< Hesabu 25 >

1 Israeli alipokuwa akikaa Shitimu, wanaume wa Israeli walianza kuzini na wanawake wa Kimoabu,
Israel se quedó en Sitim, y el pueblo comenzó a prostituirse con las hijas de Moab;
2 ambao waliwaalika kushiriki katika kutoa kafara kwa miungu yao. Watu wakala na kusujudu mbele ya miungu hii.
pues llamaron al pueblo a los sacrificios de sus dioses. El pueblo comía y se inclinaba ante sus dioses.
3 Kwa hiyo Israeli akaungana katika kumwabudu Baali wa Peori. Hasira ya Bwana ikawaka dhidi yao.
Israel se unió a Baal Peor, y la ira de Yahvé ardió contra Israel.
4 Bwana akamwambia Mose, “Uwachukue viongozi wote wa watu hawa, uwaue na uwaweke hadharani mchana peupe mbele za Bwana, ili hasira kali ya Bwana iweze kuondoka kwa Israeli.”
Yahvé dijo a Moisés: reúne a todos los jefes del pueblo y ahórcalos delante de mí, “Toma a todos los jefes del pueblo a Yahvé ante el sol, para que el furor de Yahvé se aparte de Israel.”
5 Kwa hiyo Mose akawaambia waamuzi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awaue wale wanaume wenu, walioshiriki katika kumwabudu Baali wa Peori.”
Moisés dijo a los jueces de Israel: “Maten todos a sus hombres que se han unido a Baal Peor”.
6 Ndipo mwanaume wa Kiisraeli akamleta mwanamke wa Kimidiani katika jamaa yake palepale mbele ya Mose na mkutano wote wa Israeli walipokuwa wakilia kwenye lango la Hema la Kukutania.
He aquí que uno de los hijos de Israel vino y trajo a sus hermanos una mujer madianita a la vista de Moisés y de toda la congregación de los hijos de Israel, mientras lloraban a la puerta de la Tienda de Reunión.
7 Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, alipoona jambo hili, akaondoka kwenye kusanyiko, akachukua mkuki mkononi mwake,
Cuando Finees, hijo de Eleazar, hijo del sacerdote Aarón, lo vio, se levantó de en medio de la congregación y tomó una lanza en su mano.
8 akamfuata yule Mwisraeli ndani ya hema. Akawachoma mkuki wote wawili kwa pamoja, ukapenya kwenye mwili wa yule Mwisraeli na mwili wa yule mwanamke. Ndipo tauni iliyokuwepo dhidi ya Waisraeli ikakoma.
Fue tras el hombre de Israel al pabellón, y los atravesó a ambos, al hombre de Israel y a la mujer por el cuerpo. Así se detuvo la plaga entre los hijos de Israel.
9 Lakini wale waliokufa kwa hiyo tauni walikuwa watu 24,000.
Los que murieron por la plaga fueron veinticuatro mil.
10 Bwana akamwambia Mose,
Yahvé habló a Moisés y le dijo:
11 “Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa kuhani Aroni, amegeuza hasira yangu mbali na Waisraeli, kwa sababu alikuwa na wivu kama nilio nao kwa heshima yangu miongoni mwao, hata kwamba kwa wivu wangu sikuwaangamiza.
“Finees, hijo de Eleazar, hijo del sacerdote Aarón, ha alejado mi ira de los hijos de Israel, ya que se puso celoso con mis celos entre ellos, para que yo no consumiera a los hijos de Israel en mis celos.
12 Kwa hiyo mwambie Finehasi ninafanya Agano langu la amani naye.
Por tanto, di: “He aquí que yo le doy mi pacto de paz.
13 Yeye pamoja na wazao wake watakuwa na Agano la ukuhani milele, kwa sababu alikuwa na wivu kwa ajili ya heshima ya Mungu wake, na akafanya upatanisho kwa Waisraeli.”
Será para él, y para su descendencia después de él, el pacto de un sacerdocio eterno, porque fue celoso por su Dios e hizo expiación por los hijos de Israel.’”
14 Jina la Mwisraeli ambaye aliuawa pamoja na mwanamke wa Kimidiani ni Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa jamaa ya Simeoni.
El nombre del hombre de Israel que fue asesinado con la mujer madianita era Zimri, hijo de Salu, príncipe de una casa paterna entre los simeonitas.
15 Jina la mwanamke wa Kimidiani aliyeuawa ni Kozbi binti wa Suri, aliyekuwa mkuu wa kabila la jamaa ya Wamidiani.
El nombre de la mujer madianita que fue asesinada era Cozbi, hija de Zur. Era jefe de la gente de una casa paterna en Madián.
16 Bwana akamwambia Mose,
Yahvé habló a Moisés, diciendo:
17 “Watendeeni Wamidiani kama adui na mwaue,
“Acosa a los madianitas y atácalos;
18 kwa sababu wao waliwatendea kama adui wakati waliwadanganya katika tukio la Peori na dada yao Kozbi, binti wa kiongozi wa Kimidiani, mwanamke ambaye aliuawa wakati tauni ilikuja kama matokeo ya tukio la Peori.”
porque te han acosado con sus artimañas, en las que te han engañado en el asunto de Peor, y en el incidente relativo a Cozbi, la hija del príncipe de Madián, su hermana, que fue asesinada el día de la plaga en el asunto de Peor.”

< Hesabu 25 >