< Hesabu 28 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Le Seigneur dit aussi à Moïse:
2 “Wape Waisraeli agizo hili na uwaambie: ‘Hakikisheni kwamba mnaniletea mimi kwa wakati uliowekwa chakula kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, kama harufu nzuri ya kupendeza.’
Ordonne aux enfants d’Israël, et tu leur diras: Offrez en leurs temps mon oblation, les pains et le sacrifice consumé par le feu d’une odeur très suave.
3 Waambie: ‘Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto mnayomtolea Bwana: wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasio na dosari, kama sadaka ya kawaida ya kuteketezwa kila siku.
Voici les sacrifices que vous devez offrir: deux agneaux d’un an, sans tache, tous les jours, en holocauste perpétuel;
4 Andaa mwana-kondoo mmoja asubuhi na mwingine jioni,
Vous en offrirez un le matin, et l’autre vers le soir:
5 kila mmoja atolewe pamoja na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa pamoja na robo ya hini ya mafuta ya zeituni.
La dixième partie d’un éphi de fleur de farine, qui soit arrosée d’huile très pure, et de la quatrième partie du hin.
6 Hii ni sadaka ya kawaida ya kuteketezwa iliyoanzishwa katika Mlima Sinai kama harufu nzuri ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
C’est l’holocauste perpétuel que vous avez offert sur la montagne de Sinaï, en odeur très suave d’un sacrifice au Seigneur, consumé par le feu.
7 Sadaka ya kinywaji itakayotolewa pamoja na kila mwana-kondoo ni robo ya hini ya kinywaji kilichochachuka. Mimina sadaka ya kinywaji kwa Bwana mahali patakatifu.
Et vous répandrez en libations la quatrième partie d’un hin de vin pour chaque agneau, dans le sanctuaire du Seigneur.
8 Andaa yule mwana-kondoo wa pili jioni, pamoja na sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kama ulivyofanya kwa ile sadaka nyingine ya asubuhi. Hii ni sadaka iliyotolewa kwa kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
Et l’autre agneau, vous l’offrirez de même vers le soir, selon tout le rite du sacrifice du matin, et de ses libations: oblation d’une très suave odeur pour le Seigneur.
9 “‘Siku ya Sabato, utatoa sadaka ya wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari pamoja na sadaka yake ya kinywaji na sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta.
Mais au jour du sabbat, vous offrirez deux agneaux d’un an, sans tache, et deux décimes de fleur de farine, arrosée d’huile, pour le sacrifice, et les libations,
10 Hii ni sadaka ya kuteketezwa itakayotolewa kwa ajili ya kila Sabato, pamoja na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya kinywaji.
Qui, selon les rites, sont répandues à chaque sabbat en holocauste perpétuel.
11 “‘Siku ya kwanza ya kila mwezi, mtamletea Bwana sadaka ya kuteketezwa ya fahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasiokuwa na dosari.
Mais aux calendes, vous offrirez un holocauste au Seigneur: deux veaux pris d’un troupeau, un bélier, sept agneaux d’un an, sans tache,
12 Pamoja na kila fahali, kutakuwa na sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa, uliochanganywa na mafuta, pamoja na kondoo dume mmoja, sadaka ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta;
Et trois décimes de fleur de farine, arrosée d’huile, pour le sacrifice de chaque veau, et deux décimes de fleur de farine, arrosée d’huile, pour chaque bélier;
13 pamoja na kila mwana-kondoo, sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na mafuta. Hii ni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri, sadaka ya kuteketezwa iliyotolewa kwa moto kwa Bwana.
Et la décime d’une décime de fleur de farine avec de l’huile, pour le sacrifice de chaque agneau: holocauste d’une très suave odeur et d’un sacrifice au Seigneur consumé par le feu.
14 Pamoja na kila fahali kutakuwa na sadaka ya kinywaji nusu ya hini ya divai; pamoja na kila kondoo dume, theluthi moja ya hini, na pamoja na kila mwana-kondoo robo hini. Hii ni sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi itakayotolewa kila mwandamo wa mwezi kwa mwaka.
Quant aux libations de vin qui doivent être répandues pour chaque victime, les voici: la moitié du hin pour chaque veau, la troisième partie pour le bélier, la quatrième pour l’agneau: ce sera là un holocauste pour tous les mois qui se succèdent dans le cours de l’année.
15 Zaidi ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya kinywaji, mbuzi mmoja dume atatolewa kwa Bwana kama sadaka ya dhambi.
Un bouc aussi sera offert au Seigneur pour les péchés en holocauste perpétuel avec ses libations.
16 “‘Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, itafanyika Pasaka ya Bwana.
Mais au premier mois, au quatorzième jour du mois, sera la Pâque du Seigneur,
17 Katika siku ya kumi na tano ya mwezi huo itakuwa sikukuu; kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
Et au quinzième jour, la solennité: pendant sept jours on mangera des azymes.
18 Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, msifanye kazi za kawaida.
Le premier de ces jours sera vénérable et saint: vous ne ferez aucune œuvre servile en ce jour,
19 Leteni mbele za Bwana sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo dume saba wenye umri wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
Et vous offrirez un sacrifice holocauste au Seigneur: deux veaux pris d’un troupeau, un bélier, sept agneaux d’un an, sans tache;
20 Pamoja na kila fahali, andaa sadaka ya nafaka sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa;
Et les offrandes pour chacun, de fleur de farine qui soit arrosée d’huile, trois décimes pour chaque veau et deux décimes pour le bélier;
21 pia pamoja na kila mmoja wa wale wana-kondoo saba, andaa sehemu ya kumi ya efa.
Et la décime d’une décime pour chaque agneau, c’est-à-dire, pour sept agneaux.
22 Pia mtoe beberu mmoja kama sadaka ya dhambi ambaye atafanya upatanisho kwa ajili yenu.
Et un bouc pour le péché afin qu’il serve d’expiation pour vous;
23 Andaa hizi licha ya zile sadaka za kawaida za kuteketezwa za kila asubuhi.
Outre l’holocauste du matin, que vous offrirez toujours.
24 Kwa njia hii andaa chakula cha sadaka ya kuteketezwa kila siku, kwa siku saba kama harufu nzuri impendezayo Bwana. Hii itaandaliwa licha ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa ya kila siku pamoja na sadaka yake ya kinywaji.
C’est ainsi que vous ferez à chaque jour des sept jours pour l’entretien du feu, et en odeur très suave pour le Seigneur, laquelle s’élèvera de l’holocauste et des libations de chaque victime.
25 Siku ya saba mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
Le septième jour sera aussi très solennel et saint pour vous: vous ne ferez aucune œuvre servile en ce jour.
26 “‘Siku ya malimbuko, mnapomletea Bwana sadaka ya nafaka mpya wakati wa Sikukuu ya Majuma, mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
De même, le jour des prémices, quand vous offrirez les nouveaux grains au Seigneur, les semaines étant accomplies, sera vénérable et saint: vous ne ferez aucune œuvre servile en ce jour.
27 Mlete sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na pia wana-kondoo saba wenye umri wa mwaka mmoja, kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
Et vous offrirez un holocauste en odeur très suave pour le Seigneur: deux veaux pris d’un troupeau, un bélier, et sept agneaux d’un an, sans tache;
28 Pamoja na kila fahali itatolewa sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini;
Et pour les oblations qui les accompagnent, trois décimes de fleur de farine, arrosée d’huile, pour chaque veau, deux pour les béliers,
29 na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba.
La décime d’une décime, pour les agneaux, qui font ensemble sept agneaux; et un bouc,
30 Ongeza beberu mmoja kwa kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
Qui est immolé pour l’expiation, outre l’holocauste perpétuel et ses libations.
31 Andaa hizi sadaka pamoja na sadaka zake za vinywaji, kuwa nyongeza ya sadaka za kawaida za kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya nafaka. Hakikisha kuwa wanyama hao hawana dosari.
Vous offrirez sans tache toutes ces victimes avec leurs libations.

< Hesabu 28 >