< Hesabu 27 >

1 Binti za Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, walikuwa wa koo za Manase mwana wa Yosefu. Majina ya hao binti yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa. Walikaribia
and to present: come daughter Zelophehad son: child Hepher son: child Gilead son: child Machir son: child Manasseh to/for family Manasseh son: child Joseph and these name daughter his Mahlah Noah and Hoglah and Milcah and Tirzah
2 ingilio la Hema la Kukutania na kusimama mbele ya Mose, kuhani Eleazari, viongozi na kusanyiko lote, wakasema,
and to stand: stand to/for face: before Moses and to/for face: before Eleazar [the] priest and to/for face: before [the] leader and all [the] congregation entrance tent meeting to/for to say
3 “Baba yetu alikufa jangwani. Hakuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora, ambao walifungamana pamoja dhidi ya Bwana, lakini alikufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe na hakuacha wana.
father our to die in/on/with wilderness and he/she/it not to be in/on/with midst [the] congregation [the] to appoint upon LORD in/on/with congregation Korah for in/on/with sin his to die and son: child not to be to/for him
4 Kwa nini jina la baba yetu lifutike kutoka ukoo wake kwa sababu hakuwa na mwana? Tupatie milki miongoni mwa ndugu za baba yetu.”
to/for what? to dimish name father our from midst family his for nothing to/for him son: child to give: give [emph?] to/for us possession in/on/with midst brother: male-sibling father our
5 Kwa hiyo Mose akalileta shauri lao mbele za Bwana,
and to present: bring Moses [obj] justice their to/for face: before LORD
6 naye Bwana akamwambia Mose,
and to say LORD to(wards) Moses to/for to say
7 “Wanachosema binti za Selofehadi ni sawa. Ni lazima kwa hakika uwape milki kama urithi miongoni mwa ndugu za baba yao, na kubadili urithi wa baba yao uwe wao.
right daughter Zelophehad to speak: speak to give: give to give: give to/for them possession inheritance in/on/with midst brother: male-sibling father their and to pass [obj] inheritance father their to/for them
8 “Waambie Waisraeli, ‘Ikiwa mtu atakufa naye hakuacha mwana, utampa binti yake urithi wake.
and to(wards) son: descendant/people Israel to speak: speak to/for to say man for to die and son: child nothing to/for him and to pass [obj] inheritance his to/for daughter his
9 Ikiwa hana binti, wape ndugu zake wa kiume urithi wake.
and if nothing to/for him daughter and to give: give [obj] inheritance his to/for brother: male-sibling his
10 Ikiwa hana ndugu wa kiume toa urithi wake kwa ndugu za baba yake.
and if nothing to/for him brother: male-sibling and to give: give [obj] inheritance his to/for brother: male-sibling father his
11 Ikiwa baba yake hakuwa na ndugu wa kiume, toa urithi wake kwa ndugu wa karibu katika ukoo wake, ili aumiliki. Hili litakuwa dai la sheria kwa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru Mose.’”
and if nothing brother: male-sibling to/for father his and to give: give [obj] inheritance his to/for flesh his [the] near to(wards) him from family his and to possess: possess [obj] her and to be to/for son: descendant/people Israel to/for statute justice: judgement like/as as which to command LORD [obj] Moses
12 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Panda juu ya mlima huu katika kilele cha Abarimu uione nchi ambayo nimewapa Waisraeli.
and to say LORD to(wards) Moses to ascend: rise to(wards) mountain: mount [the] Abarim [the] this and to see: see [obj] [the] land: country/planet which to give: give to/for son: descendant/people Israel
13 Baada ya kuiona, wewe pia utakusanywa pamoja na watu wako kama ndugu yako Aroni alivyokusanywa,
and to see: see [obj] her and to gather to(wards) kinsman your also you(m. s.) like/as as which to gather Aaron brother: male-sibling your
14 kwa kuwa jumuiya ilipoasi amri yangu kwenye maji katika Jangwa la Sini, wakati jumuiya ilipogombana nami, nyote wawili mliacha kuitii amri yangu ya kuniheshimu kama mtakatifu mbele ya macho yao.” (Haya yalikuwa maji ya Meriba huko Kadeshi, katika Jangwa la Sini.)
like/as as which to rebel lip: word my in/on/with wilderness Zin in/on/with provocation [the] congregation to/for to consecrate: consecate me in/on/with water to/for eye their they(masc.) water Meribah Kadesh wilderness Zin
15 Mose akamwambia Bwana,
and to speak: speak Moses to(wards) LORD to/for to say
16 “Bwana, Mungu wa roho zote za wanadamu, na amteue mtu juu ya jumuiya hii
to reckon: overseer LORD God [the] spirit to/for all flesh man upon [the] congregation
17 ili atoke na kuingia mbele yao, atakayewaongoza katika kutoka kwao na kuingia kwao, ili watu wa Bwana wasiwe kama kondoo wasio na mchungaji.”
which to come out: come to/for face: before their and which to come (in): come to/for face: before their and which to come out: send them and which to come (in): bring them and not to be congregation LORD like/as flock which nothing to/for them to pasture
18 Kwa hiyo Bwana akamwambia Mose, “Mchukue Yoshua mwana wa Nuni, mtu ambaye Roho yuko ndani yake, uweke mkono juu yake.
and to say LORD to(wards) Moses to take: take to/for you [obj] Joshua son: child Nun man which spirit in/on/with him and to support [obj] hand: power your upon him
19 Msimamishe mbele ya kuhani Eleazari pamoja na kusanyiko lote, umpe maagizo mbele yao.
and to stand: stand [obj] him to/for face: before Eleazar [the] priest and to/for face: before all [the] congregation and to command [obj] him to/for eye: seeing their
20 Mpe sehemu ya mamlaka yako ili jumuiya yote ya Waisraeli ipate kumtii.
and to give: put from splendor your upon him because to hear: obey all congregation son: descendant/people Israel
21 Atasimama mbele ya kuhani Eleazari, ambaye atapokea maamuzi kwa ajili yake, kwa kuuliza mbele za Bwana kwa ile Urimu. Kwa amri yake, yeye na jumuiya yote ya Waisraeli watatoka, na kwa amri yake, wataingia.”
and to/for face: before Eleazar [the] priest to stand: stand and to ask to/for him in/on/with justice: judgement [the] Urim to/for face: before LORD upon lip: word his to come out: come and upon lip: word his to come (in): come he/she/it and all son: descendant/people Israel with him and all [the] congregation
22 Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza. Akamtwaa Yoshua na kumsimamisha mbele ya kuhani Eleazari na kusanyiko lote.
and to make: do Moses like/as as which to command LORD [obj] him and to take: take [obj] Joshua and to stand: stand him to/for face: before Eleazar [the] priest and to/for face: before all [the] congregation
23 Kisha akaweka mikono yake juu ya kichwa cha Yoshua na kumpa maagizo, kama vile Bwana alivyoelekeza kupitia kwa Mose.
and to support [obj] hand his upon him and to command him like/as as which to speak: speak LORD in/on/with hand: by Moses

< Hesabu 27 >