< Hesabu 26 >
1 Baada ya hiyo tauni, Bwana akamwambia Mose na Eleazari mwana wa kuhani Aroni,
Or il arriva, après cette plaie, que l'Éternel dit à Moïse et à Éléazar, fils d'Aaron, le sacrificateur:
2 “Hesabu jumuiya yote ya Kiisraeli kwa jamaa zao, wale wote wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, ambao wanaweza kutumika katika jeshi la Israeli.”
Faites le compte de toute l'assemblée des enfants d'Israël, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, selon les maisons de leurs pères, tous ceux d'Israël qui peuvent aller à la guerre.
3 Hivyo Mose na kuhani Eleazari wakazungumza na watu kwenye nchi tambarare ya Moabu, ngʼambo ya Yordani kutokea Yeriko, wakasema,
Moïse et Éléazar, le sacrificateur, leur parlèrent donc dans les plaines de Moab, près du Jourdain de Jérico, en disant:
4 “Hesabuni wanaume wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.” Hawa ndio Waisraeli waliotoka Misri:
Qu'on fasse le dénombrement depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, comme l'Éternel l'a commandé à Moïse et aux enfants d'Israël, sortis du pays d'Égypte.
5 Wazao wa Reubeni, mwana mzaliwa wa kwanza wa Israeli, walikuwa: kutoka kwa Hanoki, ukoo wa Wahanoki; kutoka kwa Palu, ukoo wa Wapalu;
Ruben, premier-né d'Israël. Fils de Ruben: Hénoc; de lui sort la famille des Hénokites; de Pallu, la famille des Palluites;
6 kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Karmi, ukoo wa Wakarmi.
De Hetsron, la famille des Hetsronites; de Carmi, la famille des Carmites.
7 Hizi zilikuwa ndizo koo za Reubeni; wale waliohesabiwa walikuwa 43,730.
Telles sont les familles des Rubénites; et ceux dont on fit le dénombrement furent quarante-trois mille sept cent trente.
8 Mwana wa Palu alikuwa Eliabu,
Et les fils de Pallu: Éliab.
9 nao wana wa Eliabu walikuwa Nemueli, Dathani na Abiramu. Hawa wawili Dathani na Abiramu ndio walikuwa maafisa wa jumuiya ambao walimwasi Mose na Aroni, na walikuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora wakati walimwasi Bwana.
Et les fils d'Éliab: Némuël, Dathan et Abiram. C'est ce Dathan et cet Abiram, convoqués à l'assemblée, qui se soulevèrent contre Moïse et contre Aaron, dans l'assemblée de Coré, quand ils se soulevèrent contre l'Éternel,
10 Ardhi ilifunua kinywa chake na kuwameza pamoja na Kora, ambaye wafuasi wake walikufa wakati moto ulipowateketeza wanaume 250. Nao walikuwa kama alama ya onyo.
Et que la terre ouvrit sa bouche et les engloutit, avec Coré, alors que ceux qui s'étaient assemblés moururent, quand le feu dévora les deux cent cinquante hommes et qu'ils servirent d'exemple.
11 Pamoja na hayo, hao ukoo wa Kora hawakufa.
Mais les fils de Coré ne moururent point.
12 Wazao wa Simeoni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Nemueli, ukoo wa Wanemueli; kutoka kwa Yamini, ukoo wa Wayamini; kutoka wa Yakini, ukoo wa Wayakini;
Fils de Siméon, selon leurs familles: de Némuël, la famille des Némuélites; de Jamin, la famille des Jaminites; de Jakin, la famille des Jakinites;
13 kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera; kutoka kwa Shauli, ukoo wa Washauli.
De Zérach, la famille des Zérachites; de Saül, la famille des Saülites.
14 Hizi ndizo koo za Simeoni; walikuwa 22,200.
Telles sont les familles des Siméonites: vingt-deux mille deux cents.
15 Wazao wa Gadi kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Sifoni, ukoo wa Wasifoni; kutoka kwa Hagi, ukoo wa Wahagi; kutoka kwa Shuni, ukoo wa Washuni;
Fils de Gad, selon leurs familles: de Tséphon, la famille des Tséphonites; de Haggi, la famille des Haggites; de Shuni, la famille des Shunites;
16 kutoka kwa Ozni, ukoo wa Waozni; kutoka kwa Eri, ukoo wa Waeri;
D'Ozni, la famille des Oznites; d'Éri, la famille des Érites;
17 kutoka kwa Arodi, ukoo wa Waarodi; kutoka kwa Areli, ukoo wa Waareli.
D'Arod, la famille des Arodites; d'Aréli, la famille des Arélites.
18 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Gadi; wale waliohesabiwa walikuwa 40,500.
Telles sont les familles des fils de Gad, selon leur dénombrement: quarante mille cinq cents.
19 Eri na Onani walikuwa wana wa Yuda, lakini walifia huko Kanaani.
Fils de Juda: Er et Onan; mais Er et Onan moururent au pays de Canaan.
20 Wazao wa Yuda kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Shela, ukoo wa Washela; kutoka kwa Peresi, ukoo wa Waperesi; kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera.
Les fils de Juda, selon leurs familles, furent: de Shéla, la famille des Shélanites; de Pharets, la famille des Phartsites; de Zérach, la famille des Zérachites.
21 Wazao wa Peresi walikuwa: kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Hamuli, ukoo wa Wahamuli.
Et les fils de Pharets furent: de Hetsron, la famille des Hetsronites; et de Hamul, la famille des Hamulites.
22 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Yuda; wale waliohesabiwa walikuwa 76,500.
Telles sont les familles de Juda, selon leur dénombrement: soixante et seize mille cinq cents.
23 Wazao wa Isakari kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Tola, ukoo wa Watola; kutoka kwa Puva, ukoo wa Wapuva;
Fils d'Issacar, selon leurs familles: de Thola, la famille des Tholaïtes; de Puva, la famille des Puvites;
24 kutoka kwa Yashubu, ukoo wa Wayashubu; kutoka kwa Shimroni, ukoo wa Washimroni.
De Jashub, la famille des Jashubites; de Shimron, la famille des Shimronites.
25 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Isakari; wale waliohesabiwa walikuwa 64,300.
Telles sont les familles d'Issacar, selon leur dénombrement: soixante-quatre mille trois cents.
26 Wazao wa Zabuloni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Seredi, ukoo wa Waseredi; kutoka kwa Eloni, ukoo wa Waeloni; kutoka kwa Yaleeli, ukoo wa Wayaleeli.
Fils de Zabulon, selon leurs familles: de Séred, la famille des Sardites; d'Élon, la famille des Élonites; de Jahléel, la famille des Jahléélites.
27 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Zabuloni, wale waliohesabiwa walikuwa 60,500.
Telles sont les familles des Zabulonites, selon leur dénombrement: soixante mille cinq cents.
28 Wazao wa Yosefu kwa koo zao kutoka kwa Manase na kwa Efraimu walikuwa:
Fils de Joseph, selon leurs familles: Manassé et Éphraïm.
29 Wazao wa Manase: kutoka kwa Makiri, ukoo wa Wamakiri (Makiri alikuwa baba wa Gileadi); kutoka kwa Gileadi, ukoo wa Wagileadi.
Fils de Manassé: de Makir, la famille des Makirites; et Makir engendra Galaad; de Galaad, la famille des Galaadites.
30 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Gileadi: kutoka kwa Iezeri, ukoo wa Waiezeri; kutoka kwa Heleki, ukoo wa Waheleki;
Voici les fils de Galaad: de Jézer, la famille des Jézerites; de Hélek, la famille des Helkites;
31 kutoka kwa Asirieli, ukoo wa Waasirieli; kutoka kwa Shekemu, ukoo wa Washekemu;
D'Asriel, la famille des Asriélites; de Sichem, la famille des Sichémites;
32 kutoka kwa Shemida, ukoo wa Washemida; kutoka kwa Heferi, ukoo wa Waheferi.
De Shémida, la famille des Shémidaïtes; de Hépher, la famille des Héphrites.
33 (Selofehadi mwana wa Heferi hakuzaa wana, bali alikuwa na watoto wa kike tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.)
Or, Tselophcad, fils de Hépher, n'eut point de fils, mais des filles. Et les noms des filles de Tselophcad étaient: Machla, Noa, Hogla, Milca et Thirtsa.
34 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Manase; wale waliohesabiwa walikuwa 52,700.
Telles sont les familles de Manassé, et leur dénombrement fut de cinquante-deux mille sept cents.
35 Hawa walikuwa wazao wa Efraimu kwa koo zao: kutoka kwa Shuthela, ukoo wa Washuthela; kutoka kwa Bekeri, ukoo wa Wabekeri; kutoka kwa Tahani, ukoo wa Watahani;
Voici les fils d'Éphraïm, selon leurs familles: de Shuthélach, la famille des Shuthélachites; de Béker, la famille des Bakrites; de Thachan, la famille des Thachanites.
36 Hawa ndio walikuwa wazao wa Shuthela: kutoka kwa Erani, ukoo wa Waerani.
Et voici les fils de Shuthélach: d'Éran, la famille des Éranites.
37 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Efraimu; wale waliohesabiwa walikuwa 32,500. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yosefu kwa koo zao.
Telles sont les familles des fils d'Éphraïm, selon leur dénombrement: trente-deux mille cinq cents. Ce sont là les fils de Joseph, selon leurs familles.
38 Wazao wa Benyamini kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Bela, ukoo wa Wabela; kutoka kwa Ashbeli, ukoo wa Waashbeli; kutoka kwa Ahiramu, ukoo wa Waahiramu;
Fils de Benjamin, selon leurs familles: de Béla, la famille des Balites; d'Ashbel, la famille des Ashbélites; d'Achiram, la famille des Achiramites;
39 kutoka kwa Shufamu, ukoo wa Washufamu; kutoka kwa Hufamu, ukoo wa Wahufamu.
De Shéphupham, la famille des Shuphamites; de Hupham, la famille des Huphamites.
40 Wazao wa Bela kutoka kwa Ardi na Naamani walikuwa: kutoka kwa Ardi, ukoo wa Waardi; kutoka kwa Naamani, ukoo wa Wanaamani.
Les fils de Béla furent Ard et Naaman; d'Ard, la famille des Ardites; de Naaman, la famille des Naamites.
41 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Benyamini; wale waliohesabiwa walikuwa 45,600.
Tels sont les fils de Benjamin, selon leurs familles; et leur dénombrement fut de quarante-cinq mille six cents.
42 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Dani kwa koo zao: kutoka kwa Shuhamu, ukoo wa Washuhamu. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Dani:
Voici les fils de Dan, selon leurs familles: de Shucham, la famille des Shuchamites. Ce sont là les familles de Dan, selon leurs familles;
43 Wote walikuwa koo za Washuhamu; wale waliohesabiwa walikuwa 64,400.
Toutes les familles des Shuchamites, selon leur dénombrement, furent soixante-quatre mille quatre cents.
44 Wazao wa Asheri kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Imna, ukoo wa Waimna; kutoka kwa Ishvi, ukoo wa Waishvi; kutoka kwa Beria, ukoo wa Waberia;
Fils d'Asser, selon leurs familles: de Jimma, la famille des Jimmites; de Jishvi, la famille des Jishvites; de Beria, la famille des Beriites.
45 kutoka kwa wazao wa Beria: kutoka kwa Heberi, ukoo wa Waheberi; kutoka kwa Malkieli, ukoo wa Wamalkieli.
Des fils de Beria: de Héber, la famille des Hébrites; de Malkiel, la famille des Malkiélites.
46 (Asheri alikuwa na binti aliyeitwa Sera.)
Et le nom de la fille d'Asser, était Sérach.
47 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Asheri; wale waliohesabiwa walikuwa 53,400.
Telles sont les familles des fils d'Asser, selon leur dénombrement: cinquante-trois mille quatre cents.
48 Wazao wa Naftali kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Yaseeli, ukoo wa Wayaseeli; kutoka kwa Guni, ukoo wa Waguni;
Fils de Nephthali, selon leurs familles: de Jahtseel, la famille des Jahtséelites; de Guni, la famille des Gunites;
49 kutoka kwa Yeseri, ukoo wa Wayeseri; kutoka kwa Shilemu, ukoo wa Washilemu.
De Jetser, la famille des Jitsrites; de Shillem, la famille des Shillémites.
50 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Naftali; wale waliohesabiwa walikuwa 45,400.
Telles sont les familles de Nephthali, selon leurs familles; et leur dénombrement fut de quarante-cinq mille quatre cents.
51 Jumla ya hesabu ya wanaume wa Israeli ilikuwa 601,730.
Tels sont ceux des enfants d'Israël dont on fit le dénombrement: six cent un mille sept cent trente.
52 Bwana akamwambia Mose,
Et l'Éternel parla à Moïse, en disant:
53 “Watagawiwa nchi kama urithi kwa kulingana na hesabu ya majina.
Le pays sera partagé entre ceux-ci en héritage, selon le nombre des noms;
54 Kundi kubwa zaidi lipe urithi mkubwa zaidi, na kundi dogo zaidi lipewe urithi mdogo zaidi; kila kundi litapokea urithi wake kulingana na hesabu ya wale walioorodheshwa.
A ceux qui sont en grand nombre, tu donneras plus d'héritage, et à ceux qui sont en petit nombre, tu donneras moins d'héritage; on donnera à chacun son héritage en proportion de son recensement.
55 Hakikisha kuwa nchi inagawanywa kwa kura. Kile kitakachorithiwa na kila kikundi kitakuwa kwa kulingana na majina ya kabila la babu yao.
Mais le pays sera partagé par le sort; ils recevront leur héritage selon les noms des tribus de leurs pères.
56 Kila urithi utagawanywa kwa kura miongoni mwa makundi makubwa na madogo.”
L'héritage de chacun sera déterminé par le sort, en ayant égard au grand nombre ou au petit nombre.
57 Hawa walikuwa Walawi ambao walihesabiwa kwa koo zao: kutoka kwa Gershoni, ukoo wa Wagershoni; kutoka kwa Kohathi, ukoo wa Wakohathi; kutoka kwa Merari, ukoo wa Wamerari.
Voici les Lévites dont on fit le dénombrement, selon leurs familles: de Guershon, la famille des Guershonites; de Kéhath, la famille des Kéhathites; de Mérari, la famille des Mérarites.
58 Hizi pia zilikuwa koo za Walawi: ukoo wa Walibni; ukoo wa Wahebroni; ukoo wa Wamahli; ukoo wa Wamushi; ukoo wa wana wa Kora. (Kohathi alikuwa baba aliyemzaa Amramu;
Voici les familles de Lévi: la famille des Libnites, la famille des Hébronites, la famille des Machlites, la famille des Mushites, la famille des Corhites. Or Kéhath engendra Amram.
59 jina la mke wa Amramu ni Yokebedi, naye pia alikuwa mzao wa Lawi, ambaye alizaliwa kwa Walawi nchini Misri. Alimzalia Amramu: Aroni, Mose na dada yao Miriamu.
Et le nom de la femme d'Amram était Jokébed, fille de Lévi, qui naquit à Lévi en Égypte; elle enfanta à Amram, Aaron, Moïse et Marie leur sœur.
60 Aroni alikuwa baba yake Nadabu na Abihu, Eleazari na Ithamari.
Et à Aaron, naquirent Nadab et Abihu, Éléazar et Ithamar.
61 Lakini Nadabu na Abihu walikufa wakati walitoa sadaka mbele za Bwana kwa moto usioruhusiwa.)
Mais Nadab et Abihu moururent en offrant un feu étranger devant l'Éternel.
62 Wanaume wote wa Walawi wa umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 23,000. Wao hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine kwa sababu hawakupokea urithi miongoni mwao.
Or ceux des Lévites qu'on dénombra furent vingt-trois mille, tous mâles, depuis l'âge d'un mois et au-dessus; car ils ne furent point dénombrés avec les enfants d'Israël, parce qu'il ne leur fut point donné d'héritage au milieu des enfants d'Israël.
63 Hawa ndio walioorodheshwa na Mose na kuhani Eleazari wakati waliwahesabu Waisraeli kwenye nchi tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
Tel est le dénombrement fait par Moïse et Éléazar; le sacrificateur, qui dénombrèrent les enfants d'Israël dans les campagnes de Moab, près du Jourdain de Jérico;
64 Hakuna hata mmoja wao aliyekuwa miongoni mwa wale waliohesabiwa na Mose na kuhani Aroni wakati waliwahesabu Waisraeli katika Jangwa la Sinai.
Et parmi ceux-ci il n'y avait aucun de ceux qui avaient été dénombrés par Moïse et Aaron, le sacrificateur, quand ils firent le dénombrement des enfants d'Israël au désert de Sinaï;
65 Kwa maana Bwana alikuwa amewaambia hao Waisraeli hakika wangekufa huko jangwani, wala hakuna mmoja wao aliyeachwa, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.
Car l'Éternel avait dit d'eux: Ils mourront dans le désert; et il n'en resta pas un, excepté Caleb, fils de Jephunné, et Josué, fils de Nun.