< Hesabu 27 >

1 Binti za Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, walikuwa wa koo za Manase mwana wa Yosefu. Majina ya hao binti yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa. Walikaribia
Then drew near the daughters of Zelophehad, the son of Hepher, the son of Gilead, the son of Machir, the son of Manasseh, of the families of Manasseh the son of Joseph; and these are the names of his daughters: Mahlah, Noah, and Hoglah, and Milcah, and Tirzah.
2 ingilio la Hema la Kukutania na kusimama mbele ya Mose, kuhani Eleazari, viongozi na kusanyiko lote, wakasema,
And they stood before Moses, and before Eleazar the priest, and before the princes and all the congregation, at the door of the tent of meeting, saying:
3 “Baba yetu alikufa jangwani. Hakuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora, ambao walifungamana pamoja dhidi ya Bwana, lakini alikufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe na hakuacha wana.
'Our father died in the wilderness, and he was not among the company of them that gathered themselves together against the LORD in the company of Korah, but he died in his own sin; and he had no sons.
4 Kwa nini jina la baba yetu lifutike kutoka ukoo wake kwa sababu hakuwa na mwana? Tupatie milki miongoni mwa ndugu za baba yetu.”
Why should the name of our father be done away from among his family, because he had no son? Give unto us a possession among the brethren of our father.'
5 Kwa hiyo Mose akalileta shauri lao mbele za Bwana,
And Moses brought their cause before the LORD.
6 naye Bwana akamwambia Mose,
And the LORD spoke unto Moses, saying:
7 “Wanachosema binti za Selofehadi ni sawa. Ni lazima kwa hakika uwape milki kama urithi miongoni mwa ndugu za baba yao, na kubadili urithi wa baba yao uwe wao.
'The daughters of Zelophehad speak right: thou shalt surely give them a possession of an inheritance among their father's brethren; and thou shalt cause the inheritance of their father to pass unto them.
8 “Waambie Waisraeli, ‘Ikiwa mtu atakufa naye hakuacha mwana, utampa binti yake urithi wake.
And thou shalt speak unto the children of Israel, saying: If a man die, and have no son, then ye shall cause his inheritance to pass unto his daughter.
9 Ikiwa hana binti, wape ndugu zake wa kiume urithi wake.
And if he have no daughter, then ye shall give his inheritance unto his brethren.
10 Ikiwa hana ndugu wa kiume toa urithi wake kwa ndugu za baba yake.
And if he have no brethren, then ye shall give his inheritance unto his father's brethren.
11 Ikiwa baba yake hakuwa na ndugu wa kiume, toa urithi wake kwa ndugu wa karibu katika ukoo wake, ili aumiliki. Hili litakuwa dai la sheria kwa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru Mose.’”
And if his father have no brethren, then ye shall give his inheritance unto his kinsman that is next to him of his family, and he shall possess it. And it shall be unto the children of Israel a statute of judgment, as the LORD commanded Moses.'
12 Kisha Bwana akamwambia Mose, “Panda juu ya mlima huu katika kilele cha Abarimu uione nchi ambayo nimewapa Waisraeli.
And the LORD said unto Moses: 'Get thee up into this mountain of Abarim, and behold the land which I have given unto the children of Israel.
13 Baada ya kuiona, wewe pia utakusanywa pamoja na watu wako kama ndugu yako Aroni alivyokusanywa,
And when thou hast seen it, thou also shalt be gathered unto thy people, as Aaron thy brother was gathered;
14 kwa kuwa jumuiya ilipoasi amri yangu kwenye maji katika Jangwa la Sini, wakati jumuiya ilipogombana nami, nyote wawili mliacha kuitii amri yangu ya kuniheshimu kama mtakatifu mbele ya macho yao.” (Haya yalikuwa maji ya Meriba huko Kadeshi, katika Jangwa la Sini.)
because ye rebelled against My commandment in the wilderness of Zin, in the strife of the congregation, to sanctify Me at the waters before their eyes.' — These are the waters of Meribath-kadesh in the wilderness of Zin. —
15 Mose akamwambia Bwana,
And Moses spoke unto the LORD, saying:
16 “Bwana, Mungu wa roho zote za wanadamu, na amteue mtu juu ya jumuiya hii
'Let the LORD, the God of the spirits of all flesh, set a man over the congregation,
17 ili atoke na kuingia mbele yao, atakayewaongoza katika kutoka kwao na kuingia kwao, ili watu wa Bwana wasiwe kama kondoo wasio na mchungaji.”
who may go out before them, and who may come in before them, and who may lead them out, and who may bring them in; that the congregation of the LORD be not as sheep which have no shepherd.'
18 Kwa hiyo Bwana akamwambia Mose, “Mchukue Yoshua mwana wa Nuni, mtu ambaye Roho yuko ndani yake, uweke mkono juu yake.
And the LORD said unto Moses: 'Take thee Joshua the son of Nun, a man in whom is spirit, and lay thy hand upon him;
19 Msimamishe mbele ya kuhani Eleazari pamoja na kusanyiko lote, umpe maagizo mbele yao.
and set him before Eleazar the priest, and before all the congregation; and give him a charge in their sight.
20 Mpe sehemu ya mamlaka yako ili jumuiya yote ya Waisraeli ipate kumtii.
And thou shalt put of thy honour upon him, that all the congregation of the children of Israel may hearken.
21 Atasimama mbele ya kuhani Eleazari, ambaye atapokea maamuzi kwa ajili yake, kwa kuuliza mbele za Bwana kwa ile Urimu. Kwa amri yake, yeye na jumuiya yote ya Waisraeli watatoka, na kwa amri yake, wataingia.”
And he shall stand before Eleazar the priest, who shall inquire for him by the judgment of the Urim before the LORD; at his word shall they go out, and at his word they shall come in, both he, and all the children of Israel with him, even all the congregation.'
22 Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza. Akamtwaa Yoshua na kumsimamisha mbele ya kuhani Eleazari na kusanyiko lote.
And Moses did as the LORD commanded him; and he took Joshua, and set him before Eleazar the priest, and before all the congregation.
23 Kisha akaweka mikono yake juu ya kichwa cha Yoshua na kumpa maagizo, kama vile Bwana alivyoelekeza kupitia kwa Mose.
And he laid his hands upon him, and gave him a charge, as the LORD spoke by the hand of Moses.

< Hesabu 27 >