< Hesabu 26 >
1 Baada ya hiyo tauni, Bwana akamwambia Mose na Eleazari mwana wa kuhani Aroni,
Tämän vitsauksen jälkeen Herra puhui Moosekselle ja Eleasarille, pappi Aaronin pojalle, sanoen:
2 “Hesabu jumuiya yote ya Kiisraeli kwa jamaa zao, wale wote wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, ambao wanaweza kutumika katika jeshi la Israeli.”
"Laskekaa koko israelilaisten seurakunnan väkiluku, kaksikymmenvuotiset ja sitä vanhemmat, perhekunnittain, kaikki Israelin sotakelpoiset miehet".
3 Hivyo Mose na kuhani Eleazari wakazungumza na watu kwenye nchi tambarare ya Moabu, ngʼambo ya Yordani kutokea Yeriko, wakasema,
Ja Mooses ja pappi Eleasar puhuivat heille Mooabin arolla Jordanin luona, Jerikon kohdalla, sanoen:
4 “Hesabuni wanaume wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.” Hawa ndio Waisraeli waliotoka Misri:
"Kaksikymmenvuotiset ja sitä vanhemmat laskettakoon", niinkuin Herra oli Moosekselle käskyn antanut. Ja israelilaiset, jotka olivat lähteneet Egyptin maasta, olivat:
5 Wazao wa Reubeni, mwana mzaliwa wa kwanza wa Israeli, walikuwa: kutoka kwa Hanoki, ukoo wa Wahanoki; kutoka kwa Palu, ukoo wa Wapalu;
Ruuben, Israelin esikoinen; Ruubenin jälkeläisiä olivat: Hanokista hanokilaisten suku, Pallusta pallulaisten suku,
6 kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Karmi, ukoo wa Wakarmi.
Hesronista hesronilaisten suku, Karmista karmilaisten suku.
7 Hizi zilikuwa ndizo koo za Reubeni; wale waliohesabiwa walikuwa 43,730.
Nämä olivat ruubenilaisten suvut. Ja katselmuksessa olleita oli heitä neljäkymmentäkolme tuhatta seitsemänsataa kolmekymmentä.
8 Mwana wa Palu alikuwa Eliabu,
Ja Pallun poika oli Eliab.
9 nao wana wa Eliabu walikuwa Nemueli, Dathani na Abiramu. Hawa wawili Dathani na Abiramu ndio walikuwa maafisa wa jumuiya ambao walimwasi Mose na Aroni, na walikuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora wakati walimwasi Bwana.
Ja Eliabin pojat olivat Nemuel ja Daatan ja Abiram. Nämä olivat ne kansan edusmiehet Daatan ja Abiram, jotka taistelivat Moosesta ja Aaronia vastaan Koorahin joukossa ja taistelivat Herraa vastaan,
10 Ardhi ilifunua kinywa chake na kuwameza pamoja na Kora, ambaye wafuasi wake walikufa wakati moto ulipowateketeza wanaume 250. Nao walikuwa kama alama ya onyo.
jolloin maa avasi kitansa ja nielaisi heidät ja Koorahin, silloin kun hänen joukkonsa kuoli ja tuli kulutti kaksisataa viisikymmentä miestä; ja heistä tuli varoitusmerkki.
11 Pamoja na hayo, hao ukoo wa Kora hawakufa.
Mutta Koorahin pojat eivät kuolleet.
12 Wazao wa Simeoni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Nemueli, ukoo wa Wanemueli; kutoka kwa Yamini, ukoo wa Wayamini; kutoka wa Yakini, ukoo wa Wayakini;
Simeonin jälkeläisiä, sukujensa mukaan, olivat: Nemuelista nemuelilaisten suku, Jaaminista jaaminilaisten suku, Jaakinista jaakinilaisten suku,
13 kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera; kutoka kwa Shauli, ukoo wa Washauli.
Serahista serahilaisten suku, Saulista saulilaisten suku.
14 Hizi ndizo koo za Simeoni; walikuwa 22,200.
Nämä olivat simeonilaisten suvut, kaksikymmentäkaksi tuhatta kaksisataa.
15 Wazao wa Gadi kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Sifoni, ukoo wa Wasifoni; kutoka kwa Hagi, ukoo wa Wahagi; kutoka kwa Shuni, ukoo wa Washuni;
Gaadin jälkeläisiä, sukujensa mukaan, olivat: Sefonista sefonilaisten suku, Haggista haggilaisten suku, Suunista suunilaisten suku,
16 kutoka kwa Ozni, ukoo wa Waozni; kutoka kwa Eri, ukoo wa Waeri;
Osnista osnilaisten suku, Eeristä eeriläisten suku,
17 kutoka kwa Arodi, ukoo wa Waarodi; kutoka kwa Areli, ukoo wa Waareli.
Arodista arodilaisten suku, Arelista arelilaisten suku.
18 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Gadi; wale waliohesabiwa walikuwa 40,500.
Nämä olivat Gaadin jälkeläisten suvut; katselmuksessa olleita oli heitä neljäkymmentä tuhatta viisisataa.
19 Eri na Onani walikuwa wana wa Yuda, lakini walifia huko Kanaani.
Juudan poikia olivat Eer ja Oonan, mutta Eer ja Oonan kuolivat Kanaanin maassa.
20 Wazao wa Yuda kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Shela, ukoo wa Washela; kutoka kwa Peresi, ukoo wa Waperesi; kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera.
Ja Juudan jälkeläisiä, sukujensa mukaan, olivat: Seelasta seelalaisten suku, Pereksestä perekseläisten suku, Serahista serahilaisten suku.
21 Wazao wa Peresi walikuwa: kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni; kutoka kwa Hamuli, ukoo wa Wahamuli.
Ja Pereksen jälkeläisiä olivat: Hesronista hesronilaisten suku, Haamulista haamulilaisten suku.
22 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Yuda; wale waliohesabiwa walikuwa 76,500.
Nämä olivat Juudan suvut; katselmuksessa olleita oli heitä seitsemänkymmentäkuusi tuhatta viisisataa.
23 Wazao wa Isakari kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Tola, ukoo wa Watola; kutoka kwa Puva, ukoo wa Wapuva;
Isaskarin jälkeläisiä, sukujensa mukaan, olivat: Toolasta toolalaisten suku, Puvvasta puunilaisten suku,
24 kutoka kwa Yashubu, ukoo wa Wayashubu; kutoka kwa Shimroni, ukoo wa Washimroni.
Jaasubista jaasubilaisten suku, Simronista simronilaisten suku.
25 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Isakari; wale waliohesabiwa walikuwa 64,300.
Nämä olivat Isaskarin suvut; katselmuksessa olleita oli heitä kuusikymmentäneljä tuhatta kolmesataa.
26 Wazao wa Zabuloni kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Seredi, ukoo wa Waseredi; kutoka kwa Eloni, ukoo wa Waeloni; kutoka kwa Yaleeli, ukoo wa Wayaleeli.
Sebulonin jälkeläisiä, sukujensa mukaan, olivat: Seredistä serediläisten suku, Eelonista eelonilaisten suku, Jahlelista jahlelilaisten suku.
27 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Zabuloni, wale waliohesabiwa walikuwa 60,500.
Nämä olivat sebulonilaisten suvut; katselmuksessa olleita oli heitä kuusikymmentä tuhatta viisisataa.
28 Wazao wa Yosefu kwa koo zao kutoka kwa Manase na kwa Efraimu walikuwa:
Joosefin jälkeläisiä, sukujensa mukaan, olivat Manasse ja Efraim.
29 Wazao wa Manase: kutoka kwa Makiri, ukoo wa Wamakiri (Makiri alikuwa baba wa Gileadi); kutoka kwa Gileadi, ukoo wa Wagileadi.
Manassen jälkeläisiä olivat: Maakirista maakirilaisten suku. Ja Maakirille syntyi Gilead; Gileadista on gileadilaisten suku.
30 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Gileadi: kutoka kwa Iezeri, ukoo wa Waiezeri; kutoka kwa Heleki, ukoo wa Waheleki;
Nämä olivat Gileadin jälkeläisiä: Iieseristä iieseriläisten suku, Helekistä helekiläisten suku;
31 kutoka kwa Asirieli, ukoo wa Waasirieli; kutoka kwa Shekemu, ukoo wa Washekemu;
Asrielista asrielilaisten suku, Sekemistä sekemiläisten suku;
32 kutoka kwa Shemida, ukoo wa Washemida; kutoka kwa Heferi, ukoo wa Waheferi.
Semidasta semidalaisten suku, Heeferistä heeferiläisten suku.
33 (Selofehadi mwana wa Heferi hakuzaa wana, bali alikuwa na watoto wa kike tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.)
Mutta Selofhadilla, Heeferin pojalla, ei ollut poikia, vaan ainoastaan tyttäriä. Ja Selofhadin tyttärien nimet olivat: Mahla, Nooga, Hogla, Milka ja Tirsa.
34 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Manase; wale waliohesabiwa walikuwa 52,700.
Nämä olivat Manassen suvut; katselmuksessa olleita oli heitä viisikymmentäkaksi tuhatta seitsemänsataa.
35 Hawa walikuwa wazao wa Efraimu kwa koo zao: kutoka kwa Shuthela, ukoo wa Washuthela; kutoka kwa Bekeri, ukoo wa Wabekeri; kutoka kwa Tahani, ukoo wa Watahani;
Ja nämä olivat Efraimin jälkeläisiä, sukujensa mukaan: Suutelahista suutelahilaisten suku, Bekeristä bekeriläisten suku, Tahanista tahanilaisten suku.
36 Hawa ndio walikuwa wazao wa Shuthela: kutoka kwa Erani, ukoo wa Waerani.
Nämä olivat Suutelahin jälkeläisiä: Eeranista eeranilaisten suku.
37 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Efraimu; wale waliohesabiwa walikuwa 32,500. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yosefu kwa koo zao.
Nämä olivat efraimilaisten suvut; katselmuksessa olleita oli heitä kolmekymmentäkaksi tuhatta viisisataa. Nämä olivat Joosefin jälkeläiset sukujensa mukaan.
38 Wazao wa Benyamini kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Bela, ukoo wa Wabela; kutoka kwa Ashbeli, ukoo wa Waashbeli; kutoka kwa Ahiramu, ukoo wa Waahiramu;
Benjaminin jälkeläisiä, sukujensa mukaan, olivat: Belasta belalaisten suku, Asbelista asbelilaisten suku, Ahiramista ahiramilaisten suku,
39 kutoka kwa Shufamu, ukoo wa Washufamu; kutoka kwa Hufamu, ukoo wa Wahufamu.
Sefufamista suufamilaisten suku, Huufamista huufamilaisten suku.
40 Wazao wa Bela kutoka kwa Ardi na Naamani walikuwa: kutoka kwa Ardi, ukoo wa Waardi; kutoka kwa Naamani, ukoo wa Wanaamani.
Mutta Belan jälkeläisiä olivat Ard ja Naaman: Ardista ardilaisten suku, Naamanista naamilaisten suku.
41 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Benyamini; wale waliohesabiwa walikuwa 45,600.
Nämä olivat Benjaminin jälkeläiset sukujensa mukaan; ja katselmuksessa olleita oli heitä neljäkymmentäviisi tuhatta kuusisataa.
42 Hawa ndio waliokuwa wazao wa Dani kwa koo zao: kutoka kwa Shuhamu, ukoo wa Washuhamu. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Dani:
Nämä olivat Daanin jälkeläisiä, sukujensa mukaan: Suuhamista suuhamilaisten suku. Nämä ovat Daanin suvut sukujensa mukaan.
43 Wote walikuwa koo za Washuhamu; wale waliohesabiwa walikuwa 64,400.
Kaikista suuhamilaisten suvuista oli katselmuksessa olleita kuusikymmentäneljä tuhatta neljäsataa.
44 Wazao wa Asheri kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Imna, ukoo wa Waimna; kutoka kwa Ishvi, ukoo wa Waishvi; kutoka kwa Beria, ukoo wa Waberia;
Asserin jälkeläisiä, sukujensa mukaan, olivat: Jimnasta jimnalaisten suku, Jisvistä jisviläisten suku, Beriasta berialaisten suku.
45 kutoka kwa wazao wa Beria: kutoka kwa Heberi, ukoo wa Waheberi; kutoka kwa Malkieli, ukoo wa Wamalkieli.
Berian jälkeläisiä olivat: Heeberistä heeberiläisten suku, Malkielista malkielilaisten suku.
46 (Asheri alikuwa na binti aliyeitwa Sera.)
Mutta Asserin tyttären nimi oli Serah.
47 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Asheri; wale waliohesabiwa walikuwa 53,400.
Nämä olivat asserilaisten suvut; katselmuksessa olleita oli heitä viisikymmentäkolme tuhatta neljäsataa.
48 Wazao wa Naftali kwa koo zao walikuwa: kutoka kwa Yaseeli, ukoo wa Wayaseeli; kutoka kwa Guni, ukoo wa Waguni;
Naftalin jälkeläisiä, sukujensa mukaan, olivat: Jahselista jahselilaisten suku, Guunista guunilaisten suku;
49 kutoka kwa Yeseri, ukoo wa Wayeseri; kutoka kwa Shilemu, ukoo wa Washilemu.
Jeeseristä jeeseriläisten suku, Sillemistä sillemiläisten suku.
50 Hizi ndizo zilizokuwa koo za Naftali; wale waliohesabiwa walikuwa 45,400.
Nämä olivat Naftalin suvut sukujensa mukaan; ja katselmuksessa olleita oli heitä neljäkymmentäviisi tuhatta neljäsataa.
51 Jumla ya hesabu ya wanaume wa Israeli ilikuwa 601,730.
Nämä olivat katselmuksessa olleet israelilaiset: kuusisataayksi tuhatta seitsemänsataa kolmekymmentä.
52 Bwana akamwambia Mose,
Ja Herra puhui Moosekselle sanoen:
53 “Watagawiwa nchi kama urithi kwa kulingana na hesabu ya majina.
"Näille jaettakoon maa perintöosiksi nimien lukumäärän mukaan.
54 Kundi kubwa zaidi lipe urithi mkubwa zaidi, na kundi dogo zaidi lipewe urithi mdogo zaidi; kila kundi litapokea urithi wake kulingana na hesabu ya wale walioorodheshwa.
Isommalle suvulle anna isompi perintöosa ja pienemmälle pienempi perintöosa; kullekin annettakoon perintöosa katselmuksessa olleiden määrän mukaan.
55 Hakikisha kuwa nchi inagawanywa kwa kura. Kile kitakachorithiwa na kila kikundi kitakuwa kwa kulingana na majina ya kabila la babu yao.
Mutta maa jaettakoon arvalla. Isiensä heimojen nimien mukaan he saakoot perintöosansa.
56 Kila urithi utagawanywa kwa kura miongoni mwa makundi makubwa na madogo.”
Arvan määräyksen mukaan jaettakoon perintöosat suurilukuisten ja vähälukuisten heimojen kesken."
57 Hawa walikuwa Walawi ambao walihesabiwa kwa koo zao: kutoka kwa Gershoni, ukoo wa Wagershoni; kutoka kwa Kohathi, ukoo wa Wakohathi; kutoka kwa Merari, ukoo wa Wamerari.
Ja nämä olivat Leevin katselmuksessa olleet, sukujensa mukaan: Geersonista geersonilaisten suku, Kehatista kehatilaisten suku, Merarista merarilaisten suku.
58 Hizi pia zilikuwa koo za Walawi: ukoo wa Walibni; ukoo wa Wahebroni; ukoo wa Wamahli; ukoo wa Wamushi; ukoo wa wana wa Kora. (Kohathi alikuwa baba aliyemzaa Amramu;
Nämä olivat leeviläisten suvut: libniläisten suku, hebronilaisten suku, mahlilaisten suku, muusilaisten suku, koorahilaisten suku. Ja Kehatille oli syntynyt Amram.
59 jina la mke wa Amramu ni Yokebedi, naye pia alikuwa mzao wa Lawi, ambaye alizaliwa kwa Walawi nchini Misri. Alimzalia Amramu: Aroni, Mose na dada yao Miriamu.
Ja Amramin vaimon nimi oli Jookebed, Leevin tytär, joka oli Leeville syntynyt Egyptissä. Ja hän synnytti Amramille Aaronin ja Mooseksen sekä heidän sisarensa Mirjamin.
60 Aroni alikuwa baba yake Nadabu na Abihu, Eleazari na Ithamari.
Ja Aaronille syntyi Naadab ja Abihu, Eleasar ja Iitamar.
61 Lakini Nadabu na Abihu walikufa wakati walitoa sadaka mbele za Bwana kwa moto usioruhusiwa.)
Mutta Naadab ja Abihu kuolivat, kun toivat vierasta tulta Herran eteen.
62 Wanaume wote wa Walawi wa umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 23,000. Wao hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine kwa sababu hawakupokea urithi miongoni mwao.
Ja katselmuksessa olleita oli heitä kaksikymmentäkolme tuhatta, kaikki miehenpuolia, kuukauden vanhoja ja sitä vanhempia. Sillä heistä ei pidetty katselmusta yhdessä muiden israelilaisten kanssa, koska heille ei annettu perintöosaa israelilaisten keskuudessa.
63 Hawa ndio walioorodheshwa na Mose na kuhani Eleazari wakati waliwahesabu Waisraeli kwenye nchi tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
Nämä olivat siinä israelilaisten katselmuksessa, jonka Mooses ja pappi Eleasar pitivät Mooabin arolla lähellä Jordania, Jerikon kohdalla.
64 Hakuna hata mmoja wao aliyekuwa miongoni mwa wale waliohesabiwa na Mose na kuhani Aroni wakati waliwahesabu Waisraeli katika Jangwa la Sinai.
Eikä heidän joukossaan ollut ketään siinä israelilaisten katselmuksessa ollutta, jonka Mooses ja pappi Aaron olivat pitäneet Siinain erämaassa.
65 Kwa maana Bwana alikuwa amewaambia hao Waisraeli hakika wangekufa huko jangwani, wala hakuna mmoja wao aliyeachwa, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.
Sillä Herra oli heille sanonut, että heidän oli kuoltava erämaassa. Eikä heistä jäänyt ketään, paitsi Kaaleb, Jefunnen poika, ja Joosua, Nuunin poika.