< Hesabu 28 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Yahvé parla à Moïse, et dit:
2 “Wape Waisraeli agizo hili na uwaambie: ‘Hakikisheni kwamba mnaniletea mimi kwa wakati uliowekwa chakula kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, kama harufu nzuri ya kupendeza.’
Donne des ordres aux enfants d'Israël, et dis-leur: Veillez à ce que vous présentiez mon offrande, mon aliment pour mes sacrifices consumés par le feu, comme une odeur agréable pour moi, en son temps.
3 Waambie: ‘Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto mnayomtolea Bwana: wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasio na dosari, kama sadaka ya kawaida ya kuteketezwa kila siku.
Tu leur diras: « Voici le sacrifice consumé par le feu que vous offrirez à l'Éternel: des agneaux mâles d'un an sans défaut, deux par jour, pour l'holocauste perpétuel.
4 Andaa mwana-kondoo mmoja asubuhi na mwingine jioni,
Tu offriras l'un des agneaux le matin, et tu offriras l'autre agneau le soir,
5 kila mmoja atolewe pamoja na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa pamoja na robo ya hini ya mafuta ya zeituni.
avec un dixième d'épha de fleur de farine pour l'offrande, mélangé à un quart de hin d'huile battue.
6 Hii ni sadaka ya kawaida ya kuteketezwa iliyoanzishwa katika Mlima Sinai kama harufu nzuri ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
C'est l'holocauste perpétuel qui a été ordonné sur la montagne de Sinaï, comme un parfum agréable, un sacrifice consumé par le feu à l'Éternel.
7 Sadaka ya kinywaji itakayotolewa pamoja na kila mwana-kondoo ni robo ya hini ya kinywaji kilichochachuka. Mimina sadaka ya kinywaji kwa Bwana mahali patakatifu.
Sa libation sera de la quatrième partie d'un hin pour chaque agneau. Tu verseras une libation de boisson forte à l'Éternel dans le lieu saint.
8 Andaa yule mwana-kondoo wa pili jioni, pamoja na sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kama ulivyofanya kwa ile sadaka nyingine ya asubuhi. Hii ni sadaka iliyotolewa kwa kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
Tu offriras l'autre agneau le soir. Tu l'offriras, comme l'offrande du matin et comme sa libation, en sacrifice consumé par le feu, comme une odeur agréable à Yahvé.
9 “‘Siku ya Sabato, utatoa sadaka ya wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari pamoja na sadaka yake ya kinywaji na sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta.
"'Le jour du sabbat, tu offriras deux agneaux mâles d'un an, sans défaut, et deux dixièmes d'un épha de fleur de farine, en offrande de farine mélangée à de l'huile, avec sa libation:
10 Hii ni sadaka ya kuteketezwa itakayotolewa kwa ajili ya kila Sabato, pamoja na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya kinywaji.
C'est l'holocauste de chaque sabbat, en plus de l'holocauste perpétuel et de sa libation.
11 “‘Siku ya kwanza ya kila mwezi, mtamletea Bwana sadaka ya kuteketezwa ya fahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasiokuwa na dosari.
"'Au commencement de vos mois, vous offrirez un holocauste à Yahvé: deux jeunes taureaux, un bélier, sept agneaux mâles d'un an sans défaut,
12 Pamoja na kila fahali, kutakuwa na sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa, uliochanganywa na mafuta, pamoja na kondoo dume mmoja, sadaka ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta;
et trois dixièmes d'un épha de fleur de farine pour une offrande de farine mélangée à de l'huile, pour chaque taureau; deux dixièmes de fleur de farine pour une offrande de farine mélangée à de l'huile, pour le bélier;
13 pamoja na kila mwana-kondoo, sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na mafuta. Hii ni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri, sadaka ya kuteketezwa iliyotolewa kwa moto kwa Bwana.
et un dixième de fleur de farine mélangée à de l'huile pour une offrande de farine, pour chaque agneau, comme holocauste d'odeur agréable, un sacrifice par le feu à l'Éternel.
14 Pamoja na kila fahali kutakuwa na sadaka ya kinywaji nusu ya hini ya divai; pamoja na kila kondoo dume, theluthi moja ya hini, na pamoja na kila mwana-kondoo robo hini. Hii ni sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi itakayotolewa kila mwandamo wa mwezi kwa mwaka.
Leurs libations seront d'un demi-hin de vin pour le taureau, d'un tiers de hin pour le bélier et d'un quart de hin pour l'agneau. C'est l'holocauste de chaque mois, pendant tous les mois de l'année.
15 Zaidi ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya kinywaji, mbuzi mmoja dume atatolewa kwa Bwana kama sadaka ya dhambi.
On offrira aussi un bouc en sacrifice pour le péché à Yahvé, en plus de l'holocauste perpétuel et de la libation.
16 “‘Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, itafanyika Pasaka ya Bwana.
"'Le premier mois, le quatorzième jour du mois, c'est la Pâque de Yahvé.
17 Katika siku ya kumi na tano ya mwezi huo itakuwa sikukuu; kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
Le quinzième jour de ce mois, il y aura une fête. On mangera des pains sans levain pendant sept jours.
18 Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, msifanye kazi za kawaida.
Le premier jour, il y aura une convocation sainte. Tu ne feras aucun travail régulier,
19 Leteni mbele za Bwana sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo dume saba wenye umri wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
mais tu offriras un sacrifice consumé par le feu, un holocauste à l'Éternel: deux jeunes taureaux, un bélier et sept agneaux mâles d'un an. Ils seront sans défaut,
20 Pamoja na kila fahali, andaa sadaka ya nafaka sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa;
avec leur offrande de farine, de la fleur de farine mélangée à de l'huile. Tu offriras trois dixièmes pour le taureau, et deux dixièmes pour le bélier.
21 pia pamoja na kila mmoja wa wale wana-kondoo saba, andaa sehemu ya kumi ya efa.
Tu offriras un dixième pour chacun des sept agneaux;
22 Pia mtoe beberu mmoja kama sadaka ya dhambi ambaye atafanya upatanisho kwa ajili yenu.
et un bouc en sacrifice pour le péché, afin de faire l'expiation pour toi.
23 Andaa hizi licha ya zile sadaka za kawaida za kuteketezwa za kila asubuhi.
Tu les offriras en plus de l'holocauste du matin, qui est un holocauste perpétuel.
24 Kwa njia hii andaa chakula cha sadaka ya kuteketezwa kila siku, kwa siku saba kama harufu nzuri impendezayo Bwana. Hii itaandaliwa licha ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa ya kila siku pamoja na sadaka yake ya kinywaji.
C'est ainsi que tu offriras chaque jour, pendant sept jours, l'aliment du sacrifice consumé par le feu, d'une odeur agréable à Yahvé. Elle sera offerte en plus de l'holocauste perpétuel et de sa libation.
25 Siku ya saba mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
Le septième jour, vous aurez une sainte convocation. Vous ne ferez aucun travail régulier.
26 “‘Siku ya malimbuko, mnapomletea Bwana sadaka ya nafaka mpya wakati wa Sikukuu ya Majuma, mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
"'Le jour des prémices, lorsque vous offrirez une nouvelle offrande à Yahvé à l'occasion de votre fête des semaines, vous aurez une sainte convocation. Tu ne feras aucun travail régulier,
27 Mlete sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na pia wana-kondoo saba wenye umri wa mwaka mmoja, kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
mais tu offriras un holocauste d'agréable odeur à Yahvé: deux jeunes taureaux, un bélier, sept agneaux mâles d'un an,
28 Pamoja na kila fahali itatolewa sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini;
et leur offrande de farine fine mélangée à de l'huile, trois dixièmes pour chaque taureau, deux dixièmes pour le bélier,
29 na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba.
un dixième pour chacun des sept agneaux,
30 Ongeza beberu mmoja kwa kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
et un bouc, afin de faire l'expiation pour toi.
31 Andaa hizi sadaka pamoja na sadaka zake za vinywaji, kuwa nyongeza ya sadaka za kawaida za kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya nafaka. Hakikisha kuwa wanyama hao hawana dosari.
En plus de l'holocauste perpétuel et de l'offrande, tu les offriras avec leurs libations. Veille à ce qu'ils soient sans défaut.

< Hesabu 28 >