< Hesabu 29 >
1 “‘Katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu na msifanye kazi ya kawaida. Ni siku kwa ajili yenu ya kupiga tarumbeta.
And in the seventh month, on the first of the month, ye shall have a holy convocation: no manner of servile work shall ye do; a day of blowing the trumpets shall it be unto you.
2 Mtatayarisha sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri impendezayo Bwana ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
And ye shall offer a burnt-offering for a sweet odour to Jehovah: one young bullock, one ram, seven yearling lambs without blemish;
3 Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume, andaa unga sehemu ya kumi mbili za efa;
and their oblation of fine flour mingled with oil, three tenth parts for the bullock, two tenth parts for the ram,
4 na pamoja na wana-kondoo saba kila mmoja aandaliwe na sehemu ya kumi ya efa ya unga.
and one tenth part for each lamb of the seven lambs;
5 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
and one buck of the goats for a sin-offering, to make atonement for you,
6 Hivi ni nyongeza ya sadaka za kuteketezwa kila mwezi na kila siku pamoja na sadaka zake za nafaka na sadaka za vinywaji kama ilivyoainishwa. Ni sadaka zinazotolewa kwa Bwana kwa moto, harufu inayopendeza.
— besides the monthly burnt-offering and its oblation, and the continual burnt-offering and its oblation, and their drink-offerings, according to their ordinance, for a sweet odour, an offering by fire to Jehovah.
7 “‘Kwenye siku ya kumi ya mwezi huu wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu. Mtajikana wenyewe na msifanye kazi.
And on the tenth of this seventh month ye shall have a holy convocation; and ye shall afflict your souls; no manner of work shall ye do.
8 Toeni sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
And ye shall present a burnt-offering to Jehovah for a sweet odour: one young bullock, one ram, seven yearling lambs (without blemish shall they be unto you);
9 Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
and their oblation of fine flour mingled with oil, three tenth parts for the bullock, two tenth parts for the ram,
10 na kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba andaa sehemu ya kumi ya unga laini kwa kila mmoja.
one tenth part for each lamb, of the seven lambs;
11 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya dhambi kwa ajili ya upatanisho, na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, na sadaka zake za vinywaji.
[and] one buck of the goats for a sin-offering, — besides the sin-offering of atonement, and the continual burnt-offering and its oblation, and their drink-offerings.
12 “‘Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu, na hamtafanya kazi za kawaida. Adhimisheni sikukuu kwa Bwana kwa siku saba.
And on the fifteenth day of the seventh month ye shall have a holy convocation: no manner of servile work shall ye do; and ye shall celebrate a feast to Jehovah seven days;
13 Toeni sadaka ya kuteketezwa mafahali wachanga kumi na watatu, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
and ye shall present a burnt-offering, an offering by fire for a sweet odour to Jehovah: thirteen young bullocks, two rams, fourteen yearling lambs (they shall be without blemish);
14 Pamoja na hao mafahali kumi na watatu, kila mmoja aandaliwe na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume wawili, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
and their oblation of fine flour mingled with oil: three tenth parts for each bullock of the thirteen bullocks, two tenth parts for each ram of the two rams,
15 na kwa wana-kondoo kumi na wanne, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi ya efa ya unga laini.
and one tenth part for each lamb of the fourteen lambs;
16 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka ya vinywaji.
and one buck of the goats for a sin-offering, — besides the continual burnt-offering, its oblation and its drink-offering.
17 “‘Katika siku ya pili andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
And on the second day, [ye shall present] twelve young bullocks, two rams, fourteen yearling lambs without blemish;
18 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
and their oblation and their drink-offerings for the bullocks, for the rams, and for the lambs, by their number, according to the ordinance;
19 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
and one buck of the goats for a sin-offering, — besides the continual burnt-offering and its oblation, and their drink-offerings.
20 “‘Katika siku ya tatu andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
And on the third day, eleven bullocks, two rams, fourteen yearling lambs without blemish;
21 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
and their oblation and their drink-offerings for the bullocks, for the rams, and for the lambs, by their number, according to the ordinance;
22 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
and one he-goat for a sin-offering, — besides the continual burnt-offering and its oblation and its drink-offering.
23 “‘Katika siku ya nne andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
And on the fourth day, ten bullocks, two rams, fourteen yearling lambs without blemish;
24 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
their oblation and their drink-offerings for the bullocks, for the rams, and for the lambs, by their number, according to the ordinance;
25 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
and one buck of the goats for a sin-offering, — besides the continual burnt-offering, its oblation and its drink-offering.
26 “‘Katika siku ya tano andaeni mafahali tisa, kondoo dume wawili na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
And on the fifth day, nine bullocks, two rams, fourteen yearling lambs without blemish;
27 Pamoja na mafahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za kinywaji kulingana na idadi iliyoainishwa.
and their oblation and their drink-offerings for the bullocks, for the rams, and for the lambs, by their number, according to the ordinance;
28 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
and one he-goat for a sin-offering, — besides the continual burnt-offering and its oblation and its drink-offering.
29 “‘Katika siku ya sita andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
And on the sixth day, eight bullocks, two rams, fourteen yearling lambs without blemish;
30 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
and their oblation and their drink-offerings for the bullocks, for the rams, and for the lambs, by their number, according to the ordinance;
31 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
and one he-goat for a sin-offering, — besides the continual burnt-offering, its oblation and its drink-offerings.
32 “‘Katika siku ya saba andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
And on the seventh day, seven bullocks, two rams, fourteen yearling lambs without blemish;
33 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
and their oblation and their drink-offerings for the bullocks, for the rams, and for the lambs, by their number, according to their ordinance;
34 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
and one he-goat for a sin-offering, — besides the continual burnt-offering, its oblation and its drink-offering.
35 “‘Katika siku ya nane mtakuwa na kusanyiko, na msifanye kazi ya kawaida.
On the eighth day ye shall have a solemn assembly: no manner of servile work shall ye do.
36 Toeni sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
And ye shall present a burnt-offering, an offering by fire of a sweet odour to Jehovah: one bullock, one ram, seven yearling lambs without blemish;
37 Pamoja na fahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka, na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
their oblation and their drink-offerings for the bullock, for the ram, and for the lambs, by their number, according to the ordinance;
38 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
and one he-goat for a sin-offering, — besides the continual burnt-offering and its oblation and its drink-offering.
39 “‘Zaidi ya kile unachoweka nadhiri na sadaka zenu za hiari, andaeni hizi kwa ajili ya Bwana kwenye sikukuu zenu zilizoamriwa: sadaka zenu za kuteketezwa, sadaka za nafaka, sadaka za vinywaji, pamoja na sadaka zenu za amani.’”
These shall ye offer to Jehovah in your set feasts, besides your vows, and your voluntary-offerings, for your burnt-offerings, and for your oblations, and for your drink-offerings, and for your peace-offerings.
40 Mose akawaambia Waisraeli yale yote Bwana alimwagiza.
And Moses told the children of Israel according to all that Jehovah had commanded Moses.