< Hesabu 29 >

1 “‘Katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu na msifanye kazi ya kawaida. Ni siku kwa ajili yenu ya kupiga tarumbeta.
Og i den syvende Maaned, paa den første Dag i Maaneden, skal der være eder en hellig Sammenkaldelse, I skulle ingen Arbejdsgerning gøre, det skal være eder en Basunklangs Dag.
2 Mtatayarisha sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri impendezayo Bwana ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Og I skulle gøre Brændoffer til en behagelig Lugt for Herren: Een ung Tyr, een Væder, syv Lam, aargamle, uden Lyde;
3 Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume, andaa unga sehemu ya kumi mbili za efa;
og deres Madoffer, Mel, blandet med Olie, tre Tiendeparter til Tyren og to Tiendeparter til Væderen
4 na pamoja na wana-kondoo saba kila mmoja aandaliwe na sehemu ya kumi ya efa ya unga.
og en Tiendepart til hvert Lam af de syv Lam;
5 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
og een Gedebuk til Syndoffer, til at gøre Forligelse for eder;
6 Hivi ni nyongeza ya sadaka za kuteketezwa kila mwezi na kila siku pamoja na sadaka zake za nafaka na sadaka za vinywaji kama ilivyoainishwa. Ni sadaka zinazotolewa kwa Bwana kwa moto, harufu inayopendeza.
foruden Maaneds Brændofret og dets Madoffer, og det bestandige Brændoffer og dets Madoffer og deres Drikofre, efter deres Vis; til en behagelig Lugt, et Ildoffer for Herren.
7 “‘Kwenye siku ya kumi ya mwezi huu wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu. Mtajikana wenyewe na msifanye kazi.
Og paa den tiende Dag i denne syvende Maaned skal der være eder en hellig Sammenkaldelse, og I skulle ydmyge eders Sjæle, I skulle intet Arbejde gøre.
8 Toeni sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
Men I skulle ofre Brændoffer for Herren til en behagelig Lugt: Een ung Tyr, een Væder, syv Lam, aargamle; uden Lyde skulle de være eder;
9 Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
og deres Madoffer, Mel, blandet med Olie, tre Tiendeparter til Tyren, to Tiendeparter til den ene Væder,
10 na kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba andaa sehemu ya kumi ya unga laini kwa kila mmoja.
een Tiendepart til hvert Lam af de syv Lam;
11 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya dhambi kwa ajili ya upatanisho, na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, na sadaka zake za vinywaji.
een Gedebuk til Syndoffer, foruden Forligelsens Syndoffer og det bestandige Brændoffer og dets Madoffer og deres Drikofre.
12 “‘Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu, na hamtafanya kazi za kawaida. Adhimisheni sikukuu kwa Bwana kwa siku saba.
Og paa den femtende Dag i den syvende Maaned skal der være eder en hellig Sammenkaldelse; I skulle ingen Arbejdsgerning gøre, og I skulle højtideligholde Højtid for Herren i syv Dage.
13 Toeni sadaka ya kuteketezwa mafahali wachanga kumi na watatu, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.
Og I skulle ofre Brændoffer, et Ildoffer til en behagelig Lugt for Herren: Tretten unge Tyre, to Vædre, fjorten Lam, aargamle; de skulle være uden Lyde;
14 Pamoja na hao mafahali kumi na watatu, kila mmoja aandaliwe na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume wawili, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini;
og deres Madoffer, Mel, blandet med Olie, tre Tiendeparter til hver Tyr af de tretten Tyre, to Tiendeparter til hver Væder af de to Vædre
15 na kwa wana-kondoo kumi na wanne, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi ya efa ya unga laini.
og een Tiendepart til hvert Lam af de fjorten Lam;
16 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka ya vinywaji.
dertil een Gedebuk til Syndoffer, foruden det bestandige Brændoffer, dets Madoffer og dets Drikoffer.
17 “‘Katika siku ya pili andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Og paa den anden Dag tolv unge Tyre, to Vædre, fjorten Lam, aargamle, uden Lyde,
18 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
og deres Madofrer og deres Drikofre til Tyrene, til Vædrene og til Lammene efter deres Tal, paa sædvanlig Vis;
19 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
dertil een Gedebuk til Syndoffer, foruden det bestandige Brændoffer og dets Madoffer og deres Drikofre.
20 “‘Katika siku ya tatu andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Og paa den tredje Dag elleve Tyre, to Vædre, fjorten Lam, aargamle, uden Lyde,
21 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
og deres Madoffer og deres Drikofre til Tyrene, til Vædrene og til Lammene efter deres Tal, paa sædvanlig Vis;
22 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
dertil een Gedebuk til Syndoffer, foruden det bestandige Brændoffer og dets Madoffer og dets Drikoffer.
23 “‘Katika siku ya nne andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Og paa den fjerde Dag ti Tyre, to Vædre, fjorten Lam, aargamle, uden Lyde,
24 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
deres Madoffer og deres Drikofre til Tyrene, til Vædrene og til Lammene efter deres Tal, paa sædvanlig Vis;
25 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
dertil een Gedebuk til Syndoffer, foruden det bestandige Brændoffer og dets Madoffer og dets Drikoffer.
26 “‘Katika siku ya tano andaeni mafahali tisa, kondoo dume wawili na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Og paa den femte Dag ni Tyre, to Vædre, fjorten Lam, aargamle, uden Lyde,
27 Pamoja na mafahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za kinywaji kulingana na idadi iliyoainishwa.
og deres Madoffer og deres Drikofre til Tyrene, til Vædrene og til Lammene efter deres Tal, paa sædvanlig Vis;
28 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
dertil een Gedebuk til Syndoffer, foruden det bestandige Brændoffer og dets Madoffer og dets Drikoffer.
29 “‘Katika siku ya sita andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Og paa den sjette Dag otte Tyre, to Vædre, fjorten Lam, aargamle, uden Lyde,
30 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
og deres Madoffer og deres Drikofre til Tyrene, til Vædrene og til Lammene efter deres Tal, paa sædvanlig Vis;
31 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
dertil een Gedebuk til Syndoffer, foruden det bestandige Brændoffer, dets Madoffer og dets Drikoffer.
32 “‘Katika siku ya saba andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Og paa den syvende Dag syv Tyre, to Vædre, fjorten Lam, aargamle, uden Lyde,
33 Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
og deres Madoffer og deres Drikofre til Tyrene, til Vædrene og til Lammene efter deres Tal, paa deres sædvanlige Vis;
34 Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.
dertil een Gedebuk til Syndoffer, foruden det bestandige Brændoffer, dets Madoffer og dets Drikofre.
35 “‘Katika siku ya nane mtakuwa na kusanyiko, na msifanye kazi ya kawaida.
Paa den ottende Dag skal der være eder en Slutningshøjtid, da skulle I ingen Arbejdsgerning gøre.
36 Toeni sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Og I skulle ofre Brændoffer, et Ildoffer til en behagelig Lugt for Herren, een Tyr, een Væder, syv Lam, aargamle, uden Lyde,
37 Pamoja na fahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka, na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa.
deres Madoffer og deres Drikoffer til Tyren, til Vædrene og til Lammene efter deres Tal, paa sædvanlig Vis,
38 Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.
dertil een Gedebuk til Syndoffer, foruden det bestandige Brændoffer og dets Madoffer og dets Drikoffer.
39 “‘Zaidi ya kile unachoweka nadhiri na sadaka zenu za hiari, andaeni hizi kwa ajili ya Bwana kwenye sikukuu zenu zilizoamriwa: sadaka zenu za kuteketezwa, sadaka za nafaka, sadaka za vinywaji, pamoja na sadaka zenu za amani.’”
Disse Ting skulle I gøre for Herren paa eders bestemte Tider, foruden eders Løfter og eders frivillige Gaver, hvad enten det er eders Brændofre eller eders Madofre eller eders Drikofre eller eders Takofre.
40 Mose akawaambia Waisraeli yale yote Bwana alimwagiza.
Og Mose sagde til Israels Børn alt dette, ligesom Herren havde befalet Mose.

< Hesabu 29 >