< Hesabu 26 >

1 Baada ya hiyo tauni, Bwana akamwambia Mose na Eleazari mwana wa kuhani Aroni,
A la suite de cette plaie, Yahweh parla à Moïse et à Eléazar, fils d'Aaron, le prêtre, en disant:
2 “Hesabu jumuiya yote ya Kiisraeli kwa jamaa zao, wale wote wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, ambao wanaweza kutumika katika jeshi la Israeli.”
« Faites le compte de toute l'assemblée des enfants d'Israël depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, selon leurs maisons patriarcales, de tous les hommes d'Israël en état de porter les armes. »
3 Hivyo Mose na kuhani Eleazari wakazungumza na watu kwenye nchi tambarare ya Moabu, ngʼambo ya Yordani kutokea Yeriko, wakasema,
Moïse et le prêtre Eléazar leur parlèrent donc dans les plaines de Moab, près du Jourdain, vis-à-vis de Jéricho, en disant:
4 “Hesabuni wanaume wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.” Hawa ndio Waisraeli waliotoka Misri:
« Vous ferez le recensement du peuple depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, comme Yahweh l'a ordonné à Moïse et aux enfants d'Israël, à leur sortie du pays d'Egypte. »
5 Wazao wa Reubeni, mwana mzaliwa wa kwanza wa Israeli, walikuwa: kutoka kwa Hanoki, ukoo wa Wahanoki; kutoka kwa Palu, ukoo wa Wapalu;
Ruben, premier-né d'Israël. Fils de Ruben: de Hénoch, la famille des Hénochites; de Phallu, la famille des Phalluites;
6 kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Karmi, ukoo wa Wakarmi.
de Hesron, la famille des Hesronites; de Charmi, la famille des Charmites.
7 Hizi zilikuwa ndizo koo za Reubeni; wale waliohesabiwa walikuwa 43,730.
Telles sont les familles des Rubénites; leurs recensés furent quarante-trois mille sept cent trente. —
8 Mwana wa Palu alikuwa Eliabu,
Fils de Phallu, Eliab. —
9 nao wana wa Eliabu walikuwa Nemueli, Dathani na Abiramu. Hawa wawili Dathani na Abiramu ndio walikuwa maafisa wa jumuiya ambao walimwasi Mose na Aroni, na walikuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora wakati walimwasi Bwana.
Fils d'Eliab: Namuel, Dathan et Abiron. C'est ce Dathan et cet Abiron, membres du conseil, qui se soulevèrent contre Moïse et Aaron, dans la troupe de Coré, lorsqu'elle se souleva contre Yahweh.
10 Ardhi ilifunua kinywa chake na kuwameza pamoja na Kora, ambaye wafuasi wake walikufa wakati moto ulipowateketeza wanaume 250. Nao walikuwa kama alama ya onyo.
La terre, ouvrant sa bouche, les engloutit avec Coré, quand la troupe périt, et que le feu consuma les deux cent cinquante hommes: ils servirent d'exemple.
11 Pamoja na hayo, hao ukoo wa Kora hawakufa.
Mais les fils de Coré ne moururent pas.
12 Wazao wa Simeoni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Nemueli, ukoo wa Wanemueli; kutoka kwa Yamini, ukoo wa Wayamini; kutoka wa Yakini, ukoo wa Wayakini;
Fils de Siméon, selon leurs familles: de Namuel, la famille des Namuélites; de Jamin, la famille des Jaminites; de Jachin, la famille des Jachinites;
13 kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera; kutoka kwa Shauli, ukoo wa Washauli.
de Zaré la famille des Zaréites; de Saül, la famille des Saülites.
14 Hizi ndizo koo za Simeoni; walikuwa 22,200.
Telles sont les familles des Siméonites: vingt-deux mille deux cents.
15 Wazao wa Gadi kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Sifoni, ukoo wa Wasifoni; kutoka kwa Hagi, ukoo wa Wahagi; kutoka kwa Shuni, ukoo wa Washuni;
Fils de Gad, selon leurs familles: de Séphon, la famille des Séphonites; d'Aggi, la famille des Aggites; de Sunit, la famille des Sunites;
16 kutoka kwa Ozni, ukoo wa Waozni; kutoka kwa Eri, ukoo wa Waeri;
d'Ozni, la famille des Oznites; de Her, la famille des Hérites;
17 kutoka kwa Arodi, ukoo wa Waarodi; kutoka kwa Areli, ukoo wa Waareli.
d'Arod, la famille des Arodites; d'Ariel, la famille des Ariélites.
18 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Gadi; wale waliohesabiwa walikuwa 40,500.
Telles sont les familles des fils de Gad, selon leurs recensés: quarante mille cinq cents.
19 Eri na Onani walikuwa wana wa Yuda, lakini walifia huko Kanaani.
Fils de Juda: Her et Onan; mais Her et Onan moururent au pays de Chanaan.
20 Wazao wa Yuda kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Shela, ukoo wa Washela; kutoka kwa Peresi, ukoo wa Waperesi; kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera.
Voici les fils de Juda selon leurs familles: de Séla, la famille des Sélaïtes; de Pharès, la famille des Pharésites; de Zaré, la famille des Zaréites. —
21 Wazao wa Peresi walikuwa: kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Hamuli, ukoo wa Wahamuli.
Les fils de Pharès furent: de Hesron, la famille des Hesronites; de Hamul, la famille des Hamulites. —
22 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Yuda; wale waliohesabiwa walikuwa 76,500.
Telles sont les familles de Juda, selon leurs recensés: soixante-seize mille cinq cents.
23 Wazao wa Isakari kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Tola, ukoo wa Watola; kutoka kwa Puva, ukoo wa Wapuva;
Fils d'Issachar selon leurs familles: de Thola, la famille des Tholaïtes; de Phua, la famille des Phuaïtes;
24 kutoka kwa Yashubu, ukoo wa Wayashubu; kutoka kwa Shimroni, ukoo wa Washimroni.
de Jasub, la famille des Jasubites; de Semran, la famille des Semranites.
25 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Isakari; wale waliohesabiwa walikuwa 64,300.
Telles sont les familles d'Issachar, selon leurs recensés: soixante-quatre mille trois cents.
26 Wazao wa Zabuloni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Seredi, ukoo wa Waseredi; kutoka kwa Eloni, ukoo wa Waeloni; kutoka kwa Yaleeli, ukoo wa Wayaleeli.
Fils de Zabulon selon leurs familles: de Sared, la famille des Sarédites; d'Elon, la famille des Elonites; de Jalel, la famille des Jalélites.
27 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Zabuloni, wale waliohesabiwa walikuwa 60,500.
Telles sont les familles issues de Zabulon, selon leurs recensés: soixante mille cinq cents.
28 Wazao wa Yosefu kwa koo zao kutoka kwa Manase na kwa Efraimu walikuwa:
Fils de Joseph selon leurs familles: Manassé et Ephraïm.
29 Wazao wa Manase: kutoka kwa Makiri, ukoo wa Wamakiri (Makiri alikuwa baba wa Gileadi); kutoka kwa Gileadi, ukoo wa Wagileadi.
Fils de Manassé: de Machir, la famille des Machirites. — Machir engendra Galaad; de Galaad, la famille des Galaadites. —
30 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Gileadi: kutoka kwa Iezeri, ukoo wa Waiezeri; kutoka kwa Heleki, ukoo wa Waheleki;
Voici les fils de Galaad: Jézer, d'où la famille des Jézérites; de Hélec, la famille des Hélicites;
31 kutoka kwa Asirieli, ukoo wa Waasirieli; kutoka kwa Shekemu, ukoo wa Washekemu;
Asriel, d'où la famille des Asriélites; Séchem, d'où la famille des Séchémites;
32 kutoka kwa Shemida, ukoo wa Washemida; kutoka kwa Heferi, ukoo wa Waheferi.
Sémida, d'où la famille de Sémidaïtes; Hépher, d'où la famille des Héphrites.
33 (Selofehadi mwana wa Heferi hakuzaa wana, bali alikuwa na watoto wa kike tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.)
Salphaad, fils d'Hépher, n'eut point de fils, mais il eut des filles. Voici les noms des filles de Salphaad: Maala, Noa, Hégla, Melcha et Thersa. —
34 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Manase; wale waliohesabiwa walikuwa 52,700.
Telles sont les familles de Manassé; leurs recensés furent cinquante-deux mille sept cents.
35 Hawa walikuwa wazao wa Efraimu kwa koo zao: kutoka kwa Shuthela, ukoo wa Washuthela; kutoka kwa Bekeri, ukoo wa Wabekeri; kutoka kwa Tahani, ukoo wa Watahani;
Voici les fils d'Ephraïm selon leurs familles: de Suthala, la famille des Suthalaïtes; de Bécher, la famille des Béchrites; de Théhen, la famille des Théhénites. —
36 Hawa ndio walikuwa wazao wa Shuthela: kutoka kwa Erani, ukoo wa Waerani.
Voici les fils de Suthala: d'Héran, la famille des Héranites. —
37 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Efraimu; wale waliohesabiwa walikuwa 32,500. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yosefu kwa koo zao.
Telles sont les familles des fils d'Ephraïm, selon leurs recensés: trente-deux mille cinq cents. Ce sont là les fils de Joseph, selon leurs familles.
38 Wazao wa Benyamini kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Bela, ukoo wa Wabela; kutoka kwa Ashbeli, ukoo wa Waashbeli; kutoka kwa Ahiramu, ukoo wa Waahiramu;
Fils de Benjamin, selon leurs familles: de Béla, la famille des Bélaïtes; d'Asbel, la famille des Asbélites; d'Ahiram, la famille des Ahiramites;
39 kutoka kwa Shufamu, ukoo wa Washufamu; kutoka kwa Hufamu, ukoo wa Wahufamu.
de Supham, la famille des Suphamites; de Hupham, la famille des Huphamites. —
40 Wazao wa Bela kutoka kwa Ardi na Naamani walikuwa: kutoka kwa Ardi, ukoo wa Waardi; kutoka kwa Naamani, ukoo wa Wanaamani.
Les fils de Béla furent Héred et Noéman; de Héred, la famille des Hérédites; de Noéman, la famille des Noémanites. —
41 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Benyamini; wale waliohesabiwa walikuwa 45,600.
Tels sont les fils de Benjamin, selon leurs familles, et leurs recensés furent quarante-cinq mille six cents.
42 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Dani kwa koo zao: kutoka kwa Shuhamu, ukoo wa Washuhamu. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Dani:
Voici les fils de Dan, selon leurs familles: de Suham descend la famille des Suhamites. Telles sont les familles de Dan, selon leurs familles.
43 Wote walikuwa koo za Washuhamu; wale waliohesabiwa walikuwa 64,400.
Total des familles des Suhamites, selon leurs recensés: soixante-quatre mille quatre cents.
44 Wazao wa Asheri kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Imna, ukoo wa Waimna; kutoka kwa Ishvi, ukoo wa Waishvi; kutoka kwa Beria, ukoo wa Waberia;
Fils d'Aser, selon leurs familles: de Jemna, la famille des Jemnites; de Jessui, la famille des Jessuites; de Brié, la famille des Briéïtes. —
45 kutoka kwa wazao wa Beria: kutoka kwa Heberi, ukoo wa Waheberi; kutoka kwa Malkieli, ukoo wa Wamalkieli.
Des fils de Brié: de Héber, la famille des Hébrites; de Melchiel, la famille des Melchiélites. —
46 (Asheri alikuwa na binti aliyeitwa Sera.)
Le nom de la fille d'Aser était Sara. —
47 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Asheri; wale waliohesabiwa walikuwa 53,400.
Telles sont les familles des fils d'Aser, d'après leurs recensés: cinquante-trois mille quatre cents.
48 Wazao wa Naftali kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Yaseeli, ukoo wa Wayaseeli; kutoka kwa Guni, ukoo wa Waguni;
Fils de Nephthali, selon leurs familles: de Jésiel, la famille des Jésiélites; de Guni, la famille des Gunites;
49 kutoka kwa Yeseri, ukoo wa Wayeseri; kutoka kwa Shilemu, ukoo wa Washilemu.
de Jéser, la famille des Jésérites; de Sellem, la famille des Sélémites.
50 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Naftali; wale waliohesabiwa walikuwa 45,400.
Telles sont les familles de Nephthali, selon leurs familles, et leurs recensés furent quarante-cinq mille quatre cents.
51 Jumla ya hesabu ya wanaume wa Israeli ilikuwa 601,730.
Tels sont les enfants d'Israël qui furent recensés: six cent un mille sept cent trente.
52 Bwana akamwambia Mose,
Yahweh parla à Moïse, en disant:
53 “Watagawiwa nchi kama urithi kwa kulingana na hesabu ya majina.
« A ceux-ci le pays sera partagé, pour être leur héritage, selon le nombre des noms.
54 Kundi kubwa zaidi lipe urithi mkubwa zaidi, na kundi dogo zaidi lipewe urithi mdogo zaidi; kila kundi litapokea urithi wake kulingana na hesabu ya wale walioorodheshwa.
Aux plus nombreux tu donneras un héritage plus grand, et aux moins nombreux tu donneras un héritage plus petit; on donnera à chacun son héritage selon ses recensés.
55 Hakikisha kuwa nchi inagawanywa kwa kura. Kile kitakachorithiwa na kila kikundi kitakuwa kwa kulingana na majina ya kabila la babu yao.
Seulement le partage du pays aura lieu par le sort. Ils le recevront en partage selon les noms des tribus patriarcales.
56 Kila urithi utagawanywa kwa kura miongoni mwa makundi makubwa na madogo.”
C'est par le sort que l'héritage sera réparti aux plus nombreux comme à ceux qui le sont moins. »
57 Hawa walikuwa Walawi ambao walihesabiwa kwa koo zao: kutoka kwa Gershoni, ukoo wa Wagershoni; kutoka kwa Kohathi, ukoo wa Wakohathi; kutoka kwa Merari, ukoo wa Wamerari.
Voici, selon leurs familles, les Lévites qui furent recensés: de Gerson, la famille des Gersonites; de Caath, la famille des Caathites; de Mérari, la famille des Mérarites. —
58 Hizi pia zilikuwa koo za Walawi: ukoo wa Walibni; ukoo wa Wahebroni; ukoo wa Wamahli; ukoo wa Wamushi; ukoo wa wana wa Kora. (Kohathi alikuwa baba aliyemzaa Amramu;
Voici les familles de Lévi; la famille des Lobnites, la famille des Hébronites, la famille des Moholites, la famille des Musites et la famille des Coréïtes. — Caath engendra Amram,
59 jina la mke wa Amramu ni Yokebedi, naye pia alikuwa mzao wa Lawi, ambaye alizaliwa kwa Walawi nchini Misri. Alimzalia Amramu: Aroni, Mose na dada yao Miriamu.
et le nom de la femme d'Amram était Jochabed, fille de Lévi, que sa mère enfanta à Lévi en Egypte; elle enfanta à Amram Aaron, Moïse et Marie, leur sœur.
60 Aroni alikuwa baba yake Nadabu na Abihu, Eleazari na Ithamari.
Il naquit à Aaron: Nadab et Abiu, Eléazar et Ithamar.
61 Lakini Nadabu na Abihu walikufa wakati walitoa sadaka mbele za Bwana kwa moto usioruhusiwa.)
Nadab et Abiu moururent lorsqu'ils apportèrent du feu étranger devant Yahweh. —
62 Wanaume wote wa Walawi wa umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 23,000. Wao hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine kwa sababu hawakupokea urithi miongoni mwao.
Leurs recensés, tous les mâles depuis l'âge d'un mois et au-dessus, furent vingt-trois mille. Car ils ne furent pas compris dans le recensement des enfants d'Israël, parce qu'ils ne leur fut point assigné d'héritage au milieu des enfants d'Israël.
63 Hawa ndio walioorodheshwa na Mose na kuhani Eleazari wakati waliwahesabu Waisraeli kwenye nchi tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
Tels sont les hommes recensés par Moïse et Eléazar, le prêtre, qui firent le recensement des enfants d'Israël dans les plaines de Moab, près du Jourdain, vis-à-vis de Jéricho.
64 Hakuna hata mmoja wao aliyekuwa miongoni mwa wale waliohesabiwa na Mose na kuhani Aroni wakati waliwahesabu Waisraeli katika Jangwa la Sinai.
Parmi eux, il n'y avait aucun des enfants d'Israël dont Moïse et Aaron le prêtre avaient fait le recensement dans le désert de Sinaï;
65 Kwa maana Bwana alikuwa amewaambia hao Waisraeli hakika wangekufa huko jangwani, wala hakuna mmoja wao aliyeachwa, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.
car Yahweh avait dit d'eux: « Ils mourront dans le désert »; et il n'en resta pas un, excepté Caleb, fils de Jéphoné, et Josué, fils de Nun.

< Hesabu 26 >