< Hesabu 29 >
1 “‘Katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu na msifanye kazi ya kawaida. Ni siku kwa ajili yenu ya kupiga tarumbeta.
V sedmem mesecu, na prvi dan meseca, boste imeli sveti sklic. Nobenega hlapčevskega dela ne boste opravljali. To vam je dan trobentanja.
2 Mtatayarisha sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri impendezayo Bwana ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Darovali boste žgalno daritev v prijeten vonj Gospodu: enega mladega bikca, enega ovna in sedem jagnjet prvega leta brez pomanjkljivosti
3 Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume, andaa unga sehemu ya kumi mbili za efa;
in njihova jedilna daritev bo iz moke, umešane z oljem, tri desetinke za bikca in dve desetinki za ovna
4 na pamoja na wana-kondoo saba kila mmoja aandaliwe na sehemu ya kumi ya efa ya unga.
in ena desetinka za eno jagnje, za sedem jagnjet,
5 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
in enega kozlička od koz za daritev za greh, da za vas opravi spravo,
6 Hivi ni nyongeza ya sadaka za kuteketezwa kila mwezi na kila siku pamoja na sadaka zake za nafaka na sadaka za vinywaji kama ilivyoainishwa. Ni sadaka zinazotolewa kwa Bwana kwa moto, harufu inayopendeza.
poleg mesečne žgalne daritve, njene jedilne daritve, dnevne žgalne daritve, njene jedilne daritve in njihovih pitnih daritev, glede na njihov način, za prijeten vonj, žrtvovanje, narejeno z ognjem, Gospodu.
7 “‘Kwenye siku ya kumi ya mwezi huu wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu. Mtajikana wenyewe na msifanye kazi.
Na deseti dan sedmega meseca boste imeli sveti sklic in prizadeli boste svoje duše. Ta dan ne boste opravljali nobenega dela,
8 Toeni sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
temveč boste darovali žgalno daritev Gospodu v prijeten vonj: enega mladega bikca, enega ovna in sedem jagnjet prvega leta, ki vam bodo brez pomanjkljivosti,
9 Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
in njihova jedilna daritev bo iz moke, umešane z oljem, tri desetinke za bikca in dve desetinki za enega ovna,
10 na kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba andaa sehemu ya kumi ya unga laini kwa kila mmoja.
nekaj desetink za eno jagnje, za sedem jagnjet,
11 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya dhambi kwa ajili ya upatanisho, na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, na sadaka zake za vinywaji.
enega kozlička od koz za daritev za greh, poleg spravne daritve za greh in nenehne žgalne daritve in njegove jedilne daritve in njihovih pitnih daritev.
12 “‘Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu, na hamtafanya kazi za kawaida. Adhimisheni sikukuu kwa Bwana kwa siku saba.
Na petnajsti dan sedmega meseca boste imeli sveti sklic. Nobenega hlapčevskega dela ne boste opravljali in sedem dni boste imeli praznovanje Gospodu.
13 Toeni sadaka ya kuteketezwa mafahali wachanga kumi na watatu, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
Darovali boste žgalno daritev, žrtvovanje, narejeno z ognjem, prijetnega vonja Gospodu: trinajst mladih bikcev, dva ovna in štirinajst jagnjet prvega leta; ti bodo brez pomanjkljivosti.
14 Pamoja na hao mafahali kumi na watatu, kila mmoja aandaliwe na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume wawili, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
Njihova jedilna daritev bo moka, umešana z oljem, tri desetinke vsakemu bikcu izmed trinajstih bikcev, dve desetinki vsakemu ovnu izmed dveh ovnov,
15 na kwa wana-kondoo kumi na wanne, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi ya efa ya unga laini.
in nekaj desetink za vsako izmed štirinajstih jagnjet
16 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka ya vinywaji.
in enega kozlička od koz za daritev za greh, poleg nenehne žgalne daritve, njegove jedilne daritve in njegove pitne daritve.
17 “‘Katika siku ya pili andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Na drugi dan boste darovali dvanajst mladih bikcev, dva ovna, štirinajst jagnjet prvega leta brez madeža,
18 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
in njihova jedilna daritev in njihove pitne daritve za bikce, za ovne in za jagnjeta bodo glede na njihovo število, po načinu:
19 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
enega kozlička od koz za daritev za greh, poleg nenehne žgalne daritve in njegovih jedilnih daritev in njihovih pitnih daritev.
20 “‘Katika siku ya tatu andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Na tretji dan enajst bikcev, dva ovna, štirinajst jagnjet prvega leta brez pomanjkljivosti
21 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
in njihova jedilna daritev in njihove pitne daritve za bikce, za ovne in za jagnjeta bodo glede na njihovo število, po načinu:
22 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
enega kozla za daritev za greh, poleg nenehne žgalne daritve in njegove jedilne daritve in njegove pitne daritve.
23 “‘Katika siku ya nne andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Na četrti dan deset bikcev, dva ovna in štirinajst jagnjet prvega leta brez pomanjkljivosti.
24 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
Njihova jedilna daritev in njihove pitne daritve za bikce, za ovne in za jagnjeta bodo glede na njihovo število, po načinu:
25 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
enega kozlička od koz za daritev za greh, poleg nenehne žgalne daritve, njegove jedilne daritve in njegove pitne daritve.
26 “‘Katika siku ya tano andaeni mafahali tisa, kondoo dume wawili na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Na peti dan devet bikcev, dva ovna in štirinajst jagnjet prvega leta brez madeža
27 Pamoja na mafahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za kinywaji kulingana na idadi iliyoainishwa.
in njihova jedilna daritev in njihove pitne daritve za bikce, za ovne in za jagnjeta bodo glede na njihovo število, po načinu:
28 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
enega kozla za daritev za greh, poleg nenehne žgalne daritve in njegove jedilne daritve in njegove pitne daritve.
29 “‘Katika siku ya sita andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Na šesti dan osem bikcev, dva ovna in štirinajst jagnjet prvega leta brez pomanjkljivosti
30 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
in njihova jedilna daritev in njihove pitne daritve za bikce, za ovne in za jagnjeta bodo glede na njihovo število, po načinu:
31 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
enega kozla za daritev za greh, poleg nenehne žgalne daritve, njegove jedilne daritve in njegove pitne daritve.
32 “‘Katika siku ya saba andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Na sedmi dan sedem bikcev, dva ovna in štirinajst jagnjet prvega leta brez pomanjkljivosti
33 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
in njihova jedilna daritev in njihove pitne daritve za bikce, za ovne in za jagnjeta bodo glede na njihovo število, po načinu:
34 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
enega kozla za daritev za greh, poleg nenehne žgalne daritve, njegove jedilne daritve in njegove pitne daritve.
35 “‘Katika siku ya nane mtakuwa na kusanyiko, na msifanye kazi ya kawaida.
Na osmi dan boste imeli slovesen zbor. Nobenega hlapčevskega dela ne boste opravljali ta dan,
36 Toeni sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
temveč boste žrtvovali žgalno daritev, žrtvovanje, narejeno z ognjem, prijetnega vonja Gospodu: enega bikca, enega ovna, sedem jagnjet prvega leta brez pomanjkljivosti.
37 Pamoja na fahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka, na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
Njihova jedilna daritev in njihove pitne daritve za bikca, za ovna in za jagnjeta bodo glede na njihovo število, po načinu:
38 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
enega kozla za daritev za greh, poleg nenehne žgalne daritve in njegove jedilne daritve in njegove pitne daritve.
39 “‘Zaidi ya kile unachoweka nadhiri na sadaka zenu za hiari, andaeni hizi kwa ajili ya Bwana kwenye sikukuu zenu zilizoamriwa: sadaka zenu za kuteketezwa, sadaka za nafaka, sadaka za vinywaji, pamoja na sadaka zenu za amani.’”
Te stvari boste storili Gospodu na svoje določene praznike, poleg svojih zaobljub in svojih prostovoljnih daritev za svoje žgalne daritve, jedilne daritve, pitne daritve in za svoje mirovne daritve.‹«
40 Mose akawaambia Waisraeli yale yote Bwana alimwagiza.
Mojzes je Izraelovim otrokom povedal glede na vse, kar je Gospod zapovedal Mojzesu.