< Hesabu 29 >

1 “‘Katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu na msifanye kazi ya kawaida. Ni siku kwa ajili yenu ya kupiga tarumbeta.
“Celebren una reunión sagrada el primer día del séptimo mes. No hagas nada de tu trabajo normal. Este es el día en que tocarás las trompetas.
2 Mtatayarisha sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri impendezayo Bwana ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Presenten un holocausto de un novillo, un carnero y siete corderos machos de un año, todos ellos sin defectos, como sacrificio aceptable al Señor,
3 Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume, andaa unga sehemu ya kumi mbili za efa;
junto con sus ofrendas de grano de la mejor harina mezclada con aceite de oliva: tres décimos de un efa para el toro, dos décimos de un efa para el carnero,
4 na pamoja na wana-kondoo saba kila mmoja aandaliwe na sehemu ya kumi ya efa ya unga.
y un décimo de un efa para cada uno de los siete corderos machos.
5 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
Presenten también una cabra macho como ofrenda por el pecado para hacerte justicia.
6 Hivi ni nyongeza ya sadaka za kuteketezwa kila mwezi na kila siku pamoja na sadaka zake za nafaka na sadaka za vinywaji kama ilivyoainishwa. Ni sadaka zinazotolewa kwa Bwana kwa moto, harufu inayopendeza.
Estas ofrendas se suman a los holocaustos mensuales y diarios junto con las ofrendas de grano y las ofrendas de bebida requeridas. Son ofrendas quemadas aceptables para el Señor.
7 “‘Kwenye siku ya kumi ya mwezi huu wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu. Mtajikana wenyewe na msifanye kazi.
“Celebrarás una reunión sagrada el décimo día de este séptimo mes, y practiquen la abnegación. No hagas nada de tu trabajo normal.
8 Toeni sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
Presenta un holocausto de un novillo, un carnero y siete corderos machos de un año, todos ellos sin defectos, aceptables para el Señor.
9 Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
Deben ir acompañados de sus ofrendas de grano de la mejor harina mezclada con aceite de oliva: tres décimas de efa para el toro, dos décimas de efa para el carnero,
10 na kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba andaa sehemu ya kumi ya unga laini kwa kila mmoja.
y una décima de efa para cada uno de los siete corderos.
11 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya dhambi kwa ajili ya upatanisho, na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, na sadaka zake za vinywaji.
Presenta también un macho cabrío como ofrenda por el pecado, además de la ofrenda por el pecado para corregirte y el holocausto continuo con su ofrenda de grano y su libación.
12 “‘Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu, na hamtafanya kazi za kawaida. Adhimisheni sikukuu kwa Bwana kwa siku saba.
“Celebrea una reunión sagrada el día quince del séptimo mes. No hagas nada de tu trabajo normal. Debes celebrar un festival dedicado al Señor durante siete días.
13 Toeni sadaka ya kuteketezwa mafahali wachanga kumi na watatu, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
Presenta como holocausto aceptable al Señor: trece novillos, dos carneros y catorce corderos machos de un año, todos ellos sin defectos.
14 Pamoja na hao mafahali kumi na watatu, kila mmoja aandaliwe na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume wawili, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
Se acompañarán con sus ofrendas de grano de la mejor harina mezclada con aceite de oliva: tres décimas de efa de la mejor harina mezclada con aceite de oliva por cada uno de los trece toros, dos décimas de efa por cada uno de los dos carneros,
15 na kwa wana-kondoo kumi na wanne, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi ya efa ya unga laini.
y una décima de efa por cada uno de los catorce corderos.
16 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka ya vinywaji.
También presentarás un macho cabrío como ofrenda por el pecado además del holocausto continuo con su ofrenda de grano y su libación.
17 “‘Katika siku ya pili andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
“El segundo día, presente doce novillos, dos carneros y catorce corderos machos de un año, todos ellos sin defectos.
18 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
Deben ir acompañados por sus ofrendas de grano y bebidas para los toros, carneros y corderos, todo según el número requerido.
19 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
Presenta también un macho cabrío como ofrenda por el pecado, además del continuo holocausto con su ofrenda de grano y su libación.
20 “‘Katika siku ya tatu andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
“Al tercer día, presenta once novillos, dos carneros y catorce corderos machos de un año de edad, todos ellos sin defectos.
21 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
Deben estar acompañados por sus ofrendas de grano y libaciones para los toros, carneros y corderos, todo de acuerdo al número requerido.
22 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
Presenta también un macho cabrío como ofrenda por el pecado además del holocausto continuo con su ofrenda de grano y su libación.
23 “‘Katika siku ya nne andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
“Al cuarto día presentarás diez novillos, dos carneros y catorce corderos machos de un año, todos ellos sin defectos.
24 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
Deben ir acompañados por sus ofrendas de grano y libaciones para los toros, carneros y corderos, todo de acuerdo al número requerido.
25 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
También presentarás un macho cabrío como ofrenda por el pecado, además del continuo holocausto con su ofrenda de grano y su libación.
26 “‘Katika siku ya tano andaeni mafahali tisa, kondoo dume wawili na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
“El quinto día presentarás nueve novillos, dos carneros y catorce corderos machos de un año, todos ellos sin defectos.
27 Pamoja na mafahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za kinywaji kulingana na idadi iliyoainishwa.
Deben ir acompañados por sus ofrendas de grano y libaciones para los toros, carneros y corderos, todo de acuerdo con el número requerido.
28 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
Presentarás también un macho cabrío como ofrenda por el pecado, además del continuo holocausto con su ofrenda de grano y su libación.
29 “‘Katika siku ya sita andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
“Al sexto día presentarás ocho novillos, dos carneros y catorce corderos machos de un año, todos ellos sin defectos.
30 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
Deben estar acompañados por sus ofrendas de grano y libaciones para los toros, carneros y corderos, todo de acuerdo al número requerido.
31 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
También se presentará un macho cabrío como ofrenda por el pecado, además del continuo holocausto con su ofrenda de grano y su libación.
32 “‘Katika siku ya saba andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
“Al séptimo día presentar siete novillos, dos carneros y catorce corderos machos de un año de edad, todos ellos sin defectos.
33 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
Deben estar acompañados por sus ofrendas de grano y libaciones para los toros, carneros y corderos, todo de acuerdo al número requerido.
34 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
También se presentará un macho cabrío como ofrenda por el pecado, además del continuo holocausto con su ofrenda de grano y su libación.
35 “‘Katika siku ya nane mtakuwa na kusanyiko, na msifanye kazi ya kawaida.
“En el octavo día todos ustedes se reunirán juntos. No hagan nada de su trabajo normal.
36 Toeni sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Presenta como holocausto aceptable al Señor: un toro, dos carneros y siete corderos machos de un año, todos ellos sin defectos.
37 Pamoja na fahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka, na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
Deben ir acompañados de sus ofrendas de grano y de las libaciones para los toros, carneros y corderos, todo según el número requerido.
38 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
También se presentará un macho cabrío como ofrenda por el pecado, además del continuo holocausto con su ofrenda de grano y su libación.
39 “‘Zaidi ya kile unachoweka nadhiri na sadaka zenu za hiari, andaeni hizi kwa ajili ya Bwana kwenye sikukuu zenu zilizoamriwa: sadaka zenu za kuteketezwa, sadaka za nafaka, sadaka za vinywaji, pamoja na sadaka zenu za amani.’”
“Presenta estas ofrendas al Señor en los momentos en que se te requiera, además de tus ofrendas para cumplir una promesa y las ofrendas de libre albedrío, ya sean holocaustos, ofrendas de grano, libaciones o sacrificios de paz”.
40 Mose akawaambia Waisraeli yale yote Bwana alimwagiza.
Moisés repitió todo esto a los israelitas como el Señor se lo ordenó.

< Hesabu 29 >