< Hesabu 28 >

1 Bwana akamwambia Mose,
And Jehovah spoke to Moses, saying,
2 “Wape Waisraeli agizo hili na uwaambie: ‘Hakikisheni kwamba mnaniletea mimi kwa wakati uliowekwa chakula kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, kama harufu nzuri ya kupendeza.’
Command the children of Israel, and say unto them, My offering, my bread for my offerings by fire of sweet odour to me, shall ye take heed to present to me at their set time.
3 Waambie: ‘Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto mnayomtolea Bwana: wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasio na dosari, kama sadaka ya kawaida ya kuteketezwa kila siku.
And say unto them, This is the offering by fire which ye shall present to Jehovah: two yearling lambs without blemish, day by day, as a continual burnt-offering.
4 Andaa mwana-kondoo mmoja asubuhi na mwingine jioni,
The one lamb shalt thou offer in the morning, and the other lamb thou shalt offer between the two evenings;
5 kila mmoja atolewe pamoja na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa pamoja na robo ya hini ya mafuta ya zeituni.
and a tenth part of an ephah of fine flour for an oblation, mingled with beaten oil, a fourth part of a hin:
6 Hii ni sadaka ya kawaida ya kuteketezwa iliyoanzishwa katika Mlima Sinai kama harufu nzuri ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
[it is] the continual burnt-offering which was ordained on mount Sinai for a sweet odour, an offering by fire to Jehovah.
7 Sadaka ya kinywaji itakayotolewa pamoja na kila mwana-kondoo ni robo ya hini ya kinywaji kilichochachuka. Mimina sadaka ya kinywaji kwa Bwana mahali patakatifu.
And the drink-offering thereof shall be a fourth part of a hin for one lamb; in the sanctuary shall the drink-offering of strong drink be poured out to Jehovah.
8 Andaa yule mwana-kondoo wa pili jioni, pamoja na sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kama ulivyofanya kwa ile sadaka nyingine ya asubuhi. Hii ni sadaka iliyotolewa kwa kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
And the second lamb thou shalt offer between the two evenings; [with the] like oblation as that of the morning, and the like drink-offering, shalt thou offer it as an offering by fire of a sweet odour to Jehovah.
9 “‘Siku ya Sabato, utatoa sadaka ya wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari pamoja na sadaka yake ya kinywaji na sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta.
And on the sabbath day two yearling lambs without blemish, and two tenth parts of fine flour as an oblation, mingled with oil, and the drink-offering thereof:
10 Hii ni sadaka ya kuteketezwa itakayotolewa kwa ajili ya kila Sabato, pamoja na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya kinywaji.
it is the burnt-offering of the sabbath, for each sabbath besides the continual burnt-offering, and its drink-offering.
11 “‘Siku ya kwanza ya kila mwezi, mtamletea Bwana sadaka ya kuteketezwa ya fahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasiokuwa na dosari.
And in the beginnings of your months ye shall present a burnt-offering to Jehovah: two young bullocks, and one ram, seven yearling lambs without blemish.
12 Pamoja na kila fahali, kutakuwa na sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa, uliochanganywa na mafuta, pamoja na kondoo dume mmoja, sadaka ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta;
And three tenth parts of fine flour as an oblation, mingled with oil, for one bullock; and two tenth parts of fine flour as an oblation, mingled with oil, for the ram;
13 pamoja na kila mwana-kondoo, sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na mafuta. Hii ni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri, sadaka ya kuteketezwa iliyotolewa kwa moto kwa Bwana.
and a tenth part of fine flour mingled with oil as an oblation for each lamb: [it is] a burnt-offering of a sweet odour, an offering by fire to Jehovah.
14 Pamoja na kila fahali kutakuwa na sadaka ya kinywaji nusu ya hini ya divai; pamoja na kila kondoo dume, theluthi moja ya hini, na pamoja na kila mwana-kondoo robo hini. Hii ni sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi itakayotolewa kila mwandamo wa mwezi kwa mwaka.
And their drink-offerings: half a hin of wine for a bullock, and the third part of a hin for the ram, and the fourth part of a hin for a lamb. This is the monthly burnt-offering for each month throughout the months of the year.
15 Zaidi ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya kinywaji, mbuzi mmoja dume atatolewa kwa Bwana kama sadaka ya dhambi.
And a buck of the goats shall be offered, for a sin-offering to Jehovah, besides the continual burnt-offering, and its drink-offering.
16 “‘Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, itafanyika Pasaka ya Bwana.
And in the first month, on the fourteenth day of the month, is the passover to Jehovah.
17 Katika siku ya kumi na tano ya mwezi huo itakuwa sikukuu; kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
And on the fifteenth day of this month is the feast; seven days shall unleavened bread be eaten.
18 Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, msifanye kazi za kawaida.
On the first day shall be a holy convocation: no manner of servile work shall ye do;
19 Leteni mbele za Bwana sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo dume saba wenye umri wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
and ye shall present an offering by fire, a burnt-offering to Jehovah: two young bullocks, and one ram, and seven yearling lambs; they shall be unto you without blemish;
20 Pamoja na kila fahali, andaa sadaka ya nafaka sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa;
and their oblation shall be of fine flour mingled with oil: three tenth parts shall ye offer for a bullock, and two tenth parts for the ram;
21 pia pamoja na kila mmoja wa wale wana-kondoo saba, andaa sehemu ya kumi ya efa.
one tenth part shalt thou offer for each lamb, of the seven lambs;
22 Pia mtoe beberu mmoja kama sadaka ya dhambi ambaye atafanya upatanisho kwa ajili yenu.
and a he-goat as a sin-offering, to make atonement for you.
23 Andaa hizi licha ya zile sadaka za kawaida za kuteketezwa za kila asubuhi.
Besides the burnt-offering of the morning, which is for a continual burnt-offering, shall ye offer this.
24 Kwa njia hii andaa chakula cha sadaka ya kuteketezwa kila siku, kwa siku saba kama harufu nzuri impendezayo Bwana. Hii itaandaliwa licha ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa ya kila siku pamoja na sadaka yake ya kinywaji.
After this manner ye shall offer daily, seven days, the bread of the offering by fire of a sweet odour to Jehovah; it shall be offered besides the continual burnt-offering, and its drink-offering.
25 Siku ya saba mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
And on the seventh day ye shall have a holy convocation; no manner of servile work shall ye do.
26 “‘Siku ya malimbuko, mnapomletea Bwana sadaka ya nafaka mpya wakati wa Sikukuu ya Majuma, mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
And on the day of the first-fruits, when ye present a new oblation to Jehovah, after your weeks, ye shall have a holy convocation: no manner of servile work shall ye do.
27 Mlete sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na pia wana-kondoo saba wenye umri wa mwaka mmoja, kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
And ye shall present a burnt-offering for a sweet odour to Jehovah: two young bullocks, one ram, seven yearling lambs;
28 Pamoja na kila fahali itatolewa sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini;
and their oblation of fine flour mingled with oil, three tenth parts for one bullock, two tenth parts for the ram,
29 na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba.
one tenth part for each lamb of the seven lambs;
30 Ongeza beberu mmoja kwa kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
[and] one buck of the goats, to make atonement for you.
31 Andaa hizi sadaka pamoja na sadaka zake za vinywaji, kuwa nyongeza ya sadaka za kawaida za kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya nafaka. Hakikisha kuwa wanyama hao hawana dosari.
Ye shall offer them besides the continual burnt-offering, and its oblation (without blemish shall they be unto you), and their drink-offerings.

< Hesabu 28 >