< Hesabu 29 >
1 “‘Katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu na msifanye kazi ya kawaida. Ni siku kwa ajili yenu ya kupiga tarumbeta.
I den syvende måned, på den første dag i måneden, skal I holde en hellig sammenkomst; I skal ikke gjøre nogen arbeidsgjerning; den dag skal basunene lyde hos eder.
2 Mtatayarisha sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri impendezayo Bwana ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Og I skal ofre et brennoffer til en velbehagelig duft for Herren: en ung okse og en vær og syv årsgamle lam uten lyte,
3 Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume, andaa unga sehemu ya kumi mbili za efa;
og som tilhørende matoffer fint mel blandet med olje, tre tiendedeler av en efa til oksen, to tiendedeler til væren
4 na pamoja na wana-kondoo saba kila mmoja aandaliwe na sehemu ya kumi ya efa ya unga.
og en tiendedel for hvert av de syv lam,
5 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
og en gjetebukk som syndoffer, til å gjøre soning for eder,
6 Hivi ni nyongeza ya sadaka za kuteketezwa kila mwezi na kila siku pamoja na sadaka zake za nafaka na sadaka za vinywaji kama ilivyoainishwa. Ni sadaka zinazotolewa kwa Bwana kwa moto, harufu inayopendeza.
foruten måneds-brennofferet med tilhørende matoffer og det stadige brennoffer med tilhørende matoffer og foreskrevne drikkoffer, til en velbehagelig duft, et ildoffer for Herren.
7 “‘Kwenye siku ya kumi ya mwezi huu wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu. Mtajikana wenyewe na msifanye kazi.
Den tiende dag i den samme syvende måned skal I holde en hellig sammenkomst; da skal I faste. I skal ikke gjøre nogen arbeidsgjerning.
8 Toeni sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
Og I skal ofre Herren et brennoffer til en velbehagelig duft: en ung okse og en vær og syv årsgamle lam - uten lyte skal de være -
9 Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
og som tilhørende matoffer fint mel blandet med olje, tre tiendedeler av en efa til oksen, to tiendedeler til væren
10 na kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba andaa sehemu ya kumi ya unga laini kwa kila mmoja.
Og en tiendedel for hvert av de syv lam,
11 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya dhambi kwa ajili ya upatanisho, na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, na sadaka zake za vinywaji.
Og en gjetebukk som syndoffer, foruten sonings-syndofferet og det stadige brennoffer med tilhørende matoffer og drikkoffer.
12 “‘Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu, na hamtafanya kazi za kawaida. Adhimisheni sikukuu kwa Bwana kwa siku saba.
Den femtende dag i den syvende måned skal I holde en hellig sammenkomst; I skal ikke gjøre nogen arbeidsgjerning; I skal holde høitid for Herren i syv dager.
13 Toeni sadaka ya kuteketezwa mafahali wachanga kumi na watatu, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
Og I skal ofre et brennoffer, et ildoffer til en velbehagelig duft for Herren: tretten unge okser og to værer og fjorten årsgamle lam - uten lyte skal de være -
14 Pamoja na hao mafahali kumi na watatu, kila mmoja aandaliwe na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume wawili, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
og som tilhørende matoffer fint mel blandet med olje, tre tiendedeler av en efa for hver av de tretten okser, to tiendedeler for hver av de to værer,
15 na kwa wana-kondoo kumi na wanne, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi ya efa ya unga laini.
og en tiendedel for hvert av de fjorten lam,
16 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka ya vinywaji.
og en gjetebukk som syndoffer, foruten det stadige brennoffer med tilhørende matoffer og drikkoffer.
17 “‘Katika siku ya pili andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Og den annen dag tolv unge okser og to værer og fjorten årsgamle lam uten lyte
18 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
med tilhørende matoffer og drikkoffer, svarende til tallet på oksene og værene og lammene, alt således som foreskrevet er,
19 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
og en gjetebukk som syndoffer, foruten det stadige brennoffer med tilhørende matoffer og drikkoffer.
20 “‘Katika siku ya tatu andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Og den tredje dag elleve okser og to værer og fjorten årsgamle lam uten lyte,
21 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
med tilhørende matoffer og drikkoffer, svarende til tallet på oksene og værene og lammene, således som foreskrevet er,
22 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
og en gjetebukk som syndoffer, foruten det stadige brennoffer med tilhørende matoffer og drikkoffer.
23 “‘Katika siku ya nne andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Og den fjerde dag ti okser og to værer og fjorten årsgamle lam uten lyte,
24 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
med tilhørende matoffer og drikkoffer, svarende til tallet på oksene og værene og lammene, således som foreskrevet er,
25 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
og en gjetebukk som syndoffer, foruten det stadige brennoffer med tilhørende matoffer og drikkoffer.
26 “‘Katika siku ya tano andaeni mafahali tisa, kondoo dume wawili na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Og den femte dag ni okser og to værer og fjorten årsgamle lam uten lyte,
27 Pamoja na mafahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za kinywaji kulingana na idadi iliyoainishwa.
med tilhørende matoffer og drikkoffer, svarende til tallet på oksene og værene og lammene, således som foreskrevet er,
28 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
og en gjetebukk som syndoffer, foruten det stadige brennoffer med tilhørende matoffer og drikkoffer.
29 “‘Katika siku ya sita andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Og den sjette dag åtte okser og to værer og fjorten årsgamle lam uten lyte,
30 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
med tilhørende matoffer og drikkoffer, svarende til tallet på oksene og værene og lammene, således som foreskrevet er,
31 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
og en gjetebukk som syndoffer, foruten det stadige brennoffer med tilhørende matoffer og drikkoffer.
32 “‘Katika siku ya saba andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Og den syvende dag syv okser og to værer og fjorten årsgamle lam uten lyte,
33 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
med tilhørende matoffer og drikkoffer, svarende til tallet på oksene og værene og lammene, således som foreskrevet er,
34 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
og en gjetebukk som syndoffer, foruten det stadige brennoffer med tilhørende matoffer og drikkoffer.
35 “‘Katika siku ya nane mtakuwa na kusanyiko, na msifanye kazi ya kawaida.
Den åttende dag skal I holde en festlig sammenkomst; I skal ikke gjøre nogen arbeidsgjerning.
36 Toeni sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Og I skal ofre et brennoffer, et ildoffer til en velbehagelig duft for Herren: en okse og en vær og syv årsgamle lam uten lyte,
37 Pamoja na fahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka, na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
med tilhørende matoffer og drikkoffer, svarende til oksen og væren og lammene efter deres tall, således som foreskrevet er,
38 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
og en gjetebukk som syndoffer, foruten det stadige brennoffer med tilhørende matoffer og drikkoffer.
39 “‘Zaidi ya kile unachoweka nadhiri na sadaka zenu za hiari, andaeni hizi kwa ajili ya Bwana kwenye sikukuu zenu zilizoamriwa: sadaka zenu za kuteketezwa, sadaka za nafaka, sadaka za vinywaji, pamoja na sadaka zenu za amani.’”
Disse offer skal I ofre Herren på eders høitider, foruten eders lovede og eders frivillige offer, enten det er brennoffer eller matoffer eller drikkoffer eller takkoffer.
40 Mose akawaambia Waisraeli yale yote Bwana alimwagiza.
Og Moses sa dette til Israels barn, i ett og alt som Herren hadde befalt ham.