< Hesabu 27 >

1 Binti za Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, walikuwa wa koo za Manase mwana wa Yosefu. Majina ya hao binti yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa. Walikaribia
And daughters of Zelophehad son of Hepher, son of Gilead, son of Machir, son of Manasseh, of the families of Manasseh son of Joseph, draw near—and these [are] the names of his daughters: Mahlah, Noah, and Hoglah, and Milcah, and Tirzah—
2 ingilio la Hema la Kukutania na kusimama mbele ya Mose, kuhani Eleazari, viongozi na kusanyiko lote, wakasema,
and stand before Moses, and before Eleazar the priest, and before the princes, and all the congregation, at the opening of the Tent of Meeting, saying,
3 “Baba yetu alikufa jangwani. Hakuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora, ambao walifungamana pamoja dhidi ya Bwana, lakini alikufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe na hakuacha wana.
“Our father died in the wilderness, and he was not in the midst of the congregation who were gathered together against YHWH in the congregation of Korah, but he died for his own sin, and had no sons;
4 Kwa nini jina la baba yetu lifutike kutoka ukoo wake kwa sababu hakuwa na mwana? Tupatie milki miongoni mwa ndugu za baba yetu.”
why is the name of our father withdrawn from the midst of his family because he has no son? Give a possession to us in the midst of the brothers of our father”;
5 Kwa hiyo Mose akalileta shauri lao mbele za Bwana,
and Moses brings their cause near before YHWH.
6 naye Bwana akamwambia Mose,
And YHWH speaks to Moses, saying,
7 “Wanachosema binti za Selofehadi ni sawa. Ni lazima kwa hakika uwape milki kama urithi miongoni mwa ndugu za baba yao, na kubadili urithi wa baba yao uwe wao.
“The daughters of Zelophehad are speaking correctly; you certainly give to them a possession of an inheritance in the midst of their father’s brothers, and have caused the inheritance of their father to pass over to them.
8 “Waambie Waisraeli, ‘Ikiwa mtu atakufa naye hakuacha mwana, utampa binti yake urithi wake.
And you speak to the sons of Israel, saying, When a man dies and has no son, then you have caused his inheritance to pass over to his daughter;
9 Ikiwa hana binti, wape ndugu zake wa kiume urithi wake.
and if he has no daughter, then you have given his inheritance to his brothers;
10 Ikiwa hana ndugu wa kiume toa urithi wake kwa ndugu za baba yake.
and if he has no brothers, then you have given his inheritance to his father’s brothers;
11 Ikiwa baba yake hakuwa na ndugu wa kiume, toa urithi wake kwa ndugu wa karibu katika ukoo wake, ili aumiliki. Hili litakuwa dai la sheria kwa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru Mose.’”
and if his father has no brothers, then you have given his inheritance to his relation who is near to him of his family, and he has possessed it”; and it has been to the sons of Israel for a statute of judgment, as YHWH has commanded Moses.
12 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Panda juu ya mlima huu katika kilele cha Abarimu uione nchi ambayo nimewapa Waisraeli.
And YHWH says to Moses, “Go up to this Mount Abarim, and see the land which I have given to the sons of Israel;
13 Baada ya kuiona, wewe pia utakusanywa pamoja na watu wako kama ndugu yako Aroni alivyokusanywa,
and you have seen it, and you have been gathered to your people, also you, as your brother Aaron has been gathered,
14 kwa kuwa jumuiya ilipoasi amri yangu kwenye maji katika Jangwa la Sini, wakati jumuiya ilipogombana nami, nyote wawili mliacha kuitii amri yangu ya kuniheshimu kama mtakatifu mbele ya macho yao.” (Haya yalikuwa maji ya Meriba huko Kadeshi, katika Jangwa la Sini.)
because you provoked My mouth in the wilderness of Zin, in the strife of the congregation—to sanctify Me at the waters before their eyes”; they [are] the waters of Meribah, in Kadesh, in the wilderness of Zin.
15 Mose akamwambia Bwana,
And Moses speaks to YHWH, saying,
16 “Bwana, Mungu wa roho zote za wanadamu, na amteue mtu juu ya jumuiya hii
“YHWH, God of the spirits of all flesh, appoint a man over the congregation,
17 ili atoke na kuingia mbele yao, atakayewaongoza katika kutoka kwao na kuingia kwao, ili watu wa Bwana wasiwe kama kondoo wasio na mchungaji.”
who goes out before them, and who comes in before them, and who takes them out, and who brings them in, and the congregation of YHWH is not as sheep which have no shepherd.”
18 Kwa hiyo Bwana akamwambia Mose, “Mchukue Yoshua mwana wa Nuni, mtu ambaye Roho yuko ndani yake, uweke mkono juu yake.
And YHWH says to Moses, “Take Joshua son of Nun to yourself, a man in whom [is] the Spirit, and you have laid your hand on him,
19 Msimamishe mbele ya kuhani Eleazari pamoja na kusanyiko lote, umpe maagizo mbele yao.
and have caused him to stand before Eleazar the priest and before all the congregation, and have charged him before their eyes,
20 Mpe sehemu ya mamlaka yako ili jumuiya yote ya Waisraeli ipate kumtii.
and have put of your splendor on him, so that all the congregation of the sons of Israel listens.
21 Atasimama mbele ya kuhani Eleazari, ambaye atapokea maamuzi kwa ajili yake, kwa kuuliza mbele za Bwana kwa ile Urimu. Kwa amri yake, yeye na jumuiya yote ya Waisraeli watatoka, na kwa amri yake, wataingia.”
And he stands before Eleazar the priest, and he has inquired before YHWH for him by the judgment of the Lights; at his word they go out, and at his word they come in, he and all the sons of Israel with him—even all the congregation.”
22 Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza. Akamtwaa Yoshua na kumsimamisha mbele ya kuhani Eleazari na kusanyiko lote.
And Moses does as YHWH has commanded him, and takes Joshua and causes him to stand before Eleazar the priest and before all the congregation,
23 Kisha akaweka mikono yake juu ya kichwa cha Yoshua na kumpa maagizo, kama vile Bwana alivyoelekeza kupitia kwa Mose.
and lays his hands on him and charges him, as YHWH has spoken by the hand of Moses.

< Hesabu 27 >