< Hesabu 26 >
1 Baada ya hiyo tauni, Bwana akamwambia Mose na Eleazari mwana wa kuhani Aroni,
Und es geschah nach der Plage, daß Jehovah sprach zu Mose und zu Eleasar, dem Sohne Aharons, des Priesters; und Er sprach:
2 “Hesabu jumuiya yote ya Kiisraeli kwa jamaa zao, wale wote wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, ambao wanaweza kutumika katika jeshi la Israeli.”
Nehmet auf die Kopfzahl der ganzen Gemeinde der Söhne Israels vom zwanzigsten Jahre und aufwärts nach dem Hause ihrer Väter, alle, die im Heer ausziehen in Israel.
3 Hivyo Mose na kuhani Eleazari wakazungumza na watu kwenye nchi tambarare ya Moabu, ngʼambo ya Yordani kutokea Yeriko, wakasema,
Und Mose und Eleasar, der Priester, redete mit ihnen in Arboth Moab am Jordan, bei Jericho und sprachen:
4 “Hesabuni wanaume wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.” Hawa ndio Waisraeli waliotoka Misri:
Vom zwanzigsten Jahre an und aufwärts, wie Jehovah dem Mose und den Söhnen Israels, die aus Ägyptenland auszogen, geboten hat.
5 Wazao wa Reubeni, mwana mzaliwa wa kwanza wa Israeli, walikuwa: kutoka kwa Hanoki, ukoo wa Wahanoki; kutoka kwa Palu, ukoo wa Wapalu;
Ruben, Israels Erstgeborener: Söhne Rubens waren Chanoch, die Familie der Chanochiten; von Phallu die Familie der Phalluiten;
6 kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Karmi, ukoo wa Wakarmi.
Von Chezron die Familie der Chezroniten, von Charmi die Familie der Charmiten;
7 Hizi zilikuwa ndizo koo za Reubeni; wale waliohesabiwa walikuwa 43,730.
Dies sind die Familien der Rubeniten. Ihrer Gemusterten aber waren es dreiundvierzigtausendsiebenhundertdreißig;
8 Mwana wa Palu alikuwa Eliabu,
Und die Söhne Phallus Eliab.
9 nao wana wa Eliabu walikuwa Nemueli, Dathani na Abiramu. Hawa wawili Dathani na Abiramu ndio walikuwa maafisa wa jumuiya ambao walimwasi Mose na Aroni, na walikuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora wakati walimwasi Bwana.
Und die Söhne Eliabs Nemuel und Dathan und Abiram - das waren Dathan und Abiram, Berufene der Gemeinde, die zankten mit Mose und mit Aharon in der Gemeinde Korachs, als sie wider Jehovah zankten.
10 Ardhi ilifunua kinywa chake na kuwameza pamoja na Kora, ambaye wafuasi wake walikufa wakati moto ulipowateketeza wanaume 250. Nao walikuwa kama alama ya onyo.
Und die Erde öffnete ihren Mund und verschlang sie und Korach, da die Gemeinde starb, indem das Feuer die zweihundertfünfzig Männer auffraß und sie zum Zeichen wurden.
11 Pamoja na hayo, hao ukoo wa Kora hawakufa.
Korachs Söhne waren aber nicht gestorben.
12 Wazao wa Simeoni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Nemueli, ukoo wa Wanemueli; kutoka kwa Yamini, ukoo wa Wayamini; kutoka wa Yakini, ukoo wa Wayakini;
Die Söhne Simeons nach ihren Familien: Von Nemuel die Familie der Nemueliten, von Jamin die Familie der Jaminiten, von Jachin die Familie der Jachiniten;
13 kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera; kutoka kwa Shauli, ukoo wa Washauli.
Von Serach die Familie der Serachiten, von Schaul die Familie der Schauliten.
14 Hizi ndizo koo za Simeoni; walikuwa 22,200.
Dies sind die Familien der Simeoniten: Zweiundzwanzigtausendzweihundert.
15 Wazao wa Gadi kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Sifoni, ukoo wa Wasifoni; kutoka kwa Hagi, ukoo wa Wahagi; kutoka kwa Shuni, ukoo wa Washuni;
Die Söhne Gads nach ihren Familien: Von Zephon die Familie der Zephoniten, von Chaggi die Familie der Chaggiten, von Schuni die Familie der Schuniten;
16 kutoka kwa Ozni, ukoo wa Waozni; kutoka kwa Eri, ukoo wa Waeri;
Von Osni die Familie der Osniten, von Eri die Familie der Eriten;
17 kutoka kwa Arodi, ukoo wa Waarodi; kutoka kwa Areli, ukoo wa Waareli.
Von Arod die Familie der Aroditen; von Areli die Familie der Areliten.
18 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Gadi; wale waliohesabiwa walikuwa 40,500.
Dies sind die Familien der Söhne Gads nach ihren Gemusterten: vierzigtausendfünfhundert.
19 Eri na Onani walikuwa wana wa Yuda, lakini walifia huko Kanaani.
Die Söhne Judahs: Er und Onan. Und Er und Onan starben im Lande Kanaan.
20 Wazao wa Yuda kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Shela, ukoo wa Washela; kutoka kwa Peresi, ukoo wa Waperesi; kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera.
Und die Söhne Judahs waren nach ihren Familien: Von Schelah die Familie der Schelaniten, von Perez die Familie der Parziten, von Serach die Familie der Sarchiten.
21 Wazao wa Peresi walikuwa: kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Hamuli, ukoo wa Wahamuli.
Und die Söhne des Perez waren: Von Chezron die Familie der Chezroniten, von Chamul die Familie der Chamuliten.
22 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Yuda; wale waliohesabiwa walikuwa 76,500.
Dies sind die Familien Judahs nach ihren Gemusterten: sechsundsiebzigtausendfünfhundert.
23 Wazao wa Isakari kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Tola, ukoo wa Watola; kutoka kwa Puva, ukoo wa Wapuva;
Die Söhne Issaschars nach ihren Familien: Von Thola die Familie der Tholaiten; von Puvah die Familie der Puniten.
24 kutoka kwa Yashubu, ukoo wa Wayashubu; kutoka kwa Shimroni, ukoo wa Washimroni.
Von Jaschub die Familie der Jaschubiten; von Schimron die Familie der Schimroniten.
25 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Isakari; wale waliohesabiwa walikuwa 64,300.
Das sind die Familien Issaschars nach ihren Gemusterten: vierundsechzigtausenddreihundert.
26 Wazao wa Zabuloni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Seredi, ukoo wa Waseredi; kutoka kwa Eloni, ukoo wa Waeloni; kutoka kwa Yaleeli, ukoo wa Wayaleeli.
Die Söhne Sebuluns nach ihren Familien: Von Sared die Familie der Sarditen; von Elon die Familie der Eloniten; von Jachleel die Familie der Jachleeliten;
27 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Zabuloni, wale waliohesabiwa walikuwa 60,500.
Dies sind die Familien der Sebuluniten nach ihren Gemusterten: sechzigtausendfünfhundert.
28 Wazao wa Yosefu kwa koo zao kutoka kwa Manase na kwa Efraimu walikuwa:
Die Söhne Josephs nach ihren Familien sind Menascheh und Ephraim.
29 Wazao wa Manase: kutoka kwa Makiri, ukoo wa Wamakiri (Makiri alikuwa baba wa Gileadi); kutoka kwa Gileadi, ukoo wa Wagileadi.
Die Söhne Menaschehs: Von Machir die Familie der Machiriten. Und Machir zeugte Gilead. Von Gilead die Familie der Gileaditen.
30 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Gileadi: kutoka kwa Iezeri, ukoo wa Waiezeri; kutoka kwa Heleki, ukoo wa Waheleki;
Das sind die Söhne Gileads: Jeser, die Familie der Jesriten; von Chelek, die Familie der Chelekiten.
31 kutoka kwa Asirieli, ukoo wa Waasirieli; kutoka kwa Shekemu, ukoo wa Washekemu;
Und Asriel, die Familie der Asrieliten; und Schechem, die Familie der Schichmiten.
32 kutoka kwa Shemida, ukoo wa Washemida; kutoka kwa Heferi, ukoo wa Waheferi.
Und Schemidah, die Familie der Schemidaiten, und Chepher, die Familie der Chephriten.
33 (Selofehadi mwana wa Heferi hakuzaa wana, bali alikuwa na watoto wa kike tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.)
Und Zelaphechad, Chephers Sohn, hatte keine Söhne, nur Töchter. Und die Namen von Zelaphechads Töchtern waren Machlah und Noah, Choglah, Milkah und Thirzah.
34 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Manase; wale waliohesabiwa walikuwa 52,700.
Das sind die Familien Menaschehs; und ihrer Gemusterten sind zweiundfünfzigtausendsiebenhundert.
35 Hawa walikuwa wazao wa Efraimu kwa koo zao: kutoka kwa Shuthela, ukoo wa Washuthela; kutoka kwa Bekeri, ukoo wa Wabekeri; kutoka kwa Tahani, ukoo wa Watahani;
Das sind die Söhne Ephraims nach ihren Familien: Von Schuthelach die Familie der Schuthalchiten; von Becher die Familie der Bachriten; von Thachan die Familie der Thachaniten.
36 Hawa ndio walikuwa wazao wa Shuthela: kutoka kwa Erani, ukoo wa Waerani.
Und dies sind die Söhne Schuthelachs: Von Eran die Familie der Eraniten.
37 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Efraimu; wale waliohesabiwa walikuwa 32,500. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yosefu kwa koo zao.
Dies sind die Familien der Söhne Ephraims nach ihren Gemusterten: zweiundreißigtausendfünfhundert. Das sind die Söhne Josephs nach ihren Familien.
38 Wazao wa Benyamini kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Bela, ukoo wa Wabela; kutoka kwa Ashbeli, ukoo wa Waashbeli; kutoka kwa Ahiramu, ukoo wa Waahiramu;
Die Söhne Benjamins nach ihren Familien: Von Bela die Familie der Baliten; von Aschbel die Familie der Aschbeliten; von Achiram die Familie der Achiramiten;
39 kutoka kwa Shufamu, ukoo wa Washufamu; kutoka kwa Hufamu, ukoo wa Wahufamu.
Von Schephupham die Familie der Schuphamiten; von Chupham die Familie der Chuphamiten.
40 Wazao wa Bela kutoka kwa Ardi na Naamani walikuwa: kutoka kwa Ardi, ukoo wa Waardi; kutoka kwa Naamani, ukoo wa Wanaamani.
Und die Söhne Belahs sind Ard und Naaman; die Familie der Arditen, von Naaman die Familie der Naamiten.
41 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Benyamini; wale waliohesabiwa walikuwa 45,600.
Dies sind die Söhne Benjamins nach ihren Familien; und ihrer Gemusterten waren es fünfundvierzigtausendsechshundert.
42 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Dani kwa koo zao: kutoka kwa Shuhamu, ukoo wa Washuhamu. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Dani:
Das sind die Söhne Dans nach ihren Familien: Von Schucham die Familie der Schuchamiten. Dies die Familien Dans nach ihren Familien.
43 Wote walikuwa koo za Washuhamu; wale waliohesabiwa walikuwa 64,400.
Alle Familien der Schuchaniten nach ihren Gemusterten waren vierundsechzigtausendvierhundert.
44 Wazao wa Asheri kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Imna, ukoo wa Waimna; kutoka kwa Ishvi, ukoo wa Waishvi; kutoka kwa Beria, ukoo wa Waberia;
Die Söhne Aschers nach ihren Familien sind: Von Jimmah die Familie der Jimniten; von Jischvi die Familie der Jischviten; von Beriah die Familie der Beriiten.
45 kutoka kwa wazao wa Beria: kutoka kwa Heberi, ukoo wa Waheberi; kutoka kwa Malkieli, ukoo wa Wamalkieli.
Von den Söhnen Beriah, von Cheber die Familie der Chebriten; von Malkiel die Familie der Malkieliten.
46 (Asheri alikuwa na binti aliyeitwa Sera.)
Und der Name der Tochter Aschers war Serach.
47 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Asheri; wale waliohesabiwa walikuwa 53,400.
Dies sind die Familien der Söhne Aschers nach ihren Gemusterten: dreiundfünfzigtausendvierhundert.
48 Wazao wa Naftali kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Yaseeli, ukoo wa Wayaseeli; kutoka kwa Guni, ukoo wa Waguni;
Die Söhne Naphthalis nach ihren Familien: Von Jachzeel die Familie der Jachzeeliten; von Guni die Familie der Guniten.
49 kutoka kwa Yeseri, ukoo wa Wayeseri; kutoka kwa Shilemu, ukoo wa Washilemu.
Von Jezer die Familie der Jizriten; von Schillem die Familie der Schillemiten.
50 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Naftali; wale waliohesabiwa walikuwa 45,400.
Das sind die Familien Naphthalis nach ihren Familien; und ihrer Gemusterten waren es fünfundvierzigtausendvierhundert.
51 Jumla ya hesabu ya wanaume wa Israeli ilikuwa 601,730.
Dies sind die Gemusterten der Söhne Israels sechshunderttausend und tausendsiebenhundertdreißig.
52 Bwana akamwambia Mose,
Und Jehovah redete zu Mose und sprach:
53 “Watagawiwa nchi kama urithi kwa kulingana na hesabu ya majina.
An diese soll das Land verteilt werden zum Erbe nach der Zahl der Namen.
54 Kundi kubwa zaidi lipe urithi mkubwa zaidi, na kundi dogo zaidi lipewe urithi mdogo zaidi; kila kundi litapokea urithi wake kulingana na hesabu ya wale walioorodheshwa.
Dem Vielen werde viel zu seinem Erbe und dem Wenigen wenig zu seinem Erbe. Jeglichem Manne werde sein Erbe gegeben nach dem Verhältnis seiner Gemusterten.
55 Hakikisha kuwa nchi inagawanywa kwa kura. Kile kitakachorithiwa na kila kikundi kitakuwa kwa kulingana na majina ya kabila la babu yao.
Man verteile jedoch das Land durch das Los; nach den Namen der Stämme ihrer Väter sollen sie es erben.
56 Kila urithi utagawanywa kwa kura miongoni mwa makundi makubwa na madogo.”
Nach dem Los soll man sein Erbe verteilen, zwischen viel oder wenig.
57 Hawa walikuwa Walawi ambao walihesabiwa kwa koo zao: kutoka kwa Gershoni, ukoo wa Wagershoni; kutoka kwa Kohathi, ukoo wa Wakohathi; kutoka kwa Merari, ukoo wa Wamerari.
Und das sind die gemusterten der Leviten nach ihren Familien: Von Gerschon die Familie der Gerschoniten; von Kohath die Familie der Kohathiten; von Merari die Familie der Merariten.
58 Hizi pia zilikuwa koo za Walawi: ukoo wa Walibni; ukoo wa Wahebroni; ukoo wa Wamahli; ukoo wa Wamushi; ukoo wa wana wa Kora. (Kohathi alikuwa baba aliyemzaa Amramu;
Dies sind die Familien Levis, die Familien der Libniten, der Familien der Chebroniten, die Familie der Machliten, die Familie der Muschiten, die Familie der Korchiten, und Kohath zeugte den Amram.
59 jina la mke wa Amramu ni Yokebedi, naye pia alikuwa mzao wa Lawi, ambaye alizaliwa kwa Walawi nchini Misri. Alimzalia Amramu: Aroni, Mose na dada yao Miriamu.
Und der Name von Amrams Weib war Jochebet, eine Tochter Levis, die dem Levi in Ägypten geboren ward. Und sie gebar dem Amram den Aharon und den Mose und Mirjam, ihre Schwester.
60 Aroni alikuwa baba yake Nadabu na Abihu, Eleazari na Ithamari.
Und dem Aharon wurden geboren Nadab und Abihu, Eleasar und Ithamar.
61 Lakini Nadabu na Abihu walikufa wakati walitoa sadaka mbele za Bwana kwa moto usioruhusiwa.)
Und Nadab und Abihu waren gestorben, da sie fremdes Feuer vor Jehovah darbrachten.
62 Wanaume wote wa Walawi wa umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 23,000. Wao hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine kwa sababu hawakupokea urithi miongoni mwao.
Und ihrer Gemusterten waren es dreiundzwanzigtausend, alles Männliche von einem Monat und aufwärts: denn sie wurden nicht inmitten der Söhne Israels gemustert, weil ihnen kein Erbe inmitten der Söhne Israels gegeben ward.
63 Hawa ndio walioorodheshwa na Mose na kuhani Eleazari wakati waliwahesabu Waisraeli kwenye nchi tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
Dies sind die von Mose und dem Priester Eleasar Gemusterten, da sie die Söhne Israels in Arboth Moab am Jordan, bei Jericho, musterten.
64 Hakuna hata mmoja wao aliyekuwa miongoni mwa wale waliohesabiwa na Mose na kuhani Aroni wakati waliwahesabu Waisraeli katika Jangwa la Sinai.
Und unter ihnen war kein Mann, der von Mose und Aharon, dem Priester, Gemusterten, da sie die Söhne Israels in der Wüste Sinai musterten.
65 Kwa maana Bwana alikuwa amewaambia hao Waisraeli hakika wangekufa huko jangwani, wala hakuna mmoja wao aliyeachwa, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.
Denn Jehovah hatte von ihnen gesprochen, daß sie in der Wüste des Todes sterben sollten. Und kein Mann blieb von ihnen übrig außer Kaleb, der Sohn Jephunnehs und Joschua, der Sohn Nuns.