< Hesabu 26 >

1 Baada ya hiyo tauni, Bwana akamwambia Mose na Eleazari mwana wa kuhani Aroni,
Et il arriva, après la plaie, que l’Éternel parla à Moïse et à Éléazar, fils d’Aaron, le sacrificateur, disant:
2 “Hesabu jumuiya yote ya Kiisraeli kwa jamaa zao, wale wote wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, ambao wanaweza kutumika katika jeshi la Israeli.”
Relevez la somme de toute l’assemblée des fils d’Israël, depuis l’âge de 20 ans et au-dessus, selon leurs maisons de pères, tous ceux qui sont propres au service militaire en Israël.
3 Hivyo Mose na kuhani Eleazari wakazungumza na watu kwenye nchi tambarare ya Moabu, ngʼambo ya Yordani kutokea Yeriko, wakasema,
Et Moïse, et Éléazar, le sacrificateur, leur parlèrent dans les plaines de Moab, près du Jourdain de Jéricho, disant: …
4 “Hesabuni wanaume wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.” Hawa ndio Waisraeli waliotoka Misri:
Depuis l’âge de 20 ans et au-dessus, comme l’Éternel le commanda à Moïse et aux fils d’Israël, qui sortirent du pays d’Égypte.
5 Wazao wa Reubeni, mwana mzaliwa wa kwanza wa Israeli, walikuwa: kutoka kwa Hanoki, ukoo wa Wahanoki; kutoka kwa Palu, ukoo wa Wapalu;
Ruben, le premier-né d’Israël. Les fils de Ruben: [de] Hénoc, la famille des Hénokites; de Pallu, la famille des Palluites;
6 kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Karmi, ukoo wa Wakarmi.
de Hetsron, la famille des Hetsronites; de Carmi, la famille des Carmites.
7 Hizi zilikuwa ndizo koo za Reubeni; wale waliohesabiwa walikuwa 43,730.
– Ce sont là les familles des Rubénites; et leurs dénombrés furent 43 730.
8 Mwana wa Palu alikuwa Eliabu,
– Et les fils de Pallu: Éliab;
9 nao wana wa Eliabu walikuwa Nemueli, Dathani na Abiramu. Hawa wawili Dathani na Abiramu ndio walikuwa maafisa wa jumuiya ambao walimwasi Mose na Aroni, na walikuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora wakati walimwasi Bwana.
et les fils d’Éliab: Nemuel, et Dathan, et Abiram. C’est ce Dathan et cet Abiram, des principaux de l’assemblée, qui se soulevèrent contre Moïse et contre Aaron dans l’assemblée de Coré, lorsqu’ils se soulevèrent contre l’Éternel;
10 Ardhi ilifunua kinywa chake na kuwameza pamoja na Kora, ambaye wafuasi wake walikufa wakati moto ulipowateketeza wanaume 250. Nao walikuwa kama alama ya onyo.
et la terre ouvrit sa bouche et les engloutit, ainsi que Coré, lorsque l’assemblée mourut, quand le feu dévora les 250 hommes; et ils furent pour signe.
11 Pamoja na hayo, hao ukoo wa Kora hawakufa.
Mais les fils de Coré ne moururent pas.
12 Wazao wa Simeoni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Nemueli, ukoo wa Wanemueli; kutoka kwa Yamini, ukoo wa Wayamini; kutoka wa Yakini, ukoo wa Wayakini;
Les fils de Siméon, selon leurs familles: de Nemuel, la famille des Nemuélites; de Jamin, la famille des Jaminites; de Jakin, la famille des Jakinites;
13 kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera; kutoka kwa Shauli, ukoo wa Washauli.
de Zérakh, la famille des Zarkhites; de Saül, la famille des Saülites.
14 Hizi ndizo koo za Simeoni; walikuwa 22,200.
– Ce sont là les familles des Siméonites, 22 200.
15 Wazao wa Gadi kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Sifoni, ukoo wa Wasifoni; kutoka kwa Hagi, ukoo wa Wahagi; kutoka kwa Shuni, ukoo wa Washuni;
Les fils de Gad, selon leurs familles: de Tsephon, la famille des Tsephonites; de Haggui, la famille des Hagguites; de Shuni, la famille des Shunites;
16 kutoka kwa Ozni, ukoo wa Waozni; kutoka kwa Eri, ukoo wa Waeri;
d’Ozni, la famille des Oznites; d’Éri, la famille des Érites;
17 kutoka kwa Arodi, ukoo wa Waarodi; kutoka kwa Areli, ukoo wa Waareli.
d’Arod, la famille des Arodites; d’Areéli, la famille des Areélites.
18 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Gadi; wale waliohesabiwa walikuwa 40,500.
– Ce sont là les familles des fils de Gad, selon leur dénombrement, 40 500.
19 Eri na Onani walikuwa wana wa Yuda, lakini walifia huko Kanaani.
Les fils de Juda: Er et Onan; et Er et Onan moururent dans le pays de Canaan.
20 Wazao wa Yuda kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Shela, ukoo wa Washela; kutoka kwa Peresi, ukoo wa Waperesi; kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera.
Et les fils de Juda, selon leurs familles: de Shéla, la famille des Shélanites; de Pérets, la famille des Partsites; de Zérakh, la famille des Zarkhites.
21 Wazao wa Peresi walikuwa: kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Hamuli, ukoo wa Wahamuli.
Et les fils de Pérets: de Hetsron, la famille des Hetsronites; de Hamul, la famille des Hamulites.
22 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Yuda; wale waliohesabiwa walikuwa 76,500.
– Ce sont là les familles de Juda, selon leur dénombrement, 76 500.
23 Wazao wa Isakari kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Tola, ukoo wa Watola; kutoka kwa Puva, ukoo wa Wapuva;
Les fils d’Issacar, selon leurs familles: [de] Thola, la famille des Tholaïtes; de Puva, la famille des Punites;
24 kutoka kwa Yashubu, ukoo wa Wayashubu; kutoka kwa Shimroni, ukoo wa Washimroni.
de Jashub, la famille des Jashubites; de Shimron, la famille des Shimronites.
25 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Isakari; wale waliohesabiwa walikuwa 64,300.
– Ce sont là les familles d’Issacar, selon leur dénombrement, 64 300.
26 Wazao wa Zabuloni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Seredi, ukoo wa Waseredi; kutoka kwa Eloni, ukoo wa Waeloni; kutoka kwa Yaleeli, ukoo wa Wayaleeli.
Les fils de Zabulon, selon leurs familles: de Séred, la famille des Sardites; d’Élon, la famille des Élonites; de Jakhleël, la famille des Jakhleélites.
27 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Zabuloni, wale waliohesabiwa walikuwa 60,500.
– Ce sont là les familles des Zabulonites, selon leur dénombrement, 60 500.
28 Wazao wa Yosefu kwa koo zao kutoka kwa Manase na kwa Efraimu walikuwa:
Les fils de Joseph, selon leurs familles, Manassé et Éphraïm.
29 Wazao wa Manase: kutoka kwa Makiri, ukoo wa Wamakiri (Makiri alikuwa baba wa Gileadi); kutoka kwa Gileadi, ukoo wa Wagileadi.
– Les fils de Manassé: de Makir, la famille des Makirites; et Makir engendra Galaad; de Galaad, la famille des Galaadites.
30 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Gileadi: kutoka kwa Iezeri, ukoo wa Waiezeri; kutoka kwa Heleki, ukoo wa Waheleki;
– Ce sont ici les fils de Galaad: [d’]Ihézer, la famille des Ihézrites; de Hélek, la famille des Helkites;
31 kutoka kwa Asirieli, ukoo wa Waasirieli; kutoka kwa Shekemu, ukoo wa Washekemu;
d’Asriel, la famille des Asriélites; [de] Sichem, la famille des Sichémites;
32 kutoka kwa Shemida, ukoo wa Washemida; kutoka kwa Heferi, ukoo wa Waheferi.
[de] Shemida, la famille des Shemidaïtes; [de] Hépher, la famille des Héphrites.
33 (Selofehadi mwana wa Heferi hakuzaa wana, bali alikuwa na watoto wa kike tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.)
– Et Tselophkhad, fils de Hépher, n’eut pas de fils, mais des filles; et les noms des filles de Tselophkhad étaient: Makhla, et Noa, Hogla, Milca, et Thirtsa.
34 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Manase; wale waliohesabiwa walikuwa 52,700.
– Ce sont là les familles de Manassé; et leurs dénombrés, 52 700.
35 Hawa walikuwa wazao wa Efraimu kwa koo zao: kutoka kwa Shuthela, ukoo wa Washuthela; kutoka kwa Bekeri, ukoo wa Wabekeri; kutoka kwa Tahani, ukoo wa Watahani;
Ce sont ici les fils d’Éphraïm, selon leurs familles: de Shuthélakh, la famille des Shuthalkhites; de Béker, la famille des Bacrites; de Thakhan, la famille des Thakhanites.
36 Hawa ndio walikuwa wazao wa Shuthela: kutoka kwa Erani, ukoo wa Waerani.
– Et ce sont ici les fils de Shuthélakh: d’Éran, la famille des Éranites.
37 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Efraimu; wale waliohesabiwa walikuwa 32,500. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yosefu kwa koo zao.
– Ce sont là les familles des fils d’Éphraïm, selon leur dénombrement, 32 500. – Ce sont là les fils de Joseph, selon leurs familles.
38 Wazao wa Benyamini kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Bela, ukoo wa Wabela; kutoka kwa Ashbeli, ukoo wa Waashbeli; kutoka kwa Ahiramu, ukoo wa Waahiramu;
Les fils de Benjamin, selon leurs familles: de Béla, la famille des Balites; d’Ashbel, la famille des Ashbélites; d’Akhiram, la famille des Akhiramites;
39 kutoka kwa Shufamu, ukoo wa Washufamu; kutoka kwa Hufamu, ukoo wa Wahufamu.
de Shephupham, la famille des Shuphamites; de Hupham, la famille des Huphamites.
40 Wazao wa Bela kutoka kwa Ardi na Naamani walikuwa: kutoka kwa Ardi, ukoo wa Waardi; kutoka kwa Naamani, ukoo wa Wanaamani.
– Et les fils de Béla furent Ard et Naaman: [d’Ard], la famille des Ardites; de Naaman, la famille des Naamites.
41 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Benyamini; wale waliohesabiwa walikuwa 45,600.
– Ce sont là les fils de Benjamin, selon leurs familles; et leurs dénombrés, 45 600.
42 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Dani kwa koo zao: kutoka kwa Shuhamu, ukoo wa Washuhamu. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Dani:
Ce sont ici les fils de Dan, selon leurs familles: de Shukham, la famille des Shukhamites. Ce sont là les familles de Dan, selon leurs familles.
43 Wote walikuwa koo za Washuhamu; wale waliohesabiwa walikuwa 64,400.
– Toutes les familles des Shukhamites, selon leur dénombrement, 64 400.
44 Wazao wa Asheri kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Imna, ukoo wa Waimna; kutoka kwa Ishvi, ukoo wa Waishvi; kutoka kwa Beria, ukoo wa Waberia;
Les fils d’Aser, selon leurs familles: de Jimna, la famille des Jimna; de Jishvi, la famille des Jishvites; de Beriha, la famille des Berihites.
45 kutoka kwa wazao wa Beria: kutoka kwa Heberi, ukoo wa Waheberi; kutoka kwa Malkieli, ukoo wa Wamalkieli.
– Des fils de Beriha: de Héber, la famille des Hébrites; de Malkiel, la famille des Malkiélites.
46 (Asheri alikuwa na binti aliyeitwa Sera.)
– Et le nom de la fille d’Aser était Sérakh.
47 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Asheri; wale waliohesabiwa walikuwa 53,400.
Ce sont là les familles des fils d’Aser, selon leur dénombrement, 53 400.
48 Wazao wa Naftali kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Yaseeli, ukoo wa Wayaseeli; kutoka kwa Guni, ukoo wa Waguni;
Les fils de Nephthali, selon leurs familles: de Jahtseël, la famille des Jahtseélites; de Guni, la famille des Gunites;
49 kutoka kwa Yeseri, ukoo wa Wayeseri; kutoka kwa Shilemu, ukoo wa Washilemu.
de Jétser, la famille des Jitsrites; de Shillem, la famille des Shillémites.
50 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Naftali; wale waliohesabiwa walikuwa 45,400.
– Ce sont là les familles de Nephthali, selon leurs familles; et leurs dénombrés, 45 400.
51 Jumla ya hesabu ya wanaume wa Israeli ilikuwa 601,730.
Ce sont là les dénombrés des fils d’Israël, 601 730.
52 Bwana akamwambia Mose,
Et l’Éternel parla à Moïse, disant:
53 “Watagawiwa nchi kama urithi kwa kulingana na hesabu ya majina.
Le pays sera partagé à ceux-ci en héritage, selon le nombre des noms.
54 Kundi kubwa zaidi lipe urithi mkubwa zaidi, na kundi dogo zaidi lipewe urithi mdogo zaidi; kila kundi litapokea urithi wake kulingana na hesabu ya wale walioorodheshwa.
À ceux qui sont nombreux, tu augmenteras l’héritage; et à ceux qui sont peu nombreux, tu diminueras l’héritage: tu donneras à chacun son héritage en proportion de ses dénombrés.
55 Hakikisha kuwa nchi inagawanywa kwa kura. Kile kitakachorithiwa na kila kikundi kitakuwa kwa kulingana na majina ya kabila la babu yao.
Seulement, le pays sera partagé par le sort; ils l’hériteront selon les noms des tribus de leurs pères.
56 Kila urithi utagawanywa kwa kura miongoni mwa makundi makubwa na madogo.”
C’est selon la décision du sort que leur héritage sera partagé, qu’ils soient en grand nombre ou en petit nombre.
57 Hawa walikuwa Walawi ambao walihesabiwa kwa koo zao: kutoka kwa Gershoni, ukoo wa Wagershoni; kutoka kwa Kohathi, ukoo wa Wakohathi; kutoka kwa Merari, ukoo wa Wamerari.
Et ce sont ici les dénombrés de Lévi, selon leurs familles: de Guershon, la famille des Guershonites; de Kehath, la famille des Kehathites; de Merari, la famille des Merarites.
58 Hizi pia zilikuwa koo za Walawi: ukoo wa Walibni; ukoo wa Wahebroni; ukoo wa Wamahli; ukoo wa Wamushi; ukoo wa wana wa Kora. (Kohathi alikuwa baba aliyemzaa Amramu;
Ce sont ici les familles de Lévi: la famille des Libnites, la famille des Hébronites, la famille des Makhlites, la famille des Mushites, la famille des Corites. – Et Kehath engendra Amram.
59 jina la mke wa Amramu ni Yokebedi, naye pia alikuwa mzao wa Lawi, ambaye alizaliwa kwa Walawi nchini Misri. Alimzalia Amramu: Aroni, Mose na dada yao Miriamu.
Et le nom de la femme d’Amram était Jokébed, fille de Lévi, qui naquit à Lévi en Égypte; et elle enfanta à Amram, Aaron et Moïse, et Marie, leur sœur.
60 Aroni alikuwa baba yake Nadabu na Abihu, Eleazari na Ithamari.
Et à Aaron naquirent Nadab, et Abihu, Éléazar, et Ithamar.
61 Lakini Nadabu na Abihu walikufa wakati walitoa sadaka mbele za Bwana kwa moto usioruhusiwa.)
Et Nadab et Abihu moururent comme ils présentaient du feu étranger devant l’Éternel.
62 Wanaume wote wa Walawi wa umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 23,000. Wao hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine kwa sababu hawakupokea urithi miongoni mwao.
– Et les dénombrés des Lévites furent 23 000, tous les mâles, depuis l’âge d’un mois et au-dessus; car ils ne furent pas dénombrés avec les fils d’Israël, parce qu’on ne leur donna pas d’héritage parmi les fils d’Israël.
63 Hawa ndio walioorodheshwa na Mose na kuhani Eleazari wakati waliwahesabu Waisraeli kwenye nchi tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
Ce sont là ceux qui furent dénombrés par Moïse et Éléazar, le sacrificateur, qui dénombrèrent les fils d’Israël dans les plaines de Moab, près du Jourdain de Jéricho.
64 Hakuna hata mmoja wao aliyekuwa miongoni mwa wale waliohesabiwa na Mose na kuhani Aroni wakati waliwahesabu Waisraeli katika Jangwa la Sinai.
Et parmi ceux-là, il n’y en eut aucun de ceux qui avaient été dénombrés par Moïse et Aaron, le sacrificateur, qui dénombrèrent les fils d’Israël dans le désert de Sinaï;
65 Kwa maana Bwana alikuwa amewaambia hao Waisraeli hakika wangekufa huko jangwani, wala hakuna mmoja wao aliyeachwa, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.
car l’Éternel avait dit d’eux: Ils mourront certainement dans le désert; et il n’en resta pas un homme, excepté Caleb, fils de Jephunné, et Josué, fils de Nun.

< Hesabu 26 >