< Hesabu 29 >
1 “‘Katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu na msifanye kazi ya kawaida. Ni siku kwa ajili yenu ya kupiga tarumbeta.
Et au septième mois, le premier [jour] du mois, vous aurez une sainte convocation; vous ne ferez aucune œuvre de service; ce sera pour vous le jour du son éclatant [des trompettes].
2 Mtatayarisha sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri impendezayo Bwana ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Et vous offrirez un holocauste en odeur agréable à l’Éternel, un jeune taureau, un bélier, sept agneaux âgés d’un an, sans défaut;
3 Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume, andaa unga sehemu ya kumi mbili za efa;
et leur offrande de gâteau de fleur de farine pétrie à l’huile, trois dixièmes pour le taureau, deux dixièmes pour le bélier,
4 na pamoja na wana-kondoo saba kila mmoja aandaliwe na sehemu ya kumi ya efa ya unga.
et un dixième pour un agneau, pour les sept agneaux;
5 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
et un bouc en sacrifice pour le péché, afin de faire propitiation pour vous,
6 Hivi ni nyongeza ya sadaka za kuteketezwa kila mwezi na kila siku pamoja na sadaka zake za nafaka na sadaka za vinywaji kama ilivyoainishwa. Ni sadaka zinazotolewa kwa Bwana kwa moto, harufu inayopendeza.
– outre l’holocauste du mois, et son gâteau, et l’holocauste continuel et son gâteau, et leurs libations, selon leur ordonnance, en odeur agréable, un sacrifice par feu à l’Éternel.
7 “‘Kwenye siku ya kumi ya mwezi huu wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu. Mtajikana wenyewe na msifanye kazi.
Et le dixième [jour] de ce septième mois, vous aurez une sainte convocation, et vous affligerez vos âmes; vous ne ferez aucune œuvre.
8 Toeni sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
Et vous présenterez à l’Éternel un holocauste d’odeur agréable, un jeune taureau, un bélier, sept agneaux âgés d’un an (vous les prendrez sans défaut);
9 Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
et leur offrande de gâteau de fleur de farine pétrie à l’huile, trois dixièmes pour le taureau, deux dixièmes pour le bélier,
10 na kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba andaa sehemu ya kumi ya unga laini kwa kila mmoja.
un dixième par agneau, pour les sept agneaux;
11 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya dhambi kwa ajili ya upatanisho, na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, na sadaka zake za vinywaji.
[et] un bouc en sacrifice pour le péché, – outre le sacrifice de péché des propitiations, et l’holocauste continuel et son gâteau, et leurs libations.
12 “‘Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu, na hamtafanya kazi za kawaida. Adhimisheni sikukuu kwa Bwana kwa siku saba.
Et le quinzième jour du septième mois, vous aurez une sainte convocation; vous ne ferez aucune œuvre de service, et vous célébrerez une fête à l’Éternel pendant sept jours.
13 Toeni sadaka ya kuteketezwa mafahali wachanga kumi na watatu, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
Et vous présenterez un holocauste, un sacrifice par feu d’odeur agréable à l’Éternel, 13 jeunes taureaux, deux béliers, 14 agneaux âgés d’un an (ils seront sans défaut);
14 Pamoja na hao mafahali kumi na watatu, kila mmoja aandaliwe na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume wawili, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
et leur offrande de gâteau de fleur de farine pétrie à l’huile, trois dixièmes par taureau, pour les 13 taureaux, deux dixièmes par bélier, pour les deux béliers,
15 na kwa wana-kondoo kumi na wanne, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi ya efa ya unga laini.
et un dixième par agneau, pour les 14 agneaux;
16 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka ya vinywaji.
et un bouc en sacrifice pour le péché, – outre l’holocauste continuel, son gâteau et sa libation.
17 “‘Katika siku ya pili andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Et le second jour, [vous présenterez] douze jeunes taureaux, deux béliers, 14 agneaux âgés d’un an, sans défaut;
18 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
et leur offrande de gâteau et leurs libations pour les taureaux, pour les béliers, et pour les agneaux, d’après leur nombre, selon l’ordonnance;
19 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
et un bouc en sacrifice pour le péché, – outre l’holocauste continuel et son gâteau, et leurs libations.
20 “‘Katika siku ya tatu andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Et le troisième jour, onze taureaux, deux béliers, 14 agneaux âgés d’un an, sans défaut;
21 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
et leur offrande de gâteau et leurs libations pour les taureaux, pour les béliers, et pour les agneaux, d’après leur nombre, selon l’ordonnance;
22 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
et un bouc en sacrifice pour le péché, – outre l’holocauste continuel et son gâteau et sa libation.
23 “‘Katika siku ya nne andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Et le quatrième jour, dix taureaux, deux béliers, 14 agneaux âgés d’un an, sans défaut;
24 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
leur offrande de gâteau et leurs libations pour les taureaux, pour les béliers, et pour les agneaux, d’après leur nombre, selon l’ordonnance;
25 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
et un bouc en sacrifice pour le péché, – outre l’holocauste continuel, son gâteau et sa libation.
26 “‘Katika siku ya tano andaeni mafahali tisa, kondoo dume wawili na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Et le cinquième jour, neuf taureaux, deux béliers, 14 agneaux âgés d’un an, sans défaut;
27 Pamoja na mafahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za kinywaji kulingana na idadi iliyoainishwa.
et leur offrande de gâteau et leurs libations pour les taureaux, pour les béliers, et pour les agneaux, d’après leur nombre, selon l’ordonnance;
28 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
et un bouc en sacrifice pour le péché, – outre l’holocauste continuel et son gâteau et sa libation.
29 “‘Katika siku ya sita andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Et le sixième jour, huit taureaux, deux béliers, 14 agneaux âgés d’un an, sans défaut;
30 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
et leur offrande de gâteau et leurs libations pour les taureaux, pour les béliers, et pour les agneaux, d’après leur nombre, selon l’ordonnance;
31 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
et un bouc en sacrifice pour le péché, – outre l’holocauste continuel, son gâteau et ses libations.
32 “‘Katika siku ya saba andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Et le septième jour, sept taureaux, deux béliers, 14 agneaux âgés d’un an, sans défaut;
33 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
et leur offrande de gâteau et leurs libations pour les taureaux, pour les béliers, et pour les agneaux, d’après leur nombre, selon leur ordonnance;
34 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
et un bouc en sacrifice pour le péché, – outre l’holocauste continuel, son gâteau et sa libation.
35 “‘Katika siku ya nane mtakuwa na kusanyiko, na msifanye kazi ya kawaida.
Le huitième jour, vous aurez une fête solennelle; vous ne ferez aucune œuvre de service.
36 Toeni sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Et vous présenterez un holocauste, un sacrifice par feu d’odeur agréable à l’Éternel, un taureau, un bélier, sept agneaux âgés d’un an, sans défaut;
37 Pamoja na fahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka, na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
leur offrande de gâteau et leurs libations pour le taureau, pour le bélier, et pour les agneaux, d’après leur nombre, selon l’ordonnance;
38 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
et un bouc en sacrifice pour le péché, – outre l’holocauste continuel et son gâteau et sa libation.
39 “‘Zaidi ya kile unachoweka nadhiri na sadaka zenu za hiari, andaeni hizi kwa ajili ya Bwana kwenye sikukuu zenu zilizoamriwa: sadaka zenu za kuteketezwa, sadaka za nafaka, sadaka za vinywaji, pamoja na sadaka zenu za amani.’”
Vous offrirez ces choses à l’Éternel dans vos jours solennels, outre vos vœux et vos offrandes volontaires en vos holocaustes et vos offrandes de gâteau, et vos libations, et vos sacrifices de prospérités.
40 Mose akawaambia Waisraeli yale yote Bwana alimwagiza.
Et Moïse parla aux fils d’Israël selon tout ce que l’Éternel avait commandé à Moïse.