< Hesabu 29 >

1 “‘Katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu na msifanye kazi ya kawaida. Ni siku kwa ajili yenu ya kupiga tarumbeta.
“Now the first day of the seventh month also shall be venerable and holy to you. In it, you shall not do any servile work, because it is the day of the sounding of the trumpets.
2 Mtatayarisha sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri impendezayo Bwana ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
And you shall offer a holocaust, as a most sweet odor to the Lord: one calf from the herd, one ram, and seven immaculate one-year-old lambs;
3 Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume, andaa unga sehemu ya kumi mbili za efa;
and, as their sacrifices, fine wheat flour sprinkled with oil: three tenths for each calf, two tenths for a ram,
4 na pamoja na wana-kondoo saba kila mmoja aandaliwe na sehemu ya kumi ya efa ya unga.
one tenth for a lamb, which all together are seven lambs;
5 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
and a he-goat for sin, which is offered as an expiation for the people,
6 Hivi ni nyongeza ya sadaka za kuteketezwa kila mwezi na kila siku pamoja na sadaka zake za nafaka na sadaka za vinywaji kama ilivyoainishwa. Ni sadaka zinazotolewa kwa Bwana kwa moto, harufu inayopendeza.
aside from the holocaust of the first day of the month with its sacrifices, and the perpetual holocaust with the usual libations. By these same ceremonies, you shall offer incense as a most sweet odor to the Lord.
7 “‘Kwenye siku ya kumi ya mwezi huu wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu. Mtajikana wenyewe na msifanye kazi.
Likewise, the tenth day of this seventh month shall be for you holy and venerable, and you shall afflict your souls. You shall do no servile work in it.
8 Toeni sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
And you shall offer a holocaust to the Lord, as a most sweet odor: one calf from the herd, one ram, seven immaculate one-year-old lambs;
9 Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
and for their sacrifices, fine wheat flour sprinkled with oil: three tenths for each calf, two tenths for a ram,
10 na kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba andaa sehemu ya kumi ya unga laini kwa kila mmoja.
one tenth for each lamb, which are all together seven lambs;
11 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya dhambi kwa ajili ya upatanisho, na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, na sadaka zake za vinywaji.
and a he-goat for sin, apart from those things which are usually offered for offenses as an expiation, and as a perpetual holocaust, with their sacrifice and libations.
12 “‘Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu, na hamtafanya kazi za kawaida. Adhimisheni sikukuu kwa Bwana kwa siku saba.
Yet truly, on the fifteenth day of the seventh month, which shall be for you holy and venerable, you shall not do any servile work in it, but you shall celebrate a solemnity to the Lord for seven days.
13 Toeni sadaka ya kuteketezwa mafahali wachanga kumi na watatu, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
And you shall offer a holocaust, as a most sweet odor to the Lord: thirteen calves from the herd, two rams, fourteen immaculate one-year-old lambs;
14 Pamoja na hao mafahali kumi na watatu, kila mmoja aandaliwe na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume wawili, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
and as their libations, fine wheat flour sprinkled with oil: three tenths for each calf, which is all together thirteen calves, and two tenths for each ram, that is, all together two rams,
15 na kwa wana-kondoo kumi na wanne, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi ya efa ya unga laini.
and one tenth for each lamb, which is all together fourteen lambs;
16 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka ya vinywaji.
and a he-goat for sin, apart from the perpetual holocaust, and the sacrifice and its libation.
17 “‘Katika siku ya pili andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
On the next day, you shall offer twelve calves from the herd, two rams, and fourteen immaculate one-year-old lambs.
18 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
And the sacrifices and libations for each of the calves and the rams and the lambs, you shall celebrate according to the rite,
19 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
with a he-goat for sin, apart from the perpetual holocaust, and the sacrifice and its libation.
20 “‘Katika siku ya tatu andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
On the third day, you shall offer eleven calves, two rams, and fourteen immaculate one-year-old lambs.
21 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
And the sacrifices and libations for each of the calves and the rams and the lambs, you shall celebrate according to the rite,
22 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
with a he-goat for sin, apart from the perpetual holocaust, and the sacrifice and its libation.
23 “‘Katika siku ya nne andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
On the fourth day, you shall offer ten calves, two rams, and fourteen immaculate one-year-old lambs.
24 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
And the sacrifices and the libations for each of the calves and the rams and the lambs, you shall celebrate according to the rite,
25 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
with a he-goat for sin, apart from the perpetual holocaust, and its sacrifice and libation.
26 “‘Katika siku ya tano andaeni mafahali tisa, kondoo dume wawili na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
On the fifth day, you shall offer nine calves, two rams, and fourteen immaculate one-year-old lambs.
27 Pamoja na mafahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za kinywaji kulingana na idadi iliyoainishwa.
And the sacrifices and libations for each of the calves and the rams and the lambs, you shall celebrate according to the rite,
28 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
with a he-goat for sin, apart from the perpetual holocaust, and its sacrifice and libation.
29 “‘Katika siku ya sita andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
On the sixth day, you shall offer eight calves, two rams, and fourteen immaculate one-year-old lambs.
30 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
And the sacrifices and libations for each of the calves and the rams and the lambs, you shall celebrate according to the rite,
31 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
with a he-goat for sin, apart from the perpetual holocaust, and its sacrifice and libation.
32 “‘Katika siku ya saba andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
On the seventh day, you shall offer seven calves, and two rams, and fourteen immaculate one-year-old lambs.
33 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
And the sacrifices and libations for each of the calves and the rams and the lambs, you shall celebrate according to the rite,
34 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
with a he-goat for sin, apart from the perpetual holocaust, and its sacrifice and libation.
35 “‘Katika siku ya nane mtakuwa na kusanyiko, na msifanye kazi ya kawaida.
On the eighth day, which is most honored, you shall not do any servile work,
36 Toeni sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
offering a holocaust as a most sweet odor to the Lord: one calf, one ram, and seven immaculate one-year-old lambs.
37 Pamoja na fahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka, na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
And the sacrifices and libations for each of the calves and the rams and the lambs, you shall celebrate according to the rite,
38 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
with a he-goat for sin, apart from the perpetual holocaust, and its sacrifice and libation.
39 “‘Zaidi ya kile unachoweka nadhiri na sadaka zenu za hiari, andaeni hizi kwa ajili ya Bwana kwenye sikukuu zenu zilizoamriwa: sadaka zenu za kuteketezwa, sadaka za nafaka, sadaka za vinywaji, pamoja na sadaka zenu za amani.’”
These things you shall offer to the Lord in your solemnities, aside from the vowed and voluntary oblations, as a holocaust, as a sacrifice, as a libation, or as peace-offering victims.”
40 Mose akawaambia Waisraeli yale yote Bwana alimwagiza.
And Moses explained to the sons of Israel all that the Lord had commanded him.

< Hesabu 29 >