< Hesabu 27 >
1 Binti za Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, walikuwa wa koo za Manase mwana wa Yosefu. Majina ya hao binti yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa. Walikaribia
Et les filles de Tselophkhad, fils de Hépher, fils de Galaad, fils de Makir, fils de Manassé, des familles de Manassé, fils de Joseph, s’approchèrent (et ce sont ici les noms de ses filles: Makhla, Noa, et Hogla, et Milca, et Thirtsa);
2 ingilio la Hema la Kukutania na kusimama mbele ya Mose, kuhani Eleazari, viongozi na kusanyiko lote, wakasema,
et elles se tinrent devant Moïse et devant Éléazar, le sacrificateur, et devant les princes et toute l’assemblée, à l’entrée de la tente d’assignation, disant:
3 “Baba yetu alikufa jangwani. Hakuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora, ambao walifungamana pamoja dhidi ya Bwana, lakini alikufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe na hakuacha wana.
Notre père est mort dans le désert, et il n’était pas dans l’assemblée de ceux qui s’ameutèrent contre l’Éternel, dans l’assemblée de Coré; mais il est mort dans son péché, et il n’a pas eu de fils.
4 Kwa nini jina la baba yetu lifutike kutoka ukoo wake kwa sababu hakuwa na mwana? Tupatie milki miongoni mwa ndugu za baba yetu.”
Pourquoi le nom de notre père serait-il retranché du milieu de sa famille parce qu’il n’a pas de fils? Donne-nous une possession au milieu des frères de notre père.
5 Kwa hiyo Mose akalileta shauri lao mbele za Bwana,
Et Moïse apporta leur cause devant l’Éternel.
6 naye Bwana akamwambia Mose,
Et l’Éternel parla à Moïse, disant:
7 “Wanachosema binti za Selofehadi ni sawa. Ni lazima kwa hakika uwape milki kama urithi miongoni mwa ndugu za baba yao, na kubadili urithi wa baba yao uwe wao.
Les filles de Tselophkhad ont bien parlé. Tu leur donneras une possession d’héritage au milieu des frères de leur père, et tu feras passer à elles l’héritage de leur père.
8 “Waambie Waisraeli, ‘Ikiwa mtu atakufa naye hakuacha mwana, utampa binti yake urithi wake.
Et tu parleras aux fils d’Israël, disant: Quand un homme mourra sans avoir de fils, vous ferez passer son héritage à sa fille.
9 Ikiwa hana binti, wape ndugu zake wa kiume urithi wake.
Et s’il n’a pas de fille, vous donnerez son héritage à ses frères.
10 Ikiwa hana ndugu wa kiume toa urithi wake kwa ndugu za baba yake.
Et s’il n’a pas de frères, vous donnerez son héritage aux frères de son père.
11 Ikiwa baba yake hakuwa na ndugu wa kiume, toa urithi wake kwa ndugu wa karibu katika ukoo wake, ili aumiliki. Hili litakuwa dai la sheria kwa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru Mose.’”
Et s’il n’y a pas de frères de son père, vous donnerez son héritage à son parent qui, de sa famille, lui est le plus proche, et il le possédera. Et ce sera pour les fils d’Israël un statut de droit, comme l’Éternel a commandé à Moïse.
12 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Panda juu ya mlima huu katika kilele cha Abarimu uione nchi ambayo nimewapa Waisraeli.
Et l’Éternel dit à Moïse: Monte sur cette montagne d’Abarim, et regarde le pays que j’ai donné aux fils d’Israël.
13 Baada ya kuiona, wewe pia utakusanywa pamoja na watu wako kama ndugu yako Aroni alivyokusanywa,
Tu le regarderas, et tu seras recueilli vers tes peuples, toi aussi, comme Aaron, ton frère, a été recueilli;
14 kwa kuwa jumuiya ilipoasi amri yangu kwenye maji katika Jangwa la Sini, wakati jumuiya ilipogombana nami, nyote wawili mliacha kuitii amri yangu ya kuniheshimu kama mtakatifu mbele ya macho yao.” (Haya yalikuwa maji ya Meriba huko Kadeshi, katika Jangwa la Sini.)
parce que, au désert de Tsin, lors de la contestation de l’assemblée, vous avez été rebelles à mon commandement, quand vous auriez dû me sanctifier à leurs yeux à l’occasion des eaux: ce sont là les eaux de Meriba à Kadès, dans le désert de Tsin.
15 Mose akamwambia Bwana,
Et Moïse parla à l’Éternel, disant:
16 “Bwana, Mungu wa roho zote za wanadamu, na amteue mtu juu ya jumuiya hii
Que l’Éternel, le Dieu des esprits de toute chair, établisse sur l’assemblée un homme
17 ili atoke na kuingia mbele yao, atakayewaongoza katika kutoka kwao na kuingia kwao, ili watu wa Bwana wasiwe kama kondoo wasio na mchungaji.”
qui sorte devant eux et entre devant eux, et qui les fasse sortir et les fasse entrer; et que l’assemblée de l’Éternel ne soit pas comme un troupeau qui n’a pas de berger.
18 Kwa hiyo Bwana akamwambia Mose, “Mchukue Yoshua mwana wa Nuni, mtu ambaye Roho yuko ndani yake, uweke mkono juu yake.
Et l’Éternel dit à Moïse: Prends Josué, fils de Nun, un homme en qui est l’Esprit, et pose ta main sur lui.
19 Msimamishe mbele ya kuhani Eleazari pamoja na kusanyiko lote, umpe maagizo mbele yao.
Et tu le feras se tenir devant Éléazar, le sacrificateur, et devant toute l’assemblée, et tu lui donneras des ordres devant leurs yeux;
20 Mpe sehemu ya mamlaka yako ili jumuiya yote ya Waisraeli ipate kumtii.
et tu mettras sur lui de ta gloire, afin que toute l’assemblée des fils d’Israël l’écoute.
21 Atasimama mbele ya kuhani Eleazari, ambaye atapokea maamuzi kwa ajili yake, kwa kuuliza mbele za Bwana kwa ile Urimu. Kwa amri yake, yeye na jumuiya yote ya Waisraeli watatoka, na kwa amri yake, wataingia.”
Et il se tiendra devant Éléazar, le sacrificateur, qui interrogera pour lui les jugements d’urim devant l’Éternel: à sa parole ils sortiront, et à sa parole ils entreront, lui et tous les fils d’Israël avec lui, toute l’assemblée.
22 Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza. Akamtwaa Yoshua na kumsimamisha mbele ya kuhani Eleazari na kusanyiko lote.
Et Moïse fit comme l’Éternel lui avait commandé; et il prit Josué et le fit se tenir devant Éléazar, le sacrificateur, et devant toute l’assemblée.
23 Kisha akaweka mikono yake juu ya kichwa cha Yoshua na kumpa maagizo, kama vile Bwana alivyoelekeza kupitia kwa Mose.
Et il posa ses mains sur lui, et lui donna des ordres, comme l’Éternel l’avait dit par Moïse.