari.
Of Merari was the family of the Mahlites, and the family of the Mushites. These are the families of Merari.
34 Hesabu ya waume wote wenye umri wa mwaka mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 6,200.
And those who were numbered of them, according to the number of all the males, from a month old and upward, were six thousand and two hundred.
35 Kiongozi wa jamaa za koo za Wamerari alikuwa Surieli mwana wa Abihaili; hawa walitakiwa kuweka kambi zao upande wa kaskazini mwa Maskani.
And the ruler of the fathers' house of the families of Merari was Zuriel the son of Abihail. They shall encamp on the side of the tabernacle northward.
36 Wamerari waliwekwa kutunza miimo ya Maskani, mataruma yake, nguzo, vitako na vifaa vyake vyote na kila kitu kilichohusika na matumizi yake,
And the appointed charge of the sons of Merari shall be the boards of the tabernacle, and the bars of it, and the pillars of it, and the sockets of it, and all the instruments of it, and all the service thereof,
37 na pia nguzo za ua unaozunguka pamoja na vitako vyake, vigingi vya hema na kamba zake.
and the pillars of the court round about, and their sockets, and their pegs, and their cords.
38 Mose, na Aroni na wanawe walitakiwa kuweka kambi zao mashariki mwa Maskani, kuelekea mawio ya jua, mbele ya Hema la Kukutania. Wao walihusika na utunzaji wa mahali patakatifu kwa niaba ya Waisraeli. Mtu mwingine yeyote aliyepasogelea mahali patakatifu angeuawa.
And those who encamp before the tabernacle eastward, before the tent of meeting toward the sunrise, shall be Moses, and Aaron and his sons, keeping the charge of the sanctuary for the charge of the sons of Israel. And the stranger that comes near shall be put to death.
39 Jumla ya hesabu ya Walawi waliohesabiwa na Mose na Aroni kwa amri ya Bwana, kufuatana na koo, pamoja na kila mume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walikuwa 22,000.
All who were numbered of the Levites, whom Moses and Aaron numbered at the commandment of Jehovah, by their families, all the males from a month old and upward, were twenty-two thousand.
40 Bwana akamwambia Mose, “Wahesabu wazaliwa wa kwanza wa kiume wote wa Waisraeli wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi na uorodheshe majina yao.
And Jehovah said to Moses, Number all the firstborn males of the sons of Israel from a month old and upward, and take the number of their names.
41 Nitwalie Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya wazaliwa wa mifugo ya Waisraeli. Mimi ndimi Bwana.”
And thou shall take the Levites for me (I am Jehovah) instead of all the firstborn among the sons of Israel, and the cattle of the Levites instead of all the firstlings among the cattle of the sons of Israel.
42 Hivyo Mose akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru.
And Moses numbered, as Jehovah commanded him, all the firstborn among the sons of Israel.
43 Jumla ya hesabu ya wazaliwa wa kwanza waume wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walioorodheshwa kwa majina, walikuwa 22,273.
And all the firstborn males according to the number of names, from a month old and upward, of those who were numbered of them, were twenty-two thousand two hundred and seventy-three.
44 Bwana akamwambia Mose,
And Jehovah spoke to Moses, saying,
45 “Watwae Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya mifugo yao. Walawi watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.
Take the Levites instead of all the firstborn among the sons of Israel, and the cattle of the Levites instead of their cattle. And the Levites shall be mine. I am Jehovah.
46 Ili kukomboa wazao wa kwanza 273 wa Waisraeli ambao wamezidi hesabu ya Walawi,
And for the redemption of the two hundred and seventy-three of the firstborn of the sons of Israel, who are over and above the number of the Levites,
47 kusanya shekeli tano kwa kila mmoja, kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu, ambayo ina uzito wa gera ishirini.
thou shall take five shekels apiece by the poll. According to the shekel of the sanctuary thou shall take them (the shekel is twenty gerahs),
48 Mpe Aroni na wanawe hizo fedha kwa ajili ya ukombozi wa idadi ya Waisraeli waliozidi.”
and thou shall give the money, with which the odd number of them is redeemed, to Aaron and to his sons.
49 Kwa hiyo Mose akakusanya fedha za ukombozi kutoka kwa wale ambao hesabu yao ilizidi wale waliokombolewa na Walawi.
And Moses took the redemption-money from those who were over and above those who were redeemed by the Levites.
50 Kutokana na wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli alikusanya fedha yenye uzito wa shekeli 1,365 kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu.
He took the money from the firstborn of the sons of Israel, a thousand three hundred and sixty-five shekels, according to the shekel of the sanctuary.
51 Mose akampa Aroni na wanawe ile fedha ya ukombozi, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.
And Moses gave the redemption-money to Aaron and to his sons, according to the word of Jehovah, as Jehovah commanded Moses.